Bishop Hiluka
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 7,147
- 14,711
- Thread starter
- #1,001
Taxi - (140)
“Don’t try to do anything stupid,” Spoiler alifoka huku akichomoa haraka kisu chake cha springi toka kwenye ala yake, akakielekeza kwenye shingo ya Tunu. Alikuwa ameghadhabika sana.
Tunu aliuma meno yake kwa hasira na kushusha pumzi za ndani kwa ndani, ujanja wake ulikuwa umegundulika. Sasa alihisi kuwa huenda huo ulikuwa mwisho wa maisha yake. Wakati gari likikata kona kuingia barabara ya Mori, Tunu akaliona gari fulani likija nyuma yao kwa kasi na kulitambua, akaachia tabasamu huku akijiegemeza kwenye siti yake. Lilikuwa ni lile gari aina ya Nissan Patrol la rangi ya bluu. Mara akahisi kuchomwa na kitu fulani ubavuni kwake mfano wa sindano na mara usingizi mzito ukaanza kumnyemelea.
Hakutaka kulala, alijaribu kufumbua macho yake lakini hakuweza na mara usingizi mzito ukammeza kabisa. Kama ndoto alianza kusikia mabishano kati ya wale watu wawili, mmoja alisema, “Tumuue kabisa maana haaminiki huyu.”
“Hapana, hana tena ujanja. Hii dawa itamlaza hadi keshokutwa hivyo ngoja tumfikishe kwa mzee, ndiye ataamua cha kumfanya!” mwingine alisema na mara akasikia kishindo kikubwa na kuanza kuyumba huku na kule.
Lile gari aina ya Nissan Patrol la rangi ya bluu lilikuwa limeifikia ile taxi na kuipiga kumbo ubavuni kiasi cha kufanikiwa kuihamisha kabisa barabarani na kuisogeza hadi kando ya barabara kwenye mfereji wa maji machafu. Tukio lile likaifanya ile taxi ianze kupoteza uelekeo huku ikiyumbayumba ovyo barabarani. Kilikuwa kitendo cha ghafla kilichowatokea kina Spoiler wakati wakiwa hawajajiandaa.
Yule mwanamume mwenye mwili ulioshiba aliyeketi kule mbele kushoto kwa dereva aliielekeza bastola yake kwenye lile Nissan Patrol na alipokuwa akijiandaa kufyatua risasi, Bob aliyekuwa akiendesha lile Nissan Patrol akawa mwerevu wa kushtukia mapema hila yake na hivyo akaliwahi lile taxi na kuligonga tena ubavuni. Mtikisiko uliotokea ukafanya bastola ya yule mtu imponyoke mkononi na kuangukia chini siti.
Lakini kabla hawajapata ufumbuzi Dumba, aliyekuwa pamoja na Bob aliachia risasi moja iliyokisambaratisha kichwa cha dereva wa ile taxi na muda huohuo uhai ukawa mbali na mwili wake. Wote ndani ya taxi walifahamu kuwa ule ungekuwa mwisho wao kwani kilichokuwa kinafuata baada ya hapo kingekuwa hatari zaidi kwao. Kwa haraka yule mwanamume mwenye mwili ulioshiba aliyekuwa ameketi mbele akawahi kuudaka usukani ili kuiongoza ile taxi.
Muda uleule ile taxi ikaparamia ukuta wa nyumba moja iliyokuwa kwenye kona kuelekea barabara ya Kwa Mwarabu na hapo yowe la hofu kutoka kwa watu waliokuwa kando kando ya ile barabara wakishuhudia kilichokuwa kinatokea likasikika wakati lile gari likiuparamia ule ukuta na kubomoa kabisa kisha likazama ndani ya nyumba.
Lile gari aina ya Nissan Patrol lililoendeshwa na Bob lilifunga breki na kusimama kando ya barabara ya Kwa Mwarabu, na kwa haraka sana Bob na mwenzake Dumba wakashuka na kuelekea kule ndani ilikokuwa ile taxi pasipo kujali macho ya watu walioanza kukusanyika eneo lile kushuhudia ajali ile ya kutisha.
Walipoifikia ile taxi wakawakuta watu watatu tu ndani ya gari. Dereva ambaye alikuwa amekufa, yule mwanamume mwenye mwili ulioshiba alikuwa amebanwa katikati ya lile gari na ukuta pale alipojaribu kuruka ili ajiokoe na damu zilikuwa zikimtoka mdomoni, na Tunu aliyekuwa amelala kwenye siti akiwa amepoteza fahamu. Spoiler alikuwa ametoweka.
Haikujulikana kama yule mwanamume mwenye mwili ulioshiba alikuwa mzima au mfu na wala hakuna kati yao aliyejihangaisha naye. Kina Bob walihitaji kumuokoa Tunu, na walipomwona amelala akiwa hana fahamu huku akitokwa damu mdomoni na sehemu ya kichwani, begi lake lenye laptop likiwa kando yake.
