Stori ya kusisimua - Taxi

Stori ya kusisimua - Taxi

Taxi (146)

ILIPOISHIA

“Tumegundua kuwa kwa siku za karibuni yamekuwepo mawasiliano ya simu kati ya Casmir Njoroge na wafanyakazi wako wawili, Silas Potela na dereva wako Madjid Chege, ambaye pia ana asili ya Kenya! Mawasiliano hayo yamemhusisha pia mtu mwingine kutoka Kenya, Robert Kamau, na tunadhani pia yumo humu nchini,” Inspekta Abel aliongeza huku akimtazama Mr. Oduya kwa makini.

“Inspekta, naona sasa unaanza kuvuka mipaka! Nimeshakwambia sihusiki na chochote kuhusu maisha binafsi ya wafanyakazi wangu lakini hutaki kunielewa!” Mr. Oduya alisema kwa kufoka. Kama sauti yake ilivyobadilika, sura yake pia ilikuwa imebadilika.

Kitambo cha sekunde kadhaa za ukimya kilipita, walibaki wakitumbuliana macho kwa namna ya kusomana mawazo yao. Kisha, taratibu tabasamu jipya lilianza kuchanua usoni kwa Mr. Oduya. Halikuwa tabasamu lile ambalo Inspekta Abel alilizoea. Hili lilikuwa tabasamu jembamba, lisilopendeza hata kidogo, tabasamu ambalo lilifuatiwa na swali, “Bado tu unataka maelezo zaidi, bwana inspekta?”

“Vifo vya watu watatu wanaokuhusu vimetokea, mmoja wao ametambuliwa kuhusika na uvamizi kwenye nyumba ya Sammy. Mwingine tena anayehusishwa na watu wako anapata ajali ya kutatanisha, pia amehusishwa kulipua nyumba ya Sammy. Kama unadhani utaweza kuwa na jambo la kuniambia, basi utanitafuta,” Inspekta Abel alisema na kunyanyuka.

Alisimama akamtazama Mr. Oduya kwa kitambo na kuachia tabasamu, “Natumai kupata msaada toka kwako, mzee wangu.” Akasema na kuanza kupiga hatua kuondoka huku akimwacha Mr. Oduya ameketi kimya akimsindikiza kwa macho makali wakati akitoka nje ya ofisi yake.

ENDELEA...

Baada ya yule inspekta wa polisi kutoka, Mr. Oduya alijiegemeza kwenye kiti chake na kushusha pumzi ndefu. Sasa aliona kuwa mambo yalianza kwenda mrama na maji kumfika kooni. Vifo vya Dulla, Uledi na Lisa vilianza kumgeuka.

Kama hiyo haitoshi, kushtukiwa kwa Casmir Njoroge na hata Robert Kamau ambaye alikuwa hajatiwa nguvuni kulianza kumweka Mr. Oduya matatani. Sasa akili yake ilianza kufanya kazi mara mbili, aliwaza jinsi ya kujinasua toka kwenye sakata hilo huku akihisi mwili wake ukipata joto zaidi.

Alifikiria kidogo kisha akachukua simu yake ya mkononi na kutafuta namba fulani za mshirika wake muhimu aliyepo ndani ya jeshi la polisi. Alipozipata namba hizo alitaka kupiga simu lakini akashtuka na kuirudisha ile simu, kisha akachukua simu nyingine ambayo hakuwa akiitumia kwa kila mtu, bali kwa watu wachache sana na kwa mawasiliano nyeti kama yale.

Alizinakiri zile namba kisha akapiga na kuiweka sikioni. Simu ikaita mara mbili na kupokelewa. “Hallo, nahitaji sana kukuona, mkuu…” Mr. Oduya aliongea mara ile simu ilipopokelewa.

“Vipi, kuna tatizo lolote?” sauti nzito ilisikika ikiuliza toka upande wa pili wa ile simu.

“Tatizo lipo, ni kuhusu mmoja wa vijana wako, Inspekta Abel… ningeomba tuonane hata sasa hivi kama inawezekana!” Mr. Oduya alisema na kusikiliza kidogo kisha asiongeze kitu, akakata simu na kuinuka lakini kabla hajatoka akakumbuka jambo. Akatafuta namba za Spoiler na kupiga kisha akaiweka ile simu sikioni.

