Swali kwa Tundu Lissu

Swali kwa Tundu Lissu

Weye yakhe unachekesha kweli kweli!
Yaani Tundu Lissu awe Punda wa Wazungu wa Dhahabu badala ya Mkapa, Kikwete,Chenge na CCM yao ambao ndo walisaini mikataba ya kuliibia Taifa kweli???Hizi ni akili za kina Makonda na Bashites.Mnakumbuka Mkapa siku anazindua Kahama old Mine alikabidhiwa Pande la DHAHABU SIJUI tANI NGAPI NA AKAONDOKA NALO?Je, hiyo ilikuwa ni ZAWADI,RUSHWA au BAKSHISHI? Wana CCM naomba mtujuze!!

TL kabla ya kuingia kwenye Siasa alikuwa ni Mwanaharakati wa Mazingira na ninakumbuka vizuri sana alivyopambana na Serikali ya Mkapa kuzuia Wachimbaji wadogo huko Kahama wasifukuzwe na kufikiwa kwenye mashimo ya Dhahabu na Wawekezaji hawahawa waliokuwa wameitwa na Mkapa.

Bado TL alipoingia Bungeni alikuwa akihoji mara kwa mara kuhus u HII MIKATABA YA WACHIMBAJI WA MIGODI KUWA SIRI BADALA YA KULETWA BUNGENI. CCM walifanya hii mikataba ni siri lakini leo wanajifanya hamnazo na kuanza kuikataa au kuivunja bila ya kufikiria madhara yake. Time gonna tell.
Kama alihoji huo mkataba mbovu akiwa bungeni, sasa unavunjwa yeye huyo huyo anaanza kuwatetea aliowaita wezi! What do you expect?
 
Kitaturu,
Kuna kitu umenikumbusha hapa. Kwamba JK aliyaona haya lakini akatuliza bori. Naona ni kwasababu JK alikuwa na upeo wa Kimataifa kuhusu Mikataba na Foreign Affairs issues. Lakini Ngosha mpaka leo hajakanyanga Ulaya, Asia wala Marekani. Yumkini ndiyo maana anafanya madudu kila kukicha....!

Siyo tu yamkini alikuwa na upeo wa mambo kimataifa, lakini pia KUSIKILIZA na KUWA MTULIVU kabla ya kuamua jambo, ni hekima na busara zaidi ambayo ni Mungu pekee ndiye atoaye hilo especially kwa viongozi wakubwa kama Magufuli aliyebeba mstakabali wa mamilioni ya watu....

Kosa dogo kwa maamuzi yasiyoongozwa na hekima na busara, ni kilio na kusaga meno kwa wanaokutegemea !!!

Binafsi sisemi kuwa, Rais Magufuli asi - review makosa ya watangulizi wake kina Nyerere, Mwinyi, Mkapa na Kikwete na kisha kufanya marekebisho inapowezekana....la hasha....

Hoja na point yetu sisi wengine ni, HOW EXACTLY THIS IS DONE ?...... baasi

Lakini inavyoonekana, wapiga zumari wengi wa huko mtaa wa pili wa - CCM hawatuelewi na merely think sisi tunapinga tu.... kumbe sisi ndiyo hasa wazalendo.....

Mzalendo wa kweli ni yule mwenye uwezo wa kutambua makosa yake na kuyarekebisha kwa busara, uwazi na hekima bila kulaumu wengine.......

This is absolutely contrary to Magufuli na wana CCM wenzake huko..... Wao kila kitu wanakipeleka kwa lengo la kupata "political scores" tu... Wengine wakijibu mapigo, wanaleta figisufigisu za kipuuzi !!

No way, hawa ni kuwadunda tu kushoto, kulia, mbele na nyuma until they get out of our way....

Makosa waliyafanya wao kwa kusaini mikataba ya hovyo na kinyonyaji utadhani walikuwa wamefumba macho yao ya nyama na yale ya ufahamu wao waliopewa na Mungu, Leo wanajitokeza kwa njia za kinafiki kutaka kurushia zigo la lawama kwa wengine wakiongozwa na jazba huku maarifa, hekima na busara wakiwa wameziweka mifukoni mwao !!!
 
