Swali Fyatu: Kwani Tatizo Gani Wameweza Kulitatua Likaisha?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,998
Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna mambo mengine yakijirudia unaweza ukafikiria bado uko ndotoni. Maana kuna baadhi ya ndoto zinajirudia rudia hata kama huzitaki. Wengine wanaita "jinamizi". Zinakuja zinatisha halafu unashtuka unasema "duh hii ndoto hii!". Unarudi kulala unafikiri itapita; kumbe ukisinzia tu jinamizi linaanzia pale lilipoishia!

Fikiria mambo ya Bodi ya Mikopo unaweza ukafikiria hili tatizo lingekuwa limeisha zaidi ya miaka ishirini toka tulipolivalia njuga suala la vijana wetu kule Ukraine enzi hizo. Suala la Sukari ni hivyo hivyo, toka miaka ya tisini bado tunazunguka nalo tu; kila baada ya muda linaibuka tena! Hapa naogopa hata kutaja suala la umeme. Yaani, unaweza kuamka asubuhi ukafikiria uko mwaka 1996! Sijagusa suala la uhaba wa fedha za kigeni, naogopa kuuliza kuchelewesha mishahara, nashindwa kuzungumzia mafao ya wazee/wastaafu, na hapa hatujataja suala la ajira kwa wahitimu.

Yaani, ukisoma sasa kuhusu "tuko mbioni", "serikali inajipanga", "tuko tayari kuanza kutekeleza", "tumetoa siku kadhaa hili liwe limeisha".. yaani, unaweza kukuta watu wanapiga makofi wakisahau kumbe baba zao na mama zao na wenyewe walipiga makofi miaka thelathini iliyopita kushangilia matamshi yale yale yaliyotolewa na watu wale wale kwenye matatizo yale yale!

Watanzania ni lazima waamue kama watu wale wale, wenye mipango ile ile, wakikabili matatizo yale yale kwa namna ile ile wanastahili kupewa nafasi zile zile za kuongoza tena! Nje ya hapo ni lazima tujiulize labda kuna vizazi vitaendelea kutushangaa sana kwanini tumeendelea kuwa vile vile! Kwani, matatizo gani wamewahi kuyatatua yakaisha kabisa? Yaani, watakuja tena kuomba miaka mitano mingine na tena wana ujasiri wa kuimba "CCM ni ile ile!"

Kwanini matokeo yasiwe vile vile?
 
Ningekuwa Rais, suala la sukari ningeamuru ndege zetu za mizigo ziende hapo Zambia tu zirudi na maximum tani zinazoweza kubeba, kisha ningesambaza kila mkoa kulingana na mahitaji yake..

Na nisingeuza jumla, ningeuza reja reja tu ili wacheza rafu wasipate nafasi..

Ila kwa kuwa huenda na yeye ana % zake, basi tunaoumia ni akina sie kajamba nani..
 
Wataamua nini na wakati "ujinga" wao ndio mitaji yao,,?
Hakuna jambo lolote lile

Elimu Bure - hakuna Walimu ,vyoo, madarasa

Kikokotoo ndio balaa

Mikopo elimu ya juu Nako janga

BRN haikuleta impact yoyote Ile

Bima ya afya Kwa wote nalo janga jipya.

CCM HAWANA JAMBO HATA MOJA LA KUJIVUNIA YAANI HAKUNA

UMEME, MAJI, AFYA NDIO MIAKA 60 YA UHURU BADO HALI TETE.

FOR 60 GOOD YEARS TUNAENDA MBELE TUNA RUDI NYUMA
 
Mliozaliwa 2000 mtasema hivyo,Ila huko nyuma lami ilikua Hadith ya kusadikika,Leo ndoto imetimia,Arusha mpaka mtwara kwa taxi
Nimezaliwa 80s. Mnaokula Kwa kutegemea ccm ndio mtasema hivyo. Njoo mikoa ya Kanda ya ziwa uongelee lami kama watakuelewa.

Hapo Dar barabara Zina mashimo na vilaka kama vyote ....

Taja jambo jingine unalojivunia kutoka serikali ya ccm.
 
Nimezaliwa 80s. Mnaokula Kwa kutegemea ccm ndio mtasema hivyo. Njoo mikoa ya Kanda ya ziwa uongelee lami kama watakuelewa.

