Sumu ya Saanene - swali kwa MASALIA a.k.a PM-7

Sumu ya Saanene - swali kwa MASALIA a.k.a PM-7

Sikonge

JF-Expert Member
Joined
Jan 19, 2008
Posts
11,635
Reaction score
6,235
Nimesoma hizi habari za Masalia na ukiunga na habari ya Zitto, unaona kabisa hii habari ya SUMU ya Panya kutumika kumuuwa Zitto imepambwa mara nyingi sana. Kwa maana nyingine, masalia wote wamekiri kwa namna moja au nyingine kuwa Saanane alikuwa na Sumu ya kuuwa Panya na alikuwa kapanga kuja kumuuwa Zitto.

Haya ni mashtaka mazito sana ambayo nina imani yataishia Mahakamani.

Swali langu kweny nyie Masalia ni hili:

Kama Zitto amesema hilo pia ila HAJAMTAJA mtu ila nyie ndiyo mmekwenda mbali zaidi hadi KUMTAJA mtu na tena kwa majina yenu kabisa, hamuoni kuwa MKIENDA Mahakamani na kuanza kurushiwa maswali mazito na mtu kama Tundu Lissu itakuwa ngumu sana kwenu kujitetea? Mtaweza kweli kujibu tuhuma zenu bila ya wasiwasi wowote kuwa Saanane alikuwa na sumu ili amuuwe Zitto?

Kumbuka tena, Zitto hajataja mtu ila nyie ndiyo mmetaja. Mwenzenu yupo upande wa pili wa mto hajavuka ila nyie ndiyo mmeshajitosa. Kuwakana au kudai ni maneno aliyoyasikia kutoka kwenu ni rahisi sana. Ila nyie mnaweza kuwekwa kikaangoni sasa hivi na mkashindwa kesi na mkaishia kulazimishwa kulipa faini kubwa tu ambayo mtakuwa hata uwezo wa kulipa hamna na muishie JELA au kulialia kwenye majukwaa ya CCM ili mlipiwe faini na Mabwana zenu wa CCM.

Nawakumbusha kuwa, NJIA nzuri kwenye bado ni kwenda kukiangukia Chama na kuomba Msamaha na kukiri yote ili mambo yaishie ndani maana vinginevyo, nina wasiwasi kuwa mwisho wenu hili swala la SUMU peke yake utakuwa ni mbaya sana. Wasikieni tu Mawakili nyie vijana mko huko nje ila ukiwekwa Kizimbani na hapo hakuna CCM wala Zitto kukusaidia, kumbukeni maneno yangu ni sehemu mbaya sana maishani. Kwa bahati mbaya sana, Kizimbani hutaruhusiwa KUMTUKANA Dr. Slaa kama njia ya kujibu maswali au kudai utetezi wako Saanane na sumu ni "Dr. Slaa na hawala yake" ingawa wote twajua ni MKE (hata adabu hamna).

You still have TIME to do the RIGHT THING. Good Luck.

Chama cha mapinduzi CCM kimesema kama chama wao hawawezi kulipa gharama ya kupinga kesi ya ubunge wa Lema kwa kuwa wao hawakuwa na mashaka na ubunge wa Lema. Kwa hiyo gharama hizo zilipwe na waliokuwa na mashaka na ubunge wa Lema.

From: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/372254-ccm-yawaruka-mussa-mkangaa-na-wenzake.html
 
Ukiwasoma kwa makini hawa vijana utagundua kuwa wanaongea mambo ambayo hawajui athari yake kwao kwa sasa na siku za usoni, tofauti na mtangulizi wao yeye alikuwa mjanja kidogo kama ulivyo sema g'wana wa mayu!
 
Yeah wawe kama Ben wajirudi na kutubu na KUACHA usaliti wao. We all make mistakes men!
 
Hiyo ni kansa tu wakafie mbali wataendelea kuisumbua chama waende kwa bwana wao CCM (magamba).
 
