Sababu za matajiri hasa Afrika kuwa machawa na kukosa ushawashi katika kuleta mabadiliko

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,620
46,261
Kuna mambo makubwa matatu,

Kwanza, matajiri wengi wa Africa wamejipatia utajiri kutokana biashara za uchuuzi tu bila kuhusika katika kufanya mabadiliko ya makubwa ya teknolojia. Hii ni tofauti sana na kwenye nchi za magharibi ambapo matajiri wake wengi wameibuka kutokana na ubunifu mbalimbali.

Pili, kupata utajiri kutumia mgongo wa serikali au viongozi wa serikali. Matajiri wengi wa nchi hizi ambao hugeuka kuwa machawa walijipatia mali za serikali kwa bei chee, wanaongeza utajiri wao kwa kupata tenda za serikali au wanashirikiana na viongozi wa serikali kukwepa kodi.

Tatu, mifumo ya utawala wa kijamaa, Kikomunisti au kidikteta huwa nayo hair hairuhusu watu wengine zaidi wa wanasiasa watawala kuwa na ushawashi mkubwa katika nchi.
 
Hilo ni kweli kabisa mkuu sema ndio hivyo tena, watu hawataki tu kuambiana ukweli ila hii nchi walioajiriwa na waliojiajiri, wengi ni watumwa tu ila wanatofautiana aina ya watu wanaowatumikia

Vigezo vya kufanikiwa kibiashara bongo ni tofauti na vigezo vya nchi za magharibi, kwahiyo binafsi nikiona mtu anaogopa kufanya biashara bongo namuelewa, maana anaepukana na mengi sana

Ndio maana wengine wako tayari waajiriwe maisha yao yote, kuliko kuingia kwenye uhuni na ufisadi wa bongo uliojificha kwenye biashara, in the name of 'financial freedom' kumbe unakuwa mtumwa wa viongozi

Ndio maana matajiri wetu wengi utajiri wao unategemeana na rais aliyepo madarakani, mtu unasikia awamu fulani ni tajiri awamu nyingine biashara zinaanza kufa, na matajiri wengi huibuka kipindi cha viongozi mafisadi

Hapa wafanyabiashara wengi wanafanikiwa kwa ufisadi, utapeli, kukwepa kodi na kudhulumu haki za watu, usipokuwa na moyo wa kibepari wa kufanya hayo sahau kuwa tajiri, utaishia kuwa middle class tu
 
Kabisa mzee, mambele matajiri wanashindana kufanya vitu vya kuleta impact katika mataifa yao, bongo issue ni uchuuzi tupu
 
Back
Top Bottom