Hapo Dar barabara Zina mashimo na vilaka kama vyote ....

Taja jambo jingine unalojivunia kutoka serikali ya ccm.
Nilitoka tabora mpaka geita,nikipita kwenye lami,Mimi ngosha,mdanganye mwingine
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna mambo mengine yakijirudia unaweza ukafikiria bado uko ndotoni. Maana kuna baadhi ya ndoto zinajirudia rudia hata kama huzitaki. Wengine wanaita "jinamizi". Zinakuja zinatisha halafu unashtuka unasema "duh hii ndoto hii!". Unarudi kulala unafikiri itapita; kumbe ukisinzia tu jinamizi linaanzia pale lilipoishia!

Fikiria mambo ya Bodi ya Mikopo unaweza ukafikiria hili tatizo lingekuwa limeisha zaidi ya miaka ishirini toka tulipolivalia njuga suala la vijana wetu kule Ukraine enzi hizo. Suala la Sukari ni hivyo hivyo, toka miaka ya tisini bado tunazunguka nalo tu; kila baada ya muda linaibuka tena! Hapa naogopa hata kutaja suala la umeme. Yaani, unaweza kuamka asubuhi ukafikiria uko mwaka 1996! Sijagusa suala la uhaba wa fedha za kigeni, naogopa kuuliza kuchelewesha mishahara, nashindwa kuzungumzia mafao ya wazee/wastaafu, na hapa hatujataja suala la ajira kwa wahitimu.

Yaani, ukisoma sasa kuhusu "tuko mbioni", "serikali inajipanga", "tuko tayari kuanza kutekeleza", "tumetoa siku kadhaa hili liwe limeisha".. yaani, unaweza kukuta watu wanapiga makofi wakisahau kumbe baba zao na mama zao na wenyewe walipiga makofi miaka thelathini iliyopita kushangilia matamshi yale yale yaliyotolewa na watu wale wale kwenye matatizo yale yale!

Watanzania ni lazima waamue kama watu wale wale, wenye mipango ile ile, wakikabili matatizo yale yale kwa namna ile ile wanastahili kupewa nafasi zile zile za kuongoza tena! Nje ya hapo ni lazima tujiulize labda kuna vizazi vitaendelea kutushangaa sana kwanini tumeendelea kuwa vile vile! Kwani, matatizo gani wamewahi kuyatatua yakaisha kabisa? Yaani, watakuja tena kuomba miaka mitano mingine na tena wana ujasiri wa kuimba "CCM ni ile ile!"

Kwanini matokeo yasiwe vile vile?
HAMNA🤓
 
Upo? Mnatabu nyinyi wakatoliki. Magu kimya. Mkapa kimya. Nyerere ulikuwa hujazaliwa MMM lkn ingalikua kimya
Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna mambo mengine yakijirudia unaweza ukafikiria bado uko ndotoni. Maana kuna baadhi ya ndoto zinajirudia rudia hata kama huzitaki. Wengine wanaita "jinamizi". Zinakuja zinatisha halafu unashtuka unasema "duh hii ndoto hii!". Unarudi kulala unafikiri itapita; kumbe ukisinzia tu jinamizi linaanzia pale lilipoishia!

Fikiria mambo ya Bodi ya Mikopo unaweza ukafikiria hili tatizo lingekuwa limeisha zaidi ya miaka ishirini toka tulipolivalia njuga suala la vijana wetu kule Ukraine enzi hizo. Suala la Sukari ni hivyo hivyo, toka miaka ya tisini bado tunazunguka nalo tu; kila baada ya muda linaibuka tena! Hapa naogopa hata kutaja suala la umeme. Yaani, unaweza kuamka asubuhi ukafikiria uko mwaka 1996! Sijagusa suala la uhaba wa fedha za kigeni, naogopa kuuliza kuchelewesha mishahara, nashindwa kuzungumzia mafao ya wazee/wastaafu, na hapa hatujataja suala la ajira kwa wahitimu.

