Swali la ugomvi: Mnataka vipi mabadiliko wakati tayari mmebadilika?

ndio wasomi wetu hawa ...waoga kweli! wamekumbatia matheory tuu.....na mbaya zaidi ni theory za copy and paste sio uhalisia wa hali halisi ya kitanzania.
 
Please pitia tena rasmu ya pili ya katiba mpya utajua watz tunataka nn? Hii uliopost si ya level yako Mkuu.

Sorry
Mzee Mwanakijiji kama hajakuelewa mkuu basi amegoma kuelewa. Sio wote tunaunga mkono mabadiliko ni vigeugeu. Actually tumesimamia kwenye hoja ya msingi ambayo ni katiba yetu wananchi kama inavyosomeka katika rasmu ya pili. Tunauhakika zaidi ya 10000000000000% kuwa CCM hawataki hilo. Na tunauhakika 100% kuwa kwenye ukawa hilo ndiyo jambo lao na letu la msingi.
Ukawa watatuongoza kupata hiyo katiba ambayo wakifanya ujinga itaanza kuwatia adabu wao wenyewe. Sisi tumesimamia hoja, Mwanakijiji na wenzako mmesimamia mtu (Personality) nani anatakiwa kubadilika?
Halafu jenga hoja usiweke chumvi. Embu niambie ni kikao gani cha chadema, kilifanyika lini na wapi ambacho kilimpitisha mtu mwingine zaidi ya Lowassa kuwa mgombea urais?
Hoja na shida yetu ni katiba iliyo kwenye rasmi na sio hii iliyopo wala katiba LAZIMISHWA AKA PENDEKEZWA.
 
Tanzania kamwe haiwezi kutawaliwa na chama kingine zaidi ya CCM.

CCM itatawala milele.

Anayebisha na alinakili hili bandiko langu kama rejea ya baadaye.

Narudia tena, CCM itatawala milele.

Nimeamini maneno ya Generali Ulimwengu kuwa wakati wa uchaguzi watu huweka akili zao sehemu fulani na kuzifuata baada ya uchaguzi kuisha. Nyani Ngabo amefikia mahali anajifanya hata maana ya neno milele hajui. Duh hii ni hatari sana. Nasubiria hoja zako baada ya uchaguzi
 
ondoa CCM basi. hayo mengine yatakuja kwa ziada. Kwa sasa hatujali aisee.
 
Dah. Kumbe Hata Nyani Naye Ameacha Kurukia Miti. Naekaja Kuisaidia Ccm? Teh. Teh. Teh.

Mimi wala si CCM.

Lakini nikiangalia Watanzania walio wengi, nikiangalia mambo mengine kama tume ya uchaguzi ya CCM (NEC), nikiangalia jinsi ambavyo watu uliodhani ni wataka mabadiliko ya kweli ila hivi sasa hata hawaeleweki ni watu wa aina gani, nakosa matumaini kabisa.

Hivyo narudia tena, CCM itatawala milele nchii hii. Kwa hiyo nawe lihifadhi tu hili bandiko langu kwa rejea ya baadaye.
 
Nimeamini maneno ya Generali Ulimwengu kuwa wakati wa uchaguzi watu huweka akili zao sehemu fulani na kuzifuata baada ya uchaguzi kuisha. Nyani Ngabo amefikia mahali anajifanya hata maana ya neno milele hajui. Duh hii ni hatari sana. Nasubiria hoja zako baada ya uchaguzi

Hoja yangu baada ya uchaguzi itakuwa 'see, I told you so'.
 