SGS ni kampuni ya kimataifa ambayo iko duniani kote ikijihusisha na kuhakiki, kukagua (vipimo vya aina yote) ubora wa mali zisafirishwazo kutoka nchi moja na kwenda nchi nyingine. Kwa hiyo basi hii kampuni iko pia hapa kwetu ikahakiki mizigo yoote itokayo na iingiayo kama iko kama inavyoonyeshwa physicaly na kwenye bill of lading au airway bill.
Mchanga kutoka machimboni unakuwa na vyeti vya TMAA (Tanzania Mines Audit Agency) vikiainisha asilimia ya madini yaliyo kwenye mchanga huo n athamani yake. Kazi ya SGS ni kuhakiki usahihi huu (kumbuka wana kila zana: laboratory, scanner etc). Hakuna njia wanayoweza ku colude na exporter au importer kwa sababu at that other end point kuna auditing.
Tushangilie tukisikilizia, kwa sababu sidhani kama ACCACIA ni maamuma kiasi cha kufanya kinyume na makubaliano yalivyo kwenye MKATABA.
Kumbuka hii mikataba imeliliwa saana na oposition kwa miaka mingi. Najiuliza swali, Je ni rahisi kuvunja mkataba na tukapona kama taifa?
wabongo mmeanza,unashauli nini sasa.
 
No tongue here, Dude... just black ink !!

Acheni ujinga, tutakataa upuuzi wowote wa kisiasa nyie CCM mnaotuchezea....

Mikataba mlisaini nyinyi wenyewe, sheria za madini mlipitisha nyie wenyewe tena kwa hati ya dharula bila hata kusoma na "ndiyoooooo" za kijiiingaaa, leo mnaanza kulialia kuwa mnapigwa ?.....I see, what à nonsense is this !!

Huyuhuyu Rais wako leo anayejifanya kulia sana kwenye msiba wa mtu waliyemuua wao wenyewe, was part and parcel of hii kitu, aliwahi hata kusimama kupingana na wenzake ? Anataka kutuambia nini leo, eti ??.....siasa tu tena za kipuuzi kabisa !!

Pathetic CCM......na sisi wengine siyo wajinga wa kiwango chenu eti, tutahoji na kuwakatalia kila aina ya ulaghai na ujinga mtakaojaribu kuuleta, no matter mtatuita majina gani !!

Wauaji na wanafiki wakubwa nyie. Acha i - back fire na mnyolewe bila maji....
Kwa hiyo nyie machadema hamtaki huu mkataba uvunjwe sio? Majizi ni majizi tu, ndio maana Yale yote majizi menzenu baadhi yalioshiriki mikataba mibovu yakiwa ccm, yamefurushwa na kutimkia huko mliko majambazi wakubwa!
 
Kama alihoji huo mkataba mbovu akiwa bungeni, sasa unavunjwa yeye huyo huyo anaanza kuwatetea aliowaita wezi! What do you expect?
Alihoji mikataba huko nyuma hakusilizwa. Wangemsilikiza wakati huo wangeanza mchakato wa kuirudia mikaba hiyo. Nchi yetu haina dira. Tunaenda kwa mapenzi ya rubani.
 
Tundu Lisu ni retarded!

Ushabiki wa kisiasa na chuki zisizo na manufaa kwa nchi ndizo zinazofanya nchi hii iwe masikini hata baada ya chama unachoshabikia kukaa madarakani kwa miaka zaidi ya hamsini.
 
Kitaturu wape wape vidonge vyao. Acha sindano izame ili dawa ikolee sawasawa.
Mimi nasubiri tu pale Rais Magufuli atakapoitwa kwenda kuhojiwa na Jopo la Majaji wa Kimataifa wanaoshughulikia Mikataba ya Biashara za Kimataifa. Bila shaka itabidi atafute mkalimani wa Kisukuma maana vinginevyo watu watabakia midomo wazi jinsi atakavyoweweseka kujibu maswali magumu!!!Tusubiri,
Eti wape wape! Unabana pua kama shoga! Mkataba tuanauvunja, na nyie manaotetea mabwana zenu wazungu, mwende mkawatetee, halafu muone 2020 wananchi watawafanya nini nyambafu!!
 
