Swali la kizalendo: Mabeberu ni kina nani?

MAKULUGA

JF-Expert Member
Jan 21, 2011
7,171
9,397
Dunia inaenda kwa kasi sana, ukizubaa unaachwa!

Wakati wa vita baridi neno Mabeberu lilitumika sana hapa Tanzania. Enzi zile beberu alikuwa ni mtu yoyote asiye mjamaa, mpinga mapinduzi, anayeamini katika soko huria na uliberali.

Polepole neno mabeberu lilianza kufifia baada ya kuanguka kwa ukuta wa Berlin, na nchi zetu zikaanza uchumi na siasa za kiliberali. Hata mabeberu makaburu tukawakaribisha na kuanza kuwaita wawekezaji!

Kimsingi neno beberu likafa.

Hivi karibuni Mh Rais ameanza kurudisha msamiati huu wa Mabeberu, akimaanisha watu wote wa nje wanaompinga sera za nchi.

Swali langu hapa ni je, hawa ambao tunawaita mabeberu tunawajuaje, kwa sera zao, imani zao, au kitu gani?

Au inategemeana tu na muktadha. Kesho Canada anaweza kuwa beberu kesho asiwe.

Ni muhimu kuweka wazi hii Sera yetu hasa inasimamia nini?

Mungu ibariki Tanzania!

BAADHI YA MAJIBU YALIYOTOLEWA NA WADAU
Dhana ya Ubeberu na siasa za Tanzania
Amani iwe nanyi wadau!

Leo napenda nitoe Elimu kwa watanzania juu ya propaganda za wana CCM kuwa yeyote anayempinga Raisi Magufuli ni kibaraka wa Mabeberu. Wanasema haya wakitaka kujenga picha kwa watanzania ( wadanganyika) kuwa ubeberu ni kama dhambi au jambo fulani ambalo halifai. Najua kwa watanzania wenzangu wengi wetu Elimu kwetu imekuwa shida na kwa sababu hiyo wanasiasa wamekuwa wakitumia kutokujua kwetu katulisha mambo ambayo wao wanataka tuyaamini. Wanafanya haya kwa maslahi yao ya kisiasa

Asili ya Ubeberu ni nini hasa?

Kwanza kwa watanzania wasiofahamu, Dunia ya leo inaongozwa na pande mbili zinazopigana kila kukicha kutawala Dunia.

Pande ya kwanza inaongozwa na Marekani na washirika wake hasa nchi za Ulaya Magharibi na Scandnavia yaaani Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Uholanzi, Canada, Sweden , Norway, Hispania, Ureno, Ubelgiji na washirika wao wengine. Hizi nchi zote zinaamini katika dhana ya maendeleo ya ubepari Yaani uhuru katika kuamua, kuwekeza na kumiliki.

Dhana hii hairuhusu serikali kukamata njia kuu za uchumi na inawapa nafasi watu binafsi kukamata njia kuu za uchumi. Dhana hii ina hatua yake ya juu ambayo wengi wanaiita kuwa Ubeberu. Kutokana na dhana ya ubepari/ ubeberu kuamini kwenye Uhuru wa watu katika maendeleo na kumiliki vitu nchi nyingi zenuw hii dhana raia wao wana maisha mazuri sana na wanaishi maisha ya kistaarabu sana na kuheshimiana.

Katika nchi hizi mtu unaweza kuwa tajiri wakati wowote kwa sababu kuna mifumo imara ya kuruhusu watu kukua kiuchumi na kimaisha ili mradi ufanye tu kazi na uwe na kipaji halali . Taasisi za hizi nchi ni imara na ndo zinawasimamia viongozi wa serikali. Viongozi hawana uimara kuzizidi taasisi zao. Na wakati wowote viongozi wanaweza kuwajibishwa.

Pande ya pili inaongozwa na Urusi na washirika wake ambao ni Venezuela, Cuba, Korea ya Kusini na nchi chache za ulaya ya mashariki. Hawa wanaamini kwenye ujamaa yani Sera ya serikali kumiliki njia zote kuu za uchumi. Nchi hizi haziamini kwenye Uhuru wa watu wao kwenye biashara, siasa, dini au maisha na hata ukiziangalia nyingi zimepiga Marufuku dini mbalimbali Tanzania Chama cha Mapinduzi nacho kinaamini kwenye Sera za ujamaa ingawa wao wanaamini kwenye uhuru wa dini Ila zile zinazokuwa chini ya uangalizi/ mkono wa serikali Mf. Bakwata.