Kingunge-udhamini.jpg
51Z4cxF7CAL._SX450_.jpg
Na. M. M. MwanakijijiMojawapo ya vitu vinanishangaza sana wakati huu wa kampeni na hasa tangu Lowassa apewe kiti cha enzi CHADEMA ni kuwa watu waliompokea na wenye kumuuza mbele ya umma wanadai kuwa wamempokea ili aongoze harakati za mabadiliko. Utawasikia watu wanasema - bila kufikiria sana "tunataka mabadiliko" na kuwa CCM ikitoka tutapata mabadiliko. Wengi wanazungumzia "mabadiliko" kama tukio fulani ambalo litatokea baadaye. Cha kusikitisha ni kuwa wao wenyewe hawajui au hawataki kujua, hawaamini au hawataki kuamini kuwa tayari mabadiliko yameshatokea; mabadiliko ambayo yamewabadilisha wao. Kama watu wenye akili timamu walishapata mgombea wao wa Urais, wakampitisha na kumthibitisha halafu wiki chache baadaye wakaenda kumchukua mgombea toka CCM na hivyo wakamtupa mgombea wao wenyewe, tena si mtu baki tu Katibu wao Mkuu wa chama, watu hawa hawa wanaweza vipi kuja na kusema ati wanataka "mabadiliko"? Yaani, watu waliobadilika wanataka kubadilika tena? Waweje?Ukiangalia kwa jicho lililotulia utaona kuwa ni sisi ambao hatujabadilika au kubadilishwa na ujio wa Lowassa ndio hasa tunataka mabadiliko au tunahitaji mabadiliko. Ndio sisi ambao tunatakiwa kubadilika! Ndio maana watu wanatuona tumekuwa wagumu na hatuungi mkono harakati zao (hatujabadilika!). Kumbe kati yetu na wao ni sisi tunaweza kwa haki kabisa kuzungumzia mabadiliko kuliko wao. WAo hawana uhalali (legitimacy) wala hoja (reason) za kusema wanataka mabadiliko. Wanayataka mabadiliko yapi na ya nini? Ndio maana mwisho wa siku jibu lao ni "kuitoa tu CCM madarakani mengine baadaye". Kumbe wakati huo huo wamechukua CCM, mgombea wa CCM na wanachama wa CCM wenye kumuunga mkono mwana CCM mwenzao ambao waliapa kuwa "alipo" na wao "wapo"! Wenzetu mnaoimba na kushabikia "mabadiliko" yajayo, hivi hamjioni kuwa tayari mmebadilika? au mtabadilika tena ikitokea mshinde au mkishindwa tena mtabakia hivyo hivyo - naamini wengi watabadilika baada ya kushindwa na kujaribu kurudi mlikokuwa - mkitaka mabadiliko tena! Isije kuwa wenzetu ni watu wa kubadilika badilika tu na ujio wa upepo wa mabadiliko! Si kiongozi mwenyewe wa mabadiliko tayari ameshabadilika? na akija kubadilika tena sijui tutawaitaje. Vinyonga wa kisiasa? Fikiria.MMM
hapo kwenye red=ni Mabadiliko mbele kwa mbele!
 
Waandishi wa RaiaMwema this is too much! Tumewasikia, tumewasoma lakini tumekataa kupanda gari lenu. Mbona kuna mengi ya kuandika kama kuchambua sera za vyama na ahadi zao, lakini wewe na Mbwambo mmekomalia Lowassa tu. Ni chadema tu! Kama mnapenda 'upinzani' ambao ni cream, nendeni kwa Zitto na ACT yake. Mpeni coverage ya kutosha maana yeye mgombea wake hana 'doa'. Kwa nguvu kubwa mnayoitumia kuibomoa chadema/ukawa/Lowassa, wengine sasa tunaona huu ni zaidi ya uchambuzi-ni personal. Sasa kama mliibiana mabibi huko mtaani msitulazimishe na sisi tuwapiganie vita yenu. Shame on you!
 
Mimi wala si CCM.

Lakini nikiangalia Watanzania walio wengi, nikiangalia mambo mengine kama tume ya uchaguzi ya CCM (NEC), nikiangalia jinsi ambavyo watu uliodhani ni wataka mabadiliko ya kweli ila hivi sasa hata hawaeleweki ni watu wa aina gani, nakosa matumaini kabisa.

Hivyo narudia tena, CCM itatawala milele nchii hii. Kwa hiyo nawe lihifadhi tu hili bandiko langu kwa rejea ya baadaye.
Naona enyi 'waMarekani' mmeamua kutukatisha tamaa na kutuchagulia Magufuli. Ingependeza mngekuja kujiandikisha na kupiga kura, ndipo tungejua kama maneno yenu yanatoka kwenye keyboard au moyoni.
 
Naona enyi 'waMarekani' mmeamua kutukatisha tamaa na kutuchagulia Magufuli. Ingependeza mngekuja kujiandikisha na kupiga kura, ndipo tungejua kama maneno yenu yanatoka kwenye keyboard au moyoni.

Hivi kweli unadhani CCM wako tayari kuachia madaraka ya nchi hii?

CCM itaitawala hii nchi milele.

Hifadhi hili bandiko kwa ajili ya rejea ya baadaye.
 
Mwanakijiji wewe unasema hujabadilika wenzio wanakuona umebadilika. Siyo yule kamanda waliyekuwa naye wakati huo.

