TFF Ni jipu linalotoa usha kila uchao.

TFF Ni jipu linalotoa usha kila uchao.

ilya mchele

New Member
Joined
Jul 16, 2023
Posts
4
Reaction score
8
Nmekuwa nashangaa kuona kila mechi inayokutanisha Simba na yanga kupangiwa kuchezwa visiwani Zanzibar, nadhani kwa kufanya hivyo ni kutukosea Sisi watanganyika(Tanzania bara)kwani Simba na yanga ni timu za Tanzania bara ambazo n tunu kwa watu wa bara kitendo cha kupeleka mechi za Simba na yanga Zanzibar ambako nako kuna timu na ligi yao n kutukosea Sana watu wa bara .

Jambo Hili linachafua taswira ya soka la Tanzania kwani limekaa kisiasa Sana! Mechi ipelekwe Zanzibar iwapo Tu timu za bara znakutana na timu za visiwani Zanzibar. Tanzania kuna shirikisho la soka na timu zake vivyo hivyo kwa Zanzibar.

NI wakati sasa wa mamlaka za soka Tanzania bara kuweka kanuni(Sheria) ili derby zikipelekwa Zanzibar timu ziingie mikataba na kulipwa pesa ndefu maana kitendo hicho wanachofanya saivi ni kutangaza biashara(utalii wa Zanzibar) kitu ambacho timu hzi hakizinufaishi ata kidgo. Napendekeza Kariakoo derby inapopelekwa Zanzibar timu hizo zilipwe na mamlaka/serikali ya Zanzibar maana derby imekaa kisiasa kwa lengo la kutangaza utalii Tu kitu ambacho NI hasara kwa timu hzi, pia ukiangalia derby ya Kariakoo haina fan base kubwa ukilinganisha na bara, pia ata gate collection sio kubwa kama ilivyo kwa Tanzania bara.
 
Huu uzi watu wanashindwa kuchangia kutokana na lugha ngumu iliyotumika hapo juu......."jipu linalotoa usaha" hata kama umeandika "usha" hii kitu inaleta kinyaa kilichopitoliza.
 
Back
Top Bottom