Swali: CCM ni Chama Cha 'Mapinduzi' Yepi?

Swali: CCM ni Chama Cha 'Mapinduzi' Yepi?

Well, nilipitia Chipukizi miaka hiyo - bado ninazielewa itikadi za CCM. Mapinduzi yako ya aina nyingi na siyo lazima yawe ya kuuondoa uongozi fulani na kuweka uongozi mwingine kwa nguvu.
Chama cha Mapinduzi ni chama kilichoanzishwa ili kuleta mapinduzi ya kilimo na viwanda nchini (jembe na nyundo). Tulianza kuongeza nguvu za kupambana na adui zetu watatu wa maendeleo na kujenga viwanda ikiwa ni pamoja na kuimarisha mashirika ya umma kama MECCO, ATC, TTCL n.k Katika kipindi hicho tulijenga viwanda vingi na kuongeza tija ya kilimo na mazao yatokanayo na kilimo au mifugo kama ngozi n.k
Kwa ujumla mapinduzi yanayoelezwa katika chama (CCM) ni mapinduzi ya kifikra na kiutendaji kwa maana ya kuweka misingi sahihi ya kujitegemea kama nchi. Tulikuwa na dira, dhamira na nia safi ya kuleta maendeleo ya haraka kwa jamii. " Wenzetu wako mbali hivyo kama wanatembea sisi inabidi tukimbie" - J.K Nyerere. Tuliangalie neno mapinduzi kwa maana hiyo ... kuwa ni chama kitakachotuongoza katika kubadili mfumo tuliourithi toka kwa wakoloni na kuweka mfumo mpya wa haki, usawa na maendeleo ya kisayansi na Teknolojia kwa mwelekeo wa kujitegemea. Hayo ndo mapinduzi yanazozungumzwa na chama (CCM).

Well, naomba nisiulizwe maswali tena kuwa nini kimetokea katika hizo dhamira, nia n.k.... Chama kilibadili haya mambo mwaka 1992 katika azimio la Zanzibar. Sijui kinachoendelea maana si mwanachama tena baada ya mabadiliko hayo!!

JEMBE NA NYUNDO,
KILIMO KWANZA...MAPINDUZI YA KIJANI
UHUISHAJI WA VIWANDA VILIVYOBINAFSISHWA...itafatia

Loh!
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo-
1. Kuna demokrasia gani chadema kwani wanawake viti maalumu wanachaguliwa kwa formula aliyo iandaa dr Kitila,Zitto alipogombea Uenyekiti wa Chama ikabidi Mtei na Wazee wengine wakatishia kumvulia nguo!
2. Maendeleo yepi kama Chama kinajiita kikubwa kwa Upinzani kina ruhusu wabunge wake wachukue milion 90 wakati wakijua maisha ya mtanzania yako hoi!
tatizo lako huan akili.............umeshachakachua maaada na kutuchfulia hali ya hewa lione kwanza wanazungumzia CCM umeleta habari zingiiine
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo-
1. Kuna demokrasia gani chadema kwani wanawake viti maalumu wanachaguliwa kwa formula aliyo iandaa dr Kitila,Zitto alipogombea Uenyekiti wa Chama ikabidi Mtei na Wazee wengine wakatishia kumvulia nguo!
2. Maendeleo yepi kama Chama kinajiita kikubwa kwa Upinzani kina ruhusu wabunge wake wachukue milion 90 wakati wakijua maisha ya mtanzania yako hoi!

Mkuu usiende nje ya mada,
Kilichopo sio vyama bali naitafiti neno 'mapinduzi' kutumiwa na chama tawala kwa zaidi ya miongo 3, siongelei ubora/uzuri/ubaya wa vyama vya siasa...LA HASHA!
 
Swali lina fanana nini maana ya Chadema je kuna demokrasia?

Mlengo wa kati swali halijibiwi kwa swali maana naona kiswahili si kigumu hivyo. Jibu ya ccm halafu kama una swali la chadem uliza but dont mix things
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo-
1. Kuna demokrasia gani chadema kwani wanawake viti maalumu wanachaguliwa kwa formula aliyo iandaa dr Kitila,Zitto alipogombea Uenyekiti wa Chama ikabidi Mtei na Wazee wengine wakatishia kumvulia nguo!
2. Maendeleo yepi kama Chama kinajiita kikubwa kwa Upinzani kina ruhusu wabunge wake wachukue milion 90 wakati wakijua maisha ya mtanzania yako hoi!