Tatizo ni nini? Tatizo kubwa kwangu mimi ni mtazamo wa mabadiliko. Wakati wewe muda wote uliangalia watu wenzio walingalia mfumo. Kwa mfano wewe unaona Lowassa ambaye alikuwa kiongozi CCM na kwa hiyo na yeye amechangia kutufikisha hapa, hawezi kuleta mabadiliko. Wenzio wanaona CCM kama mfumo ambaye imetufikisha hapa haiwezi kuleta mabadiliko. Hivyo wakati wewe unakataa mtu wa CCM asichukuliwe wenzio wanaamini yeyote atakayesaidia kubomoa mfumo CCM anafaa.

Nachoshangaa mimi ni wewe kuwaona wenzio kama hawafikirii vizuri
Nilitaka niandike kitu lakini nafikiri hapa umemaliza, ila uchaguzi huu umenifanya nione kwa nini tanzania kama taifa tumezorota
1.ni kuwa na kizazi cha wazee kama akina mwanakijiji ambao wengi wao
-waoga
-wanafki
-maslahi mbele na kujidai wanapenda taifa
Lakini wakazalisha kizazi cha watu waoga, cowards- watu waliokosa uthubutu kwenye kila nyanja. Unafikiri watoto wa mwanakijiji watakuwa watu wa aina gani..?
 
Heshima kuheshimika,
sikinai kuhekimika,
usafihi kujivika,
mbumbumbu kuwa ni sifa, upumbao ndio taji.

Ndarahima apewapo,
sipo hupasema ndipo,
panzi huwaita popo,
ndivyo zake humtuma, akidhani na wenziwe.

Ukosapo utimamu,
tuliza zako hatamu,
usije pata magumu,
yale usiyozoea, ikikuvuka chutama.

Mwanakijiji tulia,
mengi wajiharibia,
wanakujua tabia,
hata wasio kujua, nyamaa sidhalilike.

Nyamaa sizalilike,
ya mihogo yakufike,
hata tama ulishike,
ukizitafuta mbio, uziage zako nyonga.
 
Poor analysis. Kwani huyu Katibu mkuu alitoka wapi? Sio CCM? Sasa ana tofauti gani na hawa watanzania wengine waliojiunga na CHADEMA sasa? Lowasa kwa sasa ni mwanachama wa CHADEMA na kadi alipewa mbele ya macho ya watu wote. Ana haki ya kugombea urais kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA na ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mabadiliko yanatakiwa ni kuitoa CCM na mfumo wake madarakani. Kama hujakubali hulazimishwi, wengine wamestaafu siasa. Hii ni demokrasia.
This is indeed a poor thinking!Lowasa anakashfa za wizi wa mali ya umma, Slaa hana!Lowasa hajashiriki kuijenga chadema, Slaa ameshiriki mpaka kapata ulemavu wa mkono, Slaa alihamia chadema kwa kuombwa na wana karatu -Lowasa alikuja chadema kwa matakwa yake ya kutaka Urais, Chadema haikuwahi kumtuhumu Slaa kwa kashfa yoyote kabla hajajiunga nayo-Chadema ilimwita Lowasa fisadi na kutoa orodha ya mafisadi "List of shame" na kumtaja Lowasa na mengineyo. Kweli hujui utofauti wa Slaa kuja chadema na kuja kwa Lowasa huuoni wala huujui????!
 
Nilitaka niandike kitu lakini nafikiri hapa umemaliza, ila uchaguzi huu umenifanya nione kwa nini tanzania kama taifa tumezorota
1.ni kuwa na kizazi cha wazee kama akina mwanakijiji ambao wengi wao
-waoga
-wanafki
-maslahi mbele na kujidai wanapenda taifa
Lakini wakazalisha kizazi cha watu waoga, cowards- watu waliokosa uthubutu kwenye kila nyanja. Unafikiri watoto wa mwanakijiji watakuwa watu wa aina gani..?
Mkuu ukiona mtu ameanza lugha za picha jua hoja andishi zimefika kikomo, kufika mwisho wa ukomo wa kuandika humaanisha mwisho wa ukomo wa kufikiri, huleta dhana ya kukata tamaa!! hapo ndipo alipofikia mzee mwenzangu Mwanakijiji. Msameheni bure si wazee wote wasiojitambua nchi hii ni baadhi tu kama yeye. yeye ni miongoni mwa watazamao maslahi yao zaidi kuliko taifa ndio maana watu wa aina yake huabudu na kutumai katika watu.
naomba niishie hapo kwa leo. mpeni salaam zangu.
 
