Crashwise
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 22,227
- 8,735
TAARIFA KWA UMMA
TUKIO LA MHE GODBLESS LEMA (MB) KWENDA KWA RUMANDE KWA HIARI UJUMBE WA MSINGI WA KUZINGATIA.
01 NOVEMBA 2011
TUKIO LA MHE GODBLESS LEMA (MB) KWENDA KWA RUMANDE KWA HIARI UJUMBE WA MSINGI WA KUZINGATIA.
01 NOVEMBA 2011
Ndugu wanahabari na Wananchi kwa ujumla,
CHADEMA mkoa wa Arusha, imesikitishwa sana na utendaji kazi wa jeshi la polisi hususani OCD wa wilaya ya Arusha mjini. Katika kipindi na baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana OCD amekuwa akifanya kazi ya siasa kwa wazi wazi, mara nyingi tumekemea tabia hii na hata kutoa msimamo wa CHAMA kuwa huyu OCD ni chanzo cha migogoro yote hapa Arusha hivyo kuitaka mamlaka husika kuliangalia jambo hili na utendaji kazi wa OCD huyu.
CHADEMA tumesikitishwa na tunaendelea kusikitishwa sana na double standard za jeshi la polisi hapa Arusha kwa kuendelea kufanya kazi kwa maelekezo ya kisiasa. Mtakumbuka Uvccm waliandamana na kufanya mkutano na maandamano ya zaidi ya saa nane, ambayo OCD huyu huyu aliyapiga marufuku, lakini kwa ajabu ndie aliyeyapa ulinzi kwa muda wote, ajabu zaidi ni pale Kaimu RPC aliponukuliwa akisema kuwa yale maandamano ni haramu ila jeshi la polisi litatoa ONYO kwa ccm.
Walioandamana jeshi la polisi linatoa onyo na kwa CHADEMA ambao haijaandamana wanafunguliwa mashtaka,huu ni uhuni na uwendawazimu wa hali ya juu na kamwe hatutavumilia wala kukubali tabia hii ambayo ni hatari kwa usalama wa taifa.
Kwa makusudi kabisa Ijumaa ya Tarehe 28, polisi alivamia ofisi ya Mbunge akiwa na zaidi ya polisi 80, kwenye magari matatu na kuanza kuwapiga,na kuwadhalilisha wapiga kura waliokuwa ofisini,tendo hili ovu lilifanyika kwa kisingizio kuwa kuna maandamano na mkutano, hatimaye hawa wananchi walifikishwa polisi na kufunguliwa mashtaka ya kuandamana bila kibali. Wengi wa waliokamatwa alikuwemo diwani wa CHADEMA kutoka DSM aliyekuja Arusha kwa safari yake binafsi na aliamua kwenda ofisini kwa mbunge kumsalimia. Mhe Azuri (Diwani) huyu akakutana na azama hii na sasa nae ana kesi mahakamani ya maandamano na kufanya mkutano wa hadhara, aibu tupu hii kwa jeshi la polisi kufanya kitendo hiki.
Je wananchi kwenda kumwona Mbunge wao ni maandamano? Kutembea kutoka mahakamani nayo ni maandamano?
Jumatatu tarehe 31.10.2011 wananchi pamoja na mbunge walifikishwa mahakamani na kusomewa mashtaka ya kufanya mkutano kinyume cha sheria, hatimaye wapiga kura 19 walitoka kwa dhamana hadi 19 Novemba. Mbunge wa Arusha mjini alikataa dhamana kama njia ya kukataa uonevu, ukandamizaji,na dhuluma inayofanywa na polisi dhidi ya raia wema wa Arusha na Tanzania kwa ujumla.
Kimsingi ni maamuzi magumu ila lazima yafanyike. Polisi wamekuwa na tabia na utamaduni wa kutisha wananchi,na kuwaogofya kuwa watawapeleka ndani(GEREZANI) kama vile gerezani ni adhabu kubwa sana.
Mbunge Lema ameamua kwa hiari yake mwenyewe kutangulia CHADEMA tunatambua mbinu na mikakati yote inayofanywa na Serikali kwa kutumia polisi na usalama wa taifa mipango hii ina lengo la kukwamisha maendeleo ya Arusha, ili wananchi wakate tamaa na kuichukia CHADEMA, lakini pia kuna mipango michafu ya kuwabambikia Kesi viongozi wa CHADEMA pamoja na vijana na wanachama walio msitari wa mbele.
Mtakumbuka kuwa waliwahi kumtuhumu mwenyekiti wa wilaya Mhe Ephata Nanyaro kwa tuhuma za kula njama za kuua, jaribio hilo ovu pamoja na mengine yameshindwa na hata haya nayo YAMESHINDWA.Na sisi tulio upande wa haki tutashinda.
CHADEMA mkoa tunaupongeza ujasiri huu wa Mbunge wa Arusha mjini,na tunawataka wanachama wetu, wapenzi wetu na wananchi wote wa Arusha kuamka na kupinga dhuluma, uhuni, ukandamizaji na ukiukwaji huu wa sheria kwa vitendo. Ni wajibu wa kila mmoja mpenda haki kuungana nasi katika kipindi hiki.
