Stori ya kusisimua - Taxi

Stori ya kusisimua - Taxi

askofu asante sana leo kama yote kuna vitu viananiuzi kama kwann Tunu hakumuua Victor kabisa au kwann kina bob hawakumuua Casmir au kwanini walivomteka tu Tunu wasimuue hapo hapo
Haha! Uko sawa, mama... Ila angalia na mazingira yenyewe: Tunu hakuwa na muda wa kupoteza baada ya kujua Victor hana madhara, alichoangalia ni kupata vitu vyake asepe kabla wengine hawajafika. Kina Bob pia hawakuwa na muda wa kudili na Casmir wala mtu mwingine, kumbuka tayari wakati huo watu walishaanza kujaa eneo la ajali, hivyo wao walipaswa kuhakikisha wanamwondoa Tunu haraka iwezekanavyo. Kina Spoiler walipomchoma sindano Tunu waliamini kuwa wameshammaliza, wakajisahau kuwa anao washirika wake...

All in all, steringi huwa hafi ila yake ni mateso tu, na akifa na mchezo huishia hapohapo...

NB: Litro 👩
 
Hongera mkuu story iko Bomba sana kama vipi tengeneza movie itabamba kinoma
Naomba tag
Haha! Uko sawa, mama... Ila angalia na mazingira yenyewe: Tunu hakuwa na muda wa kupoteza baada ya kujua Victor hana madhara, alichoangalia ni kupata vitu vyake asepe kabla wengine hawajafika. Kina Bob pia hawakuwa na muda wa kudili na Casmir wala mtu mwingine, kumbuka tayari wakati huo watu walishaanza kujaa eneo la ajali, hivyo wao walipaswa kuhakikisha wanamwondoa Tunu haraka iwezekanavyo. Kina Spoiler walipomchoma sindano Tunu waliamini kuwa wameshammaliza, wakajisahau kuwa anao washirika wake...

All in all, steringi huwa hafi ila yake ni mateso tu, na akifa na mchezo huishia hapohapo...

NB: Litro
 
Haha! Uko sawa, mama... Ila angalia na mazingira yenyewe: Tunu hakuwa na muda wa kupoteza baada ya kujua Victor hana madhara, alichoangalia ni kupata vitu vyake asepe kabla wengine hawajafika. Kina Bob pia hawakuwa na muda wa kudili na Casmir wala mtu mwingine, kumbuka tayari wakati huo watu walishaanza kujaa eneo la ajali, hivyo wao walipaswa kuhakikisha wanamwondoa Tunu haraka iwezekanavyo. Kina Spoiler walipomchoma sindano Tunu waliamini kuwa wameshammaliza, wakajisahau kuwa anao washirika wake...

All in all, steringi huwa hafi ila yake ni mateso tu, na akifa na mchezo huishia hapohapo...

NB: Litro 👩
Basi asife baba maana akifa ningekuwa nasoma nini 🤣😂😂😂😂
 
Taxi (143)

ILIPOISHIA

“Basi fanyafanya mpango unitafutie msosi, nina njaa ya kufa,” Tunu aliongea kwa utulivu huku akipiga mwayo hafifu.

“Usijali, tayari chakula kimeshaandaliwa. Kuna mchemsho wa ndizi nyama, mchemsho wa kuku, maziwa fresh na vitafunwa. Chaguo ni lako!” Tom alisema na kumtazama Tunu kwa utulivu huku akitabasamu.

Tunu naye aliachia tabasamu lake jepesi huku akijiinua toka pale kitandani lakini akaketi tena juu ya kitanda baada ya kuhisi kizunguzungu. Akayafumba macho yake huku akivuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu.

Tom alimtazama kwa makini, “Pumzika kwanza, Tunu, nitakwenda kukuchukulia chakula na ukila kila kitu kitakuwa sawa,” Tom alisema na kumuaga Tunu kisha akaondoka kuelekea kule jikoni akimwacha pale kitandani.

