Swali: CCM ni Chama Cha 'Mapinduzi' Yepi?

Swali: CCM ni Chama Cha 'Mapinduzi' Yepi?

Hili hawawezi kujibu hili
Wazo zuri sana..! Hata mie najiuliza CDM ni chama cha demokrasia gani. .. Yakupiga matofari wanao whistleblow! Kuonekana msaliti unapo tumia haki yako ya kikatiba ya kuchagua na kuchaguliwa!
 
hata hiyo CDM ikikomaa itakuwa CCM kwani hiyo D iliyochomekwa hapo kinafiki ni alfabet inayofata baada ya C, hivyo tusitegemee mabadiliko makubwa.
 
Ndugu wana janvini naombeni kuuliza. Nimezinduka usingizini majira ya saa 11 alfajiri nikawa natafakari juu ya mstakabari wa TZ yetu juu ya huu mchakato wa katiba. Nikaanza kujiuliza hoja zinazovutaniwa juu ya wanasiasa. Lakini mwishoni nilijikuta nazama kwenye msingi wa jina la chama cha mapinduzi.

Hili lilinifanya nifikirie pia majina ya vyama vingine lakini nilikuta kidogo yanajieleza lakini kiukweli sikupata undani wa jina la "chama cha mapinduzi". Hivi ni mapinduzi yalifanywa au yanatarajiwa kufanywa? Nisaidieni ufafanuzi tafadhali.
 
... Mimi Ni Kada Wa Chama Kwa Siku Nyingi Sasa Kwahyo Najua Ninachokwambia, Ukweli Ni Kwamba, Ccm Manake Ni Chama Kinacho Pindua Mambo Ya Uharisia Na Kuwa Uwongo, Ni Chama Kizuri Sana Mkuu
 
Mapinduzi ya kupidua uwongo kuwa kweli na kweli kuwa uwongo ndio kazi ya ccm
 
CCM kama Chama si kibaya, walio wabaya ni watendaji na viongozi wake. Ni viongozi na Watendaji ambao wamekidhalilisha Chama cha Mapinduzi na kukifikisha mahali kilipo. Kama tunavyoongelea Chadema na Ukabila, Chadema kama chama si cha Kikabila, ila ni uongozi ambao umefanya kionekane kuwa ni cha Kikabila, same with CCM na Ufisadi. Viongozi na watendaji wengi wa CCM, hawafuati kwa undani imani ya Chama chao, ndio maana kinaonekana kupoteza mwelekeo. Kinachoipa CCM nguvu ni wanachama wakweli, Wakulima na Wafanyakazi ambao wamekuwa katika chama na kushuhudia uimara wake, na bado wanasubiri siku ya nuru ambapo kitarudia hadhi na heshima yake.
Mchungaji heshima kwako,ila naonmba tupishane kidogo.Ulichondika ni dhambi nyingine ya kutojua na inapotosha wengine wengi zaidi.Hii ndio maana makanisa yetu hayajui wapi si sehemu ya kukomboa watu na wapi wamejiweka ktk kuwa ukuta wa kuwashikia watu ktk mateso.Hawa watu unaowashikilia wanamkufuru Mungu zaidi ya unavyojaribu wafanya wamtukuze na kurudishia heshima yake ktk maisha yao. UNAFAHAMU KABISA KTK DEMOCRASIA WENGI HUWEZA BADILI MAMBO,SASA KM SHERIA ZA CCM ZILIRIHUSU KUANGUKA KWA NIDHANI KIASI CHA VIONGOZI NA WANACHAMA WAO WAKAAMUA ISHI KTK UVU BILA YEYOTE KUONA KUWA KAVUNJA SHERIA.NI WAZI NAO SASA NI WENGI KIASI CHA KUIFANYA CCM IFANANE NAO.CCM HAIWEZI KUWA NZURI KM IMEZAA ZAIDI YA NUSU YA WATU WABAYA,NA KUWAPA HAO WABAYA NAFASI YA KUKIPAMBA NA KUKIPA CHAMA SURA.UHAI WA CHAMA NI WATU NA CHAMA KINAKUWA NA MVUTO KM KILA KITU CHAKE KINAFANYA KAZI YA MATAMANIO YA WAOVU.
 
