Swali Chovu: Mabati Yenye Kutu Mijini...

Swali Chovu: Mabati Yenye Kutu Mijini...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
34,240
Reaction score
44,487
Hivi tukiweza kuondokana na mabati yenye kutu, yaliyochoka tutakuwa tumeondokana na alama kubwa ya miji yetu? Tunaweza kufanya nini kuhamasisha watu kuezeka kisasa? Inawezekana kuondoa bati hizi bila kuvunja nyumba zilizochoka? Kuna uwezekano miaka 25 toka sasa bado tutakuwa na nyumba hizi kama vivutio vya watalii?

Chama Tawala kina agenda yoyote kubadilisha mwonekano wa miji yetu?
 
Karibu Mkuu.Naona umekuja Likizo umekuta hali ni ile ile.Chama tawala hakiwezi kuwa na ajenda mpya juu ya...maana ni kilekile bado.
 
Hapo ni wapi? Mi nilikuwa rooftop na Mjita wangu 😉.


IMG_1119.jpeg
IMG_1116.jpeg
IMG_1115.jpeg
 
Hivi tukiweza kuondokana na mabati yenye kutu, yaliyochoka tutakuwa tumeondokana na alama kubwa ya miji yetu? Tunaweza kufanya nini kuhamasisha watu kuezeka kisasa? Inawezekana kuondoa bati hizi bila kuvunja nyumba zilizochoka? Kuna uwezekano miaka 25 toka sasa bado tutakuwa na nyumba hizi kama vivutio vya watalii?

Chama Tawala kina agenda yoyote kubadilisha mwonekano wa miji yetu?
Hata hili tunailaumu serikali! Wenye nazo si wapige rangi au wabadili mabati.
 
kwanza kwa nini mabati kwenye mji wenye joto kali kiasi hicho? kwa nini nyumba zilizojengwa na wakoloni zile ambazo ni za serikali hakuna hata moja waliwezeka mabati? hata tu zile nyumba za wafanyakazi wa chini kama magomeni kota au hata chang’ombe zote mkoloni aliweka vigae, why? Kila mahali waliezeka vigae, kwa nini mnafikiri? nani alileta mabati kwenye mji wa joto kama dar ? Jibu ni simple science, bati ni kipitisho kizuri cha joto tulifundishwa tangia shule ya msingi …
 
Hatuna utamaduni wakupiga rangi mabati wala service ya hizi roofs, japo shida kubwa ni umasikini na huwezi kulaumu hawa raia.
 
Una maanisha hizi Nyumba sio?
 

Attachments

  • Screenshot_20240730_174321_Samsung Internet.jpg
    Screenshot_20240730_174321_Samsung Internet.jpg
    595.7 KB · Views: 30
Tatizo ni Wahandisi Uchwara, Daaslam kuna asili ya chumvi chumvi wakoloni walibuni mabati/asbestos kukabiliana na kutu na baadhi ya maeneo walitumia zege na Vigae.
Wenzetu hawa Wahandisi wanashinda kununua Chopa za Rais badala ya kubuni mabati yasiyoshika kutu.
 
Kutu au rust hutokana na pale pati linaporeact with oxygen and water,hii chemical reaction huitwa Oxidation,

Hii process ndio hula bati na ndio husababisha visible rust on the "bati" surface,

Je kuna haja ya manufacturer wa haya mabati kuangalia upya materials au aina ya coating wanazotumia ili kuprevent hizi kutu? Je hua kuna maelezo kua bati linatakiwa lipigwe rangi kila baada ya muda gani? Yani sio mtu asubiri mpaka bati lionyeshe kutu ndio apige rangi,

Je kuna haja ya Serikali kuondoa kodi katika makampuni yatakayoleta mbadala wa haya mabati ili isiwe mzigo kwa wananchi kwa kuuzwa kwa bei kubwa?

Kwa mtazamo wangu hii style ya kuezeka mabati juu ya Nyumba ilishapitwa na wakati,ni nadra sana kukuta nchi nje ya Africa,Nyumba zimeezekwa kwa mabati.
 
Back
Top Bottom