Nilitarajia ujibu swali kwanza kabla ya ku-raise topic nyingine
 
Waberoya, ahsante. Lakini bado hatujajua kwa nini 'chama cha mapinduzi'. Kilipindua nini? ASP na TANU si viliungana ndio kikazaliwa? Kuna wenye umri ambao watatusaidia.

Kwa wakati huo, neno mapinduzi lilikuwa pia ni tafsiri ya neno REVOLUTION na si kupindua tu (coup de etat). Kwa hiyo chama kilikuwa Revolutionary Party ambacho ukitafsiri kwa kiswahili kinakuwa chama cha mapinduzi.
 
Guys, I just told you so..... hawatajibu hoja, hawana uwezo huo na hawajazoea

Chama Cha Mapinduzi ni jina tu la chama kama ilivyo kwa CCDM (Chama Cha Demokrasia na Maendeleo), NCCR-Mageuzi, CUF,TLP, UDP etc. sasa ukitaka kufahamu maana ya kila jina la chama ina depend na mtu mwenyewe. au mtoa mada angetuambia tafsiri ya chama chake Chadema maana yake ni nini then aulize maana ya vyama vingine. Afterall, Dr WS alikua kada mzuri tu wa CCM hata Nyerere akampa udiwani wakati ule bado akiwa padre, hivyo anajua maana halisi ya CCM. So I see no point ya kupoteza muda kutafsiri acronyms za majina ya vyama vyote vilivyopo hapa nchini lets judge them by their deeds!
 
Jibu ni rahisi tu, wakati wa vuguvugu la muungano kulifanyika makubaliano ambayo ndio yalileta muungano wetu.
Moja ya kikwazo kikubwa ni kwa wazanzibar kuogopa sana kumezwa na tanganyika kwa maana ya ukubwa wa eneo na idadi ya watu, pia kuyaenzi mapinduzi yao hii ilipelekea kutaka serikali yao ya mapinduzi iwepo na chama chao kwakuwa kinaungana na tanu basi lazima neno mapinduzi liwepo ktk chama kipya ili kuenzi mapinduzi ya chama chao, hapo ndipo neno mapinduzi likaingizwa na kuwa ccm.
Hayo ndio waasisi wa muungano walikubaliana na kupelekea huu mungano wetu, usiniulize mbona tanu na tanganyika sijui nini?aah a,nimekupa sababu mengineyo nyerere na karume ndio wangeweza kujibu
 
Acheni blablah. Ina nyie wote hamkuwahi wanachama wa CCM kabla ya mwaka 1990?
Neno mapinduzi kwenye hicho chama lina maana ya revolution. Halina maana ya kupinduapindua serikali. Mwisho mtasema na ugonjwa wa kipindupindu unahusiana na kupindua.

The Chama cha Mapinduzi (Party of the Revolution in Swahili) is the ruling political party of Tanzania.

Soma hapa:
Chama cha Mapinduzi - Wikipedia, the free encyclopedia
Political party flags in Tanzania
Revolutionary Party of Tanzania (political party, Tanzania) -- Britannica Online Encyclopedia
 
Chama Cha Mapinduzi ni jina tu la chama kama ilivyo kwa CCDM (Chama Cha Demokrasia na Maendeleo), NCCR-Mageuzi, CUF,TLP, UDP etc. sasa ukitaka kufahamu maana ya kila jina la chama ina depend na mtu mwenyewe. au mtoa mada angetuambia tafsiri ya chama chake Chadema maana yake ni nini then aulize maana ya vyama vingine. Afterall, Dr WS alikua kada mzuri tu wa CCM hata Nyerere akampa udiwani wakati ule bado akiwa padre, hivyo anajua maana halisi ya CCM. So I see no point ya kupoteza muda kutafsiri acronyms za majina ya vyama vyote vilivyopo hapa nchini lets judge them by their deeds!

