Sudan Kusini: Rais Salva Kiir amfuta kazi Waziri wa Mambo ya Nje

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
H.E._President_Salva_Kiir_Mayardit.jpg

Mayiik Ayii Deng amefutwa kazi kupitia tangazo lilitolewa kupitia Runinga ya Taifa bila kuwepo kwa taarifa zaidi za sababu ya kuondolewa kwake. Waziri huyo ni mtu wa karibu wa Rais Kiir na amewahi kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais.

Kiir amechukua uamuzi huo ikiwa ni Wiki moja tangu amfute kazi Waziri wa Ulinzi ambaye ni mke wa Makamu wa Rais wa Kwanza, #RiekMachar, uamuzi ambao umetajwa kutishia makubaliano ya amani baina ya Serikali Kuu na Upinzani unaoongozwa na Machar.

Umoja wa Mataifa (UN) umetoa wito kwa pande zote kuepusha hisia zinazoweza kuhatarisha hali ya ushirikiano uliorudisha amani kati ya Serikali na waasi kutoka upande wa Makamu wa Kwanza wa Rais.

================

South Sudanese President Salva Kiir has sacked his foreign minister, less than a week after dismissing the defence and interior ministers.

No explanation was given for the dismissal of Mayiik Ayii Deng, which was announced in a decree on the state television.

The sacked minister is an ally of Mr Kiir, and previously served as the minister in the president's office.

Last week’s sackings have threatened to derail a peace deal with opposition leader First Vice-President Riek Machar.

The opposition called for the reinstatement of Angelina Teny, who Mr Kiir dismissed as defence minister and handed the position to his party. Mrs Teny is also Mr Machar’s wife.

The UN called for the parties to "exercise restraint and engage in a collegial spirit in order to resolve such sensitive national issues”.

BBC
 
Mume makamu wa raisi, mke wake waziri wa ulinzi halafu eti hayo ndio makubaliano ya amani halafu wanawadanganya wajinga eti wawaunge mkono wanawapigania wao. Wanapigania matumbo yao ndio maana makubaliano ikawa mke awe waziri wa ulinzi na mume wake makam wa kwanza wa raisi.
 
"... amfute kazi Waziri wa Ulinzi ambaye ni mke wa Makamu wa Rais wa Kwanza, #RiekMachar ..."

Njaa kali sana ya madaraka iliyopitiliza kama kwetu tu.

Daaah!
 
Inchi ya mchongo,
Mwafrika baada ya kupata uhuru kwa miaka zaidi ya 40 anakubali inchi inagawanywa? na wazungu
Pambaf kabisa
 
Back
Top Bottom