Sikonge Mkuu hili kundi ni machokoraa na hawana adabu kabisa!!! Cha pili wote ni kundi la zitto na wanaweza kujipanga tu kusema kuwa Ben Saanane alikuwa na sumu. Ukiangalia maelezo yao ni kama vile wameandikiana ili yawe na ufanano fulani hivi. At the same time Zitto ni mjanja sana!!! Anatumia muda huu na watu hawa kuendeleza siasa zake za kukibomoa chama!!! Cha msingi wakienda mahakamani ni lazima wawe na evidence ya sumu!!! Walimrekodi Saanane akisema hayo na the so called sumu yake!!! Machokoraaa hawa wanatumika tu. Bora Ben Saanane ameungama!!
 
Last edited by a moderator:
yes vijana wamekiuka miiko ya uongozi - matusi hadharani n.k hapo unaondoa sifa ya kuwa kiongozi bora. pia wakumbuke uasi wowote kwenye taasisi yoyote haufanikiwi unless uwe na backbone (intelligensia) thabiti vinginevyo yanatokea kama ya ile CCJ, cha msingi mtoa hoja alivyosema ni muda wa kurudi chamani - kuomba msamaha na kama kuna madukuduku basi yasemwe na kuanza kazi upya pamoja.

Hakuna dhambi isiyosameheka hata petro (kwa sisi wachache tuaminio) pia akasamehewa. maswala ya matusi kwa viongozi si mazuri na uasi ndani ya chama si mzuri -- nyie vijana ndiyo wenye chama, kuweni makini sana na watu wanaotaka kuwaharibia, vishawishi vinawafuata vijana zaidi kuliko sisi watu wazima sababu wanajua akikupa mil moja basi utaanzisha vurugu vurugu tu zisizo na maana -- kumbukeni watu wana hela nyingi sana zimetengwa kuhakikisha CDM haifiki 2014 kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.

Mbona vijana wengi tu wamepitia BAVICHA lakini wametulia -- kwa nini msiwe na matendo kama ya John Mnyika (backbone ya CDM).

DR.Slaa atapita, Mbowe atapita nyie mtatoka kwenye hilo balaza mtakuja kwa wazazi na wengine watachukua nafasi zenu -- sasa na nyie mkija kuhujumiwa na BAVICHA ya wakati huo mtafurahi chama kikawafika mikononi mwenu? guys kumbukeni machozi ya watanzania wote wapenda ukombozi yako juu yenu - msiwaangushe huu ni muda wa kujenga chama si muda wa kutishiana SUMU na kurogana.

Kama kweli una hoja ya msingi, hivi huwezi kusikilizwa ndani ya CDM? sitaki kutaja hoja zenu mlizosemana ila inaonyesha kabisa someone was behind this saga. anyway!!

Mwisho we all smile for Lema -- its good friday let go back to work for M4C guys!!

--cheers!! --
 
Sumu ni sumu,tayari taarifa hizi police wanazo na si Saanane tu,kuna viongozi watatu wa CHADEMA watahojiwa na njama zao za kumtoa uhai Zitto.

Hii insu itaondoka na watu ambao hamujawai tarajia na hapo ndipo tutakapojuwa nan mnafiki na muuaji CHADEMA.
 
hakuna msamaha dr.slaa na ben wawafikishe mahakamani hawa p.an.ya...allegations nzito sana wametoa watoto hawa,..na majaji wakiwa kama wa leo wamekwisha,hawatoki hawa hakuna huruma
 
Sumu ni sumu,tayari taarifa hizi police wanazo na si Saa nane tu,kuna viongozi watatu wa chadema watahojiwa na njama zao za kumtoa uhai Zitto.Hii insu itaondoka na watu ambao hamujawai tarajia na hapo ndipo tutakapojuwa nan mnafiki na muuaji chadema.

sijui kama utabadilishana nao gereza..hawa hawatoki na uropokaji wao..na zitto atawaruka kimanga
 
jamani, hili jina masalia limetumika likimaanisha nini?
 
naona mnatishiaana nyau.WEnzake wametangulia mahakamani
 
Back
Top Bottom