Bongo tambarare! Mitambo hii iliyosifiwa na Clinton ni ile mitambo ya Dowans/Richmond iliyopigiwa kelele sana na wabunge wengi na baadhi ya mashabiki wa kisiasa Tanzania. Kinachotumaliza Tanzania ni ushabiki wa kisiasa hata katika vitu vyenye kuleta tija kwa taifia. Sasa ngoja tusikie yule atakayepiga kelele tena kama hajaambiwa wewe America, UK, Canada, etc hapana kanyaga.
Nadhani chuki za wanasiasa wa CCM ya wao kwa wao imetupelekea tuwe hapa tulipo leo. Hii pia inachangiwa na vyombo vyetu vya habari ambao nao wanaandika taarifa za kinafiki bila kufanya utafiti yakinifu na kutoa majibu ya utafiti hadharani. Nyingi utasoma tu kwa habari toka chanzo chetu, wakati mwingine unakuta mwandishi anatoa maono yake tu lakini ili ionekane habari anaandika as if kuna source.
Naunga mkono kuwashwa kwa mitambo hiyo ya Dowans kupitia Symbion na nasihi Tanesco wanunue umeme watuwekee kwenye gridi ili kupunguza huu mgao ambao kwa sasa hautangazwi lakini upo kwa sana. Kwa wanaoishi Kinondoni, M/Nyamala, K/Nyama na hata Sinza ni mashahidi kuwa mgao unaendelea kinyemela bila kutangazwa.
CCM na mipasuko ya viongozi wako wa roho wa madaraka ndiyo iliyotufikisha hapo. Hamuwezi kuwa wote mawaziri wakuu kwa wakati mmoja wala huwezi kuwa spika na waziri mkuu hapo hapo haiwezekani. Haiwezekani wote mkawa "mediocres" katika performance lazima kuna wanaofanya kazi zaidi na kama Mwenyekiti hataki kufanya kazi anaogopa sana mdogo wake anayefanya kazi kwa speed.
Haiwezekani ukapendwa na kila mtu kama unafanya kazi....ukiona unapendwa na kila mfanyakazi wakati wote (all the time) ukiwa bossi basi ujue kuwa hufanyi kazi bali umewaachia wafanyakazi wako mwanya wa kuiba, kutega na kueneza umbea katika organisation.
Tunahitaji tusimamie maamuzi yetu hata kama tulikosea sehemu fulani tunajifunza na kwenda mbele. "practice makes you perfect".
I love Tanzania, Mungu utusaidie Watanzania tufungue macho na tujue tuchohitaji. Hatuhitaji watawala bora au watakatifu...tunahitaji viongozi wenye thubutu ya kusukuma gurudumu letu mbele hata kama mbele bila kujali kuna mlima kiasi gani mbele au kuna urefu gani. Hata maili elfu zilianza na hatua moja.....