Kamwe tusikubali mtu mmoja OCD eti tu kwa kuwa ana polisi wenye silaha kututisha,au kutuogopesha. Hatuogopi wingi wa askari,au wingi wa silaha, kwani hakuna silaha itakayoweza kushindana na NGUVU YA UMMA.
Hatuogopi silaha wala magereza na wakitaka waongeze silaha na kupanua magereza kwani tupo wengi majasiri ambao tupo tayari kupoteza chochote hata ikibidi uhai wetu ili haki na ukweli,na usawa upatikane.
Tumeonewa vya kutosha tumenyanyaswa vya kutosha tumedhulumiwa vya kutosha tumekandamizwa vya kutosha na sasa tunasema HAPANA IMETOSHA. Vijana tuamke, Wanawake tuamke, wazee tuamke kwa ujumla wetu tuamke na tuipinge tabia hii ya jeshi la polisi ya kuwatia hofu wananchi na wanasiasa kwa kiasi cha kuleta mahusiano mabaya na dola hii muhimu.
Nimalizie kwa kunukuu maneno ya mhe Godbless Lema (MB) katika waraka wake wakati akikataa dhamana, ameandika;
"Wale mlionitishia kunipeleka jela sasa nimetangulia kwa hiari yangu na wale mliobaki msiogope jela endeleeni kupigania ukombozi utakaoleta usawa katika nchi yenu".
Akamalizia kwa kusema kuwa;
"Watakaotubeza na kututukana wasameheni kwani wanahitaji ukombozi wa fikra, watakaotupongeza na kutuonea huruma wafundisheni ujasiri na waambieni mapambano bado yanaendelea tunahitaji umoja wao. Nitarudi mapema. MSIOGOPE, MSIOGOPE, MSIOGOPE , MUNGU YUPO UPANDE WETU"
Kwa tukio hili tunataka masuala ya msingi ya Arusha yashughulikiwe:
CHADEMA mkoa wa Arusha, imesikitishwa sana na utendaji kazi wa jeshi la polisi hususani OCD wa wilaya ya Arusha mjini. Katika kipindi na baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana OCD amekuwa akifanya kazi ya siasa kwa wazi wazi, mara nyingi tumekemea tabia hii na hata kutoa msimamo wa CHAMA kuwa huyu OCD ni chanzo cha migogoro yote hapa Arusha hivyo kuitaka mamlaka husika kuliangalia jambo hili na utendaji kazi wa OCD huyu.
CHADEMA tumesikitishwa na tunaendelea kusikitishwa sana na double standard za jeshi la polisi hapa Arusha kwa kuendelea kufanya kazi kwa maelekezo ya kisiasa. Mtakumbuka Uvccm waliandamana na kufanya mkutano na maandamano ya zaidi ya saa nane, ambayo OCD huyu huyu aliyapiga marufuku, lakini kwa ajabu ndie aliyeyapa ulinzi kwa muda wote, ajabu zaidi ni pale Kaimu RPC aliponukuliwa akisema kuwa yale maandamano ni haramu ila jeshi la polisi litatoa ONYO kwa ccm.
Walioandamana jeshi la polisi linatoa onyo na kwa CHADEMA ambao haijaandamana wanafunguliwa mashtaka,huu ni uhuni na uwendawazimu wa hali ya juu na kamwe hatutavumilia wala kukubali tabia hii ambayo ni hatari kwa usalama wa taifa.
Kwa makusudi kabisa Ijumaa ya Tarehe 28, polisi alivamia ofisi ya Mbunge akiwa na zaidi ya polisi 80, kwenye magari matatu na kuanza kuwapiga,na kuwadhalilisha wapiga kura waliokuwa ofisini,tendo hili ovu lilifanyika kwa kisingizio kuwa kuna maandamano na mkutano, hatimaye hawa wananchi walifikishwa polisi na kufunguliwa mashtaka ya kuandamana bila kibali. Wengi wa waliokamatwa alikuwemo diwani wa CHADEMA kutoka DSM aliyekuja Arusha kwa safari yake binafsi na aliamua kwenda ofisini kwa mbunge kumsalimia. Mhe Azuri (Diwani) huyu akakutana na azama hii na sasa nae ana kesi mahakamani ya maandamano na kufanya mkutano wa hadhara, aibu tupu hii kwa jeshi la polisi kufanya kitendo hiki.
Je wananchi kwenda kumwona Mbunge wao ni maandamano? Kutembea kutoka mahakamani nayo ni maandamano?
Jumatatu tarehe 31.10.2011 wananchi pamoja na mbunge walifikishwa mahakamani na kusomewa mashtaka ya kufanya mkutano kinyume cha sheria, hatimaye wapiga kura 19 walitoka kwa dhamana hadi 19 Novemba. Mbunge wa Arusha mjini alikataa dhamana kama njia ya kukataa uonevu, ukandamizaji,na dhuluma inayofanywa na polisi dhidi ya raia wema wa Arusha na Tanzania kwa ujumla.