Mara tu Tom alipoondoka mle chumbani ile hali ya upweke ikamrudia tena Tunu pale kitandani huku akiupisha utulivu kichwani mwake. Alipoitazama saa yake ya mkononi akagundua kuwa ilikuwa ikielekea kutimia saa moja na robo ya asubuhi, hapo fikra zake zikahamia kutafakari juu ya kazi iliyokuwa mbele yake. Alitamani sana aangalie kilichomo kwenye ile memory card kabla ya mambo mengine yote na alikuwa akimuomba Mungu kusiwe na chochote kilichofutwa.

ENDELEA...

Mawazo juu ya ile memory card na kazi kwa ujumla sasa yalichukua nafasi kwenye kichwa cha Tunu hadi pale aliposhtuka baada ya kitasa cha mlango wa kile chumba kuzungushwa taratibu na ule mlango kufunguliwa, kisha ukasukumwa kwa ndani.

Tunu aliyapeleka macho yake kutazama kule mlangoni huku akitabasamu, alimwona Tom akaingia mle ndani huku akiwa ameongozana na Dumba. Tom alikuwa amebeba bakuli kubwa la udongo lenye maakuli na jagi kubwa la maji, na Dumba alikuwa amebeba begi la Tunu lenye laptop na bilauri.

Tunu aliachia tabasamu baada ya kumwona Dumba na kuliona begi lake, akalipokea lile bakuli na kutazama ndani yake, kulikuwa na mchemsho wa ndizi matoke na nyama laini ya ng’ombe. Chakula kile kilikuwa kimepikwa kwa ufundi wa hali ya juu. Tunu hakutaka kujivunga, alianza kukishambilia kile chakula kwa pupa.

Kilikuwa chakula kitamu sana ambacho Tunu hakuweza kukumbuka kuwa mara ya mwisho kula chakula kitamu namna ile ilikuwa linin a wapi. Hakuwa na shaka yoyote kuwa chakula kile hakikuwa kimeandaliwa na Tom, huenda kilinunuliwa katika mojawapo ya migahawa ya kisasa kama Elli’s au Nuru Foods Café.

Hata hivyo, Tunu hakuwa na shida ya kuuliza. Aliendelea kula kwa pupa. Utamu wa kile chakula uliifanya asubuhi ile tulivu mno kuwa ya kupendeza sana kwa Tunu. Alipomaliza kupata kifungua kinywa, alinyanyuka na kuingia bafuni, huko alichukua dakika kadhaa kujimwagia maji na alipotoka humo mwili wake ulikuwa tayari umepata nguvu mpya.

Alijiandaa vizuri na kubadili nguo. Sasa alikuwa katika mwonekano mpya wa gauni lake zuri la kitenge lililoshonwa kwa mtindo wa ‘Ankara midi tube dress’ likiishia juu kidogo ya magoti yake, likaushika vyema mwili wake ulioumbika na kulichora umbo lake maridhawa. Nywele zake fupi na laini alizozitia rangi ya dhahabu alizichana vizuri na miguuni alivaa viatu simpo visivyo na vikanyagio virefu.

Ilipofika saa mbili na robo Tunu alitoka chumbani akiwa amebeba begi la laptop na kuelekea sebuleni. Sebule ilikuwa tulivu mno na kila mtu alikuwa akiwaza lake. Ilikuwa sebule kubwa iliyopo katika mazingira ya upweke kiasi yenye nyumba chache za makazi, eneo la Kinyerezi, watu wanne walikuwa wameketi kwenye sebule kubwa ya kifahari.

Ilikuwa sebule kubwa yenye kila thamani za kisasa yakiwemo makochi ya ngozi ya sofa ya kifahari yaliyopangwa katika mtindo wa kuizunguka na meza nzuri ya kioo yenye umbo la yai ilikuwa katikati, runinga pana kutani na chini yake kulikuwa na meza fupi nyeusi yenye sistimu ya muziki na kisimbuzi chenye chaneli za ndani na za kimataifa. Ilikuwa na madirisha makubwa ya vioo yenye kupitisha hewa safi.

