Swali Fyatu la Mwezi: Wakimpa Sifa Zake, Watapunguza za Kwao?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,999
1685641114578.png

Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna watu ambao tunawakumbuka kwa umahiri na weledi katika kazi, vipaji au matendo yao. Michael Jordan aliichezea timu ya mpira wa vikapu ya Chicago Bulls na kujionesha kuwa ni mchezaji bora Zaidi wa mchezo huo duniani. Wengi wanalijua jina la Michael Jordan lakini ni wachache wanaweza kukutajia majina ya wachezaji wenzake wanne waliokuwa wanaunda kikosi cha kwanza. Hili pia ni kweli kuhusu mchezaji bora Zaidi wa soka duniani Pele. Wengi wanalijua na kukumbuka jinsi Pele alivyoongoza Brazili kwenye makombe ya dunia. Ni wachache sana wanaweza kukutajia wachezaji kumi wengine walioshinda na Pele kombe la dunia mara ya mwisho.

Hata hapa Tanzania kuna watu wanakumbukwa kwa umahiri wao lakini ni wachache wanaweza kukutajia majina ya watu wengine kwenye vikosi vyao. Mbaraka Mwinshehe, Marijan Rajabu, au hata Remmy Ongara. Tunajua nyimbo zao, tumewahi kuzisikia lakini tukiuliza wana bendi wenzao ni kina nani ni wachache wanaweza kutaja hata majina mawili.

Ukweli ni kuwa kuna watu wanatokea katika fani mbalimbali na wanakuwa vinara na bora kuliko wengine. Tunapowataja hawa wengine na kuwasifia haina maana tunadharau mchango wa wengine. Ukimtaja Lionel Messi kwa mfano au Cristiano Ronaldo mara moja watu watajua unawazungumzia kina nani lakini ni wachache wanaweza kukutajia majina ya wachezaji wenzao kwenye zile timu zilizokuza majina yao. Unaposema sifa za vinara haina maana unafuta sifa au unadharau sifa za wengine!

Juzi wakati wa uzinduzi wa Ikulu mpya ya Dodoma ambayo sasa inaifanya Ikulu ya Dar-es-Salaam kuwa Ikulu Ndogo kuna watu walisimama na kumwaga sifa mbalimbali. Niliamka mapema (huku niliko) niweze kushuhudia kama watakuwa na ujasiri wa kumtaja mchezaji kinara aliyewafanya wawepo pale siku ile. Bahati mbaya karibu kila aliyesimama ama alinyemelea kulitaja jina la mchezaji huyo bora au alilitaja kama kulipita tu kuwa “alikuwa ni mmoja wa timu”.

Jina la Joseph Pombe Magufuli, kinara wa marais wote waliowahi kutokea Tanzania, shujaa wa uthubutu, na mbunifu wa maono ya maendeleo ya haraka lilitajwa kana kwamba na yeye alikuwa na mchango kama wengine tu. Yote hiyo ilifanywa kwa makusudi kabisa wakijaribu kufifisha jina hilo na hawakutaka kusikia makofi na shangwe ambazo wangelitendea haki zingesikaka. Waliogopa kuona kuwa yumkini huyu bwana akiwa amelala kaburini milele kuna watu wanamkumbuka na kummiss!

Wanatuambia kuwa mpango wa kuhamishia Ikulu ulianza toka miaka ya sitini na hatimaye maamuzi yakachukuliwa na taratibu hatua mbalimbali zilianza kuchukuliwa ili kuhamia taratibu Dodoma. Jakaya Kikwete akatupa stori kuwa aliagiza watu waende Malaysia waone mambo yanavyofanyika huko na sisi tuje kuiga. Sikumbuki kwa miaka kumi ya Kikwete kama kuna siku ulifanyika mjadala hata mmoja Bungeni wa jinsi ya kuhamia Dodoma na kujenga Ikulu Dodoma na kuwa aliwaambia Watanzania kuwa ametuma iende Malaysia! Sijui hiyo timu iliongozwa nan ani! Lakini tunakubali.

Tunaambiwa kuwa viongozi wote waliotangulia wamekuwa wakifanya kama kupokezana vijiti kuliongoza taifa. Wanasahau kuwa Magufuli hakumwachia Samia kijiti; kamwachia gogo! Ni wazi Rais Samia anajitahidi kwa uwezo wake wote kuonekana anaweza kukamilisha miradi hii yote; na kweli tunaona ikimalizwa. Lakini ndugu zetu hawa wanataka tuamine kuwa kama Magufuli asingefanya alivyofanya leo tungekuwa na Ikulu Dodoma au Mji wa Serikali, au miradi hii mingine mikubwa siyo tu ya kimkakati kama inavyoitwa bali ya uthubutu uliopitiliza.

