the horse

JF-Expert Member
Sep 27, 2011
652
441
Katika pita pita zangu kwenye mitandao ya kijamii na kwenye spaces za Twitter zinazoendelea sasahivi za wanaharakati na wanasiasa wa vyama vya upinzani, nimeshtushwa sana na namna viongozi na wanaharakati wa upinzani wanavyomuunga mkono gaidi Hamza aliyeua Watanzania wenzetu 4 na kuwajeruhi watu wengine 6.

Nimeshangaa kuwaona watu wanaojigamba kuipenda nchi hii kama akina Lema, Fatma Karume, Mbatia na wenzao kumshadadia Hamza na kuonyesha kumuunga mkono kana kwamba kafanya jambo la maana na lenye tija kwa nchi. Leo Hamza anapata uungwaji mkono na watu wa upinzani kwa sababu ya kuua askari na Watanzania na kujeruhi wengine. Hii ni aibu na najisi kwa nchi.

Cha kushangaza watu hawa wa upinzani wanamshadadia Hamza kwa kushikilia maneno ya kubumba ya mitandaoni kwamba Hamza alidhulumiwa na polisi. Sasa kama Hamza alidhulumiwa kama wanavyobumba, njia ya kupata haki kwenye nchi hii ni kuchukua bunduki na kuanza kufyatulia watu?

Viongozi na wanaharakati wa upinzani mnaomshadadia na kumsapoti Hamza mnajiabisha sana mbele ya Watanzania na sasa mnajidhihirisha mbele za umma jinsi msivyolitakia mema Taifa hili.

Watu mnaojigamba mnaipenda nchi hii leo mnaibuka kumuunga mkono mtu aliyeleta taharuki kwa nchi, mtu aliyepeleka simanzi na umaskini kwa kuua Watanzania wenzetu ambao walikuwa wanategemewa na familia zao na Jamii yetu halafu nyie mnamuunga mkono kwa hoja nyepesi na za kusikia tu kwenye mitandao kwamba eti Hamza alidhulumiwa. Wapinzani mnajiaibisha sana mbele za Watanzania.
 
Turudi kwenye hao askari wako watanzania unaosema;

● Mbona askari wakitu bambikiza kesi hamuongei?

● Askari wamekua wote wanachama wa chama cha siasa, wanachama wa CCM, mbona hamuongei?

● Wakituomba rushwa mnasema ni hela za kusafishia viatu?

● Wakitu bambikiza makosa barabarani mnasema nchi haina hela kwaajili ya miradi?

● Wakipiga watu na kujeruhi bila sababu mnasema ndio kazi yao?

● Mnajitapa kwenye mikutano ya hadhara kwamba askari polisi wa CCM hawakosi risasi zaidi ya mbili, wakikosa basi hao sio askari?

● Wakipigana risasi na kuuwana wao kwa wao kwa kugombania siti ya mbele kwenye gari, mnasema walikua wanakimbiza wauza madawa ya kulevya?
 
Kitendo alichofanya hamza ni cha kulaaniwa na kukemewa kwa nguvu zote, shida ya upinzani wetu serikali ikiwa kulia wao ni kushoto tu katika kila jambo!

Hatuna wapinzani Tanzania, kila kitu ni ajenda hata kama halina tija kwenye jamii
 
Kitendo alichofanya hamza ni cha kulaaniwa na kukemewa kwa nguvu zote, shida ya upinzani wetu serikali ikiwa kulia wao ni kushoto tu katika kila jambo!
Hatuna wapinzani TZ, kila kitu ni ajenda hata kama halina tija kwenye jamii
Gaidi Hamza alikua ni kiongozi wa CCM na aliwajengea ofisi ya Chama.
 
Katika pita pita zangu kwenye mitandao ya kijamii na kwenye spaces za Twitter zinazoendelea sasahivi za wanaharakati na wanasiasa wa vyama vya upinzani, nimeshtushwa sana na namna viongozi na wanaharakati wa upinzani wanavyomuunga mkono gaidi Hamza aliyeua Watanzania wenzetu 4 na kuwajeruhi watu wengine 6...
Kwani uongo kuwa polisi ni wezi, majambazi na wanabambikia watu kesi za uongo?
 
