Sobby Kwa mtazamo huo jee ni CCM iliyoyafanya hayo au ni TANU?.,CCM inayo legitimacy ya kujiita Chama cha Mapinduzi bila kufanya mapinduzi yoyote?.Soma Azimio la Arusha.......
Ndipo utakapojua maana ya "Mapinduzi"
Tumeonewa kiasi cha kutosha, tumenyonywa kiasi cha kutosha,
na tumepuuzwa kiasi cha kutosha. Unyonge wetu ndio uliotufanya
tuonewe, tunyonywe, na kupuuzwa. Sasa tunataka mapinduzi;
mapinduzi ya kuondoa unyonge ili tusionewe tena, tusinyonywe tena ......
Namimih, lengo la zuio lile ni kuinusuru CCM na kashfa za jf, hapa kuna chama ukikitaja ni kusifiwa tuu kwa kwenda mbele na kuna chama ukikitaja kinakandiwa kwa sana. Lengo ni kwa watetezi wa CCM na sio wabondaji.Ndugu yangu usianzishe mada halafu unaweka condition za kujibiwa au kutoa maoni, kwani hapo nyuma kabla ya CCM unakumbuka kama kulikuwa na TANU na ASP, sasa kama ASP ilipindua huko zanzibar kwa msaada mkubwa sana kutoka upande wa bara ambao ni TANU, huoni baada ya kuungana waliona ni bora iwe chama cha mapinduzi hayo ya Zanzibar ambayo kwa pamoja yakaleta Tanzania, ni mawazo tu.
Mkuu, TANU ndiyo CCM.Sobby Kwa mtazamo huo jee ni CCM iliyoyafanya hayo au ni TANU?.,CCM inayo legitimacy ya kujiita Chama cha Mapinduzi bila kufanya mapinduzi yoyote?.
Wanabodi,
Wakati CCM ikijiandaa kusheherekea miaka 35 ya tangu kuzaliwa kwake hapo Februari 5 mwaka huu, hebu watetezi wa CCM humu jamvini nawaombeni mnielimishe, hivi hii CCM ambayo ni Chama Cha Mapinduzi, hivi kiukweli bila kutia chumvi , Jee CCM ni chama cha mapinduzi yepi?. Kimefanya nini kustahili kuitwa Chama cha Mapinduzi au ni jina tuu?!.
Angalizo!. Kama na wewe hujui CCM ni chama cha Mapinduzi ya kitu gani haswa naomba usijibu kitu wala usikibeze CCM, jinyamazie kimya ukisubiri wanaojua CCM ni Chama cha Mapinduzi yapi watuletee majibu!.
Wasalaam
Pasco (wa Jf).
Kwani chama hiki kimeitwa Chama Cha Mapinduzi? Kilipindua nini? Kilimpindua nani? Hapa kuna siri iliyonyuma ya pazia,jina hili halikuja bure tu bali lina maana fulani. Kama ni mapinduzi Zanzibar! Huku bara kinahusika vipi? Kilipindua nini? Nini siri ya Nyerere?
mara nyingi tumekuwa tukiiongelea ccm katika hali mbalimbali ,ninafahamu ukitafuta historia ya ccm huwezi kuitenganiasha na tanu,katiba ya tanu imebeba madhumuni yote ya azimio la arusha ambalo ni azimio la utu swali,je unakuweje ccm inaitwa chama cha mapinduzi baada ya kukiuka misingi ya azimio la arusha misingi ya utu? au ni mapinduzi gani haya?