Yaani, kwa miaka Zaidi ya arobaini hawa jamaa walishindwa kuhamia Dodoma walikuwa wanalipia vipindi vya CDA hata sijui tulikuwa tunaambiwa nini. Kwa miaka arobaini walikuwa wanajipanga, na kuandaa ramani, na kuandaa warsha na semina. Kwa miaka arobaini wanaenda Dodoma, usiku usiku wanawahi kurudi Dar, kwa miaka arobaini wanaimba “Dodoma Dodoma” lakini kila wakiama ni “Dar, Dar”.

Akaja Magufuli akasema maneno matupu hayaliwi na upepo haufungwi kanga! Akawakimbiza mchakamchaka watu wazima na majasho hadi kwenye kucha; mambo yakaanza Kwenda. Yaani, yaliyowashindwa kwa miaka arobaini mtu kayaweza kuyasukuma kwa miaka mitano! Halafu wanatuambia “na sisi tulicheza”. Wanasema kweli Pele alifunga goli lakini sisi tulitoa pasi; wanasema Lionel kachukua kombe la dunia lakini sisi tulimbeba! Hatutaki kuwakumbuka!

Sasa wameamua tu kuwa hawamtaja Magufuli kwa sifa zake; hawatamtaja kwa uthubutu wa barabara, meli, mashule, madaraja. Yaani, kuna watu walijenga daraja moja kubwa kwa miaka kumi halafu anakuja mtu anajenga Matano wanajilinganisha naye! “Na sisi tulijenga barabara na sisi tulijenga daraja” msimpe sifa sana yule; alikuwa ati wa kawaida tu. Ni wivu gani huu?

Hivi kweli wakisema sifa za Magufuli kwa haki kabisa, na kusema kuwa alikuwa ni mchezaji nyota wao watapunguziwa sifa zao? Hivi watakapoenda kuwasha umeme wa Bwawa la Nyerere si wataanza kutupigisha stori tena kama za Ikulu! “Oh hili wazo lilikuwa la Nyerere, na sisi wengine tukapokezana vijiti”! Hivi mkimpa sifa Magufuli anazostahili nyinyi mtapungukiwa? Mtaonekana mnamshusha Samia? Au Samia mwenyewe anaweza kuona wivu badala ya kuona Fahari kuwa alikuwa ni sehemu ya miaka mitano ya Magufuli.

Ndio maana ile sauti anayoisikia Rais Samia haikomi. Itaendelea kumlilia na kumkumbusha kutimiza miradi lakini aifanye kwa haki isiwe kana kwamba anaona ana kivuli cha Magufuli. Magufuli akishangiliwa haina maana nay eye hatoshangiliwa; sifa za Magufuli zikiimbwa haina maana za kwake na timu yake hazitaimbwa. Ikulu ya Dodoma wangeachiwa haya ingekuja 2050! Labda wajukuu zao ndio wangeweza kuthubutu! Kama kwa miaka arobaini walichofanikiwa ni kile kilichokuwepo kabla ya Magufuli basi hawa wangeendelea kutenga bajeti ya kula tu kwa kisingizio cha kupanga makao makuu.

Hili ni swali la kwani wakimpa sifa Magufuli wao watapungukiwa naamini bado linahitaji majibu muafaka kwa wakati huu. Ni swali ambalo kama halitajibiwa vyema basi tutajikuta tunaendelea kuliuliza hata kama ni kwa kung’ong’a. Lakini kama siyo wivu, kama siyo kisirani, kama siyo kukereka na kivuli cha Magufuli basi ndugu zetu hawa waanze kuwa wa kweli; mnyonge mnyongeni sifa zake mpeni; hata kama mnaona zinawapunguzia zenu. Siyo ndivyo haki yenyewe hiyo.

Kwa hiyo basi natangaza hadharani, Ikulu na uamuzi wa kuharakisha kuhamia Dodoma sasa hivi na maendeleo yote ya ujenzi tunayoyaona ni matokeo ya uthubutu, maono, na kujituma kwa Rais wa Awamu ya Tano John Joseph Pombe Magufuli. Mchango wake haulinganishwa na Rais mwingine yeyote kabla yake na baada yake. Anayebisha asimame. Wangekuwa na uwezo na uthubutu huo; wangekuwa wamehamia Dodoma miaka 40 nyuma!