Katika hizi nchi , nyingi raia wake wana maisha magumu sana kwa sababu wote wanategemea serikali ili kuishi na kukua. Kwenye nchi hizi huwezi kuwa tajiri kama serikali haijaridhia na wakati wowote hata ukiwa tajiri serikali inaweza kukufanya kuwa masikini. Wananchi wanaaminishwa serikali ni kama Mungu na haikosei. Watu wanaaminishwa kuwa kiongozi mkuu wa serikali hawezi kukosea. Vyombo vyote na taasisi za nchi lazima ziwe na utii kwa serikali na kiongozi wa serikali. Kwenye hizi nchi viongozi wa kisiasa ndo wanakuwa matajiri kuliko watu wa kawaida kwa sababu wao ndo wanakuwa na access ya vitu vizuri

Katikati ya hizi nchi kuna nchi kama China. Wao kisiasa wanaamini kwenye dhana ya Ukomunist ambayo haitofautoani sana na upande wa pili niliouelezea hapo juu ila kiuchumi wana mfumo wa kibepari/ ubeberu. China anafanya hivi kwa sababu alipeleka watu wake wengi Urusi na Marekani/ Ulaya ambao walisoma hizi dhana zote mbili na wakarudi kwao kutengeneza dhana yao.

Washirika wa Mabeberu

Hapa duniani Mabeberu/ Mabepari wana washirika wao pia. Washirika wa mabeberu ni nchi kama Korea kusini, Malyasia, Kuwait, Dubai, Saudi Arabia, Israel, Morocco, South Africa, Botswana, Ivory Coast, Ghana, Algeria, Singapore, Japan na wengineo wengi. Nchi hizi zote hizi kiujumla zimepiga hatua kubwa sana kimaendeleo hasa maendeleo ya watu na vitu. Kuna miundombinu ya uhakika, uwekezaji wa uhakika, fursa nyingi za ajira na kiwango kizuri cha elimu na teknolojia.

Washirika wa Wajamaa
Hapa kuna nchi kama Tanzania, Cuba, Venezuela, Korea ya kusini, Burundi, Congo, Sudan ya Al bashir, Sudan Kusini, Korea kaskazini na wengineo. Nchi hizi zote zina umasikini wa kutupwa na kuminywa kukubwa kwa haki za binadamu. Kuna umungu kwa viongozi wa mataifa na kiwango kikubwa cha kuzuia kukua kwa wananchi hasa wenye mawazo huru na mipango huru. Matajiri kwenye hizi nchi ni wale wanaojitoa kula na viongozi wa serikali na mara nyingi hawako stable kwa sababu wote wanategemea serikali na Viongozi wake. Vyombo vya maamuzi havo a Uhuru.

Hapa Tanzania Vyama viwili vikuu CCM na Chadema vimegawanyika kwenye mgawanyo huu. CCM wanaamini kwenye dhana ya ujamaa na Chadema wanaamini kwenye dhana ya Ubepari

Ewe mtanzania embu pata hii Elimu na ujue wanaosema huyu ni Bepari/ Beberu wanamaanisha nini na anayesema huyu mjamaa anamaanisha nini.

Mwisho niseme hakuna shida yeyote mtu kufuata dhana ya ubepari/ ubeberu ila kuna walakini mkubwa mtu anapofuata dhana ya ujamaa


Usisahau Kushare!!

Sambaza Upendo.

No hate No Fear!

Lord Denning
---
Beberu ni mtu anayekupa msaada kwa njia ya kudhalilisha
Beberu ni mtu yeyote anayetaka kukupa msaada au huduma kwa njia ya kukudhalilisha, anayetaka kuchukua uhuru wako, kwa kutumia nguvu zake au uwezo wake kifedha nk,

jina beberu linatumika kwa mfano wa mbuzi dume ambae hupenda kumtolea sauti nzito shingoni mwa mbuzi jike hasa pale anapotaka kufanya mapenzi na mbuzi jike.

Hivyo huonyesha kama anamkoromea mbuzi jike. Sasa mabeberu wa kizungu hupenda kutaka kutukoromea sisi waafrica na kutumia misaad yao kutunyanyasa na kutupangia wanachotaka wao hata kama ni cha kudhalilisha.

Mfano ni ushoga
 
Nashindwa kuandika lakini Wana-CCM wanawaona hawa watu hivi. Habari Afande
tapatalk_1574485444162.jpeg
 
Dunia inaenda kwa kasi sana, ukizubaa unaachwa!

Wakati wa vita baridi neno Mabeberu lilitumika sana hapa Tanzania. Enzi zile beberu alikuwa ni mtu yoyote asiye mjamaa, mpinga mapinduzi, anayeamini katika soko huria na uliberali.

Polepole neno mabeberu lilianza kufifia baada ya kuanguka kwa ukuta wa Berlin, na nchi zetu zikaanza uchumi na siasa za kiliberali. Hata mabeberu makaburu tukawakaribisha na kuanza kuwaita wawekezaji!

Kimsingi neno beberu likafa.

Hivi karibuni Mh Rais ameanza kurudisha msamiati huu wa Mabeberu, akimaanisha watu wote wa nje wanaompinga sera za nchi.

Swali langu hapa ni je, hawa ambao tunawaita mabeberu tunawajuaje, kwa sera zao, imani zao, au kitu gani?

Au inategemeana tu na muktadha. Kesho Canada anaweza kuwa beberu kesho asiwe.

Ni muhimu kuweka wazi hii Sera yetu hasa inasimamia nini?

Mungu ibariki Tanzania!

Zinaitwa lugha za majukwaani za kuwaponda ila hawawezi ishi bila misaada yao.Nyerere aliwaponda mabeberu lkn ndo waliomuokoa alipotaka kupinduliwa bila mabeberu awawezi kitu wanajimwambafy tu
 
Mkuu hawa wahuni wanaotumia huu msamiati hata siku moja hawajawahi kuzitaja hizo Nchi za MABEBERU ni zipi.

Dunia inaenda kwa kasi sana, ukizubaa unaachwa!

Wakati wa vita baridi neno Mabeberu lilitumika sana hapa Tanzania. Enzi zile beberu alikuwa ni mtu yoyote asiye mjamaa, mpinga mapinduzi, anayeamini katika soko huria na uliberali.

Polepole neno mabeberu lilianza kufifia baada ya kuanguka kwa ukuta wa Berlin, na nchi zetu zikaanza uchumi na siasa za kiliberali. Hata mabeberu makaburu tukawakaribisha na kuanza kuwaita wawekezaji!

Kimsingi neno beberu likafa.

Hivi karibuni Mh Rais ameanza kurudisha msamiati huu wa Mabeberu, akimaanisha watu wote wa nje wanaompinga sera za nchi.

Swali langu hapa ni je, hawa ambao tunawaita mabeberu tunawajuaje, kwa sera zao, imani zao, au kitu gani?

Au inategemeana tu na muktadha. Kesho Canada anaweza kuwa beberu kesho asiwe.

Ni muhimu kuweka wazi hii Sera yetu hasa inasimamia nini?

Mungu ibariki Tanzania!
 
Ubeberu ni hatua ya juu ya Ukoloni(imperialism), ambapo nchi tajiri zinaendelea kuzinyonya nchi maskini kwa njia ya uchukuaji wa rasilimali na pia misaada na mikopo yenye masharti magumu.
 
Dunia inaenda kwa kasi sana, ukizubaa unaachwa!

Wakati wa vita baridi neno Mabeberu lilitumika sana hapa Tanzania. Enzi zile beberu alikuwa ni mtu yoyote asiye mjamaa, mpinga mapinduzi, anayeamini katika soko huria na uliberali.

Polepole neno mabeberu lilianza kufifia baada ya kuanguka kwa ukuta wa Berlin, na nchi zetu zikaanza uchumi na siasa za kiliberali. Hata mabeberu makaburu tukawakaribisha na kuanza kuwaita wawekezaji!

Kimsingi neno beberu likafa.

Hivi karibuni Mh Rais ameanza kurudisha msamiati huu wa Mabeberu, akimaanisha watu wote wa nje wanaompinga sera za nchi.

Swali langu hapa ni je, hawa ambao tunawaita mabeberu tunawajuaje, kwa sera zao, imani zao, au kitu gani?

Au inategemeana tu na muktadha. Kesho Canada anaweza kuwa beberu kesho asiwe.

Ni muhimu kuweka wazi hii Sera yetu hasa inasimamia nini?

Mungu ibariki Tanzania!
Mabeberu in wale wanaowakopesha ccm ambao huwaita wahisani
 
Ubeberu ni hatua ya juu ya Ukoloni(imperialism), ambapo nchi tajiri zinaendelea kuzinyonya nchi maskini kwa njia ya uchukuaji wa rasilimali na pia misaada na mikopo yenye masharti magumu.
Kwa tafsiri hii inawezekana China ni Beberu?
 
Back
Top Bottom