Taa za umeme za LED huleta nafuu katika bili ila ni hatari kwa afya

Transistor

JF-Expert Member
Aug 8, 2013
970
1,461
Heri ya mwaka mpya wakuu,

Taa za LED zimepata umaarufu miaka ya hivi karibuni kutokana na kuwa na mwanga mkubwa huku ulaji wake wa umeme ukiwa ni kidogo.

Licha ya faida hiyo kutokana na tafiti mbalimbali taa za LED,zimeonekana kuwa na madhara kiafya,licha ya wataalamu wanao unda taa hizi kuzidi kuziboresha,ili kuepukana na madhara hayo.

Mwaka 2016,shirika la kimarekani la American Medical Association(AMA),lilisema tekinolojia ya taa za LED,yana athari kwa afya ya binadamu.

Taa za LED zinazalisha mwanga wake kwa kutumia mawimbi mafupi,mawimbi haya yana kiasi cha nguvu ya juu cha miale ya blue na violet yaliyo katika kiwango cha kuonwa na jicho la binadamu.

Endapo macho ya binadamu yatazama mwanga huu huweza kuathirika kwa kiasi fulani katika uwezo wake wa kulala,mara kadhaa baadhi ya watu wamekuwa wakikumbwa na tatizo la kuwashwa macho ama kichwa kuuma baada ya kuwa katika mwanga wa taa za LED kwa muda mrefu.

Endapo mtu atakua katika mazingira haya ya mwanga wa taa za LED,basi miale ya blue inayozalishwa na mwanga wa taa hizi huweza kusababisha ugonjwa wa mtoto wa jicho (cataract) ,au tatizo la uoni hafifu (Macular degeneration).

Pia tafiti zinaonesha kuwa miale inayozalishwa na mwanga wa taa za LED,husababisha mabadiliko ya "retinal" katika jicho hata kwa matumizi ya muda mfupi tu ya taa hizi.

Tafiti ya mwaka 2014 ya shirika la afya ya mazingira inaonesha panya ambao waliwekwa katika mazingira ya taa za mwanga wa LED,walionekana kuathirika macho zaid dhidi ya wale waliowekwa katika vyanzo vya mwanga mwingine.

Watafiti wanashauri matumizi ya mwanga kuepuka matumizi ya mwanga mweupe hasa unaozalishwa na taa za LED,ambao una kiasi kikubwa cha miale ya blue,ambayo ni hatari kwa afya ya macho,na watumie taa za tubelight hasa sehemu za kupumzikia au sehemu ya kulala.

Wataalamu wanasisitiza kuwa macho ya binadamu yana uwezo wa kupambana na miale hii ya blue,lakini uwezo huu hutofautiana kati ya mtu na mtu kwa sababu za kimaumbile lakini pia sababu ya umri,ambapo watoto na watu wazima wapo katika hatari zaidi ya kudhurika na miale hii.

Taa hizi pia husababisha kichwa kuuma kwasababu huwaka na kuzima kwa kila hatua kwa asilimia 100,hii husababisha ubongo kufanya kazi kwa kasi zaidi wakati ukiutafsiri mwanga,kwa kifupi taa hizi hazifai kwa kusomea.wakati taa za kawaida za mwanga mweupe tubelight zenyewe huwaka na kuzima kwa asilimia 30 tu,hivyo hizi hua haziumizi kichwa.

Wataalam wanashauri kuzuiwa kwa miale ya blue katika taa hizi angalau kwa kiwango cha 415-455 nanometer kwa taa ambazo zinatumika majumbani.

Imeandaliwa na Transistor.
 
Yani huo mwanga wa LED kwa sasa haukwepeki sababu screen au display za vifaa vya kielectroniki kama Simu, TV, Computer, na kadharika hutumia mwanga wa LED kama backlight.

Ukitaka kukwepa huo mwanga usitumie simu, TV, Computer na kifaa chochote chenye display hizi za kisasa.
Kwa wale watumiaji wazuri na kwa masaa mengi simu au computer unaweza kwenda kwa mtaalamu wa macho akakuandikia miwani inayopunguza huo mwanga wenye tatizo.

Mimi nilipewa lakini inanishinda kuitumia naona kama ndio inanifanya nichoke haraka na akili haitulii.
Magnification yake ni ndogo sana, ile namba ya mwisho ya chini lakini bado naona inakuza zaidi ya uhitaji wangu.
 
Labda watu wanunue miwani ya anti-glare ya kawaida tu yaani zero magnification lakini inapunguza huo mwanga mbaya.
 
Yani huo mwanga wa LED kwa sasa haukwepeki sababu screen au display za vifaa vya kielectroniki kama Simu, TV, Computer, na kadharika humia mwanga wa LED kama backlight.

Ukitaka kukwepa huo mwanga usitumie simu, TV, Computer na kifaa chochote chenye display hizi za kisasa.
Kwa wale watumiaji wazuri wa masaa mengi wa simu au computer unaweza kwenda kwa mtaalamu wa macho akakuandikia miwani inayopunguza huo mwanga wnye tatizo.

Mimi nilipewa lakini inanishinda kuitumia naona kama ndio inanifanya nichoke haraka na akili haitulii.
Magnification yake ni ndogo sana, ile namba ya mwisho ya chini lakini bado naona inakuza zaidi ya uhitaji wangu.
Uko sahihi mkuu
 
Yani huo mwanga wa LED kwa sasa haukwepeki sababu screen au display za vifaa vya kielectroniki kama Simu, TV, Computer, na kadharika humia mwanga wa LED kama backlight.

Ukitaka kukwepa huo mwanga usitumie simu, TV, Computer na kifaa chochote chenye display hizi za kisasa.
Kwa wale watumiaji wazuri wa masaa mengi wa simu au computer unaweza kwenda kwa mtaalamu wa macho akakuandikia miwani inayopunguza huo mwanga wnye tatizo.

Mimi nilipewa lakini inanishinda kuitumia naona kama ndio inanifanya nichoke haraka na akili haitulii.
Magnification yake ni ndogo sana, ile namba ya mwisho ya chini lakini bado naona inakuza zaidi ya uhitaji wangu.
Kwa sasa vifaa vya electronics ambavyo ni high quality wamekuwa wakifilter blue light.

Hasa hili nimeliona kwenye simu TV na computers...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yani huo mwanga wa LED kwa sasa haukwepeki sababu screen au display za vifaa vya kielectroniki kama Simu, TV, Computer, na kadharika humia mwanga wa LED kama backlight.

Ukitaka kukwepa huo mwanga usitumie simu, TV, Computer na kifaa chochote chenye display hizi za kisasa.
Kwa wale watumiaji wazuri wa masaa mengi wa simu au computer unaweza kwenda kwa mtaalamu wa macho akakuandikia miwani inayopunguza huo mwanga wnye tatizo.

Mimi nilipewa lakini inanishinda kuitumia naona kama ndio inanifanya nichoke haraka na akili haitulii.
Magnification yake ni ndogo sana, ile namba ya mwisho ya chini lakini bado naona inakuza zaidi ya uhitaji wangu.
Ukichoka inabidi ukalale. Hiyo blue light inaendelea kukufanya ubaki macho. Ushindwe kupata usingizi...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nileshakuwa addict wa LED. Mwanga Murua kabisa. Hasa nyumba ikiwa umepaka rangi nyeupe.....Safiiii. Yaani inapendeza sana.
 
Back
Top Bottom