Niandikie:klhnews@gmail.com
 
Kutoka moyoni kabisa, jiwe ameirudisha nchi hii miaka 50 nyuma . Ameinajisi nchi hii kiasi kwamba ktk muda wa miaka 5 amejenga nyufa za kijamii, kisiasa na kiuchumi

Matatizo ya kiuchumi tunayopitia Sasa yametengenezwa na jiwe. Aliwachukia wafanyabiashara kwa kiasi kikubwa hata akatamaka hadharani kuwa wataishi kama mashetani.

Kauli ya kishenzi na kifedhuli kabisa. Mpuunzi mkubwa huyu. Hakujua kuwa hawa ndiyo miyo ya uchumi na watoa ajira wakubwa. Ndiyo mpk leo mama anahangaika kuurejesha uchumi ktk mstari.

Kijamii na kisiasa kila mtu anajua jinsi jiwe alivyoivua nguo nchi hii. Kwahiyo siandiki kitu.

Kumsifia jiwe kunahitaji mtu kuwa na roho ya usherani
 
View attachment 2642893
Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna watu ambao tunawakumbuka kwa umahiri na weledi katika kazi, vipaji au matendo yao. Michael Jordan aliichezea timu ya mpira wa vikapu ya Chicago Bulls na kujionesha kuwa ni mchezaji bora Zaidi wa mchezo huo duniani. Wengi wanalijua jina la Michael Jordan lakini ni wachache wanaweza kukutajia majina ya wachezaji wenzake wanne waliokuwa wanaunda kikosi cha kwanza. Hili pia ni kweli kuhusu mchezaji bora Zaidi wa soka duniani Pele. Wengi wanalijua na kukumbuka jinsi Pele alivyoongoza Brazili kwenye makombe ya dunia. Ni wachache sana wanaweza kukutajia wachezaji kumi wengine walioshinda na Pele kombe la dunia mara ya mwisho.

Hata hapa Tanzania kuna watu wanakumbukwa kwa umahiri wao lakini ni wachache wanaweza kukutajia majina ya watu wengine kwenye vikosi vyao. Mbaraka Mwinshehe, Marijan Rajabu, au hata Remmy Ongara. Tunajua nyimbo zao, tumewahi kuzisikia lakini tukiuliza wana bendi wenzao ni kina nani ni wachache wanaweza kutaja hata majina mawili.

Ukweli ni kuwa kuna watu wanatokea katika fani mbalimbali na wanakuwa vinara na bora kuliko wengine. Tunapowataja hawa wengine na kuwasifia haina maana tunadharau mchango wa wengine. Ukimtaja Lionel Messi kwa mfano au Cristiano Ronaldo mara moja watu watajua unawazungumzia kina nani lakini ni wachache wanaweza kukutajia majina ya wachezaji wenzao kwenye zile timu zilizokuza majina yao. Unaposema sifa za vinara haina maana unafuta sifa au unadharau sifa za wengine!

Juzi wakati wa uzinduzi wa Ikulu mpya ya Dodoma ambayo sasa inaifanya Ikulu ya Dar-es-Salaam kuwa Ikulu Ndogo kuna watu walisimama na kumwaga sifa mbalimbali. Niliamka mapema (huku niliko) niweze kushuhudia kama watakuwa na ujasiri wa kumtaja mchezaji kinara aliyewafanya wawepo pale siku ile. Bahati mbaya karibu kila aliyesimama ama alinyemelea kulitaja jina la mchezaji huyo bora au alilitaja kama kulipita tu kuwa “alikuwa ni mmoja wa timu”.

Jina la Joseph Pombe Magufuli, kinara wa marais wote waliowahi kutokea Tanzania, shujaa wa uthubutu, na mbunifu wa maono ya maendeleo ya haraka lilitajwa kana kwamba na yeye alikuwa na mchango kama wengine tu. Yote hiyo ilifanywa kwa makusudi kabisa wakijaribu kufifisha jina hilo na hawakutaka kusikia makofi na shangwe ambazo wangelitendea haki zingesikaka. Waliogopa kuona kuwa yumkini huyu bwana akiwa amelala kaburini milele kuna watu wanamkumbuka na kummiss!