Mkuu, HESHIMA KWAKO.
sijajiongelea mimi ni mfuasi wa chama gani, tatizo lisiwe pale mtanzania anapohoji mambo muhimu na ya msingi basi atafsiriwe kwa itikadi ya chama anachoegemea. Naomba urejee thread yangu, nahitaji kutoa ukungu ili nitambue maana halisi ama uwakilishi wa mtanganyika katika alama za chama tawala tangu enzi hizoooooo.
Nisaidie na tubaki kwenye mada hii.
 
Naomba urejee thread yangu, nahitaji kutoa ukungu ili nitambue maana halisi ama uwakilishi wa mtanganyika katika alama za chama tawala tangu enzi hizoooooo.
Nisaidie na tubaki kwenye mada hii.

Mkuu nimekupa sababu ya kuingiza mapinduzi ktk chama lakini sasa naona unataka na uwakilishi wa tanganyika ktk hili, hapo sasa unakwenda ktk kero za muungano ambazo ni tata na nyingi mno.
Sidhani neno mapinduzi kama ni tatitizo its only a name it doesnt effect anything, unless unamatatizo na muungano kwa mambo mengine ya msingi hapo ntakubaliana na wewe
 
Mkuu nimekupa sababu ya kuingiza mapinduzi ktk chama lakini sasa naona unataka na uwakilishi wa tanganyika ktk hili, hapo sasa unakwenda ktk kero za muungano ambazo ni tata na nyingi mno.
Sidhani neno mapinduzi kama ni tatitizo its only a name it doesnt effect anything, unless unamatatizo na muungano kwa mambo mengine ya msingi hapo ntakubaliana na wewe

Nimekusoma, ahsante.
 
Acheni blablah. Ina nyie wote hamkuwahi wanachama wa CCM kabla ya mwaka 1990?
Neno mapinduzi kwenye hicho chama lina maana ya revolution. Halina maana ya kupinduapindua serikali. Mwisho mtasema na ugonjwa wa kipindupindu unahusiana na kupindua.

The Chama cha Mapinduzi (Party of the Revolution in Swahili) is the ruling political party of Tanzania.

Soma hapa:
Chama cha Mapinduzi - Wikipedia, the free encyclopedia
Political party flags in Tanzania
Revolutionary Party of Tanzania (political party, Tanzania) -- Britannica Online Encyclopedia

Ahsante kwa hizo links mkuu,
 
Wadau,

Nimekuwa nikijiuliza na sijapata majibu murua yenye kunikidhi juu chama kinachotutawala hapa TZ.

  • Ya kwamba sioni tafsiri halisia juu ya 'mapinduzi' kutumika kwa chama hicho kinachotawala.
  • Ya kwamba je, iliwahi kutokea mapinduzi Tanganyika kupelekea neno 'mapinduzi' kuwepo kwenye alama ya bendera yao tangu enzi za mwalimu mpaka sasa?
  • Iwapo hatukuwa na mapinduzi...kwa nini neno hilo liwepo tangu enzi ya chama kimoja? Je kuna siri gani imefichika?
  • Ama neno hilo limeibeba Zanzibar na ni kielelezo cha alama ya muungano na kutambua kiitwacho mapinduzi 'MATUKUFU' ya znz?
  • Iwapo nchi yetu inatambulika ki-ngonjera kuwa ni kisiwa cha amani...kwa nini neno mapinduzi/revolution litumike kwa chama tawala toka enzi za mwalimu?

Naomba nisaidiwe ili niondoe ukungu na tongotongo waungwana, NAOMBA KUWASILISHA.

...Chama Cha Mafisadi befits them!
 