Katika pita pita zangu kwenye mitandao ya kijamii na kwenye spaces za Twitter zinazoendelea sasahivi za wanaharakati na wanasiasa wa vyama vya upinzani, nimeshtushwa sana na namna viongozi na wanaharakati wa upinzani wanavyomuunga mkono gaidi Hamza aliyeua Watanzania wenzetu 4 na kuwajeruhi watu wengine 6...
Screenshot hayo wanayosema hao wanaharakati na sisi tuone...au naomba link
 
Kazi ipo

20210826_052251.jpg
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Watu wanatoa mawazo yao kulingana na jinsi tukio lilivyotokea,sidhani kama hilo linahusisha upinzani au huarakati wa mtu.na unatakiwa ujiulize kwanini watu wawe na mawazo tofauti kuhusu hilo tukio hadi kufikia kumuunga mkono marehemu dhidi ya jeshi la polisi.

Ukiona hadi rais wa nchi analikemea jeshi la polisi hadharani unatakiwa ujue iko shida kubwa ndani ya hilo jeshi."what goes arounds comes arounds".
 
Katika pita pita zangu kwenye mitandao ya kijamii na kwenye spaces za Twitter zinazoendelea sasahivi za wanaharakati na wanasiasa wa vyama vya upinzani, nimeshtushwa sana na namna viongozi na wanaharakati wa upinzani wanavyomuunga mkono gaidi Hamza aliyeua Watanzania wenzetu 4 na kuwajeruhi watu wengine 6...
Loud and clear
 
Katika pita pita zangu kwenye mitandao ya kijamii na kwenye spaces za Twitter zinazoendelea sasahivi za wanaharakati na wanasiasa wa vyama vya upinzani, nimeshtushwa sana na namna viongozi na wanaharakati wa upinzani wanavyomuunga mkono gaidi Hamza aliyeua Watanzania wenzetu 4 na kuwajeruhi watu wengine 6.

Nimeshangaa kuwaona watu wanaojigamba kuipenda nchi hii kama akina Lema, Fatma Karume, Mbatia na wenzao kumshadadia Hamza na kuonyesha kumuunga mkono kana kwamba kafanya jambo la maana na lenye tija kwa nchi. Leo Hamza anapata uungwaji mkono na watu wa upinzani kwa sababu ya kuua askari na Watanzania na kujeruhi wengine. Hii ni aibu na najisi kwa nchi.

Cha kushangaza watu hawa wa upinzani wanamshadadia Hamza kwa kushikilia maneno ya kubumba ya mitandaoni kwamba Hamza alidhulumiwa na polisi. Sasa kama Hamza alidhulumiwa kama wanavyobumba, njia ya kupata haki kwenye nchi hii ni kuchukua bunduki na kuanza kufyatulia watu?

Viongozi na wanaharakati wa upinzani mnaomshadadia na kumsapoti Hamza mnajiabisha sana mbele ya Watanzania na sasa mnajidhihirisha mbele za umma jinsi msivyolitakia mema Taifa hili.

Watu mnaojigamba mnaipenda nchi hii leo mnaibuka kumuunga mkono mtu aliyeleta taharuki kwa nchi, mtu aliyepeleka simanzi na umaskini kwa kuua Watanzania wenzetu ambao walikuwa wanategemewa na familia zao na Jamii yetu halafu nyie mnamuunga mkono kwa hoja nyepesi na za kusikia tu kwenye mitandao kwamba eti Hamza alidhulumiwa. Wapinzani mnajiaibisha sana mbele za Watanzania.
Watu wana point.

Kwa hali ilivyo na jinsi Watanzania wanavyoonewa na jeshi la police ..... siyo ajabu kuona wakifurahia kupunguzwa kwao. Our police force is too brutal ......!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom