KERO Taarifa Binafsi: Kampuni ya mkopo mtandaoni (online loan app) imenidhalilisha sana

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Huenda ni mimi nilifanya makosa kwa kutopitia terms & conditions vizuri ila hawa jamaa walicho nifanyia ni uzalilishaji mkubwa sana.

Kuna app moja mtandaoni (play store) inaitwa "PESA M FINANCE".

Hawa jamaa walinikopesha elfu 42 mtandaoni kwa muda wa siku 7.

Siku jana nilitakiwa ndiyo nilipe, na jana hiyo nilikuwa kazini nikitegemea nitoke kazini jioni niwalipe pesa yao.

Lakini nashangaa jana mida ya mchana saa saba, watu wanaanza kunitumia kunipigia simu na kunifoadia sms kuwa nadaiwa.

Kumbe hii kampuni ilichofanya baada ya kunikosa hewani jana mda flani, wakatuma sms kwa watu wote walioko kwenye phone book yangu (watu zaidi ya 200) kuwajuza kuwa wananidai na nataka kuwatapeli.

Nikawa napata simu ngingi sana kutoka kwa hao watu waliotumiwa hiyo sms.

Aisee niliona ni udhalilishaji sana hii kampuni imenifanyia.

Sasa nikajiuliza walipataje majina yaliyopo kwenye simu yangu, hapo ndipo nilipokumbuka kwenye app yao ukiwa unafungua kuna sehemu itaandika "allow access to your contacts, messeges n.k" hapo ndipo walipopata majina ya phone book yangu.

Sasa tangu jana hiyo nimekosa raha kabisa baada ya kuzalilishwa na mimi nimeamua kutowalipa mpaka sasa.

Nimepata wazo la kutafta mwanasheria nikawafungulie kesi ya kunidhadhalisha wanilipe fidia, kwanini wanidhalilishe wakati dead line ya malipo ilikuwa bado haijapita
View attachment 2910966View attachment 2910967
Fungua kesi ya defamation watakulipa fidia na litakuwa funzo kwao na kwa makampuni uchwara kama hayo.

Hawana credibility ya kukutangaza kwa watu ambao hukuwaweka kama wadhamini wako.

Pia deadline ilikuwa bado na pia hata deadline ingepita bado wangekupa muda wa ziada wa kulipa deni lao.
 
Hii adha alikutana nayo PS wa ofisini kwetu, tulimshauri atafute mwanasheria akaogopa akaishia kulalamika. ila yeye case yake ni tofauti kidogo, walimdhalilisha akiwa ameshafanya malipo tayari na wao ndio walichelewa kuconfirm malipo.
Kwanini watu wanaacha pesa za wazi wazi hivi? Hapo akifungua kesi ya defamation anashinda maana sheria ipo wazi huwezi kumtangaza mtu mitandaoni kwamba unamdai pasipo kufuata procedures zote.
 
Hiyo access uliwapa wewe mwenyewe....
Mara ya kwanza ulipoanza kutumia hiyo app ilikutaka uruhusu matumizi kama location,storage na some authority options ndio maana yamekutokea hayo....

Hao dawa yao simu inakua rooted,Una remove acces ya contact unawaomba mkopo,wanakupa....
Unafungua lucky patcher unaedit custom firmware za app halafu unafuta na application
Kuwapa access haimaanishi watumie namba zake unless wametaja hicho kipengele.
 
Wananitishia kuwa watanitafta niwatejeshe na gharama walizotumia, au ni mikwara tu.

Sema wameniaibisha sana
Matapeli tu hao wanafanya online business kitapeli hawalipi kodi mbalimbali za serikali na ukute hawana kibali kutoka wizara ya fedha kufanya biashara mtandao.

Hao wakifikishwa mahakamani wataumbuka kwa mambo mengi sana na kukulipa fidia juu.
 
Screenshot_20240221-140022.png

benki kubwa wanaonya watu kila siku
 
H
Fungua kesi ya defamation watakulipa fidia na litakuwa funzo kwao na kwa makampuni uchwara kama hayo.

Hawana credibility ya kukutangaza kwa watu ambao hukuwaweka kama wadhamini wako.

Pia deadline ilikuwa bado na pia hata deadline ingepita bado wangekupa muda wa ziada wa kulipa deni lao.
Hata kama dead line ingekuwa imepita kuna due interest (ada ya ucheleweshaji) huwa wanaweka.

Ndiyo maana mimi naona kwa kunitangaza kisheria wamenikosea.
 
Nipo kwenye cycle ya hii industry, ni ngeni kwa Tz ila Kenya, Nigeria, Ghana kote hii industry ilishapita.

Kuna sheria za kudai na kuwasiliana na mteja, kuna sheria pia za kuwasiliana na 'wadhamini' wa mteja.

Kampuni hujitahidi kucheza ndani ya hizi sera na sheria. Inatarajiwa mkopaji akipigiwa apokee kama ana plan mpya ya ulipaji aiseme ama ana changamoto n.k

Anayekupigia ana target ya kuifikia kwa siku ili alipwe mshahara, na wengi hua na prejudice kua mteja hataki kulipa ndiyo sababu wengi hufanya hivyo.

Consult mwanasheria, angalia wapi wamekosea na kama sheria inakupa locus standi
 
Hiyo access uliwapa wewe mwenyewe....
Mara ya kwanza ulipoanza kutumia hiyo app ilikutaka uruhusu matumizi kama location,storage na some authority options ndio maana yamekutokea hayo....

Hao dawa yao simu inakua rooted,Una remove acces ya contact unawaomba mkopo,wanakupa....
Unafungua lucky patcher unaedit custom firmware za app halafu unafuta na application
ukiunstall application vp bado wanaweza kuaccess your phonebook?
 
Back
Top Bottom