Wandugu, mimi kuna mambo mawili yananitatiza kuhusu huu mradi:
1) Kwenye vile vituo vyao vya kupanda/kushusha abiria, ile floor yake iko juu sana, sasa ni basi gani hilo ambalo likisimama kwenye kituo mlango wake wa kuingilia huko juu kiasi kile? Kwa maneno mengine kuna big height mismatch between bus door na floor ya vituo ambapo abiria watakuwa wamesimama. Hapo sasa itakuwaje?
2) Kwa utaratibu wa traffick flow yetu TZ, magari yanaendeshwa kushoto kwa barabara, na hivyo milango ya mabasi yote iko kushoto kwa basi. Sasa kwa kuwa BRT stations ziko kati maana yake ni kuwa kama basi linapita lane ya kushoto milango ya mabasi hayo lazima iwe KULIA ili abiria anashuka moja kwa moja anaingia kituoni!! Sasa hayo mabasi yenye milango KULIA yako wapi? au kwenye BRT mabasi yakuwa yaendeshewa upande wa kulia?
Naomba ufafanuzi..