Symbion Power acquires DOWANS Power plant

Symbion Power acquires DOWANS Power plant

Hakika kama umefuatilia series ya richmond ni kituko,richmond kampuni tata ambayo iliingia mkatababa wa kufua umeme kimadili,kila muda ulivyokua ukienda inakuwa na jina linabadilka mzunguko uko kama ifuatavyo richmond akazazaliwa tanzania,akakua akaitwa dowans na sasa amebalehe anaitwa symbion. Jamani jamani tumewakosea nini ninyi watu,miezi mitatu iliyopita kulikuwa kuna mjadala mkali juu ya malipo ya dowans,leo imebadilishwa jina clinton kaja,ngereja naye yumo,raisi naye anatoa pongezi kwa symbion,sasa mnataka kumvua gamba lowasa na rostam kwa kitu gani?kama kampuni waliyoileta ndio inazalisha umeme?nyie semeni mmedhulumiana kwenye mgawo,jamani jamani mpaka lini nchi hii mtaifanya kuwa shamba la bibi kila anayetaka kuchimba muhogo anachimba,hii ni ndani ya miaka 6 yote haya yanatokea na ndio kwanza series imeingia kwenye episode ya sita itakapofika episode ya 24 itakuwaje?
 
Hivi, hivi.... mdogo mdogo..... hadi waTZ msahau Ujamaa na mwelewe maana halisi ya Capitalism. Somebody's gotta b on Top......
 
wasi wasi wangu ni kama kila mmoja analalamika tu humu ndani tuamue tufanye nini? maana kwa kweli tumeshachoshwa na hizi siasa za majitaka. lets wake up and do something.

Mikakati yoyote huanzia hapa kwenye kulalamika, ambapo watu huamua kukaa chini na kupanga cha
kufanya. Haya leta plan, ungependa tufanye nini?
 
ka,Unaweza Ukakuta, Wamarekani walimuomba Mkulu awaachie Uranium waicontrol wao in exchange ya Kuipatia Tanzania vitu kama vile umeme. wakati kumbe thamani ya uraniuma yetu ni kubwa, na kama tuna deal na nchi zenye kuihitaji kwa udi na uvumba kama vile Iran, tungeweza kupata pesa nyingi za kujijengea vituo vya kuzalisha umeme sisi wenyewe, na pia wa Irani wako tayari kuuza technolojia ya kueinrich uranium ama kushirikiana na nchi mbali mbali katika katika sekta hiyo, kumbe basi tungeweza kujirahisishia route yetu ya kuwa na umeme wa Nyuklia kwa kudeal na nchi ambazo ziko tayari kushare technolojia hiyo, lakini maamuzi magumu yangetakiwa kufanywa maana mataifa makubwa wanaitolea macho Irani si kikawaida
 
