Tabia ya kubagua kazi ni kwa sababu ya kutokujua hili

matunduizi

JF-Expert Member
Aug 20, 2018
6,587
15,371
Mwanadamu umeumbwa kwa mfano wa Mungu. Baadhi ya sifa za Mungu ni kufanya kazi. Tena kwa ufanisi na ubora, huu uwezo kila mtu ameumbwa nao maana kila mtu ameumbwa kwa mfano wa Mungu.

Watu wengi wanabagua kazi, na wengine kufanya kazi kwa uvivu bila morali ni kwa sababu wanafikiri dhumuni la kazi ni kuwaingizia wao kitu (fedha) tu.

Kimsingi kwa mujibu wa bibilia, Kila kazi halali ina faida. Kazi nyingine zinakusaidia kukuondolea tabia mbaya kama kujiinua, matumizi mabaya ya fedha, kukuongezea kufikiri, kukufanya uone mambo ambayo usingeyaona kama ungepata kazi unayoipenda.

Katika kila kazi halali kuna faida. Jifunze kutanua wigo wa faida unazopata nje ya kipato chako kazini.

Ni hilo tu.

Barikiwa.

Mithali 14:23​

Katika kila kazi mna faida; Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.
 
Mimi naona usomi, wasomi hawapendi/wanadharau kazi za mikono
Tatizo muda wote wanaopata mafunzo wanajengewa taswira ya kufanya kazi za taaluma zao tena maofisini au wakiwa wasimamizi,Sasa anapokosa hiyo nafasi na anatokea familia duni ndio anajikuta analazimika kufanya Yale aliyoaminishwa kuwa sio ya hadhi yake au yawasio na akili,ila kiuhalisia Kila kazi ukiifanya vizuri itakupa matokeo mazuri

Sent from my Infinix X693 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom