Tabia zake utata mtupu

Tabia zake utata mtupu

Niendelee naye?

  • Ndiyo

    Votes: 2 28.6%
  • Hapana

    Votes: 5 71.4%

  • Total voters
    7
Ungetumia tu kiswahili ungeeleweka vizuri sana yanini kujipa shida na milugha ya watu hii.
Hili ni lugha za kujibia mitihani na kufanyia usahili.
Jaribu tu kutumia lugha iliyo rahisi isiyo kupa shida au basi kama unatumia kiingereza basi uaandike kiingereza tu ili ueleweke..
Ebu ona sasa ulichokifanya hapo.

Niushauri tu ukikufaa ufanyie kazi.

@lara1 effect hiyo.,!! Wanachanganya changanya tu swanglish... lara 1 anajiweza kidogo.
 
Last edited by a moderator:
Mimi na dada wa kitanzania mwenye umri wa miaka 26, nilianza mahusiano na kijana mmoja ambaye hadi sasa tuna muda wa miez 5, kijana huyu analikua akionyesha kutonijali wakati tunaanza mahusiano mimi ndiyo nilikua nikililia attention yake mara nyingi na tuna kaa mji mmoja ala alikua hajali hata zikipita siku3-4 hatujaonana, hapo nikaanza mwambia ukweli akaniona mimi mlalamikaji tu, ikafika wakati nikamwambia nina mimba yake,(nia kujua ataamua nini, ila sikua na mimba kweli, (baada ya kujua afya zetu)), majibu yake yalikua ni kunishauri nikatoe mimba since hakuwa tayari kuwa na familia na anafanya kazi na ni mwanafunzi wa masomo ya masters, well nikampa ukweli kwamba sina mimba nilitaka jua maamuz yake na kama yupo siriaz since hapendi condomise.

Pili wakati tunajuana alinidanganya kuhusu habari zake binafsi, kuhusu amekulia wapi, kwamba yeye ni mgeni katika huu mji tuliokutana, only to find out ni mwenyeji sana, alisoma nini akiwa chuo pia, hivyo vyote alinidanganya na hata kuna wakati nilikua nikimkamata anaongea tofauti na alivyoniambia alibisha, then niliamua vunja uhusiano kwa hvyo vigezo, ila alikuja omba msamaha sana na sababu zake kama hakuwa tayari na majukum ya mtoto, alidanganya sababu ya mazingira tuliyokutana(social network).

Then recently alikuwa darasani kwake anaposoma akawa anaongea na wenzake ana mawazo sana kwamba mke wake anatarajia jifungua na nyumba ndogo inamsumbua kama vile hawaelewani.

Yeye yupo darasa moja mbele yangu, my colleagues they overheard akiwa anasema hivyo, mimi nikaingia darasani na wenzangu wakaanza kumrejea aliyokua akisema sababu kuna mmoja aliona ni kitendo cha ajabu mtu kuongea hivyo vitu mbele za watu kama kuwa na mpango wa kando ni jambo la kawaida sana, wale wenzangu wakamchambua sababu walianza nihadithia mimi, (but walikua hawajui kama namfaham vizuri), mimi nkapata shauku ya kujua ukweli ya hayo, well baadae nikamuuliza akakubali alisema hayo na kusema alikua akitania tu na si kweli kwamba ana mke.

Haya yote yametokea wakati ananiomba msamaha turudiane, na anasema yeye anataka kuwa siriaz na mimi na kupeleka uhusiano wetu mbali, ila nina mashaka kama ni mkweli na nilishaanza msamehe ila imani yangu imenitoweka na yeye.Nimesha msamehe ila kurudiana naona kigugumizi sababu hata mimi ni binadamu naweza kosea siku moja,

USHAURI WAKO WA BUSARA PLEASE,
Where is that idiot from? Kwa kifupi hakufai.
 
@lara1 effect hiyo.,!! Wanachanganya changanya tu swanglish... lara 1 anajiweza kidogo.

Dah..binafsi huo mchanganyiko wa mlenda na pirau unanipa shida sana kumeza..
Sikuwahi kufundishwa pishi la namna hiyo.

Huyo wa kwenye blue nae ni yale yale tu.
 
hizi ni hadithi za kutunga,ila kama kweli basi naamini wanawake wameumbwa kwa ajili yetu wanaume na tuwatawale kwa kila jinsi,yaani dalili zote hizo bado mtu unauliza niendelee naye! kuna mtu alisema waalimu wa wanawake ni vipofu! achana naye acha ujinga unchezewa wewe!
 
na wewe pole kama hujaweza elewa code mixing na switching, yes ni lugha ya watu so nitaichakachua vile i please.. sikuomba ushauri wa language, kama hukuelewa, ahsante pia

Ni ushauri wa aina gani ulio uomba????
Lugha ndio tunayotumia kuwasilia na kutolea ushauri pia.
Sasa kama lugha unayo itumia haieleweki tutawezaje kukushauri???
 
Anyway ngoja tu tufupishe maelezo...

Kimbia haraka mno na siku nyingine kabla hujajipendekeza kwa mwanaume hakikisha umemchunguza vizuri...

Yaani usimkabidhi moyo wako mtu asiyeweza kuujali, utaishia kuumia mdogo wangu...

well, the same institute, yeye alitangulia mwaka mmoja mbele eg, 2009, mm nikajoin 2010. yes ni ndani ya 5, now 2 month imekata since tume na tofauti,
the point ya mimi kuingia darasani, ni kwamba tupo institute moja and was on for a group discussion ambapo na yeye na wenzake wamekaa upande mwingine wa darasa..so before mimi sijafika kulikua na classmets ambao mimi ndy nilikua nina discuss nao, wakaanza kuhadithia..
 
Mapenzi kuvumiliana Dada yangu. Inaonekana anakupenda. Asingekukua nakupenda asingekuomba msamaha. Kuhusu mimba ujue sisi wavulana huwa tunadetect kitu. alikua anajua tu unamdanganya ndo maana akakuambia ukatoe coz alijua hutatoa kitu. Kama yeye hajakwambia hakutaki basi endelea naye kuliko kuutesa moyo wako kwa mawazo yako hasi juu yake.

Jua binadamu tumeumbwa tofauti. Watu wengine hawajui kubembeleza wapenzi wao japo wanawapenda. So nakushauri uendelee na Mpenzi wako kwani mwapendana. Ungekua Umemuona huyo mke wake au hata mtoto hapo tungeongea Mengine. Nakushauri usimuache mpenzi wako please bali mshauri afanye mambo ya kukufurahisha. Na wewe usiwe unamtwega kwani watu wengine ukututega tunategeka. Acha kumvizia hata kama unaenda room kwake mpigie simu kabisa kwamba nakuja room kwako. Ukifanya hivyo Mapenzi yatadumu lakini ukitaka kumchunguza yatasambalatika. Bata ukimchunguza sana hautamla.

Usisikilize ushauri wa watu wasiojua thamani ya Penzi. ukishindwa kabisa njoo PM nikupe ushauri jinsi gani ya kuishi na Mchumba.

Pole sana

mhhh matango pori haya! Mume wa mtu huyo tayar! Afu unataka umshaur jins ya kuish naye kama mchumba! U cnt be crious!....
 
jinsi mapenzi yanavochanganya ndivo na taaarifa yako ilivonichanganya,,,,hebu iweke vizur.
 
Anyway ngoja tu tufupishe maelezo...

Kimbia haraka mno na siku nyingine kabla hujajipendekeza kwa mwanaume hakikisha umemchunguza vizuri...

Yaani usimkabidhi moyo wako mtu asiyeweza kuujali, utaishia kuumia mdogo wangu...

asante watu8
 
Hapo kwenye Poll ongeza kipengele cha "Amua mwenyewe" ili tuitumie haki yetu kiufasaha...
 
Back
Top Bottom