Mbele ya sebule ile kulikuwa na ukumbi wa kulia chakula wenye meza kubwa ya duara iliyozungukwa na viti sita vya sponji. Kwa kweli ilikuwa ni nyumba nzuri ya kupendeza na yenye hadhi ya kukaliwa na kiongozi yeyote wa serikali mwenye cheo cha juu. Hata hivyo, pamoja na ufahari wa nyumba ile lakini ilikuwa haikaliwi na mtu yeyote, Tom alipenda kuifanya makazi yake ya siri kila alipokuwa na kazi za dharura kama ile.

Pale sebuleni Tunu aliwakuta Tom, Bob na Dumba wakiwa wameketi tayari sebuleni wakishushia na mvinyo ghali na mtamu aina ya Madeira wenye kiwango kikubwa cha asilimia 20 cha kilevi. Kulikuwa na bilauri nne, moja ikiwa tupu ikimsubiri Tunu na bilauri nyingine tatu zilikuwa zimejazwa mvinyo. Bob alikuwa ameshika kitabu cha Behind the Presidential Curtain kilichoandikwa na Noble Marara, mpambe wa zamani wa Rais wa Rwanda, Paul Kagame.

Alikuwa akisoma taratibu aya kwa aya na kifungu kwa kifungu huku akishushia mvinyo aina ya Madeira. Alipomwona Tunu alifunika kile kitabu na kukiweka juu ya meza ndogo ya kioo mbele yake, macho yake yakiwa kwa Tunu.

“Dah! Hakika Mungu kakupendelea, nilidhani unapendeza zaidi ukivaa suruali ya jeans kumbe hata ukiwa katika mwonekano wa vazi la kitenge! Ningekuwa promota wa mitindo ya mavazi ya Kiafrika ningekusajili, sina shaka yoyote wewe ungeweza kuiletea nchi hii ushindi usio na shaka,” Bob alisema kwa mzaha na kuwafanya wote waangue kicheko. Kisha walimkaribisha Tunu mvinyo.

Hakujivunga, alichukua ile chupa kubwa ya mvinyo na kujimiminia kwenye ile bilauri tupu kisha akapiga tarumbeta mafunda kadhaa na kuikita ile bilauri juu ya meza huku akisisimkwa mwili wake. Kisha akaketi kwenye sofa huku mvinyo ule ukionekana kuamsha ari mpya katika mwili wake na kumchangamsha vizuri kiasi cha kupunguza nishai machoni.

* * * * *

Saa mbili na nusu asubuhi ilimkuta Mr. Oduya akiwa bado ameketi kwenye kiti chake, moyo wake ulikuwa bado hauna amani. Hii ilikuwa ni baada ya kuwa na kikao kifupi na washirika wake muhimu sana. Kikao hicho kilifanyika kwenye ofisi yake iliyopo ndani ya jengo lake la ghorofa kumi na mbili lililopo barabara ya Bagamoyo, eneo la Kijitonyama, jijini Dar es Salaam.

Katika kikao hicho, washirika wake walikuwa wameshtushwa sana kusikia kwamba ni yeye Mr. Oduya aliyekuwa nyuma ya sakata lote la kuvamiwa nyumba ya Sammy na kisha yeye na mkewe kujeruhiwa. Baada ya kuwasihi sana walikubali kumsaidia, japo kwa shingo upande ili kulimaliza tatizo hilo na kuuanza ukurasa mpya.

Sasa Mr. Oduya alikuwa na uhakika wa kumalizana na jambo la kwanza kati ya mawili makubwa yaliyomkabili, sasa alikuwa anawasubiri watu wake maalumu wa kupanga mikakati ili kumalizia jambo la pili. Muda huo alikuwa ametulia mbele ya computer yake, macho yake yalikuwa matulivu yakipitia taarifa muhimu za mpango-kazi zilizokuwa zimetumwa kwake na wahisani walio nje ya nchi.

Inaendelea...

CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater Bigjahman moneytalk marybaby nipo2 ram kisukari Smart911 Madame S carbamazepine Astelia culture gal Prisoner of hope Mine eyes kuku mweus Thad hearly Shunie Tumosa Mine eyes Kudo swahiba92 ludist Toyota escudo Clkey macson3 boga la kiangazi LEGE Smart911 Richard irakunda skfull popie Krizy Beat hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Mlenge Kacheda mjasiliamali Laki Si Pesa cocochanel kinusikwetu big jambo mludego Shupavu Kacheda mjasiliamali Mweweso Songa Heri esiankiki mnadhimu mkuu wa jf red apple the-sniper MR KUO dan oseko Jackal kuku mweus mtugani wa wapi huyo chiqutitta ndukulusudicho ADK

NB: Litro 👩
 
Taxi (144)

Akiwa anaendelea kuipitia taarifa ile, akakumbuka jambo muhimu sana na kuinua simu yake ya mezani iliyokuwa kando ya meza yake, kisha akapiga kwa katibu muhtasi wake.

“Mariam, leo nina mambo mengi sana ya kufanya, hivyo sitapenda kusumbuliwa kwa matatizo madogomadogo, sawa?” Mr. Oduya alisema kwa sauti yake nziti ya kimamlaka.

“Sawa, Bosi,” katibu muhtasi wake aliitikia kwa sauti iliyoashiria heshima zote, kisha simu ikakatwa.

Baada ya kukata simu Mr. Oduya alivuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu kisha akatoa sigara moja toka kwenye paketi na kujiwashia, akaanza kuvuta taratibu huku akiipitia ile taarifa ya mpango-kazi kwa umakini zaidi na kunukuu kwenye kitabu chake kidogo cha kutunza kumbukumbu baadhi ya mambo aliyoyaona ni muhimu zaidi.

Mara simu yake ya mezani ikaanza kuita, Mr. Oduya aliitazama ile simu kwa hasira kwa kitambo fulani na kuamua kuidharau. Ile simu iliendelea kuita na mwito wake ukageuka kero masikioni mwake, aliitazama kwa makini huku akijishauri, mara akashawishika kutaka kuipokea huku akijiuliza, ni nani aliyekuwa akimsumbua kiasi kile!

Alinyoosha mkono wake kuichukua ile simu, hata hivyo, kabla mkono wake haujakigusa kiwambo cha kusikilizia simu ikakatika. Mr. Oduya akaminya midomo yake huku akijiuliza ni nani aliyekuwa akipiga simu, kisha akavuta mkupuo mkubwa wa moshi wa sigara na kuutoa nje kupitia mdomo na tundu za pua huku akiutazama kwa makini.

Akaachana na habari ya simu na kuendelea kupitia ile taarifa kwenye computer huku kitambo kifupi cha ukimya kikipita, mara ile simu ya mezani ikaanza kuita tena. Safari hii hakutaka ile simu iendelee kuita zaidi, hivyo haraka akakinyakuwa kiwambo chake na kukiweka sikioni huku akiipa akili yake utulivu wa hali ya juu. “Hallo!” aliongea kwa sauti tulivu iliyoficha hasira.

“Samahani, Bosi, kuna mgeni anahitaji kukuona...” yule katibu muhtasi wa Mr. Oduya alisema kwa sauti iliyoashiria woga fulani. Mr. Oduya alimkatisha kwa hasira.

“Binti, sikukwambia kuwa sitapenda usumbufu! Sijui umenielewa?” Mr. Oduya aliongea kwa ukali huku akitaka kuikata ile simu.

“Nimekuelewa, Bosi, ila huyu mgeni amesisitiza kuwa lazima akuone sasa hivi kwa hali yoyote,” yule katibu muhtasi aliongea kwa sauti yenye wasiwasi mkubwa.

“Sasa hivi! Amekutajia jina lake?” Mr. Oduya aliuliza huku akihisi donge la hasira likimkaba kooni kutokana na usumbufu ulioanza kujitokeza.

“Anasema yeye ni Inspekta Abel...” sauti ya yule katibu muhtasi ilipenya kwenye ngoma ya sikio la Mr. Oduya na kumfanya ahisi ubaridi mwepesi ukisambaa kwenye mwili wake.

“Nani? Inspekta Abel!” Mr. Oduya alimaka kwa mshtuko kwenye simu kiasi cha kutaka kuipasua ngoma ya sikio la katibu muhtasi wake.

Hakujua kwa nini alishtuka kiasi kile. Mapigo ya moyo wake yalikuwa yakienda mbio isivyo kawaida na jasho jepesi likaanza kumtoka usoni. Hata hivyo, alijikaza na kushusha pumzi za ndani kwa ndani. Hofu ilikuwa imepenya katika moyo wake kiasi cha kumshangaza zaidi ya ilivyomtisha. Alijiuliza, anahofia nini? Kama yule inspekta alifika pale kwa ajili ya suala la Sammy hilo halikumtia hofu. Alijua kuwa hakukuwa na ushahidi wa moja kwa moja ambao ungemuunganisha Mr. Oduya kwenye suala hilo.

Hata hivyo, hofu ilizidi kuutekenya moyo wake! Je, aliogopa nini? Alijiuliza tena. Kuna nini cha kuhofia? Hakupata jibu! Upuuzi ulioje! Akawaza, kwanza Inspekta Abel siyo saizi yake, yeye saizi yake ni kuanzia makamishna wasaidizi wa polisi hadi mkuu wa jeshi la Polisi.

“Sasa, Bosi, nimwambieje?” sauti tulivu ya katibu muhtasi wake ikamzindua Mr. Oduya toka kwenye mawazo yake.

Okay, mruhusu aingie,” Mr. Oduya alisema na kisha akaiweka ile simu pembeni na kujiegemeza kwenye kiti chake kumsubiri yule mgeni.

Mwanamume mrefu mwenye mwili mpana akiwa ndani ya sare nadhifu za kipolisi zilizokuwa na cheo cha alama mbili za nyota mabegani kwake aliingia, mkononi mwake alikuwa amebeba mkoba mdogo mweusi wa ngozi. Ni Inspekta Abel, aliyekuwa amepewa jukumu la kufanya uchunguzi wa kesi ya shambulio katika nyumba ya Sammy. Inspekta Abel alipoingia alinyoosha mkono wake wa salamu kwa Mr. Oduya na kumsalimia huku akitabasamu.

“Karibu sana, karibu uketi,” Mr. Oduya alisema huku akimwonesha kiti baada ya kusalimiana. Inspekta Abel akaketi.

“Naweza kukusaidia, Inspekta?” Mr. Oduya alimuuliza Inspekta Abel huku akimwangalia kwa makini.

“Naam,” Inspekta Abel aliitikia huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani. Kisha alimweleza Mr. Oduya kuwa alikuwa amefika hapo kwa ajili ya suala la vijana wake waliouawa.

Alimweleza kuwa kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na polisi juu ya vifo vya kutatanisha vya watu watatu akiwemo msichana mmoja, waliouawa kwa kupigwa risasi kwenye nyumba moja huko Karakata, ilibainika kuwa wote walikuwa wafanyakazi katika kampuni zilizokuwa chini ya The Splendid Group, mali ya Mr. Oduya.

Kilichowavutia zaidi polisi ni kwamba mmoja wa watu hao, Dulla Mcomoro, alikuwa amepigwa risasi katika makabiliano na polisi katika uvamizi nyumbani kwa Sammy kule Tabata Chang’ombe na mwili wake kukutwa na wenzake wawili Uledi na Lisa huko Karakata. Kwa hali hiyo, Inspekta Abel aliona kuwa, kulikuwa na haja ya kuonana na Mr. Oduya ili apate kujua tokea kwenye mzizi, juu ya kuhusishwa kwa vijana wake watatu huku akiamini kuwa angekuwa na kitu fulani cha kumweleza.

Mr. Oduya alikubali kuwa wote walikuwa vijana wake na wafanyakazi wake, lakini alipinga kufahamu chochote na kwa namna yoyote ile kama kulikuwa na yeyote kati yao aliyekuwa akijihusisha na uhalifu wa aina yoyote.