Walimchomoa haraka toka kwenye siti yake. Bob akambeba na wakati huohuo Dumba alilichukuwa lile begin a kuiona bastola ya Tunu, akaichukua na kutoka haraka kumfuata Bob kwenye gari lao.
Muda mfupi baadaye lile gari aina ya Nissan Patrol liliondoka toka eneo lile kwa mwendo wa kasi huku watu waliokuwa wameanza kujaa eneo lile wakiwa wamepigwa na butwaa.
* * * * *
Gari dogo aina ya Land-Rover 110 jeupe la POLISI lilifika katika eneo ilipotokea ajali nusu saa baada ya gari la kina Bob aina ya Nissan Patrol kuondoka. Polisi walikuwa wametaarifia uwepo wa ajali ile na mmiliki wa nyumba iliyogongwa na kubomoka. Ndani ya gari lile la polisi kulikuwa na watu wane. Mbele ya gari kulikuwa na watu wawili, dereva wa gari aliyekuwa amevaa sare ya kazi ikiwa na cheo cha koplo na mtu mwingine aliyekuwa amevaa suti ya kijivu na shati jeusi akiwa ameketi upande wa kushoto.
Nyuma ya gari lile kulikuwa na askari wawili wengine waliokuwa wamebebelea bunduki na vifua vyao vimekingwa na mavazi maalumu yanayozuia risasi maarufu kama ‘bullet proof’. Askari wote walikuwa na sura ya kazi.
Wale askari wawili walioketi nyuma pamoja na yule kiongozi wao mwenye suti ya kijivu ambaye kimwonekano alikuwa mweusi wa miaka arobaini wakashuka haraka na kuuliza kilichotokea, baada ya kuelezwa kwa ufupi wakaanza kupenya kuelekea kule ndani ilipokuwa ile taxi wakipita kwenye makundi ya watu waliokuwa wamekusanyika pale wakishangaa.
Walipozama ndani wakakutana na mmiliki wa ile nyumba ambaye alijitambulisha kwao na kuwaeleza kilichotokea: tangu aliposikia mshindo mkubwa wakati yeye na familia yake wakiwa mezani wanakula kisha wakaona ukuta wa nyumba yao ukianguka na gari kupenya ndani, kisha alivyoweza kumwona mtu mmoja akitoka ndani ya lile gari akiwa ameshika kisu na kupotelea kizani, na mwisho alivyowashuhudia wanaume wengine wawili wakiingia pale na kumbeba msichana mmoja aliyekuwa ndani ya ile taxi akiwa amezirai na kuondoka naye.
inaendelea...
NB: Litro 👩
“Don’t try to do anything stupid,” Spoiler alifoka huku akichomoa haraka kisu chake cha springi toka kwenye ala yake, akakielekeza kwenye shingo ya Tunu. Alikuwa ameghadhabika sana.
Tunu aliuma meno yake kwa hasira na kushusha pumzi za ndani kwa ndani, ujanja wake ulikuwa umegundulika. Sasa alihisi kuwa huenda huo ulikuwa mwisho wa maisha yake. Wakati gari likikata kona kuingia barabara ya Mori, Tunu akaliona gari fulani likija nyuma yao kwa kasi na kulitambua, akaachia tabasamu huku akijiegemeza kwenye siti yake. Lilikuwa ni lile gari aina ya Nissan Patrol la rangi ya bluu. Mara akahisi kuchomwa na kitu fulani ubavuni kwake mfano wa sindano na mara usingizi mzito ukaanza kumnyemelea.
Hakutaka kulala, alijaribu kufumbua macho yake lakini hakuweza na mara usingizi mzito ukammeza kabisa. Kama ndoto alianza kusikia mabishano kati ya wale watu wawili, mmoja alisema, “Tumuue kabisa maana haaminiki huyu.”
“Hapana, hana tena ujanja. Hii dawa itamlaza hadi keshokutwa hivyo ngoja tumfikishe kwa mzee, ndiye ataamua cha kumfanya!” mwingine alisema na mara akasikia kishindo kikubwa na kuanza kuyumba huku na kule.
Lile gari aina ya Nissan Patrol la rangi ya bluu lilikuwa limeifikia ile taxi na kuipiga kumbo ubavuni kiasi cha kufanikiwa kuihamisha kabisa barabarani na kuisogeza hadi kando ya barabara kwenye mfereji wa maji machafu. Tukio lile likaifanya ile taxi ianze kupoteza uelekeo huku ikiyumbayumba ovyo barabarani. Kilikuwa kitendo cha ghafla kilichowatokea kina Spoiler wakati wakiwa hawajajiandaa.
Yule mwanamume mwenye mwili ulioshiba aliyeketi kule mbele kushoto kwa dereva aliielekeza bastola yake kwenye lile Nissan Patrol na alipokuwa akijiandaa kufyatua risasi, Bob aliyekuwa akiendesha lile Nissan Patrol akawa mwerevu wa kushtukia mapema hila yake na hivyo akaliwahi lile taxi na kuligonga tena ubavuni. Mtikisiko uliotokea ukafanya bastola ya yule mtu imponyoke mkononi na kuangukia chini siti.