Yaani, ukisoma sasa kuhusu "tuko mbioni", "serikali inajipanga", "tuko tayari kuanza kutekeleza", "tumetoa siku kadhaa hili liwe limeisha".. yaani, unaweza kukuta watu wanapiga makofi wakisahau kumbe baba zao na mama zao na wenyewe walipiga makofi miaka thelathini iliyopita kushangilia matamshi yale yale yaliyotolewa na watu wale wale kwenye matatizo yale yale!

Watanzania ni lazima waamue kama watu wale wale, wenye mipango ile ile, wakikabili matatizo yale yale kwa namna ile ile wanastahili kupewa nafasi zile zile za kuongoza tena! Nje ya hapo ni lazima tujiulize labda kuna vizazi vitaendelea kutushangaa sana kwanini tumeendelea kuwa vile vile! Kwani, matatizo gani wamewahi kuyatatua yakaisha kabisa? Yaani, watakuja tena kuomba miaka mitano mingine na tena wana ujasiri wa kuimba "CCM ni ile ile!"

Kwanini matokeo yasiwe vile vile?
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna mambo mengine yakijirudia unaweza ukafikiria bado uko ndotoni. Maana kuna baadhi ya ndoto zinajirudia rudia hata kama huzitaki. Wengine wanaita "jinamizi". Zinakuja zinatisha halafu unashtuka unasema "duh hii ndoto hii!". Unarudi kulala unafikiri itapita; kumbe ukisinzia tu jinamizi linaanzia pale lilipoishia!

Fikiria mambo ya Bodi ya Mikopo unaweza ukafikiria hili tatizo lingekuwa limeisha zaidi ya miaka ishirini toka tulipolivalia njuga suala la vijana wetu kule Ukraine enzi hizo. Suala la Sukari ni hivyo hivyo, toka miaka ya tisini bado tunazunguka nalo tu; kila baada ya muda linaibuka tena! Hapa naogopa hata kutaja suala la umeme. Yaani, unaweza kuamka asubuhi ukafikiria uko mwaka 1996! Sijagusa suala la uhaba wa fedha za kigeni, naogopa kuuliza kuchelewesha mishahara, nashindwa kuzungumzia mafao ya wazee/wastaafu, na hapa hatujataja suala la ajira kwa wahitimu.

Yaani, ukisoma sasa kuhusu "tuko mbioni", "serikali inajipanga", "tuko tayari kuanza kutekeleza", "tumetoa siku kadhaa hili liwe limeisha".. yaani, unaweza kukuta watu wanapiga makofi wakisahau kumbe baba zao na mama zao na wenyewe walipiga makofi miaka thelathini iliyopita kushangilia matamshi yale yale yaliyotolewa na watu wale wale kwenye matatizo yale yale!

Watanzania ni lazima waamue kama watu wale wale, wenye mipango ile ile, wakikabili matatizo yale yale kwa namna ile ile wanastahili kupewa nafasi zile zile za kuongoza tena! Nje ya hapo ni lazima tujiulize labda kuna vizazi vitaendelea kutushangaa sana kwanini tumeendelea kuwa vile vile! Kwani, matatizo gani wamewahi kuyatatua yakaisha kabisa? Yaani, watakuja tena kuomba miaka mitano mingine na tena wana ujasiri wa kuimba "CCM ni ile ile!"

Kwanini matokeo yasiwe vile vile?
Mkuu Pascal Mayalla nineona nikutag tu kwa heshima na hekima zako🙂
 
Mkuu Pascal Mayalla nineona nikutag tu kwa heshima na hekima zako🙂
Asante
Na. M. M. Mwanakijiji

Watanzania ni lazima waamue kama watu wale wale, wenye mipango ile ile, wakikabili matatizo yale yale kwa namna ile ile wanastahili kupewa nafasi zile zile za kuongoza tena! Nje ya hapo ni lazima tujiulize labda kuna vizazi vitaendelea kutushangaa sana kwanini tumeendelea kuwa vile vile! Kwani, matatizo gani wamewahi kuyatatua yakaisha kabisa? Yaani, watakuja tena kuomba miaka mitano mingine na tena wana ujasiri wa kuimba "CCM ni ile ile!"

Kwanini matokeo yasiwe vile vile?
Na tutawapa tena mitano mingine!. Hivi ndivyo Watanzania tulivyo!.
P
 
Back
Top Bottom