Itaendelea...

NB: Litro 👩
 
Taxi (145)

“Ofisa, kama umekuja hapa kwa sababu ya hilo basi jua sina chochote cha kukusaidia,” Mr. Oduya alisema huku akimtazama Inspekta Abel kwa makini na kuyatuliza macho yake kwenye uso wake.

“Waweza kuniambia, inakuwaje wafanyakazi watatu wa kampuni zako wakauawa kwa risasi katika usiku mmoja, wawili wakiwa ndani ya nyumba moja, tena nyumba ya mmojawao? Je, walikuwa na ugomvi na mtu yeyote?” Inspekta Abel aliuliza huku akiwa ameyatuliza macho yake usoni kwa Mr. Oduya.

Mr. Oduya alimtazama Inspekta Abel kwa kitambo kidogo kisha akatingisha kichwa chake kulia na kushoto taratibu, “Hayo siwezi kuyafahamu. Walikuwa na maisha yao binafsi nje ya kazi, mimi siwezi kujua, samahani kwa hilo.”

Inspekta Abel aliachia tabasamu kisha akakohoa kidogo kusafisha koo lake kabla hajauliza, “Mr. Oduya, unaweza kuniambia hadi sasa umechukua hatua zipi, hata kuomba uchunguzi baada ya kupokea taarifa za vifo vyao? Kumbuka ndugu wa marehemu wanataka uchunguzi ufanyike...”

“Bwana Inspekta, mimi ni Mwenyekiti Mtendaji wa The Splendid Group, kampuni hii ina kampuni kubwa ishirini chini yake na zote zina wakurugenzi watendaji na mameneja, siyo jukumu langu kuchukua hatua za moja kwa moja kwa wafanyazi kwani sina ‘link’ ya moja kwa moja na wao. Mimi ni mmiliki lakini wao wana viongozi wao,” Mr. Oduya alisema kwa sauti tulivu na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Ni kweli wana viongozi wao ambao ni waajiriwa wako, kwani wewe ndiye mmiliki... kumbuka wana ndugu na wategemezi wao ambao walikuwa wanawategemea!” Inspekta Abel alisema, kisha kukawa na ukimya wa kitambo fulani kabla ya Inspekta Abel kuuvunja ule ukimya, “Na vipi kuhusu tetesi kwamba kampuni yako inawatenga ndugu wa marehemu?”

“Sijapokea malalamiko kama hayo, sijui wewe umeyapata wapi?” Mr. Oduya aliuliza huku akimtazama Inspekta Abel kwa mshangao.

“Wenyewe wanasema kuwa wanatengwa...” Inspekta Abel alisema na kuongeza, “anyway... tuyaache hayo, pia kuna mwanamume mmoja anaitwa Casmir Njoroge ambaye amejeruhiwa kwenye ajali ya taxi iliyogonga nyumba usiku wa kuamkia leo huko Sinza Mori na baadaye kukimbizwa katika Hospitali ya Mwananyamala. Je. Unamfahamu vipi huyu bwana?”

“Hadi sasa sifahamu chochote kuhusu mtu anayeitwa Casmir Njoroge aliyejeruhiwa kwenye ajali ya taxi, labda yeye amekwambia chochote kuhusu mimi?” Mr. Oduya aliuliza kwa sauti tulivu huku akijitahidi kuifanya sauti yake iwe ya kawaida.

“Hapana, kusema ukweli Casmir hakutwambia chochote kuhusu wewe kwani yupo chumba cha wagonjwa mahututi na hawezi kuongea, ila kuna watu wawili wamemtambua kuwa walimwona akifika na kuingia kwenye kichochoro cha nyumba ya Sammy kule Tabata Chang’ombe dakika tano tu kabla hajatoka na bomu kulipuka,” Inspekta Abel alisema huku akiilamba midomo yake.

