Swali kwa Tundu Lissu

Swali kwa Tundu Lissu

Hata ACCACIA zaidi ya kusema kwamba hawakubaliani na ripoti ya tume ya rais, wamesisitiza kwamba hawatatoa msimamo wao officially hadi hapo watakapokabidhiwa repoti hiyo. Ila wamesisitiza wamekuwa wakifanya kazi kwa mujibu wa sheria za nchi hii.
Nadhani basi ingekuwa hekima kwa Tundu Lissu kuacha kumkejeli na kumtishia RAIS wetu kuwa tutashindwa mahakamani wakati ngoma yenyewe bado ni mbichi kabisa. Na ni vizuri akashauriwa na hao anaowaona ni bora kuliko RAIS wetu atumie uwezo wake aliojaliwa na Mwenyezi Mungu kusoma sheria na mianya itakayotuokoa ili mwisho wa siku watanzania wote na vizazi vyetu tuwe washindi dhidi ya UFISADI huu.
 
Nimesoma maelezo ya Tundu Lissu kuwa kutokana na mikataba ilivyo madini na Mchanga ni mali ya wawekezaji.

TL anasema "Badala ya a smart president, tuna JPM anayeamini kwamba ametumwa na Mungu kuinyoosha nchi hii na neno lake ndio sheria. Matokeo yake, atagombana na wawekezaji na serikali zao na mabwana wakubwa wa kifedha duniani ambao ndio wamiliki halisi wa rasilmali zetu."

Anaendelea kusema "Watampeleka kwenye arbitral tribunals za kimataifa ambazo Mkapa na Kikwete walizikubali kuwa ndio mahakama za migogoro kati yetu na hao tuliowapa rasilmali zetu. Na tukipelekwa huko hatuponi kwa sababu tutakuwa tumevunja mikataba na sheria zinazolinda wawekezaji."

SWALI: Kwa nini wanatakiwa kudeclare concentrates za madini yaliyomo kwenye mchanga?

Je TL anaamini kuwa Declaration hiyo haina maana yeyote kisheria?

Mbona maelezo ya Brad Gordon (CEO wa ACACIA) haelezi kuwa Declaration ya quantities of concentrates ni non sense na haiwabani kisheria? badala yake anasema "We do not agree with the committee's findings"
Ni kwa nini basi anasema "I want to reassure you that ACACIA fully declares everything of commercial value that we produce" iwapo False declaration haina consequences zozote kisheria?
Hili swali gumu sana wajameni kwa Tundu! Huyo bado mchanga kazaliwa juzi tu. Haya mambo kayaona wapiii. Muacheni Lissu wajameni yeye aendelee kujifunza na masakatahaya mazito. Hapo baadae Yes tutaweza mtegemea kiasi fulani baada ya kupata mauzoefu. Narudia msimsonge Lissu, yeye anajaribu ku test hypothesis zake alizofundishwa
 
Lissu ni mtaalamu wa sheria, raisi amebobea kwenye kemia. Nani kati yao utapenda akuwakilishe mahakamani?
Sasa kama mwanasheria mwenyewe anaona haki za ACACIA tu na haoni haki zetu kuwa udanganyifu kwenye declaration ni wizi kwa watanzania - Huyu mwanasheria atawafaa zaidi ACACIA kuliko watanzania.
 
Kwanza machadema labda ni wewe...

Pili, I doubt kama unatambua hata kinachojadiliwa....

Tatu, do you think is that easy kuvunja mikataba hii ?

Nne, uko aware kuwa tuna mikataba mibovu na ya hovyo kabisa ya ufuaji umeme ya Songas, IPTL, Richmond > Dowan > Symbion and the likes ambayo CCM hawahawa walisaini na ilishawatoa kamasi kutaka kuivunja, bila mafanikio ??

Tano, Laiti kama Magufuli angekuwa na guts za kuweza kuvunja mikataba, basi angeanza na hii ya vikampuni vya umeme vidogo na iliiyo wazi kabisa.....lakini maskini wa Mungu, hata kunusa tu hajawi kunusa huko ghafla ameparamia sekta ya madini ambayo iko so complicated.....!!

Sita, no... siyo kwamba sitaki, nataka sana na ofcoz kama ana ubavu huo angeuvunja siku ileile sambamba na utumbuaji wa Prof. Muhongo na wale sijui wa TMAA.....lakini nasikitika kukuambia kuwa, atakula bonge la "about turn" sooner or later!!

