Nadhani mko salama kabisa.
Mimi nikiwa na stress za kuachwa au kukataliwa kwanza nafuta namba ha huyo mtu, narestore simu kabisa
Naingia chumbani kwangu, nafanya usafi, nafua, napika nakula chakula kizuri ninachopendelea.
Natoka naenda shopping huko naenda nunua kila ninachohitaji, nitanunua shuka, nguo, kila kitu hadi na ambavyo sivihitaji
Nikirudi nyumbani nafanya usafi tena mara ya pili naoga, nakaa sasa naangalia movie na series.
Hapo sasa nakuwa afadhali stress zimepungua.
Vipi kwako mdau wa JF ni kitu gani unafanya ukiwa na stress za kuachwa/ kukataliwa?