Niliwahi andika kitu hapa ila Mods na wengine hawakuwa wamekomaa kiakili wakachukulia km mizaha na kitu cha kuchanganya na vingine.Mapinduzi ni mageuzi,ila kuna mageuzi ya kuhama ktk Kitu fulani na kuingia ktk kingine tofauti kabisa.Ila kuna mapinduzi ya ku "overthrow" utawala fulani.CCM imefanya hiyo kazi ya kupindua viongozi Africa km vibaraka wa Ukomunist na wachina kwa gia ya ukombozi.Kwingine si kweli.Ingawa over time kuna wengine baada ya kuingizwa waligeuka na kuchukua taswira inayoendana na ukombozi.
 
Wakuu hebu nipeni ushauri.
Kwani ni mapinduzi gani ambayo C.C.M(Chama Cha Mapinduzi) hakijatimiza.
Si ingekuwa bora wakiite moja kati ya:
*Chama Cha Maendeleo.
*Chama Cha Mwananchi.
*Chama Cha Matajiri
*Chama Cha Maskini
 
kiongozi umeongea maneno mazuri na matamu sana. Lakini hayana msingi kwa maana historia unayo itoa imeacha vitu vingi sana nje ya uwanja ambao wewe unataka mada ifike kwa jamii, nyanja unazoziongelea ccm imefanya mapinduzi makubwa sana,tukianzia katika siasa, kujenga mfumo wa demokrasia, ingawa mapungufu yapo, uchumi umekua kulinganisha na matatizo mengi ambayo tumepitia katika vita, SAPs conditions ukipitia matukio yote hayo unaweza kufahamu jinsi gani ccm imefanya kuirudisha nchi katika mahala salama,kijamii, ccm imefanikiwa kujenga tanzania moja isiyo na ukabila wala udini ispokuwa watu wachache wanataka kuyavunja hayo kwa kuleta ukanda, kukashifu dini nyengine{ gwajima}. tukio lakimanduzi zaidi ambalo mimi kama mtanzania naweza kujivunia kwa ccm kwa kipindi hiki cha uchaguzi ni kuvunja mfumo m'bovu ambao ulikuwa umejengeka ndani ya ccm kutokana na watu wachache ambao walitumia fedha kukiharibu chama, chama kikawatoa kuhakikisha kila mwanachama awe na haki ya kupata nafasi nasio utawala wakichifu ambao ni lazima fulani awe kiongozi, swali kwako inakuaje unahubiria kitu ambacho chama cha ccm kimepambana kwa muda mrefu mpaka kimefanikiwa kuondoa uozo huo, chakushangaza wewe unawakumbatia watu wa aina hiyo, ambao wanatumia hela kutafuta ikulu kinguvu.jipange kama utakua unataka kujua nchi inaendaje rudi shule ukasome usije na mada ambazo kama ungesoma usinge iweka mezani kwasababu historia inaeleza wapi tulipokua, kwa sababu gani, na hapa tulipo na tunapoelekea.
 
Hahahaha inafurahisha sana kuona mtu ambae mwaka 1997 ulikua kidato cha tatu unakuja na mada ambayo haina mashiko kwa sababu kama kipindi tajwa ulikua kidato cha tatu niwazi mapinduzi ya nyanja ulizotaja unayafahamu, kuliko sisi ambao historia tumeisoma kwenye vitabu,lakini kwa kukusaidia linganisha miaka ambayo ulikua hicho kidato na sasa hivi kuna ufanano wowote, katika nyanja ambazo unatumia kama sababu zako katika kuonyesha juu ya hakuna kilichofanyika. njoo na mada yenye uhitaji wa tafakuri katika kujenga nchi sio hadithi za sungura na fisi kuleta ujanja ujanja tuh ili kuyumbisha Watanzania
 
Tarehe 5 mwezi februari mwaka 1977 nikiwa mwanafunzi wa Form 3, nilikuwa mmojawapo wa waliochukuliwa kutoka shuleni kwetu kuunda gadi moja ya kucheza halaiki tukishirikiana na wanafunzi wa shule za msingi.

Katika hotuba yake Mwalimu Nyerere aliyoitoa kutokea uwanja wa Aman kule Zanzibar alituahidi kuwa waliamua kuunganisha vyama vya TANU na ASP ili kuunda chama kiomoja chenye nguvu kitakacholeta mapinduzi ya haraka kiuchumi, kisiasa na kijamii kwa watanzania wote. Wakati huo TANU ilikuwa imefikisha umri wa miaka 23 wakati ASP ilikuwa na umri wa miaka 20 tu. Katika kipindi cha uhai wa vyama hivyo vya TANU na ASP vilikuwa vimeshaleta mafanikio makubwa sana nchini. Vyote viliondoa ukoloni nchini na vilikuwa vimeshaanza kuboresha maisha ya mtanzania. Vilijenga mazingira ambamo wanachi walikuwa wanajivunia nchi yao na viongozi walikuwa wanajua kuwa wao ni watumishi wa wananchi; malalamiko ya wananchi yalikuwa yakichukuliwa kwa uzito sana na ule msingi wa CHEO NI DHAMANA ulikuwa na uzito sana.

Leo hii ni miaka 31 tangu CCM izaliwe; huo ni umri mkubwa sana zaidi ya ule wa vyama vilivyoizaa. Mazingira yaliyojengwa na chama hiki ni yale ambamo wananchi hawana imani na utawala, na vile vile watawala wamekuwa hawaogopi malalamiko ya wananchi. Yote hayo kwa pamoja yameondoa uzalendo kabisa miongoni mwa watu wetu ambapo, viongozi wetu bila woga wanaweza kusaini mkataba wa kukodisha yetu kwa mtu mwingine milele!! !!. na mtu akiuliza kulikoni, basi anapewa vitisho vikali.

Mfano mzuiri ni hili tishio lililotolewa na Katibu Mkuu wa CCM dhidi ya kijana Nape Nnauye kufuatia tamko lake kuhusu ufisadi ndani ya UVCCM. Tihio hilo linaonyesha jinsi gani chama hicho kinavyoheshimu mafisadi na kuwapuuza wananchi tofauti na ilivyokuwa wakati wa TANU na ASP. Kwa nini Makamba amtishie kijana yule badala ya kumtaka alete ushahidi ili yeye (Makamba) aweze kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya watuhumiwa hao badala ya kutoa onyo kabla ya kuangalia ushahidi unasemaje. Huko siyo kujenga mazingira ya mapinduzi.

Ndiyo maana najiuliza, je kweli chama hiki bado ni chama cha Mapinduzi yale tuliyoahidiwa mwaka 1977?
ccm bado ni chama cha mapinduzi kwa sababu kimefukuza mafisadi wakapokelewa upawa,na kukumbatiwa na chadem
 
Umechelewa sana kuuliza swali hili, kama ulikuwepo ulitakiwa uulize mwaka 1977.

Tulikuwa tunaimba hivi:-

Kiongozi; CCM JUU
Waitikiaji: NDIYO, JUU, JUU, JUU ZAIDI.

Kwenye gwaride la chipukizi:-

Kamanda: VIJANA WA CCM, WI MBELE
Waitikiaji: NDIYO, MBELE, MBELE, MBELE ZAIDI, GARI LA CCM HALINA REVERSE

Swali la kutuuliza leo, ungenuliza mabadiliko tunayoyataka ni yapi? Ningekupa majibu
 
Umenikumbusha mgombea mmoja wa CCM nafasi ya udiwani kura za maoni alishindwa kutamka; Kidumu chama cha Mapinduzi badala yake akatamka; Kidumu chama cha mapipapipa😀😀
 
Back
Top Bottom