Wanatuambia kuwa mpango wa kuhamishia Ikulu ulianza toka miaka ya sitini na hatimaye maamuzi yakachukuliwa na taratibu hatua mbalimbali zilianza kuchukuliwa ili kuhamia taratibu Dodoma. Jakaya Kikwete akatupa stori kuwa aliagiza watu waende Malaysia waone mambo yanavyofanyika huko na sisi tuje kuiga. Sikumbuki kwa miaka kumi ya Kikwete kama kuna siku ulifanyika mjadala hata mmoja Bungeni wa jinsi ya kuhamia Dodoma na kujenga Ikulu Dodoma na kuwa aliwaambia Watanzania kuwa ametuma iende Malaysia! Sijui hiyo timu iliongozwa nan ani! Lakini tunakubali.

Tunaambiwa kuwa viongozi wote waliotangulia wamekuwa wakifanya kama kupokezana vijiti kuliongoza taifa. Wanasahau kuwa Magufuli hakumwachia Samia kijiti; kamwachia gogo! Ni wazi Rais Samia anajitahidi kwa uwezo wake wote kuonekana anaweza kukamilisha miradi hii yote; na kweli tunaona ikimalizwa. Lakini ndugu zetu hawa wanataka tuamine kuwa kama Magufuli asingefanya alivyofanya leo tungekuwa na Ikulu Dodoma au Mji wa Serikali, au miradi hii mingine mikubwa siyo tu ya kimkakati kama inavyoitwa bali ya uthubutu uliopitiliza.

Yaani, kwa miaka Zaidi ya arobaini hawa jamaa walishindwa kuhamia Dodoma walikuwa wanalipia vipindi vya CDA hata sijui tulikuwa tunaambiwa nini. Kwa miaka arobaini walikuwa wanajipanga, na kuandaa ramani, na kuandaa warsha na semina. Kwa miaka arobaini wanaenda Dodoma, usiku usiku wanawahi kurudi Dar, kwa miaka arobaini wanaimba “Dodoma Dodoma” lakini kila wakiama ni “Dar, Dar”.

Akaja Magufuli akasema maneno matupu hayaliwi na upepo haufungwi kanga! Akawakimbiza mchakamchaka watu wazima na majasho hadi kwenye kucha; mambo yakaanza Kwenda. Yaani, yaliyowashindwa kwa miaka arobaini mtu kayaweza kuyasukuma kwa miaka mitano! Halafu wanatuambia “na sisi tulicheza”. Wanasema kweli Pele alifunga goli lakini sisi tulitoa pasi; wanasema Lionel kachukua kombe la dunia lakini sisi tulimbeba! Hatutaki kuwakumbuka!

Sasa wameamua tu kuwa hawamtaja Magufuli kwa sifa zake; hawatamtaja kwa uthubutu wa barabara, meli, mashule, madaraja. Yaani, kuna watu walijenga daraja moja kubwa kwa miaka kumi halafu anakuja mtu anajenga Matano wanajilinganisha naye! “Na sisi tulijenga barabara na sisi tulijenga daraja” msimpe sifa sana yule; alikuwa ati wa kawaida tu. Ni wivu gani huu?

Hivi kweli wakisema sifa za Magufuli kwa haki kabisa, na kusema kuwa alikuwa ni mchezaji nyota wao watapunguziwa sifa zao? Hivi watakapoenda kuwasha umeme wa Bwawa la Nyerere si wataanza kutupigisha stori tena kama za Ikulu! “Oh hili wazo lilikuwa la Nyerere, na sisi wengine tukapokezana vijiti”! Hivi mkimpa sifa Magufuli anazostahili nyinyi mtapungukiwa? Mtaonekana mnamshusha Samia? Au Samia mwenyewe anaweza kuona wivu badala ya kuona Fahari kuwa alikuwa ni sehemu ya miaka mitano ya Magufuli.

Ndio maana ile sauti anayoisikia Rais Samia haikomi. Itaendelea kumlilia na kumkumbusha kutimiza miradi lakini aifanye kwa haki isiwe kana kwamba anaona ana kivuli cha Magufuli. Magufuli akishangiliwa haina maana nay eye hatoshangiliwa; sifa za Magufuli zikiimbwa haina maana za kwake na timu yake hazitaimbwa. Ikulu ya Dodoma wangeachiwa haya ingekuja 2050! Labda wajukuu zao ndio wangeweza kuthubutu! Kama kwa miaka arobaini walichofanikiwa ni kile kilichokuwepo kabla ya Magufuli basi hawa wangeendelea kutenga bajeti ya kula tu kwa kisingizio cha kupanga makao makuu.