Kimsingi ni maamuzi magumu ila lazima yafanyike. Polisi wamekuwa na tabia na utamaduni wa kutisha wananchi,na kuwaogofya kuwa watawapeleka ndani(GEREZANI) kama vile gerezani ni adhabu kubwa sana.
Mbunge Lema ameamua kwa hiari yake mwenyewe kutangulia CHADEMA tunatambua mbinu na mikakati yote inayofanywa na Serikali kwa kutumia polisi na usalama wa taifa mipango hii ina lengo la kukwamisha maendeleo ya Arusha, ili wananchi wakate tamaa na kuichukia CHADEMA, lakini pia kuna mipango michafu ya kuwabambikia Kesi viongozi wa CHADEMA pamoja na vijana na wanachama walio msitari wa mbele.
Mtakumbuka kuwa waliwahi kumtuhumu mwenyekiti wa wilaya Mhe Ephata Nanyaro kwa tuhuma za kula njama za kuua, jaribio hilo ovu pamoja na mengine yameshindwa na hata haya nayo YAMESHINDWA.Na sisi tulio upande wa haki tutashinda.
CHADEMA mkoa tunaupongeza ujasiri huu wa Mbunge wa Arusha mjini,na tunawataka wanachama wetu, wapenzi wetu na wananchi wote wa Arusha kuamka na kupinga dhuluma, uhuni, ukandamizaji na ukiukwaji huu wa sheria kwa vitendo. Ni wajibu wa kila mmoja mpenda haki kuungana nasi katika kipindi hiki.
Kamwe tusikubali mtu mmoja OCD eti tu kwa kuwa ana polisi wenye silaha kututisha,au kutuogopesha. Hatuogopi wingi wa askari,au wingi wa silaha, kwani hakuna silaha itakayoweza kushindana na NGUVU YA UMMA.
Hatuogopi silaha wala magereza na wakitaka waongeze silaha na kupanua magereza kwani tupo wengi majasiri ambao tupo tayari kupoteza chochote hata ikibidi uhai wetu ili haki na ukweli,na usawa upatikane.
Tumeonewa vya kutosha tumenyanyaswa vya kutosha tumedhulumiwa vya kutosha tumekandamizwa vya kutosha na sasa tunasema HAPANA IMETOSHA. Vijana tuamke, Wanawake tuamke, wazee tuamke kwa ujumla wetu tuamke na tuipinge tabia hii ya jeshi la polisi ya kuwatia hofu wananchi na wanasiasa kwa kiasi cha kuleta mahusiano mabaya na dola hii muhimu.
Nimalizie kwa kunukuu maneno ya mhe Godbless Lema (MB) katika waraka wake wakati akikataa dhamana, ameandika;
"Wale mlionitishia kunipeleka jela sasa nimetangulia kwa hiari yangu na wale mliobaki msiogope jela endeleeni kupigania ukombozi utakaoleta usawa katika nchi yenu".
Akamalizia kwa kusema kuwa;
"Watakaotubeza na kututukana wasameheni kwani wanahitaji ukombozi wa fikra, watakaotupongeza na kutuonea huruma wafundisheni ujasiri na waambieni mapambano bado yanaendelea tunahitaji umoja wao. Nitarudi mapema. MSIOGOPE, MSIOGOPE, MSIOGOPE , MUNGU YUPO UPANDE WETU"
Kwa tukio hili tunataka masuala ya msingi ya Arusha yashughulikiwe:
- Uonevu wenye nia ya kujenga hofu kwa wananchi, wanachama wa CHADEMA, Mbunge na viongozi wa chama – njama hizo zikome na jeshi lifanye kazi yake kwa haki.
- Suala la UMEYA – Haki ni msingi wa maendeleo. Dhambi iliyofanywa ya kumchagua MEYA wa CCM mhe Gaudence Lyimo kwa hila bila kufuata utaratibu itaitafuna Arusha na itakuwa kikwazo cha maendeleo. Haki ifuatwe na uchaguzi urudiwe. CHADEMA hatumtambui MEYA huyo.
Tunawaomba wakazi wa Arusha na wanachama wetu wote waendelee kudumisha utulivu, umoja na amani vitu ambavyo ndivyo hasa tabia yetu na kamwe tusishiriki katika vurugu na tusiharibu mahusiano yetu na jeshi la polisi ambao tunawatarajia watafanya kazi zao kwa haki. Wakazi wa Arusha tufanye kazi na tujitume kwa bidii kwa maendeleo ya jimbo letu.
Mungu Ibariki Arusha, Mungu Ibariki Tanzania.
Amani Golugwa
KATIBU WA CHAMA MKOA – ARUSHA.
Mungu Ibariki Arusha, Mungu Ibariki Tanzania.
Amani Golugwa
KATIBU WA CHAMA MKOA – ARUSHA.