Kingunge-udhamini.jpg


51Z4cxF7CAL._SX450_.jpg

Na. M. M. Mwanakijiji

Mojawapo ya vitu vinanishangaza sana wakati huu wa kampeni na hasa tangu Lowassa apewe kiti cha enzi CHADEMA ni kuwa watu waliompokea na wenye kumuuza mbele ya umma wanadai kuwa wamempokea ili aongoze harakati za mabadiliko. Utawasikia watu wanasema - bila kufikiria sana "tunataka mabadiliko" na kuwa CCM ikitoka tutapata mabadiliko. Wengi wanazungumzia "mabadiliko" kama tukio fulani ambalo litatokea baadaye.

Cha kusikitisha ni kuwa wao wenyewe hawajui au hawataki kujua, hawaamini au hawataki kuamini kuwa tayari mabadiliko yameshatokea; mabadiliko ambayo yamewabadilisha wao. Kama watu wenye akili timamu walishapata mgombea wao wa Urais, wakampitisha na kumthibitisha halafu wiki chache baadaye wakaenda kumchukua mgombea toka CCM na hivyo wakamtupa mgombea wao wenyewe, tena si mtu baki tu Katibu wao Mkuu wa chama, watu hawa hawa wanaweza vipi kuja na kusema ati wanataka "mabadiliko"? Yaani, watu waliobadilika wanataka kubadilika tena? Waweje?

Ukiangalia kwa jicho lililotulia utaona kuwa ni sisi ambao hatujabadilika au kubadilishwa na ujio wa Lowassa ndio hasa tunataka mabadiliko au tunahitaji mabadiliko. Ndio sisi ambao tunatakiwa kubadilika! Ndio maana watu wanatuona tumekuwa wagumu na hatuungi mkono harakati zao (hatujabadilika!). Kumbe kati yetu na wao ni sisi tunaweza kwa haki kabisa kuzungumzia mabadiliko kuliko wao. WAo hawana uhalali (legitimacy) wala hoja (reason) za kusema wanataka mabadiliko. Wanayataka mabadiliko yapi na ya nini?

Ndio maana mwisho wa siku jibu lao ni "kuitoa tu CCM madarakani mengine baadaye". Kumbe wakati huo huo wamechukua CCM, mgombea wa CCM na wanachama wa CCM wenye kumuunga mkono mwana CCM mwenzao ambao waliapa kuwa "alipo" na wao "wapo"!

Wenzetu mnaoimba na kushabikia "mabadiliko" yajayo, hivi hamjioni kuwa tayari mmebadilika? au mtabadilika tena ikitokea mshinde au mkishindwa tena mtabakia hivyo hivyo - naamini wengi watabadilika baada ya kushindwa na kujaribu kurudi mlikokuwa - mkitaka mabadiliko tena! Isije kuwa wenzetu ni watu wa kubadilika badilika tu na ujio wa upepo wa mabadiliko! Si kiongozi mwenyewe wa mabadiliko tayari ameshabadilika? na akija kubadilika tena sijui tutawaitaje.

Vinyonga wa kisiasa?

Fikiria.

MMM

Mzee Mwanakijiji
The only thing that will remain constant hapa duniani ni change ... And there is no single step of change ambayo ndo utakuwa umeshafika mwisho wa changes... na steji ya mwisho ni kubadilika kutoka kwenye uzima na kuingia kwenye kifo.. Na kidini bado hiyo si step ya mwisho, kuna changes za maisha mengine as per imani za dini na madhehebu mbalimbali

''Life is a series of natural and spontaneous changes. Don't resist them - that only creates sorrow. Let reality be reality. Let things flow naturally forward in whatever way they like''.
By Lao Tzu






 
Mwanakijiji unachoshindwa kuelewa ni kuwa wananchi wamechoshwa na utawala wa ccm na njia pekee ya kuuondoa ni kumtumia KADA aliyetoka ccm maana hata Mwl Nyerere alisema mpinzani wa kweli wa ccm atatoka ndani ya ccm. EL ameonesha kuwa na nguvu ndani ya ccm na hata nje ya ccm huyo Dr Slaa unayemlilia ww alikuwa na nguvu kwa wanachama na wapenzi wa chadema lakini alikuwa hakubaliki nje ya chama na Prof Lipumba vile vile. Watu wanataka ushindani wa kweli siyo wa kusindikiza
 
Back
Top Bottom