“Silas, ni nini sasa umefanya?” Mr. Oduya alimdaka Spoiler juu kwa juu, aliongea kwa sauti iliyoashiria hasira. Spoiler hakujibu, alibaki kimya.

“Hivi umekuwaje? Mbona umeanza kuwa mzembe kiasi hicho?” Mr. Oduya aliuliza kwa hasira.

“Usijali, mkuu, mambo yatakuwa sawa tu,” Spoiler aliongea kwa wasiwasi.

“Ninahitaji actions na siyo hizo soga zako!” Mr. Oduya alifoka. “Hivi unajua imenigharimu kiasi gani tangu uliposhindwa kutii agizo langu la kuliteketeza lile gari lililonunuliwa na Sammy?”

“Nisamehe, mkuu, naahidi kurekebisha makosa yote na kufuta kabisa ushahidi wote,” Spoiler alisema kwa kujitetea.
“Una uhakika?” Mr. Oduya aliuliza kwa sauti ya kufoka kidogo.

“Ninaamini hilo, mkuu. Kuanzia sasa nalishughulikia kwa umakini zaidi na wala jua halitakuchwa kabla sijafuta ushahidi wote,” Spoiler aliongea kwa msisitizo.

“Omba Mungu mpango huo utimie, vinginevyo hatutaelewana…” Mr. Oduya alisema kwa hasira na kukata simu kisha akaanza kupiga hatua kutoka nje, akaelekea kwenye chumba cha lifti na kushuka hadi chini. Sura yake ilionesha wazi hasira alizokuwa nazo.

Aliposhuka chini ya lile jengo alitembea taratibu huku mawazo yakiwa yamemtawala. Kitendo cha Spoiler kushindwa kizembe kukamilisha misheni aliyotumwa kilimuumiza kichwa, alianza kupoteza imani. Alielekea kwenye gari lake la kifahari aina ya Range Rover Velar la rangi nyeupe, akamkuta dereva wake Chege akimsubiri. Dakika mbili baadaye lile gari lilikuwa linayaacha maegesho yake na kuelekea mjini.

* * * * *

Baada ya kutoka katika jengo la makao makuu ya ofisi za The Splendid Group lililopo barabara ya Bagamoyo, eneo la Kijitonyama, jijini Dar es Salaam, Inspekta Abel alielekea moja kwa moja katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kinondoni, ya Mwananyamala.

Ilimchukua takriban dakika arobaini na tano kutoka ofisini kwa Mr. Oduya hadi Hospitali ya Mwananyamala, hali ambayo ilisababishwa na msongamano wa magari na ubovu wa barabara. Aliingia kwenye geti la kuingilia la hospitali hiyo na kwenda hadi katika viunga vya maegesho vya hospitali hiyo, akaliegesha gari lake jirani na gari nyingine aina ya Toyota Alphard jeusi lenye vioo vyenye tinted nyeusi.

Alishuka na kuanza kupiga hatua taratibu kuelekea katika jengo maalumu la wagonjwa mahututi alikolazwa Casmir Njoroge. Nje ya kile chumba maalumu cha wagonjwa wenye kuhitaji uangalizi maalumu alicholazwa Casmir, alimkuta askari wake Koplo Rashid, kijana mwembamba, mrefu, aliyevalia sare rasmi za polisi, akimsubiri.

Wakati Inspekta Abel anapokewa na Koplo Rashid pale nje ya kile chumba alicholazwa Casmir, Spoiler alikuwa analifikia gari lake aina ya Toyota Alphard jeusi na kujipakia kisha akaliondoa taratibu kutoka eneo lile na kutokomea mtaani.

Mara Inspekta Abel akashangaa kumwona muuguzi wa kile chumba alicholazwa Casmir akitoka mle chumbani huku akiwa na uso uliojaa wasiwasi na kukimbilia kwenye ofisi ya daktari wa jengo lile. Kabla hajajua akamwona tena yule muuguzi akiwa ameongozana na daktari wakikimbilia kuelekea kwenye chumba alicholazwa Casmir.

