Sio laana Mzee!.Ni khali ngumu ya maisha sio wanapenda ila wanashindwa wafanyeje.!.ila ushauri wangu shughuli zipo nyingi za kufanya.Natoa mfano kuna rafiki angu ila siwezi kumtaja humu ni askari huyu jamaa huwezi kudhania kuwa ni askari ni fundi huyu jamaa alikuja nyumbani kwangu kunifungia dishi nilipewa namba tu kweli alifanya kazi fresh na akaondoka alitaka 30000 nikalia kama kawaida yetu wa bongo akapunguza hadi 25.akaenda zake siku nimepoteza reseni yangu nimekwenda pale kituoni kwa ajili ya loss report nikamkuta yule jamaa nikahisi labda nimefananisha kwa kuwa alikuwa ndani ya gwanda.nikatoa simu yangu wakati ye hanioni nikabip kucheki hivi kiwiziwizi nikaona anaingiza mkono mfukoni anatoa simu nikakata.Kweli nikaamini ni yeye nikamfuata nikamsalimia kweli alinikumbuka tena akanisaidia nikafanyiwa faster sikupanga foleni nilipotoka kiaibu aibu nikampa buku tano alikataa kabisa ile pesa nilishangaa sana.kama kawaida mi nimfuatiliaji sana nikapata undani wa yule Polisi kumbe ni Fundi mzuri sana na anajina kubwa sana hapa Mjini.nilichojifunza Polisi kuwa omba omba ni hulka yao na uvivu wa kufikiri!.