Taarifa: Usalama Wangu Hatarini


Dha dha dha dha!!! Lakini Yuko Mungu aliye hai!! Mwamini Malaika wako mlinzi kuwa yuko tayari kwa lolote!!
 
Kwani akihama itasaidia nini kulinda usalama wake? mbona mnaandika utafikiri unakimbizwa? Kutishiwa kwake si kwasababu ya UCCM wake bali maneno yake yanawachukiza wanaoguswa! @Dr Slaa yuko Chadema mbona anawindwa kila siku?

Magamba hawawezi kumuwinda "Mchambuzi", yakimtaka yanamkamata kama kuku! Magamba yanawinda mtu aliyeyaa gamba kisha anawachokonoa huku naye anafaidi matunda ya ufisadi, umesahau alivosema EL kuwa, maadui wake wabaya ni wale walioko ndani ya CCM, walioko nje ya CCM hawamsumbui hata kidogo kwani ni rahisi kuwashughulikia!

Sisi kama watanzania tutaonea huruma wangapi wanaolamba viatu vya mafisadi kwa unafiki wao? Sita kila siku anawasema mafisadi live na halalamiki kuwa wanataka kumtoa meno! Mchambuzi ni mjinga (natumia neno zuri 'mjinga' siyo mpumbavu), sasa tuna muelimisha ujinga umtoke ili avue gamba. Kama taendelea kukaa huko watam-sodomize ndipo atakapopata akili ya kuhama!
 
Mwandishi wa makala katika gazeti la raia mwema anaeitwa Joseph Mihangwa, alishawahi kuandika makala yenye kichwa "TAIFA LETU MIKONONI MWA GENGE LA MAFIA"
 
pole sana Kamanda,mapinduzi daimaa,usirudi nyuma,ulizaliwa mala moja na utakufa mala moja,hata atakayekudhuru nae atakufa mala moja,hakuna atakaye baki ktk hii dunia.
ujio wa xijiping ni matunda ya baba wa taifa,aliweka misingi na sasa wanaofaidi ni sisi,nawe usihofu,weka misingi imala na manufaa yake utayaona,hata kama hutofaidi wewe na mimi watafaidi vijana wetu
Tupo pamoja ktk hili na ikiwezekana lipoti visa hivi polisi ili likitokea wajue wapi pa kuanzia
 

Jipange upya kuongopa ktk mazingira ya kificho hapo umecheka hizo ni sanaa ndogondogo sana
 
You are coward and i don't think wewe ni mpiganaji wa ccm kama niaje angalia uwezekano...,ccm ina wanajeshi wakutosha wa kukipigania si kama cdm inanguzo chache moja ikidondoka nacho kinapumulia machine .

huko magambani mnapigania nini?
 

Daaaah, mkuu una moyo wa ajabu sana, kwa haya tu inaonyesha huna sababu ya kuwa CCM
 
Hivi nchi yetu inaelekea wapi? Kwani kutofautiana kwa mtazamo unakuwa adui wa kuuliwa?
 

Alishajitaja mwenyewe hapa jamvini,anaitwa Mpoki
 

Hapo kwenye red ndio kunakufanya useme yote hayo!
 

Tatizo anatumia picha yake halisi
 
That is the thing...nakubaliana nawe Ngalikihinja. Hiyo ndiyo ilipaswa kuwa hoja. Pamoja.

Tumani wewe wakati mwingine una matatizo sana, unakosa staha za kichadema. Mwenzako katishwa maisha wewe unajenga hoja uchwara hapa. Wakati mwingine unakosoa hadharani hata thread za viongozi wenzako wa Chadema hadharani. Halafu sisi wengine mnatufundisha nini?
 
Nyerere mwenye(RIP),nahisi walimfanyia.Kuna Sokoine,Kolimba,Mwakyembe,Mwandyosa na wengineo wengi tu,achilia mbali walioteswa na kuuwawa chini ya serikali ya ccm kama kina Dr Ulimboka,Kibanda,Mwangosi na wengineo wengi tu.

