Namche Bazar
Senior Member
- Apr 8, 2019
- 105
- 152
Nawasalimu wote kwa jina la Jamhuri.
Ni zaidi ya wiki sasa moto unaendelea kuwaka katika mlima Kilimanjaro.
Na kinachoonekana ni kujaza watu mlimani ambao wanaitwa kikosi kazi bila kufanya kazi ya kuzima moto,wengi wao wameenda kula na kupiga picha tu (selfie) na kuwa kero hata kwa watalii wanaolala kwenye kambi kwa mfano kambi ya Mweka juzi 27/10/ kuna kundi kubwa la wazima moto walikuwa wanapiga kelele usiku kucha kwenye mahema yao yaliyokuwa sio mbali na mahema ya watalii wa kigeni hivyo kupelekea kuwa kero kubwa sana.
Pia suala la uchafuzi wa mazingira na kutupwa ovyo chupa na maji na mifuko ya mikate,kwanini mamlaka husika isikemee utupaji wa taka hovyo ili hata baada ya moto kuzimika mlima uendelee kuwa safi na kuokoa gharama ambazo zitatumika kulipa vibarua ili wakasafishe na kubeba hizo takataka.
Ushauri:
Waache kupeleka watu wanaoenda kupiga picha badala ya kuzima moto,watu ambao hata wao wenyewe kutembea ni shida eti anapewa kazi ya kuzima moto kwa kuwa tu ni mwajiriwa toka fire brigade,polisi,NCCA nk
Watangaze kazi kwa vijana porters(wagumu) na mountain guides hawa wanaujua mlima vizuri na wana nguvu na spidi ya kutembea na kuzima moto kwa haraka kuliko kupeleka watu useless.
Viongozi na misafara yao wamejaa getini Mweka wakiamini kazi ya uzimaji moto inaendelea vizuri huko juu,kumbe watu wamepumzika,kupiga stori na kula na kunywa maji ya chupa ya Kilimanjaro for free of charge huku wakiendelea kulipwa.
Leo hii 29/10/2022 moto umezuia wageni waliokuwa wanatoka Baranco kwenda Karanga,bado tatizo lipo.
Nayaandika haya sio kwa nia ya kumuaharibia mtu/watu ila ni kutaka kumaliza suala la moto na biashara ya utalii irejee kama zamani bila watu kupata adha ya Moshi,kelele nk wawapo mlimani.
Asanteni.
Ni zaidi ya wiki sasa moto unaendelea kuwaka katika mlima Kilimanjaro.
Na kinachoonekana ni kujaza watu mlimani ambao wanaitwa kikosi kazi bila kufanya kazi ya kuzima moto,wengi wao wameenda kula na kupiga picha tu (selfie) na kuwa kero hata kwa watalii wanaolala kwenye kambi kwa mfano kambi ya Mweka juzi 27/10/ kuna kundi kubwa la wazima moto walikuwa wanapiga kelele usiku kucha kwenye mahema yao yaliyokuwa sio mbali na mahema ya watalii wa kigeni hivyo kupelekea kuwa kero kubwa sana.
Pia suala la uchafuzi wa mazingira na kutupwa ovyo chupa na maji na mifuko ya mikate,kwanini mamlaka husika isikemee utupaji wa taka hovyo ili hata baada ya moto kuzimika mlima uendelee kuwa safi na kuokoa gharama ambazo zitatumika kulipa vibarua ili wakasafishe na kubeba hizo takataka.
Ushauri:
Waache kupeleka watu wanaoenda kupiga picha badala ya kuzima moto,watu ambao hata wao wenyewe kutembea ni shida eti anapewa kazi ya kuzima moto kwa kuwa tu ni mwajiriwa toka fire brigade,polisi,NCCA nk
Watangaze kazi kwa vijana porters(wagumu) na mountain guides hawa wanaujua mlima vizuri na wana nguvu na spidi ya kutembea na kuzima moto kwa haraka kuliko kupeleka watu useless.
Viongozi na misafara yao wamejaa getini Mweka wakiamini kazi ya uzimaji moto inaendelea vizuri huko juu,kumbe watu wamepumzika,kupiga stori na kula na kunywa maji ya chupa ya Kilimanjaro for free of charge huku wakiendelea kulipwa.
Leo hii 29/10/2022 moto umezuia wageni waliokuwa wanatoka Baranco kwenda Karanga,bado tatizo lipo.
Nayaandika haya sio kwa nia ya kumuaharibia mtu/watu ila ni kutaka kumaliza suala la moto na biashara ya utalii irejee kama zamani bila watu kupata adha ya Moshi,kelele nk wawapo mlimani.
Asanteni.