Wana-JF,
Wakati suala la posho ya wabunge linaendelea kushika na kutengeneza vichwa vya habari, binafsi naanza kupata wasiwasi wa masuala mengine ya msingi kuwekwa kapuni (kama hili la DOWANS na SYMBION). Ni kweli suala la posho kubwa kwa wabunge wetu ni la mates makubwa kwetu na lina umuhimu wake, pamoja na hilo, suala la ujio wa SYMBION na ununuzi wake wa DOWANS naona lina umuhimu sana kwa taifa letu na wananchi wangependa kujua wawakilishi wetu (CHADEMA) wana msimamo gani katika hili. Kimya cha wanasiasa wetu na woga wa ghafla wa kushindwa hata kuizungumzia SYMBION unanitia mashaka, kimya chao kinanitia wasiwasi kwa sababu kama suala hili likiachiwa basi natumaini mafisadi watakuwa wametufunga bao la kisigino, na binafsi nisingependa hilo litokee katika kipindi hiki tunachoelekea kusherehekea miaka 50 ya Uhuru katika nchi ambayo haiwezi kuwachukulia hatua wezi na wabadhifu wa mali ya umma.
Katika hali kama hii, kama CHADEMA na vyama vingine mtaamua kukaa kimya, basi hatutakumbuka kelele za CCM lakini tutakumbuka daima kimya cha CHADEMA na vyama vingine vinavyotaka tuvione kuwa ni mbadala wa CCM.