MIE NAOMBA MNISAIDIE HUYU MTU UTAMWITAJE???? KWENYE UTAWALA WA MKAPA ALIKUWA ANA LALAMIKA MIKATAPA MIBOVU NA UWEKEZAJI WA HOVYO.KWENYE UTAWALA WA KIKWETE PIA ANA LALAMIKA NCHI INAIBIWA.RAIS ANACHEKACHEKA TU.NI MPOLE MNO.UCHUMI WA NCHI UNAIBIWA TU NA KUPELEKWA ULAYA.YEYE ANADHURULA TU.MARAFIKI ZAKE WANAIBA NA HAWACHUKULII HATUA ZOZOTE.TUNATAKIWA TUWE NA RAIS MKALI.AWADHIBITI HAWA WEZI WA MALI ZA UMMA.NA IKIWEZEKANA NCHI IPINDULIWE NA JESHI ILI TUKIMBIE MCHAKA MCHAKA.SIO KIKWETE RAISI MWENYE NYOTA YA KIKE NA MPENDA KUCHEKA CHEKA. TUMEMPATA MAGUFULI MKALI.MBABE.HAPENDI MCHEZO KWENYE MASUALA YA NCHI.HANA URAFIKI NA MZEMBE ASIETIMIZA WAJIBU WAKE.HATAKI NGONJERA YA NJOO KESHO NJOO KESHO.LKN PIA ANATUKANWA NI MBABE.HAFUATI SHERIA.HEBU NIAMBIENI WANA JF.HUYU MTU ANAEMLALAMIKIA KILA ANAYEKUJA TUMWITEJE??? HEBU NISAIDIENI WANA JAMVI.
 
Asante Mkuu.
Swali langu ni je huo mkataba unawaruhusu kutudanganya kwenye declaration? maana hapo ndipo kamati ilipogundua kuwa tunadanganywa na kuibiwa sana. Msaidie basi TL kutujibu hilo! maana hata wao hawajasema kama wana uhalali kutudanganya.
Wanachosema ni kuwa hawaamini matokeo ya uchunguzi wa kimaabara wa kamati ya RAIS. Tafsiri yangu ya kilayman ni kuwa tunachopaswa kukifanya ni kuwaaminisha tu! jambo ambalo naamini kamati yetu inaweza kulifanya kirahisi tu.

..hakuna mkataba wowote unaoruhusu kudanganya.

..acacia hawaruhusiwi kudanganya.

..serikali ya tanzania pia hairuhusiwi kudanganya.

..tume ya wataalamu imesema acacia imedanganya.

..acacia nao wamejibu kwamba hawajadanganya.

..hatua inayopaswa kuchukuliwa kwa sasa hivi ni pande hizo mbili kupeleka shauri lao kwa mahakama ya kimataifa ya masuala ya uwekezaji. katika mahakama hiyo kila upande utawasilisha hoja zake na huenda ikateuliwa kampuni independent kutafuta ukweli kuhusu suala hili.
 
Waheshimiwa, tunabishia gizani.
1)Aliyeiona mikataba husika atuwekee ukumbini tujadiri vipengele vyake.
2)Wakati JPM analalama kuibiwa na mchanga alikuwa ndani ya baraza la mawaziri. Kama msomi alishauri nini na iliishia wapi?
3)Huko nyuma kabisa iliwahi kupendekezwa tujenge smelter, hilo wazo lilizimwa na nani na kwa manufaa ya nani?
4)Tulipokubali usafirishaji wa mchanga tulijua ni madini gani yamo ndani au ndiyo tumegundua?
5)SGS wana jukumu la kubainisha madini aina ngapi zimo mchangani au ni kubaini dhahabu kiasi gani tu?
6)Mbele ya safari tukifika mahakama za usuruhishi, ni mahabara gani yatatumika kuhakiki michanga inanyosombwa?

Siyo mpenzi wa kuibiwa lakini, walipoangusha wino (nasikia wengine waliangushia wino hotelini), ndiyo hapo walitutia kitanzi.
Nakubaliana na Lissu. La kwanza ni kujiondoa kwenye mahakama za kimataifa, mambo yamalizikie kwenya mahakama zetu. Ni mtego pia kwani wawekezaji wachache watakubali yaishie Tanzania.
Maswli yako ni ya msingi sana.
Lakini kama nimelielewa vizuri andiko la TL ni kuwa RAIS wetu kachemka kwa kuwa hakuanza na kujiondoa kwenye mahakama za kimataifa. Ndio maana nikauliza kama RAIS wetu kakosea hapo tayari hivi hata tukiprove kuwa tunaibiwa na kwamba declaration ya ACACIA ni ya uongo bado sheria na mikataba yao inatubana?
 
..hakuna mkataba wowote unaoruhusu kudanganya.

..acacia hawaruhusiwi kudanganya.

..serikali ya tanzania pia hairuhusiwi kudanganya.

..tume ya wataalamu imesema acacia imedanganya.

..acacia nao wamejibu kwamba hawajadanganya.

..hatua inayopaswa kuchukuliwa kwa sasa hivi ni pande hizo mbili kupeleka shauri lao kwa mahakama ya kimataifa ya masuala ya uwekezaji. katika mahakama hiyo kila upande utawasilisha hoja zake na huenda ikateuliwa kampuni independent kutafuta ukweli kuhusu suala hili.
Asante mkuu.
Sasa sijaelewa kwa nini Tundu Lissu anamkejeli sana RAIS wetu na kumtishia kuwa watatushinda mahakamani.
Au anawaamini sana ACACIA kuliko wataalam wetu?
 