Ccm wamechoka kufikiri walichobaki sasa ni kuwaibia tu watz kukiwa mchana kweupe na wezi tunawafahamu wote na wala hatuwachukulii hatua yoyote wanatamba hii ndiyo alama halisi ya ccm na mapinduzi yake..........wametupindua watz hatuiwezi hata kudai haki zetu
 
Good News ni kuwa hawa waliomo kwenye Chama hiki na huko historia inavyojionyesha ni cha kupigania uhuru, leo hatukihitaji tena kwani tumeshajikomboa na sasa tupo Nchi huru. Muda wake wa kuwepo madarakani umekwisha kama hakitaki kujiuzulu ni lazima kwa hali yeyote ile kiuzuliwe na kuwajibishwa, wanaotaka kuendeleza siasa za kujenga nchi ambao wamo katika chama hicho kilichotukomboa kutoka kwa mkoloni wajiunge na vyama vya siasa ya kujenga nchi. Mwisho wa CCM ulikuwa ni siku ile ilipopita sheria ya kuruhusu vyama vingi vya siasa.

Hiki Chama Cha CCM ni Chama ambacho wengi wa WaTanzania walikuwa nacho na ilikuwa ndio Chama chao, habari zake zikisomeshwa hata mashule, kwa leo hakina umuhimu na kimeshafulia, kinaongoza kama kinafanya harakati za kugombea uhuru kwa mtutu wa bunduki.

Mali zote za Chama hiki ni za WaTanzania wote, kumbuka baada ya kuanzishwa kwa Vyama vingi, ilitakiwa maliza zake zote zikabidhiwe kwa serikali kwani ni mali za WaTanzania wote.
Haaa! wewe ni Mwiba au nimekosea? na kama kweli wewe ni mwiba basi nimefurahi sana kupita maelezo.
Mara nyingi tunawahubiria sana watu humu jamvini kuwa ccm ni maafa na haifai hata kwa bure.
kama wewe mwiba ushaona hilo,basi hata jeykey,topical,maralia sugu nk. nao watakubaliana na sisi tu oneday
 
Mkuu, HESHIMA KWAKO.
sijajiongelea mimi ni mfuasi wa chama gani, tatizo lisiwe pale mtanzania anapohoji mambo muhimu na ya msingi basi atafsiriwe kwa itikadi ya chama anachoegemea. Naomba urejee thread yangu, nahitaji kutoa ukungu ili nitambue maana halisi ama uwakilishi wa mtanganyika katika alama za chama tawala tangu enzi hizoooooo.
Nisaidie na tubaki kwenye mada hii.

Samahani Mpevu kama nimeenda nje ya mada na thanx kwa kunirekebisha and tuko pamoja.
 
jibu hoja kijana,
acha kuruka ruka kama jogoo,
hili ni jukwaa la great thinkers


Mlengo wa Kati
Join Date : 16th February 2011
Posts : 42
Thanks4Thanked 6 Times in 5 Posts

Rep Power : 0

Chama cha Demokrasia na Maendeleo-
1. Kuna demokrasia gani chadema kwani wanawake viti maalumu wanachaguliwa kwa formula aliyo iandaa dr Kitila,Zitto alipogombea Uenyekiti wa Chama ikabidi Mtei na Wazee wengine wakatishia kumvulia nguo!
2. Maendeleo yepi kama Chama kinajiita kikubwa kwa Upinzani kina ruhusu wabunge wake wachukue milion 90 wakati wakijua maisha ya mtanzania yako hoi!
 
Mwiba alishabadirika, tena siku hizi amekuwa mstari wa kwanza wa kuyaanika madudu ya CCM
Inaonyesha wazi kabisa kuwa watu wengi walikuwa hawajui CDM wanafanya nini na wako kwa ajiri ya nani?
Haaa! wewe ni Mwiba au nimekosea? na kama kweli wewe ni mwiba basi nimefurahi sana kupita maelezo.
Mara nyingi tunawahubiria sana watu humu jamvini kuwa ccm ni maafa na haifai hata kwa bure.
kama wewe mwiba ushaona hilo,basi hata jeykey,topical,maralia sugu nk. nao watakubaliana na sisi tu oneday
 
Naomba ufafanuzi juu ya hili jambo manake jina la chama mara nyingi kama si zote huwa ni kama kifupisho cha lengo na madhumuni yake. Sasa hiki chama cha mapinduzi kwetu MAPINDUZI maana yake nini sitaki kuamini kuwa ni Mapinduzi ya Zanzibar ndio yanayozungumziwa hapo. Tell me Greatthinkers
 
Back
Top Bottom