CCM walishawahi hadi kuwekeana uchawi bungeni wakati wa issue ya "unga unga" wa kina Chenge.

Mkuu kama ni kweli huogopi kufa na unaipenda ccm kiasi hiki,basi kila la kheri.
 
pole sana Mchambuzi

vema umelitambua hilo mapema

hao watishaji wanaamini wakikumaliza ndio moto wa mapinduzi utazimika?
 
huko magambani mnapigania nini?

maslahi ya watanzania wote kwa ujumla si ya sehemu flani au kabila au dini.
Chama cha CCM kina wajali wananchi wake si chama cha kusacrifice watu kwa manufaa ya wachache.
 
Tunapitia katika kipindi cha mateso. Watesaji ni Watanzania wenzetu wanatumia kodi zetu kututenda. Kwa post hii inaminisha kabisa watoa meno, kucha, macho, wauaji nk ni viongozi wa CCM wakitumia wanausalama wetu.

Ukiishi naye lazima ukubaliane naye, ukipingana naye hawezi kukupenda wala kukubali ndio maana wengi wakamkimbia.
Mchambuzi sioni ni kwa jinsi gani utaweza kuibadilisha CCM ukiwa ndani.

Moja unaowaita wazee tayari wameandaa vijana wenye mawazo kama yao, utesaji kama wao na kulindana. Tayari vijana walio wengi wa CCM wameshiriki kumtesa mtanzania kwa wizi, rushwa, ufisadi,hujuma nk haiwezekani hawa vijana wa CCM kuja kuwa bora hata siku moja.

Angalia Mwigulu na matukio yote ya utesaji, mauaji anatajwa, Sikiliza Nape alivyokeli kuteswa kwa Kibanda. Sikiliza Riz alivyolihadaa taifa kwa kukana maandishi yake, wapi Ngeleja na masha na utendaji wao. Wapo Jerry Slaa na matamshi yake. Je hawa ni wazee mkubwa???

Watesaji na wauaji wako ni vijana ambao kwao ndio anguko la CCM ni hatari kuliko wazee. Vijana wa CCM ndio wabaya zaidi kuliko hao wazee unaowaogopa. Kwa kifupi ukipingana na CCM ndani ya CCM kila mmoja mzee na kijana atakutoa menu na kucha bila ganzi.

Vitisho ni real, na lazima uwe makini, ila kama tayari fungu la kukutoa kucha limeshatolewa kaka sioni pa kutokea. Mwakyembe aliripoti kila sehemu mpaka ikulu ila walimkabidhi kitu yake.

Maaskofu walitoa ripoti za kuuwawa wao na mapadri ila haikusaidia kubeep watawala wakafanya kweli. Mwangosi aliwapelekea taarifa za vitisho wakamaliza wenyewe. Kama wamempofua dingi na wameishi naye kwa miaka mingi wanajuana vizuri ijekuwa wewe ???

Unatetea vipi mfu? Ili CCM iwe imara lazima ife kwanza. Uhai wako ni bora sana, ni vyema ungetumia busara kupima kama unatetea mabadiliko au unapoteza nguvu kutetea wafu. Hakuna kitu wanaCCM viongozi hawajui wameamua kufanya wafanyavyo kwa makusudi. wanajua kabisa kwamba wao ni wezi, wavivu, walafi, hawana huruma, wanyama, wako tayari kula rushwa kuliko kutengeneza choo wanachotumia. Angalia ofisi zao zilivyochafu, angalia hospitalia zao zilivyo mbovu. Mtu asiyejijali yeye mwenyewe hawezi kukujali wewe.

Kubali kung'olewa kucha au achana na wang'oa kucha.
 


Afadhali baada ya kuedit kidogo. Lazima ujue nafasi yako siyo kukosoa tu kila kitu. Unatuaibisha wakati mwingine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…