Hapa Tanzania watu mbalimbali wamejitokeza kutengeneza sinema nyingi lakini kuna hii iliyoanzia kwenye igizo dogo tu lenye maudhui ya vita dhidi ya rushwa na ufisadi la Richmond, linaloonesha jinsi watawala walivyo tayari kuumiza wananchi wao ili kutibu majeraha yao wenyewe au rafiki zao ni sinema tamu sana. Sinema hii ndefu ilianza kama mzaha vile: wahusika wakuu wakiwa ni wale wanaojua kufisadi Taifa hili. Jinsi sinema ilivyoanza wengi tulidhani itaishia sehemu moja tu ya Richmond, kumbe jamaa ni wajanja sana kwani walipoona kuwa Watanzania tumepiga kelele nyingi kuhusu Richmond, wakatubadilishia 'Angle' na kutuwekea sehemu ya pili ya filamu; Dowans.Mwandishi wa kisa hiki: Richmond/Dowans, ni mwandishi mahiri sana mwenye kuijua vyema kazi yake. Hubadilisha msuko wa hadithi (plot) kila anapoona ipo haja ya kufanya hivyo bila kuharibu maudhui yake, mwanzoni tulipohoji tuliambiwa kuwa mmiliki wa Dowans hajulikani! Wakati huohuo Waziri wa Nishati na Madini akikomalia kuilipa Dowans! Upepo ulipobadilika ghafla baada ya kelele nyingi zilizopigwa na wananchi, mmiliki wa Dowans akajitokeza na kukataa kupigwa Picha. Ila alitaja kuwa alitoa mamlaka kwa Mbunge Rostam Aziz (ingawa Rostam aliwahi kuikana) kuisimamia Kampuni ya Dowans hapa Tanzania!Watazamaji wa sinema wakaishtukia, mwandishi akabadilisha 'angle' na kutangaza kuwa serikali ikinunua mitambo ya Dowans watafuta kesi. Watanzania wakagoma tena safari hii kwa kelele kubwa sana. Sasa ameleta kitu kipya zaidi kinachoitwa Symbion Power!Hapa ndipo sinema hii inaponoga zaidi, kwani alichokifanya mwandishi wa kisa hiki ni kuuhadaaumma wa Watanzania na mgawo wa umeme ili tuingie mkenge wa nguvu, na tuikukubali Symbion Power ambayo ni Mrithi wa Dowans.Hii yote ni kuwafanya Watanzania majuha wasiojua kitu au kusoma alama za nyakati. Hainiingii akilini kuwa Symbion Power na watuhumiwa wa Richmond/Dowans ni vitu viwili tofauti, watakuwa wamebuni mkakati huu wa kuibua kampuni hii ili kufuta madoa ya Richmond/Dowans usoni kwao. Na sasaTanesco inaingia mkataba na kampuni hiyo ili ituuzie umeme.'Angle' ya mwandishi katika kisa hiki imebadilika sana baada ya kuona kwamba jina la Dowans halitakiwi kabisa na Watanzania ametuletea jina jipya, na kama tuliukataa umeme wa Dowans basi tutasahau itakapoanza Symbion Power. Na wote tutapongeza maana tutaiona kama mkombozi kwa kuwa tayari tumeghiribiwa kwanza kwa kuletewa mgawo wa umeme mkali ili ionekane kuna shida. Sinema hii ndefu ya Richmond/Dowans, na sasa Symbion ina mafundisho mazuri sana kwa jamii: mojawapo ni kuwa nchi yetu haipaswi kabisa kuwa na umeme ulio imara kwa kuwa watu watakosa ulaji. Mgawo wa umeme ni lazima uwepo hata kama tulikwishaambiwa kuwa utabaki kuwa historia. Bila mgawo wa umeme zile kampuni zao za kuuza majenereta zitakufa. Hivyo kwao mgao wa umeme ni dili zuri, zuri mno. Dili litakalowahakikishia ulaji milele na kuendelea kujenga heshima ya kuwa na vitambi vya kuvimbiwa ufisadi.Wasiwasi wangu tu ni kuhusu mwisho wa sinema hii ndefu isiyochosha, kwani watawala wakizidisha ulafi, wa kunywa mchuzi wote, wananchi wanaweza kuingilia kati na kuamua kumwaga ugali, kama watawala wakimwaga mboga. Yatakayotokea baada ya hapo ni dhambi kuyaeleza.
Wahenga walisema bora ukose mali kuliko akili,wako sawa kabisa kwani umasikini wa watanzania si kwa sababu hatuna mali bali hatuna akili hapa namaanisha watanzania wote toka maprof mpaka wahitimu wa chekechea tuna matatizo ya akili.Anayebisha aseme,kwani haingii akilini kama mtu anakuibia zaidi ya mara moja (richmond,dowans-symbion) bado tunawachea tu.Tunafanya makosa makubwa sana na tutahukumiwa kwa dhambi hii tunayoifanya.Mungu hawezi kutuhurumia kwa dhambi hii ya makusudi tunayoifanya.WAKO WAPI WAKOMBOZI WA NG'AMBO cdm walifanikiwa kuzuia malipo ya dowans sasa wako kimya,CDM iko wapi nguvu ya uma?.NASIKITIKA KUHITIMISHA KWA KUSEMA KWAMBA-Kwa hili la simbioni cdm wako upande wa mafisadi,vinginevyo watuambie wanaionaje hii filam mpya!
 
Uporoto01,

kwa taarifa yako kule Mtwara kuna mafuta ambayo ayajaanza kuchimbwa. Namtumbo-Songea pamoja na Bahi-Dodoma kuna Uranium. Hivi vyote ni vyanzo vya nishati ambayo Marekani inahitaji. Pili China inainfluence kubwa Tanzania kwa hiyo njia ya kuakikisha malighafii hii haiangukii mikononi mwa China basi Marekani wataleta makampuni yao uwekeza kutumia fedha za MCC.
 
Hoja yangu ni kuwa kwa nini mitambo ya Tanesco ambayo haihitaji capacity charge wala gharama ya kununua umeme inazimwa ili kuipisha Symbion wakati tutahitaji kulipia umeme utakaozalishwa na kampuni hiyo?

Mitambo ya Songas sio ya Tanesco.
Tanesco hatosherezi matumizi ya sasa.
Mtumiaji umeme anachotaka ni umeme wa uhakika ,salama,na nafuu.Hatujali mtoa huduma ni Shetani au ni Malaika
Tusitafute umaarufu bila kuwa na jibu la matatizo.
 
Mitambo ya Songas sio ya Tanesco.
Tanesco hatosherezi matumizi ya sasa.
Mtumiaji umeme anachotaka ni umeme wa uhakika ,salama,na nafuu.Hatujali mtoa huduma ni Shetani au ni Malaika
Tusitafute umaarufu bila kuwa na jibu la matatizo.

Mkuu Ubungo Gas Plant sio Songas. Huu ni mtambo unaomilikiwa na Tanesco na kuendeshwa na Wartsilla ya Finland ambao ndio watengenezaji wa mtambo huo.
Kwa kukufahamisha tu Songas ipo pembezoni mwa barabara ya Mandela upande wa kushoto karibu kabisa na mataa ya Ubungo kama ukitokea Ubungo kuelekea Buguruni wakati hiyo Ubungo Gas Plant ipo barabara ya Morogoro upande wa kushoto pembezoni mwa ghorofa la Tanesco ukitokea Ubungo kuelekea Morogoro.

Sijasema Tanesco inatosheleza mahitaji. Hoja yangu ni kuwa utaratibu ufuatwe ili Taifa lisije likaingia kwenye matatizo ambayo yanaweza kuepukika na si kukurupuka kama utakavyo wewe.
Sijatafuta umaarufu. Nikuthibitishie tu kuwa jibu la matatizo ninalo: uwezo wa hiyo Ubungo Gas Plant 110MW ni sawa na ule wa Symbion 110MW. Nilichosema ni kuwa kwa nini tunazima Ubungo Gas Plant na badala yake tunawasha Symbion wakati Ubungo Gas Plant ni mali ya Tanesco? Tujadili hapo.
 
Mkuu Ubungo Gas Plant sio Songas. Huu ni mtambo unaomilikiwa na Tanesco na kuendeshwa na Wartsilla ya Finland ambao ndio watengenezaji wa mtambo huo.
Kwa kukufahamisha tu Songas ipo pembezoni mwa barabara ya Mandela upande wa kushoto karibu kabisa na mataa ya Ubungo kama ukitokea Ubungo kuelekea Buguruni wakati hiyo Ubungo Gas Plant ipo barabara ya Morogoro upande wa kushoto pembezoni mwa ghorofa la Tanesco ukitokea Ubungo kuelekea Morogoro.

Sijasema Tanesco inatosheleza mahitaji. Hoja yangu ni kuwa utaratibu ufuatwe ili Taifa lisije likaingia kwenye matatizo ambayo yanaweza kuepukika na si kukurupuka kama utakavyo wewe.
Sijatafuta umaarufu. Nikuthibitishie tu kuwa jibu la matatizo ninalo: uwezo wa hiyo Ubungo Gas Plant 110MW ni sawa na ule wa Symbion 110MW. Nilichosema ni kuwa kwa nini tunazima Ubungo Gas Plant na badala yake tunawasha Symbion wakati Ubungo Gas Plant ni mali ya Tanesco? Tujadili hapo.

Mkeshaji hapa kinachosumbua ni 10% ya capacity charge hakuna jingine.
 
Mkeshaji hapa kinachosumbua ni 10% ya capacity charge hakuna jingine.

Ni kweli kabisa mkuu. Itawezekanaje uache kutumia gari lako halafu uende kukodi la mwenzio na yote yana sifa sawa?
 
symbion imeongeza mgawo wa umeme..arusha ilikuwa masaa 7 hadi 8 ya kukatika kwa umeme sasa hivi hadi masaa 12.sawa tu Mungu yupo nyie magamba
 
Duh
hilisi mchezo nahisi kuona misukule ya gwajima ikizunguka zungka na kutafuta pa kutokea na kuishia kujikuta iko
viwanja vya kawe kwenye moto usiozimika


wapi ulipo sendeka
wapi ulipo xspika sita
wapi ulipo mwakyembe

wapi wale watanzania tuliokuwa tukipiga kelele ya dowans atuitaki sasa tumebadilishiwa jina na kuitwa symbiona tumekaa kimya

raha ya milele umpe ee richmond na mwanga wa amani
apumzike kwa dowans

amin
 
Duh apo umenimaliza kabisaaaaaaaaaaaa natafuta visa ya afghanistan msaada jamani....umesahau wapi nyepesi mana sio z....
 
Watu hawakurupuki kihivyo.......data zintafutwa na kukusanywa........soon SYMBION nayo itaning'inia tu
 
Naimagine siku ya mwisho parapanda itakapopigwa hawa watu waserikalini wish wangekuwa hai....jamani
 
watu hawakurupuki kihivyo.......data zintafutwa na kukusanywa........soon symbion nayo itaning'inia tu
mkuu
mmhh mbona dowans iliwashwa kwa nguvu na fasta wakairukia huyu symbiona ana nini ama ni sababu mmarekani??
 
wote wale wale ila ninamkubal sana zitto mana ndo kimbilio letu hv sasa
 
symbion imeongeza mgawo wa umeme..arusha ilikuwa masaa 7 hadi 8 ya kukatika kwa umeme sasa hivi hadi masaa 12.sawa tu Mungu yupo nyie magamba

Mgawo tena...? Si walisema umeisha, tena utakuwa ni historia.
Ndo maana nasema inabidi hawa Symbion pia waangaliwe.
 
Kwa sababu ya Wamarekani, lakini soon tutajua kama nayo ni Dowans nyingine..
 
Back
Top Bottom