Ndiyo maana watu wengine tunasema, hizi siasa zingine ni za kipuuzi na zitatugharimu na kwa lugha ya Tundu Lissu, "tutanyolewa bila kutia maji !!"
Duh! Afadhali umenikumbusha na Richmond!
 
Nimeuliza je DECLARATION ya concentrates za minerals sio takwa la kisheria? Msaidieni TL basi kujibu.

Kwani Mruma alionaje ktk uchunguzi wake na wenzake ?

Ni utashi tu wa kampuni za madini ama wanalazimishwa na sheria ?

Alipendekeza nini kwa aliyemtuma ?

Well, tu - assume ni takwa la kisheria na kimkataba na ACACIA wamekiuka takwa hilo......

What do you think the government (actualité, here is Mr Magufuli) would have done in the first place ?

Nadhani Lissu kwa hapa, yuko precisely clear kwamba, tutapelekwa mahakama za kusuluhisha migogoro ya kibiashara za kimataifa kwa sbb tulikubaliana hivyo....

Sasa, huko ndiko kutakakojulikana kuwa declaration ya minéral concentrates ni takwa la kimkataba na kisheria ama vipi na who is right.... Magufuli na kamati yake ama Acacia....

Huwa tukifika ktk hili, experience, inatushitaki dearly....!!
 
Sasa kama mwanasheria mwenyewe anaona haki za ACACIA tu na haoni haki zetu kuwa udanganyifu kwenye declaration ni wizi kwa watanzania - Huyu mwanasheria atawafaa zaidi ACACIA kuliko watanzania.
Mbona ameshauru tutumie njia gani.
 
Duh! Afadhali umenikumbusha na Richmond!

Yes, ndio utambue kuwa wengine tuko kizalendo na kitaifa zaidi....

Sijui umenusa nini tu, maana naona kabisa ulitaka kumwingiza EL hapa lakini ukashtuka... hongera !!

Ishu za itikadi za vyama vyenu ni hukohuko kwenu bhana... tutaelewana na mtatuelewa tu..
 
Mkuu mimi sio mwanasheria. Natumia common sense tu kujenga hoja na ndio maana nikamuuliza mwanasheria pengine yeye ataanza kunielewesha kwa kunijulisha neno mkataba na jinsi neno hilo linavyojustify declaration kuwa upuuzi.
Nakukumbusha kukataliwa kwa hoja za upinzani toka 2007/08 na kupitishwa sheria za madini bungeni.

Nakushauri waulize maCCM yaliyopitisha hizo sheria TL hahusiki kukupa maelezo
 
Wametengeneza Virus kwa Ndioooooo halafu leo wamekuja na Anti Virus wanataka tuwapigie makofi
Wabunge wa CCM ndio walioifikisha nchii hii katika ufukara huu kwa kutengeneza by genetic engineering kirusi cha Ndioooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooo, leo wanataka tutengeneze antivirus yake. Polepole anawalaumu viongozi wa dini na watanzania eti wamekataa kutengeneza anti virus. Mpuuzi mkubwa!
 
Siku hizi kila nikimsikiliza TL huwa namkumbuka saaana marehemu Banza Stone, kwa ule wimbo wake "ELIMU YA MJINGA" au kwa jina jingine "MTAJI WA MASIKINI". Kuna verse aliimba "mjinga hupenda majivuno,
hupendo majisifuu,
asichokijua hujifanya anajua,
mazuri ya kwakee mabaya ya wenzake......" TL ana sifa zote hizo. Anajifanya anajua kila kitu humu Duniani. TL angekuwa "smart" basi hata CDM wasingebeba oil chafu toka CCM kuwa mgombea wa urais.
Yaani afadhali ya mjinga kuliko mpumbavu wewe.
 
Kweli umeongea matako kabisa, mbona huo wimbo unaongelea mjinga? Tena umeenda mbali mpaka ukasema ni majungu, sasa wewe utaegemea wapi? Kuwa Mh TL ana majungu, mbona umeandika kama unahala!!
Hakuna mjinga duniani kama TL, na anapenda majisifu, na kujifanya anajua.
 