“Nini kimetokea?” Inspekta Abel aliwauliza kwa wasiwasi huku akitaka kuzama ndani lakini lakini akazuiwa kwa kuwa mtu yeyote hakuruhusiwa kuingia humo muda huo. Inspekta Abel alitii na kusubiri pale nje huku akiwa na wasiwasi, alijaribu kuchungulia mle ndani kupitia kioo kidogo cha mlangoni lakini hakuweza kuona kitu

Baada ya dakika zisizopungua tano, yule daktari alitoka nje huku uso wake ukiwa umesawajika na jasho jepesi lilikuwa linamtoka usoni.

“Nini kimetokea, daktari?” Inspekta Abel aliuliza tena kwa wasiwasi. Alikuwa amepigwa na butwaa, mikono yake ilikuwa imeshika kiuno huku akimtazama yule daktari kwa makini. “Ni nini kimetokea?” akauliza tena baada ya kuona hajibiwi.
“Nashangaa, hali ya mgonjwa ilikuwa inaanza kuimarika vizuri na muda mfupi tu uliopita nilimwona, lakini imebadilika ghafla na mapigo ya moyo wake kushuka isivyo kawaida...” yule daktari alisema kwa huzuni na kunyamaza kidogo.

Inaendelea...

CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater Bigjahman moneytalk marybaby nipo2 ram kisukari Smart911 Madame S carbamazepine Astelia culture gal Prisoner of hope Mine eyes kuku mweus Thad hearly Shunie Tumosa Mine eyes Kudo swahiba92 ludist Toyota escudo Clkey macson3 boga la kiangazi LEGE Smart911 Richard irakunda skfull popie Krizy Beat hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Mlenge Kacheda mjasiliamali Laki Si Pesa cocochanel kinusikwetu big jambo mludego Shupavu Kacheda mjasiliamali Mweweso Songa Heri esiankiki mnadhimu mkuu wa jf red apple the-sniper MR KUO dan oseko Jackal kuku mweus mtugani wa wapi huyo chiqutitta ndukulusudicho ADK aggyd BAHARI J

NB: Litro 👩
 
Taxi (147)

Inspekta Abel alimtazama kwa makini, moyo wake ulipiga kite kwa nguvu, alianza kuomba Mungu ili hali isiendelee kuwa mbaya zaidi, kwani alimhitaji sana Casmir ili kukamilisha kesi yake.

“Kwa hiyo, unataka kuniambia nini, daktari?” Inspekta Abel aliuliza huku akiwa ameyatuliza macho yake kwenye uso wa daktari.

“Tumeshindwa kuyaokoa maisha yake... amefariki dunia,” yule daktari alisema, uso wake ulikuwa umejawa na mashaka na woga.

Ilikuwa ni kama pigo la kisu likipenya mwilini na kuujeruhi moyo wa Inspekta Abel. Katika yote aliyoyatarajia asubuhi hiyo, taarifa ya kifo cha Casmir haikuwamo kabisa akilini mwake. Alimtazama yule daktari kama aliyekuwa anataka ufafanuzi juu ya kifo cha Casmir, akili yake ilikuwa inakataa kabisa kuipokea ile taarifa.

“Ni kweli amekufa, bwana inspekta,” yule daktari alijibu shaka ya Inspekta Abel baada ya kuisoma katika macho yake.
Bila kujua atendalo, Inspekta Abel alijikuta akimkwida yule daktari kwa mikono yake yenye nguvu na kumbana kwa vidole vyake huku akimsogeza karibu yake na kumtazama kwa hasira. “Kwa nini amekufa?” alimuuliza yule daktari akiwa amemkazia macho.

Yule daktari alipigwa na butwaa, alijaribu kujitoa katika mikono yenye nguvu ya Inspekta Abel, hata hivyo ilikuwa ni sawa na kujaribu kujitoa toka katika pingu. Kila alivyojaribu kujitoa ndivyo vidole vya Inspekta Abel vilivyozidi kudidimia katika ngozi yake. Licha ya kuwa alihisi maumivu makali lakini hali ile ilimshangaza zaidi.

“Unaniumiza, Inspekta,” yule daktari alimwambia Inspekta Abel huku akimtazama usoni kwa wasiwasi. Alikuwa amekunja ndita na jasho likimchuruzika usoni.

Ndiyo kwanza Inspekta Abel akashtuka baada ya kugundua kuwa alikuwa amemkwida yule daktari. Alimwachia huku akiomba radhi. “Nisamehe sana daktari, nilichanganyikiwa maana huyu mtu alikuwa muhimu sana kwenye kesi yangu!”

“Najua, lakini ndiyo mapenzi ya Mungu, mimi ni nani hadi nipingane na mapenzi yake?” yule daktari alisema kwa sauti tulivu. Inspekta Abel alibaki kimya akiwa ameduwaa.

* * * * *

Katika viunga vya maegesho ya magari vya klabu ya mabilionea na vigogo wa serikalini ya Paradise Club, Mr. Oduya na kigogo mmoja wa jeshi la polisi walikuwa wameketi kwenye siti ya nyuma ndani ya gari la kifahari aina ya Range Rover Velar la Mr. Oduya. Gari lile lilikuwa linanguruma taratibu na ndani ya lile gari walikuwa wamebakia wao wawili tu.

Yule kigogo wa polisi alikuwa amefika pale Paradise Club akitembea kwa miguu baada ya kumwacha dereva wake katika viunga vya maegesho ya magari vya jengo la mbele la hoteli ya kitalii ya Udzungwa Beach Resort. Hakutaka mtu mwingine ajue kama alikuwa amefika pale kuonana na Mr. Oduya.

Muda huo Mr. Oduya alikuwa ameketi kwa kukunja mguu wake wa kulia na alikuwa akimtazama yule kigogo wa polisi katika namna ya kuhitaji msaada. Uso wake ulionesha kuwa alikuwa ameelemewa na fikra za kukata tamaa.

“Hofu yako ni kwamba, unahisi Inspekta Abel anaweza kuwa amepata ushahidi kamili kukuhusu?” yule kigogo wa polisi alimuuliza Mr. Oduya huku akimtazama kwa makini.

“Sijajua...” Mr. Oduya alisema kwa wasiwasi na kushusha pumzi za ndani kwa ndani. “Ila ni wazi huyu inspekta amekuwa mtu wa kumtazama kwa ukaribu sana, anaweza kuwa hatari zaidi ya yule binti wa usalama wa taifa.”

“Kwa nini unadhani hivyo?” yule kigogo wa polisi aliuliza tena kwa sauti tulivu.

“Kwa sababu yeye ameweza kupiga hatua kwa kuunganisha matukio jambo linaloonesha kuwa amegundua uhusiano uliopo kati yangu na watu waliofanya uhalifu huo. Kitu ambacho bado sina uhakika ni kama ameshagundua uhusiano uliopo kati yangu na wewe,” Mr. Oduya alisema kwa wasiwasi.

Yule kigogo wa polisi alitulia kidogo akitafakari, kisha alikohoa kidogo kusafisha koo lake. “Kwa hiyo, unafikiriaje? Nadhani atakuwa anakushuku tu lakini hana kithibitisho chochote cha kukutia hatiani,” alisema na kuongeza, “Tunachopaswa kufanya ni kuhakikisha hapati anachokitafuta.”

“Hilo ndilo neno! Na ninadhani, kama inawezekana, anyamazishwe mapema! Sijui tutafanyaje?” Mr. Oduya aliuliza huku akimtulizia macho yule kigogo wa polisi.

“Mr. Oduya, you are not serious, brother! Unadhani utaua wangapi?” yule kigogo wa polisi alisema huku akimtazama Mr. Oduya kwa mshangao. Kisha kikaibuka kitambo kifupi cha ukimya, kila mmoja alionekana kufikiria kwa muda na kushusha pumzi.

“Sioni namna nyingine ya kufanya ili kuepuka janga hili, kumbuka kuwa akizidi kuchimba kiundani basi hata wewe huwezi kukwepa kwenye hili, ndiyo maana nadhani kuwa yeyote atakayekaa mbele yetu anapaswa kunyamazishwa haraka!” Mr. Oduya alisema baada ya kitambo kile cha ukimya.

