Mkuu Kiranga! Opposition inaweza kuwa ya uchungu, lakini ikiwa ni ya hasira inaweza isifikie matarajio yake na ya jamii, au madhara yake yakawa ya hasi isiyo na tija. Kama Red Brigade ya Chadema ni "blunder", alternative yake ni ipi katika mazingira ya kisiasa yaliyopo?
Pili, seriousness ya opposition unai - define vipi... maana tunao wanasiasa wa upinzani wanaoonyesha uwezo mzuri wa kuchanganua na kukosoa mambo. Na hata Chadema ikichukua dola uwezekano wa kupata mabadiliko/mapinduzi ya nguvu katika kipindi kifupi halitakuwa jambo rahisi, unless tukubaliane kuwafurusha watu wengi tu kwa kuwapeleka kunako ahera !
Nimesema hapo awali kwamba sifagilii vi militia vya vyama vya siasa, vyote, si Red Brigade wala Green Guard wala Blue whatever. Nakumbuka polisi walishavipiga marufuku. Ila tatizo polisi (policcm kama wanavyoiita wafuasi wa CHADEMA, not without reason) inafanya kazi kwa kuogopa CCM. Hence wamepiga mkwala, halafu wanaona CCM wanaendeleza vi militia hivi, wanashindwa kusimama thabiti kusema vifutwe vyote. Matokeo yake vinaachiwa.
Sasa basi, maadam vi militia vimeachiwa, I am all for fairness. Kama CCM wanaweza kuachiwa wawe na Green Guard, CHADEMA nao waachiwe wawe na ki-militia chao.
Kwa hiyo kimsingi mimi sina tatizo na idea ya CHADEMA kuwa na militia ya ulinzi wao. Actually kama mtu ninayeamini katika watu kuchukua jukumu la kujilinda wenyewe na kutoitegemea serikali, ningewaona wapumbavu kama wangekuwa wanapigwa mabomu kila siku halafu wanasema "hewalla" tu wasingefikiria kujiimarisha kwa ulinzi.
Tatizo langu liko sehemu ndogo sana, lakini linabeba uzito mkubwa sana.
Hili jina la Red Brigade. Kwangu mimi jina hili halina tofauti na Al-Qaeda. Na kama Matanzania ambaye najua kuna Watanzania wenzangu wameuawa kwa ugaidi wa bomu la Al-Qaeda liliopiga ubalozi wa Marekani 1998, na ninayepinga ugaidi kokote duniani, kusikia chama ambacho kina "a real chance" ya kuchukua madaraka Tanzania kinaiita security organ yake "Red Brigade" kunanikera. Kwa sababu kunamaanisha ama wana endorse ugaidi, au ni ignorant hawajui historia ya hilo jina. Tumeona kwamba Dr. Slaa kaja hapa kusema kwamba anajua historia ya hilo jina, na alivyokuwa anasoma sheria Italy maprofesa walikuwa wanaleta kesi za Red Brigade kufundishia, sasa kwa nini kutumia jina hili? Majina yameisha? This was really immature. Na inaumiza kabisa kwa sababu CHADEMA si chama cha briefcase kinasubiri uchaguzi, ni chama chenye mass appeal.
Seriousness inaanzia hapo kwenye kuchagua jina la security organ. Watu walio serious na kuongoza nchi, wako conscious na image ya chama, hawataki chama kionekane cha kigaidi gaidi, hawawezi kuipa security organ ya chama jina la "Red Brigade".
I would expect watoto wa shule kama pale Tambaza niliposoma, in their youthful indiscretion, kuunda vikundi na kuvipa majina kama haya ya "Red Brigade", they could later discount that as a youthful experiment, a phase in life.
Hawa CHADEMA ni watu wazima, wasomi, kuna ma prominent lawyers, ma doctors of philosophy, imekuwaje wamekubali kujipaka mashonde bila sababu?
Is that what you call a serious opposition?