Lakini kabla hawajapata ufumbuzi Dumba, aliyekuwa pamoja na Bob aliachia risasi moja iliyokisambaratisha kichwa cha dereva wa ile taxi na muda huohuo uhai ukawa mbali na mwili wake. Wote ndani ya taxi walifahamu kuwa ule ungekuwa mwisho wao kwani kilichokuwa kinafuata baada ya hapo kingekuwa hatari zaidi kwao. Kwa haraka yule mwanamume mwenye mwili ulioshiba aliyekuwa ameketi mbele akawahi kuudaka usukani ili kuiongoza ile taxi.
Muda uleule ile taxi ikaparamia ukuta wa nyumba moja iliyokuwa kwenye kona kuelekea barabara ya Kwa Mwarabu na hapo yowe la hofu kutoka kwa watu waliokuwa kando kando ya ile barabara wakishuhudia kilichokuwa kinatokea likasikika wakati lile gari likiuparamia ule ukuta na kubomoa kabisa kisha likazama ndani ya nyumba.
Lile gari aina ya Nissan Patrol lililoendeshwa na Bob lilifunga breki na kusimama kando ya barabara ya Kwa Mwarabu, na kwa haraka sana Bob na mwenzake Dumba wakashuka na kuelekea kule ndani ilikokuwa ile taxi pasipo kujali macho ya watu walioanza kukusanyika eneo lile kushuhudia ajali ile ya kutisha.
Walipoifikia ile taxi wakawakuta watu watatu tu ndani ya gari. Dereva ambaye alikuwa amekufa, yule mwanamume mwenye mwili ulioshiba alikuwa amebanwa katikati ya lile gari na ukuta pale alipojaribu kuruka ili ajiokoe na damu zilikuwa zikimtoka mdomoni, na Tunu aliyekuwa amelala kwenye siti akiwa amepoteza fahamu. Spoiler alikuwa ametoweka.
Haikujulikana kama yule mwanamume mwenye mwili ulioshiba alikuwa mzima au mfu na wala hakuna kati yao aliyejihangaisha naye. Kina Bob walihitaji kumuokoa Tunu, na walipomwona amelala akiwa hana fahamu huku akitokwa damu mdomoni na sehemu ya kichwani, begi lake lenye laptop likiwa kando yake.
Walimchomoa haraka toka kwenye siti yake. Bob akambeba na wakati huohuo Dumba alilichukuwa lile begin a kuiona bastola ya Tunu, akaichukua na kutoka haraka kumfuata Bob kwenye gari lao.
Muda mfupi baadaye lile gari aina ya Nissan Patrol liliondoka toka eneo lile kwa mwendo wa kasi huku watu waliokuwa wameanza kujaa eneo lile wakiwa wamepigwa na butwaa.
* * * * *
Gari dogo aina ya Land-Rover 110 jeupe la POLISI lilifika katika eneo ilipotokea ajali nusu saa baada ya gari la kina Bob aina ya Nissan Patrol kuondoka. Polisi walikuwa wametaarifia uwepo wa ajali ile na mmiliki wa nyumba iliyogongwa na kubomoka. Ndani ya gari lile la polisi kulikuwa na watu wane. Mbele ya gari kulikuwa na watu wawili, dereva wa gari aliyekuwa amevaa sare ya kazi ikiwa na cheo cha koplo na mtu mwingine aliyekuwa amevaa suti ya kijivu na shati jeusi akiwa ameketi upande wa kushoto.
Nyuma ya gari lile kulikuwa na askari wawili wengine waliokuwa wamebebelea bunduki na vifua vyao vimekingwa na mavazi maalumu yanayozuia risasi maarufu kama ‘bullet proof’. Askari wote walikuwa na sura ya kazi.
Wale askari wawili walioketi nyuma pamoja na yule kiongozi wao mwenye suti ya kijivu ambaye kimwonekano alikuwa mweusi wa miaka arobaini wakashuka haraka na kuuliza kilichotokea, baada ya kuelezwa kwa ufupi wakaanza kupenya kuelekea kule ndani ilipokuwa ile taxi wakipita kwenye makundi ya watu waliokuwa wamekusanyika pale wakishangaa.
Walipozama ndani wakakutana na mmiliki wa ile nyumba ambaye alijitambulisha kwao na kuwaeleza kilichotokea: tangu aliposikia mshindo mkubwa wakati yeye na familia yake wakiwa mezani wanakula kisha wakaona ukuta wa nyumba yao ukianguka na gari kupenya ndani, kisha alivyoweza kumwona mtu mmoja akitoka ndani ya lile gari akiwa ameshika kisu na kupotelea kizani, na mwisho alivyowashuhudia wanaume wengine wawili wakiingia pale na kumbeba msichana mmoja aliyekuwa ndani ya ile taxi akiwa amezirai na kuondoka naye.
inaendelea...
NB: Litro 👩