“Hapana, sidhani kama kuua litakuwa jambo jema, kwani hali inaweza kuwa mbaya zaidi kwako kuliko hata kwangu!” yule kigogo wa polisi alishauri.

“Sasa tutafanyaje wakati naona maji yanaanza kuzidi unga?” Mr. Oduya aliuliza kwa sauti yenye mchanganyiko wa hasira na wasiwasi.

Yule kigogo wa polisi aliwaza kidogo kisha akasema, “Wacha niende, hadi nikifika ofisini kwangu nitakuwa nimeshapata jibu!” yule kigogo wa polisi alisema kisha akaangalia huku na kule ili kuhakikisha hakuna mtu aliyemwona, akashuka haraka toka ndani ya gari la Mr. Oduya na kuondoka.

Muda huohuo simu ya Mr. Oduya ikaanza kuita. Mr. Oduya aliitazama kwa makini na kuliona jina la Spoiler. Akaipokea ile simu mara moja na kuipeleka kwenye sikio lake. ”Niambie!” alisema kwa sauti tulivu huku akiilamba midomo yake iliyoanza kukauka.

“Nimekamilisha kila kitu, mzee. Casmir amekufa,” Spoiler alisema kwenye simu kwa sauti ya ushindi.

“Una uhakika?” Mr. Oduya aliuliza kwa sauti iliyoonesha kutoamini kile alichokuwa akiambiwa.

“Ninao uhakika, mzee... daktari aliyekuwa anamhudumia ndiye ameifanya kazi hiyo kwa umakini na amenihakikishia. Nimetoka kuongea naye sasa hivi kwenye simu, ameniambia kuwa Inspekta Abel amechanganyikiwa kwelikweli baada ya kuambiwa kuhusu kifo cha Casmir!” Spoiler alisema huku akiachia kicheko hafifu.

Okay, hiyo ni habari nzuri. Sasa nataka na yule binti anayejitia mpelelezi wa kimataifa afuate. Hakikisha unampata kabla jua halijatua,” Mr. Oduya alisema kisha simu ikakatwa.

Endelea kufuatilia simulizi hii ya kusisimua ili kuujua mwisho wake...

NB: Litro 👩
 
Taxi (146)

ILIPOISHIA

“Tumegundua kuwa kwa siku za karibuni yamekuwepo mawasiliano ya simu kati ya Casmir Njoroge na wafanyakazi wako wawili, Silas Potela na dereva wako Madjid Chege, ambaye pia ana asili ya Kenya! Mawasiliano hayo yamemhusisha pia mtu mwingine kutoka Kenya, Robert Kamau, na tunadhani pia yumo humu nchini,” Inspekta Abel aliongeza huku akimtazama Mr. Oduya kwa makini.

“Inspekta, naona sasa unaanza kuvuka mipaka! Nimeshakwambia sihusiki na chochote kuhusu maisha binafsi ya wafanyakazi wangu lakini hutaki kunielewa!” Mr. Oduya alisema kwa kufoka. Kama sauti yake ilivyobadilika, sura yake pia ilikuwa imebadilika.

Kitambo cha sekunde kadhaa za ukimya kilipita, walibaki wakitumbuliana macho kwa namna ya kusomana mawazo yao. Kisha, taratibu tabasamu jipya lilianza kuchanua usoni kwa Mr. Oduya. Halikuwa tabasamu lile ambalo Inspekta Abel alilizoea. Hili lilikuwa tabasamu jembamba, lisilopendeza hata kidogo, tabasamu ambalo lilifuatiwa na swali, “Bado tu unataka maelezo zaidi, bwana inspekta?”

“Vifo vya watu watatu wanaokuhusu vimetokea, mmoja wao ametambuliwa kuhusika na uvamizi kwenye nyumba ya Sammy. Mwingine tena anayehusishwa na watu wako anapata ajali ya kutatanisha, pia amehusishwa kulipua nyumba ya Sammy. Kama unadhani utaweza kuwa na jambo la kuniambia, basi utanitafuta,” Inspekta Abel alisema na kunyanyuka.

Alisimama akamtazama Mr. Oduya kwa kitambo na kuachia tabasamu, “Natumai kupata msaada toka kwako, mzee wangu.” Akasema na kuanza kupiga hatua kuondoka huku akimwacha Mr. Oduya ameketi kimya akimsindikiza kwa macho makali wakati akitoka nje ya ofisi yake.

ENDELEA...

Baada ya yule inspekta wa polisi kutoka, Mr. Oduya alijiegemeza kwenye kiti chake na kushusha pumzi ndefu. Sasa aliona kuwa mambo yalianza kwenda mrama na maji kumfika kooni. Vifo vya Dulla, Uledi na Lisa vilianza kumgeuka.

Kama hiyo haitoshi, kushtukiwa kwa Casmir Njoroge na hata Robert Kamau ambaye alikuwa hajatiwa nguvuni kulianza kumweka Mr. Oduya matatani. Sasa akili yake ilianza kufanya kazi mara mbili, aliwaza jinsi ya kujinasua toka kwenye sakata hilo huku akihisi mwili wake ukipata joto zaidi.

Alifikiria kidogo kisha akachukua simu yake ya mkononi na kutafuta namba fulani za mshirika wake muhimu aliyepo ndani ya jeshi la polisi. Alipozipata namba hizo alitaka kupiga simu lakini akashtuka na kuirudisha ile simu, kisha akachukua simu nyingine ambayo hakuwa akiitumia kwa kila mtu, bali kwa watu wachache sana na kwa mawasiliano nyeti kama yale.

Alizinakiri zile namba kisha akapiga na kuiweka sikioni. Simu ikaita mara mbili na kupokelewa. “Hallo, nahitaji sana kukuona, mkuu…” Mr. Oduya aliongea mara ile simu ilipopokelewa.

“Vipi, kuna tatizo lolote?” sauti nzito ilisikika ikiuliza toka upande wa pili wa ile simu.

“Tatizo lipo, ni kuhusu mmoja wa vijana wako, Inspekta Abel… ningeomba tuonane hata sasa hivi kama inawezekana!” Mr. Oduya alisema na kusikiliza kidogo kisha asiongeze kitu, akakata simu na kuinuka lakini kabla hajatoka akakumbuka jambo. Akatafuta namba za Spoiler na kupiga kisha akaiweka ile simu sikioni.

“Silas, ni nini sasa umefanya?” Mr. Oduya alimdaka Spoiler juu kwa juu, aliongea kwa sauti iliyoashiria hasira. Spoiler hakujibu, alibaki kimya.

“Hivi umekuwaje? Mbona umeanza kuwa mzembe kiasi hicho?” Mr. Oduya aliuliza kwa hasira.

“Usijali, mkuu, mambo yatakuwa sawa tu,” Spoiler aliongea kwa wasiwasi.

“Ninahitaji actions na siyo hizo soga zako!” Mr. Oduya alifoka. “Hivi unajua imenigharimu kiasi gani tangu uliposhindwa kutii agizo langu la kuliteketeza lile gari lililonunuliwa na Sammy?”

“Nisamehe, mkuu, naahidi kurekebisha makosa yote na kufuta kabisa ushahidi wote,” Spoiler alisema kwa kujitetea.
“Una uhakika?” Mr. Oduya aliuliza kwa sauti ya kufoka kidogo.

“Ninaamini hilo, mkuu. Kuanzia sasa nalishughulikia kwa umakini zaidi na wala jua halitakuchwa kabla sijafuta ushahidi wote,” Spoiler aliongea kwa msisitizo.

“Omba Mungu mpango huo utimie, vinginevyo hatutaelewana…” Mr. Oduya alisema kwa hasira na kukata simu kisha akaanza kupiga hatua kutoka nje, akaelekea kwenye chumba cha lifti na kushuka hadi chini. Sura yake ilionesha wazi hasira alizokuwa nazo.

Aliposhuka chini ya lile jengo alitembea taratibu huku mawazo yakiwa yamemtawala. Kitendo cha Spoiler kushindwa kizembe kukamilisha misheni aliyotumwa kilimuumiza kichwa, alianza kupoteza imani. Alielekea kwenye gari lake la kifahari aina ya Range Rover Velar la rangi nyeupe, akamkuta dereva wake Chege akimsubiri. Dakika mbili baadaye lile gari lilikuwa linayaacha maegesho yake na kuelekea mjini.