Asante Mkuu lakini Bahati mbaya kwenye link uliyotoa sijapata majibu niliyotaka zaidi ya anwani hii SGS Headquarters

1 Place des Alpes
P.O. Box 2152
1211 Geneva 1
Switzerland
t +41 22 739 91 11
f +41 22 739 98 86

Sina hakika kama nimekosa majibu kwa sababu nilitumia simu kufingua link hiyo. Nikipata PC nijaribu tena kutafuta majibu
Jipe muda usome hapa mdogo wangu: SGS in Brief | SGS na hii kampuni inatoka Ufaransa.
 
Kwani Mruma alionaje ktk uchunguzi wake na wenzake ?

Ni utashi tu wa kampuni za madini ama wanalazimishwa na sheria ?

Alipendekeza nini kwa aliyemtuma ?

Well, tu - assume ni takwa la kisheria na kimkataba na ACACIA wamekiuka takwa hilo......

What do you think the government (actualité, here is Mr Magufuli) would have done in the first place ?

Nadhani Lissu kwa hapa, yuko precisely clear kwamba, tutapelekwa mahakama za kusuluhisha migogoro ya kibiashara za kimataifa kwa sbb tulikubaliana hivyo....

Sasa, huko ndiko kutakakojulikana kuwa declaration ya minéral concentrates ni takwa la kimkataba na kisheria ama vipi na who is right.... Magufuli na kamati yake ama Acacia....

Huwa tukifika ktk hili, experience, inatushitaki dearly....!!

Kama nimekupata vyema unachosema ni kuwa hata Tundu Lissu hajui kama Declaration ni takwa la kisheria au la. Bali ametumia experience tu kutabiri kuwa tutashindwa.
Hivi haingekuwa jambo jema kwa yeye kama nguli kwenye sheria na kwa kujua experience ya kushindwa mahakamani angejitolea kulisaidia Taifa kuwa hata ACACIA wakitushitaki yeye atajitolea kuwabana ili tukawashinde? Ni kwa nini anapenda kumkejeli RAIS wakati hajui udanganyifu kwenye Declaration ya madini ni kosa au la?
 
Nakukumbusha kukataliwa kwa hoja za upinzani toka 2007/08 na kupitishwa sheria za madini bungeni.

Nakushauri waulize maCCM yaliyopitisha hizo sheria TL hahusiki kukupa maelezo

Una maana upinzani ulikataliwa kuweka Declaration of mineral concentrates kuwa takwa la kisheria?
 
Asante mkuu.
Sasa sijaelewa kwa nini Tundu Lissu anamkejeli sana RAIS wetu na kumtishia kuwa watatushinda mahakamani.
Au anawaamini sana ACACIA kuliko wataalam wetu?

..sasa hivi migodi ya acacia imezingirwa na polisi.

..makontena yenye "mchanga" nayo yamezuiliwa.

..kwa hiyo utaona kuwa serikali imeizuia acacia kuendesha shughuli zake.

..TL anaamini huko ni kwenda kinyume na mkataba na muwekezaji.

..mahakama ya usuluhishi baina ya serikali na mwekezaji ndiyo ilipaswa kuipa "baraka" serikali kufunga shughuli za mwekezaji na siyo serikali kujiamulia yenyewe.

..hoja nyingine ya Lissu ni kwamba ikiwa Tz tutashindwa ktk madai yetu basi tunaweza kupigwa faini na kusababisha mzigo wa deni kwa walipa kodi wa Tz.

NB.

..Lissu ameshauri Raisi na serikali. Hajamkejeli hata kidogo.

..madudu ktk sekta ya madini Lissu amekuwa akiyapinga toka enzi za JK akiwa waziri wa madini.

..it is unfortunate kuwa tumechukua muda mrefu namna hii kuunga mkono juhudi na kilio cha Tundu Lissu na wanaharakati wenzake na wabunge wa upinzani.
 
..sasa hivi migodi ya acacia imezingirwa na polisi.


..hoja nyingine ya Lissu ni kwamba ikiwa Tz tutashindwa ktk madai yetu basi tunaweza kupigwa faini na kusababisha mzigo wa deni kwa walipa kodi wa Tz.

Mkuu, ni afadhali angetumia hilo neno nililolibold "ikiwa"ningemuelewa. Lakini yeye anauhakika tutashindwa ndio maana anamkejeli RAIS wetu hovyohovyo tu.
 
Sioni amekasirika wapi. Naona anakumbusha na shushauri njia ya kufuata. Wewe umeona hasira wapi?
Kuna siku uliwahi kumuona TL anaongea bila Ku shout na mishipa ya shingo kumsimama?
 
Back
Top Bottom