Asante Mkuu. Kwa maana hiyo Kamati ya RAIS imeichallenge SGS?
Kwa hiyo TL anawaamini SGS kuliko wataalam wetu?
Lakini hiyo haijawa hoja ya TL katika andiko lake. Hoja yake imebase kwenye sheria na kwamba wakienda mahakamani watatushinda. Na ndio maana nikauliza mikataba na sheria inasemaje kuhusu kudanganya katika kudeclare?
Maana hoja yetu ni kuwa tunadanganywa katika declaration. Na wataalam wetu wapo tayari kuprove hilo scientifically. Ni vema basi hao SGS wakaja na hivyo vipimo vyao kama wana uhakika navyo tuweze kujua nani ni muongo kati ya wataalam wetu na wao.

Hata ACCACIA zaidi ya kusema kwamba hawakubaliani na ripoti ya tume ya rais, wamesisitiza kwamba hawatatoa msimamo wao officially hadi hapo watakapokabidhiwa repoti hiyo. Ila wamesisitiza wamekuwa wakifanya kazi kwa mujibu wa sheria za nchi hii.
 
Kwa hiyo nyie machadema hamtaki huu mkataba uvunjwe sio? Majizi ni majizi tu, ndio maana Yale yote majizi menzenu baadhi yalioshiriki mikataba mibovu yakiwa ccm, yamefurushwa na kutimkia huko mliko majambazi wakubwa!

Kwanza machadema labda ni wewe...

Pili, I doubt kama unatambua hata kinachojadiliwa....

Tatu, do you think is that easy kuvunja mikataba hii ?

Nne, uko aware kuwa tuna mikataba mibovu na ya hovyo kabisa ya ufuaji umeme ya Songas, IPTL, Richmond > Dowan > Symbion and the likes ambayo CCM hawahawa walisaini na ilishawatoa kamasi kutaka kuivunja, bila mafanikio ??

Tano, Laiti kama Magufuli angekuwa na guts za kuweza kuvunja mikataba, basi angeanza na hii ya vikampuni vya umeme vidogo na iliiyo wazi kabisa.....lakini maskini wa Mungu, hata kunusa tu hajawi kunusa huko ghafla ameparamia sekta ya madini ambayo iko so complicated.....!!

Sita, no... siyo kwamba sitaki, nataka sana na ofcoz kama ana ubavu huo angeuvunja siku ileile sambamba na utumbuaji wa Prof. Muhongo na wale sijui wa TMAA.....lakini nasikitika kukuambia kuwa, atakula bonge la "about turn" sooner or later!!

Ndiyo maana watu wengine tunasema, hizi siasa zingine ni za kipuuzi na zitatugharimu na kwa lugha ya Tundu Lissu, "tutanyolewa bila kutia maji !!"
 
Asante mkuu.
Sasa sijaelewa kwa nini Tundu Lissu anamkejeli sana RAIS wetu na kumtishia kuwa watatushinda mahakamani.
Au anawaamini sana ACACIA kuliko wataalam wetu?
Lissu ni mtaalamu wa sheria, raisi amebobea kwenye kemia. Nani kati yao utapenda akuwakilishe mahakamani?
 
Alihoji mikataba huko nyuma hakusilizwa. Wangemsilikiza wakati huo wangeanza mchakato wa kuirudia mikaba hiyo. Nchi yetu haina dira. Tunaenda kwa mapenzi ya rubani.
Kwa hiyo amekasirika na ndio ameamua Ku turn hostile?
 
Siku hizi kila nikimsikiliza TL huwa namkumbuka saaana marehemu Banza Stone, kwa ule wimbo wake "ELIMU YA MJINGA" au kwa jina jingine "MTAJI WA MASIKINI". Kuna verse aliimba "mjinga hupenda majivuno,
hupendo majisifuu,
asichokijua hujifanya anajua,
mazuri ya kwakee mabaya ya wenzake......" TL ana sifa zote hizo. Anajifanya anajua kila kitu humu Duniani. TL angekuwa "smart" basi hata CDM wasingebeba oil chafu toka CCM kuwa mgombea wa urais.
Kweli umeongea matako kabisa, mbona huo wimbo unaongelea mjinga? Tena umeenda mbali mpaka ukasema ni majungu, sasa wewe utaegemea wapi? Kuwa Mh TL ana majungu, mbona umeandika kama unahala!!
 
Back
Top Bottom