Hili ni swali la kwani wakimpa sifa Magufuli wao watapungukiwa naamini bado linahitaji majibu muafaka kwa wakati huu. Ni swali ambalo kama halitajibiwa vyema basi tutajikuta tunaendelea kuliuliza hata kama ni kwa kung’ong’a. Lakini kama siyo wivu, kama siyo kisirani, kama siyo kukereka na kivuli cha Magufuli basi ndugu zetu hawa waanze kuwa wa kweli; mnyonge mnyongeni sifa zake mpeni; hata kama mnaona zinawapunguzia zenu. Siyo ndivyo haki yenyewe hiyo.

Kwa hiyo basi natangaza hadharani, Ikulu na uamuzi wa kuharakisha kuhamia Dodoma sasa hivi na maendeleo yote ya ujenzi tunayoyaona ni matokeo ya uthubutu, maono, na kujituma kwa Rais wa Awamu ya Tano John Joseph Pombe Magufuli. Mchango wake haulinganishwa na Rais mwingine yeyote kabla yake na baada yake. Anayebisha asimame. Wangekuwa na uwezo na uthubutu huo; wangekuwa wamehamia Dodoma miaka 40 nyuma!

Niandikie:klhnews@gmail.com
Kumbe bado hupogo tu? Nimeona mwamba GT MTAZAMO amekuwa wa kwanza kulike.
 
Kutoka moyoni kabisa, jiwe ameirudisha nchi hii miaka 50 nyuma . Ameinajisi nchi hii kiasi kwamba ktk muda wa miaka 5 amejenga nyufa za kijamii, kisiasa na kiuchumi

Matatizo ya kiuchumi tunayopitia Sasa yametengenezwa na jiwe. Aliwachukia wafanyabiashara kwa kiasi kikubwa hata akatamaka hadharani kuwa wataishi kama mashetani.

Kauli ya kishenzi na kifedhuli kabisa. Mpuunzi mkubwa huyu. Hakujua kuwa hawa ndiyo miyo ya uchumi na watoa ajira wakubwa. Ndiyo mpk leo mama anahangaika kuurejesha uchumi ktk mstari.

Kijamii na kisiasa kila mtu anajua jinsi jiwe alivyoivua nguo nchi hii. Kwahiyo siandiki kitu.

Kumsifia jiwe kunahitaji mtu kuwa na roho ya usherani

Hapa nakubaliana na Pascal Mayalla kwamba kuwa CHIZI sio lazima uonekane mtaani ukiokota makopo
 
Mwisho wa siku hizo hela zilizotumika/zinazotumika kujengea hiyo moundombinu, ni kodi za Watanzania! Ni mikopo ambayo italipwa na watanzania wote!

Na siyo hao wanasiasa unaotaka wapewe acknowlegment.


Swali linakuja kwanini hao wengine hawakutumia hizo kodi za wananchi kufanya hayo mambo kwa miaka yote 40? Au kodi ilianza kukusanywa kipindi cha JPM?
 
Hakuna aliyeweza kuhitimisha na kujibu kwa ufasaha na busara kama Mzee wetu, Rais mstaaf.....nanukuu



"...Nilipata matatizo sana ya fikra, utadhani Kijana hafi...."

"...Miongoni ya mambo aliyotuachia:Jambo la kwanza, nalo ni kubwa ni pale alipofanya kijana huyu, alipoamua kutekeleza maagizo ya Baba wetu wa Taifa Marehemu Mzee Nyerere..."

'...amewaza na kuamua tuhamie Dodoma, nakutekeleza hilo kwa miaka miwili, jambo ambalo sisi wengine tulichukua miaka arobaini, bado hatujatekeleza, amefanya jambo kubwa sana!..."


~Ali Hassan Mwinyi, Raisi mstaafu wa Tanzania.
 
Swali linakuja kwanini hao wengine hawakutumia hizo kodi za wananchi kufanya hayo mambo kwa miaka yote 40? Au kodi ilianza kukusanywa kipindi cha JPM?
Una uhakika hawakufanya? Na kama wangekuwa hawajafanya chochote, hii nchi ingekuwepo hapa tulipo?

Unayafahamu mambo yote aliyoyafanya Nyerere tangu alipoichukua nchi kutoka kwa Wakoloni?

Tatizo mnalazimisha wote tuamini kama huyo JPM wenu alikuwa ni the best, kumbe wengine tunamuona alikuwa ni the worst.
 
Back
Top Bottom