* * * * *

Baada ya kutoka katika jengo la makao makuu ya ofisi za The Splendid Group lililopo barabara ya Bagamoyo, eneo la Kijitonyama, jijini Dar es Salaam, Inspekta Abel alielekea moja kwa moja katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kinondoni, ya Mwananyamala.

Ilimchukua takriban dakika arobaini na tano kutoka ofisini kwa Mr. Oduya hadi Hospitali ya Mwananyamala, hali ambayo ilisababishwa na msongamano wa magari na ubovu wa barabara. Aliingia kwenye geti la kuingilia la hospitali hiyo na kwenda hadi katika viunga vya maegesho vya hospitali hiyo, akaliegesha gari lake jirani na gari nyingine aina ya Toyota Alphard jeusi lenye vioo vyenye tinted nyeusi.

Alishuka na kuanza kupiga hatua taratibu kuelekea katika jengo maalumu la wagonjwa mahututi alikolazwa Casmir Njoroge. Nje ya kile chumba maalumu cha wagonjwa wenye kuhitaji uangalizi maalumu alicholazwa Casmir, alimkuta askari wake Koplo Rashid, kijana mwembamba, mrefu, aliyevalia sare rasmi za polisi, akimsubiri.

Wakati Inspekta Abel anapokewa na Koplo Rashid pale nje ya kile chumba alicholazwa Casmir, Spoiler alikuwa analifikia gari lake aina ya Toyota Alphard jeusi na kujipakia kisha akaliondoa taratibu kutoka eneo lile na kutokomea mtaani.

Mara Inspekta Abel akashangaa kumwona muuguzi wa kile chumba alicholazwa Casmir akitoka mle chumbani huku akiwa na uso uliojaa wasiwasi na kukimbilia kwenye ofisi ya daktari wa jengo lile. Kabla hajajua akamwona tena yule muuguzi akiwa ameongozana na daktari wakikimbilia kuelekea kwenye chumba alicholazwa Casmir.

“Nini kimetokea?” Inspekta Abel aliwauliza kwa wasiwasi huku akitaka kuzama ndani lakini lakini akazuiwa kwa kuwa mtu yeyote hakuruhusiwa kuingia humo muda huo. Inspekta Abel alitii na kusubiri pale nje huku akiwa na wasiwasi, alijaribu kuchungulia mle ndani kupitia kioo kidogo cha mlangoni lakini hakuweza kuona kitu

Baada ya dakika zisizopungua tano, yule daktari alitoka nje huku uso wake ukiwa umesawajika na jasho jepesi lilikuwa linamtoka usoni.

“Nini kimetokea, daktari?” Inspekta Abel aliuliza tena kwa wasiwasi. Alikuwa amepigwa na butwaa, mikono yake ilikuwa imeshika kiuno huku akimtazama yule daktari kwa makini. “Ni nini kimetokea?” akauliza tena baada ya kuona hajibiwi.
“Nashangaa, hali ya mgonjwa ilikuwa inaanza kuimarika vizuri na muda mfupi tu uliopita nilimwona, lakini imebadilika ghafla na mapigo ya moyo wake kushuka isivyo kawaida...” yule daktari alisema kwa huzuni na kunyamaza kidogo.

Inaendelea...

CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater Bigjahman moneytalk marybaby nipo2 ram kisukari Smart911 Madame S carbamazepine Astelia culture gal Prisoner of hope Mine eyes kuku mweus Thad hearly Shunie Tumosa Mine eyes Kudo swahiba92 ludist Toyota escudo Clkey macson3 boga la kiangazi LEGE Smart911 Richard irakunda skfull popie Krizy Beat hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Mlenge Kacheda mjasiliamali Laki Si Pesa cocochanel kinusikwetu big jambo mludego Shupavu Kacheda mjasiliamali Mweweso Songa Heri esiankiki mnadhimu mkuu wa jf red apple the-sniper MR KUO dan oseko Jackal kuku mweus mtugani wa wapi huyo chiqutitta ndukulusudicho ADK aggyd BAHARI J

NB: Litro 👩
thnks bro
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom