.Chunguza vizuri hicho kitu kisije kikawa ni pepo mchafu..
watashindana naye.... lakini watashindwa🙂
.Chunguza vizuri hicho kitu kisije kikawa ni pepo mchafu..
wakuu naomba kuuliza swali hapa,pamoja ni hio Symbion kununua mitambo ya Dowans,bado ile kesi yao wanayodai serikali yetu inaendelea!!!!!!
wakuu naomba kuuliza swali hapa,pamoja ni hio Symbion kununua mitambo ya Dowans,bado ile kesi yao wanayodai serikali yetu inaendelea!!!!!!
yaani kwa taarifa rasmi,
mama alivyokuja wazungu walibadilisha mawazo,nafikiri kuna kitu hata sisi tumetolea macho hapo
Symbion imekuja kufanya biashara(kuvuna shamba la bibi) au kusaidia?kuna taarifa zilizopatika kutoka symbion power..taarifa zaidi zinasema symion imekuja kwa msaada mkubwa wa serikali ya marekani kuisaidia tanzania.
WAZIRI wa Mambo ya Nje wa Marekani, Hillary Clinton jana alitembelea mitambo ya kuzalisha umeme ya Kampuni ya Symbion iliyopo Ubungo jijini Dar es Salaam na kuipongeza kwa kuwekeza Tanzania.Clinton alisema ana imani kampuni hiyo inatekeleza majukumu yake vizuri ili kupunguza tatizo la nishati hiyo hapa nchini.
Alisema hayo mara baada ya kutembelea mitambo hiyo na kupokelewa na Ofisa Mtendaji wa Kampuni hiyo, Paul Hinks. "Kutokana na tatizo la umeme linalowakabili Wananchi wa Tanzania, juhudi zaidi za ushirikiano zinahitajika ili kuwekeza zaidi kwenye sekta hiyo, nawapongeza Symbion kwa kuchagua kuwekeza Tanzania," alisema Clinton.
Alisema hakuna maendeleo bila kuwa na umeme kwani viwanda vinavyozalisha bidhaa havitafanya kazi na hivyo nchi kukosa maendeleo.
Alisema Marekani itaendelea kuisaidia Tanzania katika masuala ya umeme ili iweze kufikia upatikanaji wa megawati 3,000 ifikapo mwaka 2015.
" Umeme ni muhimu katika upatikanaji wa huduma za kijamii kama vile hospitali, usipokuwepo huduma hizi na zinakuwa tabu kuzipata, serikali iendelee kuwekeza kwenye sekta ya umeme,"alisema Clinton.
Naye Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja alisema imekuwa ikifanya juhudi mbalimbali ili kukabiliana na tatizo la umeme.
Alisema juhudi hizo ni pamoja Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) kuagiza mitambo ya ufuaji umeme ya dharura.
Ofisa Mtendaji wa Symbion, Hinks alisema mtambo huo una uwezo wa kuzalisha megawati 120 na kuiuzia Tanesco.
Waziri Clinton leo anatarajia kukutana na Rais Jakaya Kikwete Ikulu na kufanya naye mazungumzo kabla hajaondoka nchini.
Marekani yasaidia Tanzania Sh 12 bilioni
Serikali ya Marekani na Ireland zitaipatia Tanzania msaada wa dola 8.7 milioni za Marekani sawa na Sh12.8 bilioni ili kusaidia mpango wa kuboresha lishe kwa watoto.Kati ya fedha hizo, Marekani itatoa dola 6.7 milioni sawa na Sh9.3 bilioni katika mwaka wa fedha 2012/13 wakati Ireland itatoa mwaka huu dola2 milioni za Marekani sawa na Sh2.8 bilioni.
Kiasi hicho cha fedha kilitangazwa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Hillary Clinton na Naibu Waziri Mkuu wa Ireland, Eamon Gilmore.Walitangaza hayo kwenye mkutano wa majadiliano ya namna ya kuboresha lishe uliokuwa chini ya Uenyekiti wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Akizungumza, Waziri Clinton ambaye yuko nchini kwa ziara ya siku tatu, alisema serikali ya Marekani imeamua kutoa fedha hizo ili kusaidia juhudi zinazofanywa na Tanzania katika sekta ya afya." Tumefurahishwa na hatua zinazochukuliwa na Tanzania katika suala la lishe kwa watoto, ndiyo maana tumeamua katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha, tutatoa zaidi ya mara nne ya kiasi ambacho tumekuwa tukichangia katika lishe,"alisema Clinton.
Alisema fedha hizo zitasaidia kujenga uelewa miongoni mwa jamii kuhusu umuhimu wa lishe katika mpango maalumu wa siku 1,000 za kupunguza vifo vinavyotokana na ukosefu wa lishe.Clinton ambaye ni Mke wa Rais Mstaafu wa Marekani, Bill Clinton, alisema watoto wanaokosa lishe bora hupata magonjwa ambayo yatasababisha madhara maishani mwao.
" Kama watoto hawapati lishe bora, hawataweza kupata elimu bora, hivyo taifa litakuwa na watu goigoi ambao watakuwa maskini,"alisema Clinton.Waziri Mkuu, Pinda alisema kwa kuthamini umuhimu wa lishe kwa wanawake na watoto, Serikali kuanzia 2012/13 itakuwa ikitenga fedha kwa ajili kuimarisha lishe.
Aidha, Pinda alisema Serikali itaunda mpango wa kitaifa kuhusu lishe pamoja na kuunda kamati ya utendaji itakayosimamia." Pia tunataka kuandaa utaratibu wa kuweka virutubisho kwenye vyakula ili viweze kusaidia kutoa lishe bora kwa watoto na wanawake,"alisema Pinda.
Kwa upande wake, Naibu Waziri Mkuu wa Ireland, Gilmore alisema serikali yake itaendelea kushirikiana na Marekani katika kuisadia Tanzania ili iweze kufikia malengo yake ya kupambana na magonjwa yatokanayo na lishe duni.Alisema ili kupata lishe bora, serikali haina budi kuwekeza zaidi katika kilimo na hivyo kuwa na chakula cha kutosha.
source -Gazeti mwananchi
wale wengine walikuwa waislamu na symbion ya wakristo.
hutawasikia akina mwanakijiji wakiandika barua ndefu ndefu kupinga bungeni na seneti usa maana wanaweza kutupwa nje ya mipaka yao.
kwa symbion tutapiga makofi kumi. hata kesi mahakamani tuifunge tu.
nini tofauti kati ya dowans na symbion mimi siioni. wote wezi wale wale ila ngozi tofauti.
amri ya mahakama iko wapi. mwanahalisi wako wapi. daktari wa wakatoliki yuko wapi.
.Chunguza vizuri hicho kitu kisije kikawa ni pepo mchafu..