“Sasa, labda mimi nahusikaje na mtu huyu anayehusishwa na ugaidi?” Mr. Oduya aliuliza kwa sauti iliyoonesha kuwa alikwisha anza kushindwa kuidhibiti hasira yake.

“Katika uchunguzi wetu tumegundua kuwa Casmir Njoroge anatokea nchi jirani ya Kenya na anao uhusiano wa karibu sana na mfanyakazi wako Silas Potela, kwani wote wanatoka Kenya na waliwahi kuhusishwa na vikundi vya uhalifu nchini humo, hasa kikundi cha Mungiki,” Inspekta Abel alisema huku akimtazama Mr. Oduya kwa makini.

“Bado sijaelewa, inspekta, mimi nahusikaje hapo? Silas Potela ni mfanyakazi wangu, historia yake ya yote aliyoyafanya Kenya enzi hizo hayanihusu kwa kuwa hapa kwangu anafanya kazi vizuri na ana tabia njema, pia sina uwezo wa kumzuia mfanyakazi wangu yeyote kuwa na uhusiano na mtu mwingine hata kama mtu huyo ana historia ya uhalifu huko alikotoka. Sidhani kama ni sahihi kunituhumu kwa jambo hili, bwana inspekta!” Mr. Oduya alisema kwa msisitizo huku macho yake yakiwaka kwa hasira.

“Wala hakuna mtu anayekutuhumu, bwana mkubwa... nilidhani ipo haja ya kukuona ili nipate maelezo yako juu ya kuhusishwa kwa vijana wako na matukio ya hivi karibuni ya uhalifu...” Inspekta Abel alisema na kunyamaza kidogo, akameza mate kutowesha koo lake.

“Tumegundua kuwa kwa siku za karibuni yamekuwepo mawasiliano ya simu kati ya Casmir Njoroge na wafanyakazi wako wawili, Silas Potela na dereva wako Madjid Chege, ambaye pia ana asili ya Kenya! Mawasiliano hayo yamemhusisha pia mtu mwingine kutoka Kenya, Robert Kamau, na tunadhani pia yumo humu nchini,” Inspekta Abel aliongeza huku akimtazama Mr. Oduya kwa makini.

“Inspekta, naona sasa unaanza kuvuka mipaka! Nimeshakwambia sihusiki na chochote kuhusu maisha binafsi ya wafanyakazi wangu lakini hutaki kunielewa!” Mr. Oduya alisema kwa kufoka. Kama sauti yake ilivyobadilika, sura yake pia ilikuwa imebadilika.

Kitambo cha sekunde kadhaa za ukimya kilipita, walibaki wakitumbuliana macho kwa namna ya kusomana mawazo yao. Kisha, taratibu tabasamu jipya lilianza kuchanua usoni kwa Mr. Oduya. Halikuwa tabasamu lile ambalo Inspekta Abel alilizoea. Hili lilikuwa tabasamu jembamba, lisilopendeza hata kidogo, tabasamu ambalo lilifuatiwa na swali, “Bado tu unataka maelezo zaidi, bwana inspekta?”

“Vifo vya watu watatu wanaokuhusu vimetokea, mmoja wao ametambuliwa kuhusika na uvamizi kwenye nyumba ya Sammy. Mwingine tena anayehusishwa na watu wako anapata ajali ya kutatanisha, pia amehusishwa kulipua nyumba ya Sammy. Kama unadhani utaweza kuwa na jambo la kuniambia, basi utanitafuta,” Inspekta Abel alisema na kunyanyuka.

Alisimama akamtazama Mr. Oduya kwa kitambo na kuachia tabasamu, “Natumai kupata msaada toka kwako, mzee wangu.” Akasema na kuanza kupiga hatua kuondoka huku akimwacha Mr. Oduya ameketi kimya akimsindikiza kwa macho makali wakati akitoka nje ya ofisi yake.

Mambo bado ni 🔥🔥🔥. Kule Tunu huku Inspekta Abel. Je, Mr. Oduya atafanyaje ili kujinasua? Usikose kufuatilia simulizi hii ya kusisimua...

NB: Litro 👩
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom