Stori ya kusisimua - Taxi

Stori ya kusisimua - Taxi

Taxi - (27)

Joyce alimsindikiza Sammy kwa macho na kushusha pumzi za ndani kwa ndani, kisha aligeuka kumtazama Winifrida huku akiwa amekunja sura yake, alitaka kusema neno lakini akasita.

* * * * *

Saa 2:30 usiku ilimkuta Mr. Oduya akiwa amesimama chumbani kwake mbele ya meza nzuri ya kisasa ya vipodozi maarufu kama ‘dressing table’ iliyokuwa na vioo virefu vitatu vilivyowekwa kuizunguka ile meza na kumfanya mtu ajione mara tatu, alionekana yupo katika harakati za kujiandaa ili atoke.

Mr. Oduya alikuwa amevaa suti ya bei ghali nyeusi aina ya Kenzo, shati jeupe la mikono mirefu na viatu vyeusi vya ngozi, alikuwa anachana nywele zake taratibu huku akijitazama kwenye vile vioo, kisha mikono yake ilianza kurekebisha tai yake ya rangi nyekundu shingoni.

Alionekana kuwa mtulivu sana huku akiwa amezama katika lindi la fikra, hata hivyo, alikuwa makini akimtupia jicho la wizi mkewe, Dk. Salma Oduya aliyekuwa amesimama kando yake akimtazama kwa makini huku amekunja sura yake.

Dk. Oduya alikuwa mwanamke mnene wa wastani, hakuwa mfupi wala mrefu bali alikuwa na kimo cha wastani na rangi ya maji ya kunde iliyokuwa ina mng’aro wa aina yake.

Akiwa na umri wa miaka hamsini na tano, alikuwa Mhadhiri Mwandamizi wa Sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na mama wa watoto wawili: Omari Oduya aliyekuwa na miaka 30 na kwa wakati huo alikuwa anaishi nchini Marekani, na Zuhura Oduya aliyekuwa na miaka 26 na wakati huo alikuwa anachukua Shahada ya Umahili ya Maendeleo ya Uchumi wa Kimataifa nchini Uingereza.

Usiku ule Dk. Oduya alikuwa amevaa nguo nyepesi ya kulalia maarufu kama ‘night dress’ ya rangi ya samawati na alijifunga kitenge kiunoni, juu alivaa sweta la mikono mirefu na kichwani alikuwa amevaa kofia laini maalumu kwa kukinga nywele.

Muda ule wa saa mbili na nusu usiku upepo ulikuwa unavuma na kutengeneza sauti ya mvumo wa kustaajabisha kwenye matawi ya miti mikubwa ya kivuli iliyozunguka jumba la kifahari la Mr. Oduya, kadiri matawi ya miti yalivyocheza huku na kule kwa utulivu ndivyo mvumo ule ulivyosikika na kutengeneza sauti kama ya chatu mkali aliyehisi hatari kichakani.

Upepo ulivuma ukayasonga songa mapazia marefu yaliyokuwa yamefunika madirisha mawili makubwa mle chumbani.

Jumba la Mr. Oduya ambalo lilistahili kuitwa kasri, lilikuwa katika eneo la ufukweni mwa Bahari ya Hindi, Mbezi Beach, eneo lililokuwa na makazi ya watu wenye ukwasi mkubwa au viongozi wa ngazi za juu wa serikali ya Tanzania. Katika eneo lile tulivu yalionekana majumba kadhaa ya kifahari yaliyozungukwa na kuta ndefu na mageti makubwa mbele yake.

Lilikuwa jumba kubwa la ghorofa mbili lenye vyumba saba vya kulala kila kimoja kikiwa na maliwato yake, sebule tatu kubwa, kumbi mbili za chakula, majiko mawili ya kisasa, kaunta ya baa iliyokuwa katika sehemu ya chini ya jengo na sehemu mbili za ghorofani za kubarizi zenye kochi safi za sofa.

Eneo lile lilikuwa na barabara pana ya lami yenye usafi wa hali ya juu, iliyopandwa miti mizuri ya kivuli kando ya barabara. Muda ule wa usiku eneo lile lilikuwa na utulivu mkubwa sana huku likimulikwa na taa nzuri zenye mwanga mkali. Ni sauti kali za mbwa waliokuwa wakibweka eneo lile bila sababu za msingi ndizo zilizokuwa zinasikika kwa mbali na magari machache sana yalipita barabarani.

Ndani ya lile jumba waliishi watu kumi, watu wazima wanane na watoto wawili: Mr. Oduya mwenyewe na mkewe Dk. Oduya, ndugu watatu wa familia ya mkewe na watoto wao wawili, wahudumu wawili wa kike wa ndani na mhudumu mmoja wa kiume aliyesaidia shughuli za mifugo na shamba. Pia kulikuwa na walinzi watatu waliolinda kwa kupokezana, lakini hawakuwa wakiishi pale.

Hata hivyo, lile jumba lilikuwa na ulinzi madhubuti kwa kujengewa ukuta mrefu uliofungwa mfumo maalumu wa umeme wa kuzuia wezi juu yake na usiomwezesha mtu yeyote kuona mle ndani.

“Hivi wewe mwanamume, unajua mimi sikuelewi kabisa!” sauti ya Dk. Oduya ilimgutusha Mr. Oduya kutoka kwenye lindi la mawazo.

Muda wote Dk. Oduya alikuwa anamwangalia mumewe akionesha wazi kuwa alikuwa na hasira na sura yake alikuwa kaikunja na kutengeneza matuta madogo usoni.

“Kwa nini hunielewi?” Mr. Oduya alimwuliza mkewe bila kugeuka ingawa alikuwa akimtazama kupitia vioo vya kwenye meza ya vipodozi.

“Eti eeh! Unajifanya huelewi ninachomaanisha!” Dk. Oduya aliongea kwa hasira huku sasa akiwa ameshika kiuno chake kwa mikono yote miwili na kumkazia macho mumewe.

“Hapana naelewa,” Mr. Oduya alimjibu huku akigeuza shingo yake kumtazama kwa makini.

“Unaelewa nini?” Dk. Oduya alihoji huku macho yake yakiwa hayabanduki usoni kwa mumewe.

“Naelewa kwamba hunielewi kabisa!” Mr. Oduya alijibu huku hasira zikianza kuchipua ndani yake.

“Haya wewe endelea tu… huo umalaya wako wa uzeeni utakugharimu siku moja… ila usisahau kutumia condom usije ukaniletea maradhi,” Dk. Oduya alisema huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Naomba tusianze kuharibiana siku, unaropoka tu wala hujui naenda kukutana na kina nani saa hizi, hivi kwa mwendo huu nitaweza kweli kushinda uchaguzi wa urais kama hata kwenda kukutana na washirika muhimu wa kisiasa inakuwa nongwa!” Mr. Oduya alianza kulalamika.

“Wadau gani wa kisiasa? Hivi unaniona mimi mtoto mdogo siyo! Wewe si umetoka huko huko muda huu! Hata hujapumzika vizuri unataka kuondoka tena, eti kuwaona wadau wa kisiasa, ni wadau gani wasiokupa hata muda wa kupumzika na familia yako?” Dk. Oduya alizidi kuhoji,

Mr. Oduya alimtazama kwa makini, akataka kumjibu lakini alisita na kuamua kumpuuza, ni mwanamke aliyeishi naye katika ndoa kwa miaka therathini na moja. Alimchukulia kama mwanamke wa kawaida tu ambaye hakuwa na jipya zaidi ya maneno mengi mithili ya chiriku kila uchao.

Badala yake Mr. Oduya alichukua mkoba wake wa kiofisi na kugeuka, akaanza kupiga hatua za taratibu kuondoka, aliazimia kwenda kuumaliza usiku wa siku ile akiwa na Zainab, mwanadada mtundu mno na aliyekuwa amemuonesha ulimwengu mpya wa mapenzi, pamoja na umri wake mkubwa, alikiri kuwa hakuwa mjuzi kabisa.

Inaendelea...
 
Taxi - (28)

Zainab Semaya, mtoto wa ki-Tanga, alikuwa binti mwenye busu za kusisimua sana na kila mara walipomaliza mchezo alimwachia Mr. Oduya maswali kibao na kubaki akijiuliza alijifunzia wapi yale mahaba! Kwani Zainab alikuwa wa aina ya pekee, mwenye majibu yote ya maswali yahusuyo mapenzi.

Hivyo, Mr. Oduya aliona kuwa hakutakiwa kumpa nafasi mkewe aharibu utaratibu mzima wa siku ile wa kwenda kufurahia penzi la mrembo asiyechuja, bibie Zainab, kwani lingekuwa kosa kubwa sana kumwacha alale peke yake wakati alikuja kwa ajili yake.

“Sawa bwana, endelea kunidharau… lakini nakwambia mbio za sakafuni huishia ukingoni,” Dk. Oduya alisema huku akiwa bado kakunja uso wake kwa hasira, alikuwa anamsindikiza mumewe kwa macho.

Mr. Oduya hakugeuka wala kusema neno bali alitoka nje ya chumba kile na kuufunga mlango nyuma yake kisha alizifuata ngazi za kuelekea sehemu ya chini ya lile jumba la kifahari huku akiwa amechefukwa kweli kweli.

Asingeweza kuahirisha safari yake ya kwenda Paradise Club kufurahia maisha na kipenzi cha moyo wake, hakuwa na shaka kuwa suala la mkewe angelimaliza kiutu-uzima kwani alijua namna nzuri ya kumdhibiti.

* * * * *

Saa tatu na ushee usiku Joyce alikuwa amekaa kwenye kona ya kitanda chumbani kwao, alikuwa amevaa nguo nyepesi nyeupe ya kulalia iliyolichora vizuri umbo lake zuri na kuifichua nguo yake nyeusi ya ndani.

Joyce alikuwa ameketi akimtazama mumewe Sammy kwa wasiwasi lakini kwa macho yaliyojaa ubembe wa huba huku akihisi moyo wake ukienda mbio kama saa mbovu! Hata hivyo, moyoni alionekana wazi kusimamia kile alichopanga kufanya na hakuwa tayari kuyumbishwa, kwani aliamini kuwa bahati kama iliyomtokea siku ile haiji mara mbili!

Ni kweli alimpenda sana na kumheshimu Sammy, lakini isingekuwa rahisi kwake kuachana na mpango wake wa kwenda kumuona Madame Norah.

Kilipita kitambo kirefu cha ukimya, Joyce alikuwa akimwangalia Sammy kwa makini. Macho yake yalishatoa taswira ya kilichokuwa moyoni mwake. Alishajua kabisa kuwa mwenzake alikuwa katika hasira, alikasirishwa na jambo ambalo lilikuwa na faida, si kwao wawili bali kwa familia nzima.

Tangu Sammy aliporudi nyumbani na kuelezwa na Winifrida kuhusu simu ya Madame Norah aliyompigia Joyce, alionekana kutokufurahia jambo hilo, kwani siku zote hakukubaliana na mkewe kutaka kuonana na Madame Norah. Alikuwa na wasiwasi kuwa Madame Norah angeweza kumwambukiza tabia zake Joyce.

Muda ule kila mmoja alikuwa na mawazo yake, Sammy alikuwa amejiegemeza ukutani pale kitandani alipokaa na kutazama juu ya dari kwa muda mrefu. Joyce naye alikuwa na mawazo yake, alijaribu kufikiria ni kwa namna gani angemlainisha Sammy akubali kumruhusu kwenda kuonana na Madame Norah.

Kwa hakika ilikuwa kazi ngumu, tena ngumu kweli kweli! Pengine ingekuwa rahisi kwa ngamia kupenya kwenye tundu la sindano kuliko kumlainisha Sammy, maana alikuwa na msimamo thabiti! Sammy alimtazama Joyce kwa makini na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Sijakuelewa kabisa, Baba Pendo! Kwa nini hutaki niende kuonana na Madame Norah?” Joyce alimwuliza Sammy kwa mara nyingine tena baada ya kitambo kirefu cha ukimya na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Kwani hujaelewa nini katika yote niliyosema?” Sammy aliuliza huku akipitisha ulimi wake kulamba midomo yake iliyoanza kukauka.

“Yote uliyosema ni uvumi tu, hayana ukweli wowote. Mambo mengi dhidi ya Madame Norah ni ya kuzushwa tu, tena yanazushwa na watu wenye wivu, wasiopenda maendeleo yake,” Joyce alisema.

“Ya kuzushwa ki-vipi wakati kila kitu kinajionesha?” Sammy alihoji huku akimtazama Joyce kwa mshangao.

“Mimi siamini! Isitoshe mimi siyo mtoto mdogo useme kwamba naweza kushikiwa akili, ninatambua mabaya na mazuri,” Joyce alisema huku akitingisha kichwa chake taratibu.

“Hata kama huamini lakini kumbuka kuwa hakuna moshi bila moto!” Sammy alisema kwa sauti tulivu akijitahidi kuizuia hasira iliyokuwa imechipua ndani yake.

Joyce alimtazama Sammy kwa makini kwa kitambo kifupi na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Usidhani kuwa nazuia maendeleo yako bali nafanya hivi kwa sababu nakupenda…” Sammy alisema huku akijiweka vizuri pale kitandani.

“Unafanya hivi kwa sababu una wivu. Kwa sababu Madame Norah ana misimamo juu ya wanaume na anaelimisha wanawake!” Joyce alisema kwa unyonge huku akiinamisha kichwa chake kutazama chini. Sammy alishtuka sana, hakutegemea jibu kama lile kutoka kwa mkewe.

“Sijawahi kukudharau hata siku moja na wala sifikirii kuja kukudharau, lakini nalazimika kufuata ndoto zangu,” Joyce alisema na kuinua uso wake kumtazama Sammy.

Sammy alionekana kuchukizwa sana na ile kauli, alikunja sura yake na hasira ikaanza kuibuka upya ndani yake. Alikunja ngumi ya mkono wa kushoto na kwa kutumia vidole viwili; kidole gumba na kidole cha shahada akaibana pua yake na kuvuta hewa ndani kama aliyekuwa anavuta kamasi.

Joyce aligundua kuwa alikuwa amemuudhi sana mumewe, aliamua kumsogelea na hapo hapo mikono yake yote miwili ikaanza kufanya ziara kwenye mwili wa Sammy, huku mkono wa kulia ukienda moja kwa moja kwenye kifua chake na kuanza kukipapasa kile kifua chenye vinyweleo vingi.

Can you please stop this?” Sammy alisema kwa sauti iliyoonesha hasira huku akikunja sura yake, pumzi zake zilianza kumpaa.

Stop what?” Joyce aliuliza huku akimwangalia Sammy moja kwa moja machoni.

“Niangalie machoni,” Joyce alisema kwa sauti ya upole na kwa utulivu mkubwa huku akiendelea kumpapasa kifuani kwake. Sammy akamwangalia. Wakaangaliana kwa sekunde kadhaa, Sammy akakiona kile ambacho hakutarajia kukiona katika macho ya Joyce.

“Nisamehe sana mume wangu, sikukusudia kukukwaza wala kukuhuzunisha, unajua ni kiasi gani nakupenda sana na kukuheshimu, lakini sijui kwa nini wewe hutaki kuniamini!” Joyce alisema kwa sauti ya mhemo huku mikono yake ikiendelea kujivinjari kwenye mwili wa Sammy.

Sammy hakusema neno bali alibaki kimya huku akifumba macho yake kuusikilizia ule mpapaso wa mikono ya Joyce kwa makini. Hata hivyo, Joyce hakusubiri jibu la Sammy, alipeleka mkono wake wa kushoto ndani ya bukta ya Sammy na kuanza kuvinjari eneo la ikulu huku mkono wa pili ukienda moja kwa moja mgongoni.

Endelea kufuatilia stori hii ili kujua kilichojiri...
 
Poti ongeza maana leo nipo kwenye majukumu ili cku iende vyema poti
 
Joyce anataka kututia majaribuni asubuhi asubuhi jamani
 
Taxi - (29)

Ilipoishia

“Niangalie machoni,” Joyce alisema kwa sauti ya upole na kwa utulivu mkubwa huku akiendelea kumpapasa kifuani kwake. Sammy akamwangalia. Wakaangaliana kwa sekunde kadhaa, Sammy akakiona kile ambacho hakutarajia kukiona katika macho ya Joyce.

“Nisamehe sana mume wangu, sikukusudia kukukwaza wala kukuhuzunisha, unajua ni kiasi gani nakupenda sana na kukuheshimu, lakini sijui kwa nini wewe hutaki kuniamini!” Joyce alisema kwa sauti ya mhemo huku mikono yake ikiendelea kujivinjari kwenye mwili wa Sammy.

Sammy hakusema neno bali alibaki kimya huku akifumba macho yake kuusikilizia ule mpapaso wa mikono ya Joyce kwa makini. Hata hivyo, Joyce hakusubiri jibu la Sammy, alipeleka mkono wake wa kushoto ndani ya bukta ya Sammy na kuanza kuvinjari eneo la ikulu huku mkono wa pili ukienda moja kwa moja mgongoni.

Sasa endelea...

Wakati akiendelea kumpapasa, Sammy aliamua kuvunja ukimya huku akimtazama Joyce usoni.

“Joyce!” Sammy aliita kwa sauti tulivu.

“Abee, mume wangu,” Joyce aliitikia kwa sauti laini iliyokuwa na kila aina ya kiashiria cha kuhemkwa na tamaa za kimwili.

“Nimekuelewa,” Sammy alisema huku akihema kwa nguvu.

“Kweli?”

“Ndiyo.”

Joyce alitabasamu, mikono yake iliendelea kujivinjari kwenye mwili wa Sammy, macho yake bado yalikuwa usoni kwa Sammy yakimwangalia kwa makini, Sammy naye alikuwa akimwangalia Joyce kwa makini. Macho ya Joyce yalipepesa, kope zikacheza kidogo kuruhusu usafi wa macho yake. Kisha taratibu alianza kufumba macho yake.

“Nenda kazime taa,” Sammy alimwambia Joyce huku akijinyoosha na kujilaza chali kitandani, alionekana kusubiri kile ambacho kila mmoja wao alikihitaji kwa wakati huo. Joyce aliinuka haraka na kwenda kuzima taa.

Muda mfupi uliofuata walikuwa wamehama kabisa kutoka katika sayari hii, wakajikuta wakiwa katika sayari nyingine ya mbali, sayari ya mahaba mazito yenye kila aina ya vionjo vya kumtoa nyoka pangoni.

_____

Ilikuwa imetimu saa sita na nusu za usiku, Sammy na Joyce walikuwa wamelala kitandani na kupitiwa na usingizi mtamu wa uchovu baada ya kwenda mizunguko miwili iliyowafanya washindwe hata kujimudu, wote walikuwa hoi.

Sammy alikuwa amelala chali na Joyce alikuwa amelala kifuani kwake kama kifaranga cha kuku kilichokuwa kimekumbatiwa na mama yake. Mguu wake mmoja ulikuwa katikati ya mapaja ya Sammy huku mkono wake mmoja akiwa ameuzungusha shingoni kwa Sammy na alikuwa akikoroma kwa sauti hafifu ya uchovu.

Mara mlango wa chumba chao ulianza kugongwa taratibu, Joyce alishtuka na kufumbua macho yake kivivuvivu, alimtazama Sammy usoni kisha alinyanyua kichwa chake na kugeuza shingo yake kutazama kule kwenye mlango huku akipiga miayo ya uchovu.

Alijaribu kumpuuza mgongaji wa mlango na kukilaza tena kichwa chake kifuani kwa Sammy, lakini mlango ulizidi kugongwa, safari hii uligongwa kwa nguvu zaidi na kusababisha kero masikioni mwake. Joyce aliposikiliza kwa makini aliweza kuisikia sauti ya Winifrida nje ya mlango ikiita kwa hofu.

Kabla hajajua cha kufanya, yeye na Sammy kwa apamoja walijikuta wakikurupuka kutoka pale kitandani na kusimama kwa wasiwasi huku wakilitupa shuka walilokuwa wamejifunika. Walitazamana lakini hakuna aliyekuwa na jibu.

Winifrida aliendelea kugonga mlango huku akiwaita kwa nguvu, Joyce alichukua haraka khanga yake akajifunga kifuani na kuelekea mlangoni akiwa na wasiwasi, wakati huo Sammy alikuwa amekwishavaa bukta na fulana, akaelekea mlangoni na kusimama nyuma ya Joyce.

“Pendo amezidiwa hawezi kupumua vizuri, anatapatapa huku akilalamika maumivu…” Winifrida alisema kwa hofu huku akilia kilio cha kwikwi baada ya mlango kufunguliwa na kuwaona Sammy na Joyce wakimtazama kwa wasiwasi.

Bila kusubiri, Joyce na Sammy walikimbilia kwenye chumba alikokuwa amelala Pendo na kumkuta akiwa anatapatapa huku akihema kwa shida. Pendo alipowaona alianza kulalamika maumivu ya mikono na miguu.

Kwa kuwa Sammy alielewa zile dalili ziliashiria tatizo gani kwa Pendo, hakusubiri, alichukua haraka simu yake na kumpigia dereva mmoja wa teksi jirani yao ili wamkimbize Pendo hospitali.

* * * * *

Ilikuwa saa kumi na mbili na nusu ya asubuhi, sauti ya aina yake iliyoburudisha ya maji ya baharini yaliyokuwa yanachapa kingo za baharini ilipenya kwenye madirisha makubwa ya chumbani hadi pale kitandani walipolala Zainab na Mr. Oduya.

Mr. Oduya alijigeuza na wakati huo huo Zainab naye alijinyoosha kisha akamkumbatia. “Good morning, my darling!” Zainab alimsalimia Mr. Oduya huku akikishika kidevu chake kwa utani kama vile mjukuu akimtania babu yake.

Morning, my darling!” Mr. Oduya aliitika huku akipiga miayo na kuachia tabasamu, kisha akaongeza, “Mungu ni mwema, tumeamshwa salama.”

“Mungu ni mwema kweli kweli,” Zainab naye aliirudia ile kauli huku akiachia tabasamu.

Mr. Oduya alijinyoosha kisha akainuka na kuketi pale kitandani, miguu yake ikakanyaga sakafuni, alishusha pumzi na kuinuka huku akiendelea kujinyoosha na kusogea upande wa pili ilipokuwa simu yake ya mkononi, akaichukua na kuiwasha, kwani ilikuwa imezimwa.

Alikuwa amelazimika kuizima simu yake kwani shughuli iliyofanyika usiku wa kuamkia siku ile ilikuwa supa. Zainab alikuwa amemtaka aizime ili kusiwe na kitu chochote cha kuingilia faragha yao, naye akatii.

“Sihitaji simu yoyote saa hizi, nimekuja kwa ajili yako, ni mimi na wewe tu hadi lyamba…” Mr. Oduya alikumbuka kuambiwa na Zainab usiku kabla hawajalala.

Usiku wa kuamkia siku ile Mr. Oduya alipofika Paradise Club ilikuwa imeshatimu saa nne za usiku. Alimkuta Zainab akiwa amejifunga khanga moja tu nyepesi na alipogonga mlango haraka Zainab alimfungulia na kumrukia, akakumbatia kwa mahaba.

“Waoo… pole mpenzi wangu, naona umechoka sana,” Zainab alimwambia huku akiupokea mkoba wa kiofisi aliokuwa kaubeba na kuupeleka moja kwa moja chumbani.

“Asante sana, mke wangu mpenzi,” Mr. Oduya alisema huku akimfuata Zainab kule chumbani, kisha akajipweteka juu ya kitanda.

Inaendelea...
 
Taxi - (30)

Zainab alimsogelea akaimvua koti lake kisha alimvua viatu na soksi, halafu akamfungua tai yake shingoni na kufungua vifungo vya shati lake huku akimtazama usoni kwa tabasamu.

“Samahani mpenzi, naomba nikufungue mkanda wa suruali,” Zainab alisema kwa sauti tamu ya mahaba akiomba ruhusa kwa Mr. Oduya.

Mr. Oduya alimtazama kwa makini na kuachia tabasamu huku akishusha pumzi.

Darling!” Mr. Oduya aliita kiwa sauti ya kunong’ona.

“Abee!”

“Unaweza kufanya chochote, mwili huu ni mali yako.”

“Asante sana mpenzi, unapaswa kuhudumiwa maana unachoka na kazi nyingi, una mambo mengi ya kufanya, pole sana ninajua akili yako haijatulia.”

“Asante sana, mpenzi wangu, ndiyo maana nakupenda kuliko kitu chochote,” Mr. Oduya alisema na kupitisha mkono wake kichwani, kuanzia kwenye paji la uso kuelekea usogoni na alipofika mwisho wa kichwa alipitisha mkono wake shingoni mwake na akawa kama anayejinyoosha.

Kisha aligeuka upande wa kushoto na kulia huku akitoa miguno ya uchovu hasa.

“Pole sana. Umeshakula?” Zainab alimuuliza Mr. Oduya huku akiivua suruali yake na kumwacha akiwa na boksa tu.

“Hapana sijala,” Mr. Oduya alijibu huku akijilegeza.

“Sijui utakula kwanza ndiyo ule au unakula kwanza halafu ndiyo utakula?” Zainab alimuuliza Mr. Oduya kwa sauti laini ya mahaba na kumfanya Mr. Oduya amwangalie kwa makini kabla ya kuachia tabasamu lililozaa kicheko hafifu.

“Kabla hujajibu ngoja kwanza nikupunguze uchovu,” Zainabu alisema kabla hata Mr. Oduya hajajua ajibu nini.

Haraka bila kuchelewa, Zainab alimsukuma Mr. Oduya, akaanguka chali pale kitandani kisha alimgeuza vyema akalalia tumbo lake kisha alipanda juu yake akakaa vyema, alichukua mafuta laini (lotion) aliyokuwa ameyaandaa na kuanza kumpaka Mr. Oduya eneo la mgongoni na shingoni kisha akaanza kumsinga kwa ufundi wa hali ya juu. Wenyewe huita kumfanyia masaji.

Mr. Oduya alitulia kimya wakati Zainab akifanya kazi yake kwa ufundi, alikuwa akifurahia sana kila kitu alichokuwa anafanyiwa na Zainab.

“Darling, yaani namna unavyonikanda najisikia burudani hasa, kwa kweli nimemisi sana kufanyiwa haya mambo,” Mr. Oduya alisema huku akihisi faraja ya aina yake.

“Usijali mpenzi, nimekuja Tanzania kwa ajili yako… hii ndiyo kazi yangu,” Zainab alisema huku akiendelea kuukanda kanda mgongo wa Mr. Oduya, kisha akashuka mapajani na baadaye akapanda hadi shingoni, mpaka kichwani.

Hadi muda huo Mr. Oduya alikuwa kazidiwa, kwani macho yake yalishabadilika na kuwa mekundu kabisa. Hii ndiyo faraja aliyokuwa akiikosa ndani ya ndoa yake na kuamua kuitafuta nje ya ndoa yake. Hakika kwenye ndoa nyingi mambo kama haya hukosekana.

Wanawake wengi ni wavivu sana kwenye ndoa zao, na ndiyo maana shetani ameweza kutumia mbinu hii kusambaratisha ndoa nyingi… cha ajabu wanawake hawa wanajituma sana kwenye uzinzi lakini kwenye ndoa zao wala hawajitumi!

Baada ya kazi ile ya kusingwa, kilichofuata kiliiongeza njaa ya Mr. Oduya mara dufu, alihisi kizunguzungu kutokana na garidwe la aina yake alilochezeshwa na Zainab, gwaride lililomuacha akihema ovyo kama bata.

Walipomaliza waliingia maliwatoni, kilikuwa chumba kikubwa cha maliwato yenye hadhi yake yaliyoweza kumsahaulisha majonzi hata aliyefiwa na ampendaye.

Waliingia kwenye jakuzi na kutulia humo miili yao ikiwa inakandwa na maji ya uvuguvugu…

“Unawaza nini, mpenzi?” sauti ya Zainab ilimzindua Mr. Oduya aliyekuwa amesimama wima akimkodolea macho Zainab pasipo kumuona.

“Ah, wala usijali… nilikuwa nayakumbuka mautundu yako,” Mr. Oduya alisema huku akipiga miayo mfululizo na kuchukua taulo lake, akajifunga kiunoni kisha akaelekea jikoni. Alitengeneza vikombe viwili vya kahawa na baada ya dakika chache alirudi chumbani, kikombe kimoja akampatia Zainab.

Welcome, my darling,” Mr. Oduya alisema kwa mahaba huku akiachia tabasamu pana usoni kwake.

Thank you,” Zainab alisema huku akiinuka, akajifunga kipande cha khanga nyepesi kifuani na kukaa pembeni ya Mr. Oduya.

No, darling…” Mr. Oduya alisema huku akitingisha kichwa chake taratibu. “Ukiona nimekaa, unatakiwa kukaa hapa,” alisema huku akijipigapiga juu ya paja lake.

“Kaa hapa mpenzi wangu…” Mr. Oduya alisisitiza na kumfanya Zainab aangue kicheko hafifu cha mahaba huku akiinuka na kumkalia juu ya paja lake, kisha wakawa wanakunywa kahawa taratibu.

Walipomaliza kunywa kahawa wakaelekea maliwato, walijimwagia maji na kurudi chumbani wakiwa wamepata nguvu mpya. Mr. Oduya alivaa bukta na kukaa kitandani kisha akaanza kuvuta mkoba wake wa kiofisi, Zainab alimtazama kwa makini na kuufuata ule mkoba.

Darling, nikusaidie?” Zainab alimuuliza kwa sauti ya mahaba.

No… unajua sipaswi kukusumbua na kukuchosha, wewe ni malkia… isitoshe mwanamke siyo roboti, relax…” Mr. Oduya alisema huku akimpapasa Zainab mgongoni kwa mahaba.

“Wala hunisumbui mpenzi, it’s just loves, najisikia tu kukusaidia…” Zainab alisema lakini akakatishwa na mlio wa sauti ya kengere ya mlangoni iliyoita kwa fujo huko sebuleni na sauti yake kupenya hadi chumbani, wakatazamana. Ni kama walikuwa wanaulizana ‘ni nani?’

Zainab alitoka chumbani akaelekea sebuleni na kuchungulia kwenye tundu maalumu la mlangoni lenye kioo cha lenzi, akamuona Lilian akiwa amesimama nje ya mlango. Akashusha pumzi na kuufungua mlango.

“Ooh, Lilian… karibu mdogo wangu, naona umeniwahi,” Zainab alisema huku akisogea kando kumpisha Lilian aingie.

“Asante sana madame, habari za asubuhi?” Lilian alisema huku akiingia na kusimama pale sebuleni.

“Nzuri Lilian… unaweza kuendelea na kazi, kama kutakuwa na chochote utaniita nipo chumbani,” Zainab alimwambia Lilian na kurejea chumbani alikomwacha Mr. Oduya.

Inaendelea...
 
Taxi - (31)

“Nzuri Lilian… unaweza kuendelea na kazi, kama kutakuwa na chochote utaniita nipo chumbani,” Zainab alimwambia Lilian na kurejea chumbani alikomwacha Mr. Oduya.

* * * * *

Saa nne asubuhi siku ya Jumapili, katika chumba kikubwa cha wadi maalumu ya VIP ya Hospitali ya Dar Group iliyopo barabara ya Nyerere jirani na Tazara, jijini Dar es Salaam, Sammy alikuwa amesimama kando ya kitanda alicholala Pendo, akionekana mwenye huzuni.

Chumba kile kilikuwa kikubwa chenye vitanda viwili na dirisha kubwa lililokuwa linaingiza hewa safi, na juu kulikuwa na dari nzuri iliyotengenezwa kwa gypsum ya rangi nyeupe na katika sehemu za dari ile kulining’inizwa taa nzuri na pangaboi.

Kitanda alicholala Pendo kilikuwa cheupe cha chuma chenye godoro nene la foronya laini na mto laini wa kuegemeza kichwa. Pendo alikuwa bado anapumua kwa shida kutokana na kusumbuliwa na tatizo la seli mundu lililosababisha kupungukiwa damu na matatizo ya kupumua.

Kando ya kile kitanda kulikuwa na stendi ndefu ya chuma ya kitabibu iliyokuwa imetundikiwa chupa ndogo ya damu na mrija wake ukipeleka damu kwenye mshipa wa damu mkononi kwa Pendo.

Kando ya ile stendi ya chuma kulikuwa na meza ndogo na juu yake kulikuwa na trei ndogo ya chuma iliyokuwa na vifaa-tiba kama mkasi, plasta, bomba la sindano, glovu, chupa kubwa ya maji, bilauri na dawa za vidonge kwa ajili ya tatizo la seli mundu.

Baadhi ya vile vifaa vilikuwa vimefunguliwa na kuachwa wazi kitendo kilichoashiria kuwa tayari vilikuwa vimekwisha tumika.

Winifrida alikuwa ameketi kwa utulivu juu ya kitanda cha pili mle chumbani akimtazama Pendo kwa huzuni, alionekana mbali kimawazo na machozi yalikuwa yanamlenga machoni. Chumba kilikuwa na ukimya wa aina yake.

Muda ule ule mlango wa kile chumba ulifunguliwa, Daktari wa magonjwa ya watoto, Daktari Beda Msimbe aliingia akiwa ameongozana na muuguzi wa wodi ile ya watoto

Daktari Msimbe alikuwa mwanamume mfupi mnene na rangi ya ngozi yake ilikuwa ya maji ya kunde, akiwa na umri wa miaka hamsini na saba alikuwa na nywele fupi zenye mvi kiasi na uso wake ulikuwa mpana huku miwani yake mikubwa ikiwa imeyahifadhi macho yake makubwa.

Alikuwa amevaa suruali ya kitambaa cha kadeti cha rangi ya khaki, shati kubwa jeusi lililokuwa na mistari myeupe ya pundamilia na juu yake alikuwa amevaa koti refu jeupe la kidaktari na kuning’iniza shingoni kwake kifaa maalumu cha kupimia, kwa kitaalamu kiliitwa ‘stethoscope’.

Daktari Msimbe alikwenda moja kwa moja kitandani kwa Pendo akapishana na Winifrida aliyeinuka na kutoka nje. Daktari Msimbe alisimama akimchunguza Pendo kwa macho na kumgusa kwenye paji la uso wake, kisha aliiangalia kwa makini damu iliyokuwamo ndani ya chupa aliyotundikiwa Pendo.

Aliangalia kwa makini jinsi matone ya damu yalivyokuwa yakidondoka na kuingia kwenye mrija maalumu uliopeleka damu kwenye mshipa wa damu mkononi kwa Pendo na kuonekana kuridhika kisha alipeleka macho yake kusoma maelezo kwenye faili la ugonjwa wa Pendo alilokuwa amelishika mkononi na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

Baada ya kusoma maelezo kwa kitambo kifupi aliinua uso wake kumtazama muuguzi mmoja aliyefuatana naye, wakaonekana kuongea jambo fulani kwa lugha ya kitabibu, kuhusiana na tatizo la Pendo. Yule muuguzi alibetua kichwa chake kukubali.

Muuguzi alikuwa mwanamke wa umri wa kati ya miaka ishirini na nane na therathini, mrefu wa wastani, si mweusi wala si mweupe kwa rangi. Alikuwa na mashavu mfano wa chungwa na alikuwa na nywele nyingi kichwani, nyeusi fii.

Alikuwa amevaa gauni jeupe refu na pana kiasi lakini lililokuwa limeushika vyema mwili wake na kulichora vyema umbo lake kubwa. Kiunoni alikuwa amevaa mkanda mpana mweusi na kofia ndogo nyeupe ya kiuguzi yenye lesi iliyofunika sehemu ya utosi wa mbele kichwani kwake.

Baada ya mazungumzo mafupi ya kitabibu kati ya Daktari Msimbe na muuguzi, Daktari Msimbe aliandika taarifa fulani kwenye lile faili la ugonjwa wa Pendo kisha alimgeukia Sammy aliyekuwa amesimama kando ya kile kitanda akionekana mwenye huzuni.

“Poleni sana na kuuguza, Mungu atamsaidia mtoto na atakuwa sawa,” Daktari Msimbe alisema na kuachia tabasamu.

“Asante sana daktari,” Sammy alisema huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani na kumeza mate kutowesha koo lake lililokauka.

Kisha Daktari Msimbe aliachia tabasamu pana la kufariji na kuanza kupiga hatua kuondoka, alifungua mlango na kutoka huku akifuatwa na yule muuguzi.

Kule nje Winifrida alikuwa amesimama na kujiegemeza kwenye ukuta wa korido pana na ndefu iliyozitenganisha zile wodi, alionekana kutafakari sana. Aligeuka kumwangalia Joyce aliyekuwa ameketi kwenye benchi huku akiongea na simu.

Muda huo huo alimuona muuguzi mmoja wa kiume aliyekuwa akipita eneo lile akisukuma kiti cha magurudumu kilichokuwa kimekaliwa na mgonjwa mmoja aliyeonekana kama nusu mfu huku akiwa ametundikiwa chupa ya maji na mrija wake ulipeleka maji kwenye mshipa wa damu wa mkono wake wa kulia.

Joyce akiwa na uso wenye huzuni aligeuza shingo yake kumwangalia yule mgonjwa na kushusha pumzi za ndani kwa ndani huku akiendela kusikiliza simu. Alionekana kukubali jambo kwa kubetua kichwa chake na kuvuta pumzi ndefu kisha akazishusha taratibu. Muda mwingi alionekana kama aliyekuwa katikati ya mtihani mgumu sana.

“Ni kweli mama, lakini hapa nipo njia panda… hali ya mjukuu wako hadi sasa siyo nzuri kabisa…” Joyce alisema huku akivuta kamasi nyepesi kutokana na machozi mepesi yaliyokuwa yakimtoka machoni.

Aliyazungusha macho yake na kumwona Winifrida akiwa amejiegemeza kwenye ukuta huku akifuta machozi yaliyomtoka, Joyce alimtazama kwa makini na kuonekana kusita kidogo, kisha alishusha pumzi za ndani kwa ndani.

Inaendelea...
 
Taxi - (32)

“Haya mama, ngoja nione itakavyokuwa halafu nitakupigia simu kukujulisha… lakini nisingependa kabisa kuikosa fursa hii muhimu kwangu!” Joyce alisema na kukata simu yake akionekana kuchanganyikiwa.

Aliinuka na kuondoka haraka eneo lile, akaingia wodini na kusimama karibu na Sammy huku akimwangalia Pendo kwa makini, huzuni ilikuwa inajionesha waziwazi kwenye macho yake. Sammy aligeuza shingo yake kumtazama Joyce, wakatazamana bila kusema neno. Joyce alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kubetua juu mabega yake.

* * * * *

Saa saba mchana Paradise Club, Zainab alikuwa ameketi kwenye sofa sebuleni akisoma magazeti ya siku ile, uso wake ulikuwa umeliinamia gazeti moja la kila siku lililokuwa limeandikwa kwa lugha ya Kiingereza, hali iliyoonesha kuwa alikuwa amenogewa na habari iliyoandikwa gazetini.

Ilikuwa ni habari-muendelezo iliyohusu kutoweka kwa mwandishi mahiri wa habari za uchunguzi wa gazeti la MamboLeo, Abbas Dalali, ambaye hakuna yeyote aliyejua yupo wapi, na kama ni mzima au mfu.

Kabla ya hapo, Zainab alikuwa amesoma habari nyingine mbili, moja ilihusu mke kumuua mumewe kwa kumchoma na kitu chenye ncha kali, na nyingine ilihusu mume kumuua mkewe kwa kumbanika kwenye mkaa wa moto kama ndafu. Hizi ni habari alizokutana nazo kwenye magazeti karibu yote ya siku ile.

Hii ndiyo Tanzania ambayo utafiti ulionesha kuwa ilikuwa miongoni mwa nchi zilizoongoza kwa watu wake kutokuwa na furaha! Ndiyo maana kila kukicha habari za matukio ya wenzi kuuana zilitawala!

Lakini… mbona hata nchi zilizoendelea zenye watu wanaoishi kwa furaha bado matukio kama hayo yalikuwepo, tena ni kwa kiwango kikubwa? Zainab alikumbuka kushuhudia matukio mengi ya mke kumuua mume au mume kuua familia yake yote, au mtoto kuua wazazi wake nchini Canada na hata Marekani!

“Sasa nini kifanyike?” alijiuliza bila kupata jibu huku akiyatupa yale magazeti kando. Alikumbuka kuwa hata yeye aliwahi kutuhumiwa kumuua mumewe Hemed miaka kumi na miwili iliyopita, na vyombo vya habari viliandika sana kuhusu hilo.

Zainab alimeza funda kubwa la mate kutowesha koo lake lililokuwa limekauka, alitamani sana habari ile ya mauaaji ya Hemed ibaki kuwa hadithi ya kutunga, hakupenda kukumbuka, lakini haikuwa hivyo. Mawazo sasa yalianza kupita kichwani kwake utadhani alikuwa akitazama sinema, aliyakumbuka maisha ya kijijini Mkuzi katika Wilaya ya Muheza mkoani Tanga, alikozaliwa akiwa mtoto wa tatu na wa mwisho kwa mama, Bi Rehema, ambaye hakuwahi kuolewa.

Zainab ndiye mtoto pekee aliyesoma hadi kumaliza kidato cha nne ingawa hakuwa na ujuzi wowote wa maana, kwani hata hiyo elimu ya kidato cha nne aliimaliza kwa mbinde baada ya baba yake mzazi, Adam Semaya kufa na mama yao kuugua ugonjwa wa ajabu.

Zainab alipozaliwa aliwakuta dada zake wawili waliomtangulia, Nuru Mhina na Zuena Shauri ambao kila mmoja alikuwa na baba yake na hakuna kati yao aliyewahi kumfahamu baba yake, ni Zainab pekee aliyebahatika kumfahamu baba’ake, ingawa hata yeye alikuwa mtoto wa nje ya ndoa, kwani Bi Rehema hakuwa mmoja wa wake wanne wa Adam Semaya.

Japo maisha ya Bi Rehema hayakuwa mazuri lakini alijitahidi sana kuhakikisha binti zake wanasoma. Alikubali kufanya kazi dhalili katika mazingira magumu mno, kiasi cha kumuondolea utu na heshima kwa jamii ili tu binti zake wapate elimu aliyoamini ingewakomboa toka katika lindi la ufakiri.

Aliwahimiza sana binti zake kusoma kwani hakutaka na wao waishie alikoishia yeye, akiwa na wasiwasi kuwa kama angekufa wasingepata msaada kwa ndugu, kwa kuwa yeye alikuwa na ndugu wachache sana aliowafahamu upande wa mama yake, ambao hawakuwa ndugu wa damu, na hakumjua ndugu yeyote upande wa baba.

Bi Rehema hakujua alikotokea mama yake wala ndugu wa baba’ake, na siku zote alikuwa akisononeka zaidi, kwa kujua kuwa binti zake pia wangefuruka na kuishi maisha ya kubangaiza kijijini kama yeye endapo wasingetia bidii kusoma, ndiyo maana aliwahimiza sana kusoma.

Lakini maisha yalibadilika sana baada ya binti zake wakubwa, Nuru na Zuena kupachikwa ujauzito, kwa nyakati tofauti, wakiwa sekondari na kufukuzwa shule. Nuru hakurudi nyumbani, alitorokea kusikojulikana! Lakini Zuena alirudi kulea ujauzito wake nyumbani, na alipojifungua mtoto hakukaa hata mwezi akafa. Zuena akawa amekosa mwana na masomo, hivyo aliondoka nyumbani na kuelekea Arusha na kuanzia hapo hakuna tena aliyejua taarifa zake.

Kuanzia hapo Bi Rehema alianza kuumwa hiki na kile na miaka kadhaa baadaye Mzee Semaya alikufa ghafla baada ya kuanguka chooni, wakati huo Zainab alikuwa kidato cha kwanza. Hali ya Bi Rehema ilibadilika zaidi, alianza kuwa mtu wa kuuguzwa. Hakuna aliyejua alikuwa anaumwa ugonjwa gani, walipima na kupima lakini hawakuona ugonjwa wowote.

Aliendelea kuugua tu. Mara alalamike kuhusu miguu, mara alalamikie maumivu ya mgongo, mara kichwa! Ili mradi, hakukuwa na machweo yaliyopita asiwe katika hali ya kulalamikia maumivu. Katika kuhangaika huku na kule ikasemekana kuwa alikuwa amelogwa. Waliambiwa kuwa mchawi wake alikuwa ni mke mkubwa wa Adam Semaya

Lakini Daktari wa afya ya akili wa Hospitali Teule ya Muheza aligundua kilichokuwa kinamsumbua na kuwaeleza kuwa alisumbuliwa zaidi ni msongo mkali wa mawazo. Hili la msongo mkali wa mawazo hakuna aliyelielewa, hivyo walichagua kuamini katika ushirikina kuwa alilogwa, kwani ilikuwa rahisi kwao kuelewa hilo kuliko kuambiwa mawazo yakizidi huleta ugonjwa.

Zainab alikuwa na miaka kumi na nane alipomaliza kidato cha nne huko Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Korogwe. Rafiki wa baba yake aliyeitwa Julius Mhilu, ambaye alikuwa mhariri wa gazeti moja maarufu jijini Dar es Salaam, alimfanyia mpango wa kumpatia kazi katika hoteli ya kitalii ya Kilimanjaro, kwani alikuwa akifahamiana na wakubwa wengi serikalini.

Zainab hakwenda popote kwa ajili ya mafunzo ya kazi hiyo kama wafanyavyo wasichana wengine, kwa kuwa alipenda sana kufanya kazi, hivyo ilimchukua muda mfupi tu kuimudu kazi hiyo.

Alifanya kazi kwa bidii huku akijitahidi sana kumsaidia mama yake mgonjwa, kwa kutuma fedha kidogo nyumbani kila mwezi, kwani wakati huo ni yeye pekee aliyebakia kumsaidia mama yake kwa kuwa dada zake wote hawakuwepo nyumbani na hakuna aliyejua walikokuwa, isitoshe hakukuwa na mtu mwingine wa kumsaidia mama yao.

Ni katika hoteli ile ya Kilimanjaro ndipo siku moja alikutana na Hemed Kimaro, mfanyabiashara wa madini. Kama ilivyokuwa kwa dada zake, Zainab alikuwa msichana mrembo kweli kweli na kila mwanamume alikuwa yuko tayari kutoa roho yake ili amuoe.

Inaendelea...
 
Taxi - (33)

Hemed alishindwa kuvumilia baada ya kumwona Zainab na kuamua kuingia mzima mzima kwenye mbio za kumfukuzia. Aliporusha ndoano hakuamini baada ya kuona akiibuka na ushindi. Hawakuwa na muda mrefu wa mazungumzo, na huo mfupi ulitosha kabisa kuwajulisha kuwa kila mmoja alitokea kumpenda mwenziwe. Miezi michache baadaye wakafunga ndoa.

Miezi ikaanza kusonga na hatimaye mwaka mmoja ukakatika lakini Hemed hakuwa mjuzi wa masuala ya ndoa, aliyachukulia kama jambo la kawaida sana na hakujali hisia za mwenzi wake wala kumfikisha alikotaka kufika kimapenzi. Muda mwingi alikuwa ‘bize’ na biashara zake na akirudi nyumbani amechoka, analala, wakati Zainab alitaka kufurahia ndoa yake…

Miaka mingine miwili ikapita tangu na hali ilikuwa ile ile, hatimaye mwaka wa nne ukafika lakini mambo haya kubadilika, yalibaki kuwa yale yale! Tena yalianza kuwa mabaya zaidi. Hemed alikuwa bize zaidi kiasi cha kuchelewa hata kurudi nyumbani na wakati mwingine hadi usiku wa manane. Siku moja Zainab alilala sebuleni kumsubiri mumewe kwa saa nyingi lakini hakurejea kabisa.

Hata aliporejea siku iliyofuata Zainab alimkabili kumuuliza alilala wapi, lakini alijibiwa kirahisi rahisi tu, Zainab kwa kumpenda mumewe alijitahidi kuvumilia akiamini kuwa huo ulikuwa ni upepo mbaya tu uliokuwa ukipita na muda si mrefu maisha yangesonga vyema.

Kutahamaki mwaka wa tano! Zainab alishangaa, mwaka wa tano katika ndoa lakini mambo ni yale yale na hawakuwa na mtoto, wala Hemed hakuonesha kushtuka. Ni wazi Hemed aliendelea kuchukulia mambo ya ndoa kirahisi rahisi.

Usiku Zainab alikuwa hapati usingizi, muda mwingi alikuwa anawaza kuhusu hatma ya ndoa yake, akibaki peke yake alikuwa analia tu, donge la hasira lilimkaba kooni na hakuweza kulihimili mpaka atoe kilio. Siku moja alijiuliza sana na kuamua kupeleka shauri lao kwa wifi yake mkubwa, Dk. Salma Oduya.

Hapo ndipo mume wa wifi yake, Mr. Oduya alipopata mwanya wa kuwa na ukaribu na Zainab na baadaye kupenyeza ushawishi wake, haikuchukua muda wote wawili wakagundua kuwa kila mmoja alihitaji faraja lakini wote walionekana kuikosa katika ndoa zao. Hawakuwa na njia nyingine isipokuwa kuitafuta nje ya ndoa na hatimaye Zainab akapata ujauzito…

_____

“Madame, kuna tatizo lolote?” sauti laini ya Lilian ilipenya hadi kwenye ngoma ya masikio ya Zainab na kumzindua kutoka kwenye lindi la mawazo. Aliinua uso wake kumtazama Lilian aliyesimama mbele yake na kushusha pumzi za ndani kwa ndani huku akilazimisha tabasamu.

Lilian alikuwa amesimama pale kwa kitambo kirefu akimsemesha Zainab lakini ilionesha kuwa Zainab alikuwa mbali kimawazo. Alimtazama Zainab kwa macho yenye udadisi na mkononi alikuwa ameshika bilauri na chupa ndefu ya mvinyo mwekundu wa bei ghali aina ya Romanee-Conti uliotengenezwa nchini Ufaransa.

“Kinywaji chako hiki hapa, madame,” Lilian aliongea kwa sauti tulivu huku macho yake yakiendelea kuweka kituo kwenye uso wa Zainab.

Na hapo Zainab akakumbuka kuwa alipokuwa anasoma magazeti alimuagiza Lilian kumtafutia mvinyo mwekundu wa Kifaransa aina ya Navette de Marseille au Romanee-Conti.

Ah, usijali mdogo wangu… weka hapo,” Zainab alisema huku akimuonesha Lilian ilipo meza, alijitahidi kuupamba uso wake na tabasamu na kuyakwepa macho ya Lilian. Alikuwa analengwa na machozi kutokana na kukumbuka mengi katika maisha yake ya zamani.

Kumbukumbu zile zilikuwa zimemuumiza sana, hasa kwa kuwa mama yake Bi Rehema alikufa kwa msongo mkali wa mawazo miezi miwili tu baada ya yeye Zainab kutuhumiwa kushiriki katika mauaji ya mumewe, Hemed.

“Asante sana mdogo wangu, unaweza kuendelea na kazi zako kama nikihitaji kitu nitakujulisha,” Zainab alimwambia Lilian baada ya kuona alikuwa bado amesimama mbele yake akisubiri maagizo. Lilian aligeuka na kuondoka haraka kutoka eneo lile, akaelekea jikoni huku akiwa na wasiwasi.

* * * * *

Saa saba mchana katika ofisi za Mr. Oduya zilizo ghorofa ya sita ya jengo la ghorofa kumi na mbili lililomilikiwa na Mr. Oduya, jengo lililokuwa katika barabara ya Bagamoyo eneo la Kijitonyama jijini Dar es Salaam, mfanyabiashara huyo na mgeni wake, Balozi Aldolf Mageuzi, walikuwa wanabadilishana mawili matatu.

Ni Balozi Mageuzi aliyeomba kuonana na Mr. Oduya mchana ule, na yeye hakuweza kukataa ombi lake kwa kuwa alikuwa mmoja kati ya watu muhimu na walioheshimika sana. Balozi Mageuzi alikuwa kati ya washauri muhimu sana wa Rais wa Tanzania, Dk. Yohana Funguo, hasa katika masuala ya diplomasia, ulinzi na usalama wa taifa.

Ni kwa sababu ya kutambua umuhimu wake ndiyo maana mchana wa Jumapili ile Mr. Oduya aliondoka Paradise Club akimwacha kipenzi chake Zainab, badala yake alitenga muda ili aweze kuonana na Balozi Mageuzi.

Balozi Mageuzi alifika pale kuongea na Mr. Oduya ili kujua upepo wa kisiasa kwa upande wake ulikuwaje, hasa baada ya kushuhudia vuguvugu la urais ndani ya Chama Cha Ukombozi (CCU) likizidi kupamba moto, kwani Rais Yohana Funguo alikuwa mbioni kumaliza muhula wake wa pili.

“Niseme ukweli, upepo wa kisiasa si mbaya, unavuma vizuri sana licha ya changamoto za hapa na pale kutok kwa washindani wangu lakini nimekwisha jiweka vizuri sana kwani nina sapoti kubwa ya mabilionea wa Paradise Club na wamekubali kufadhili kampeni zangu nchi nzima,” Mr. Oduya alimwambia Balozi Mageuzi.

“Ni jambo zuri lakini kumbuka awamu hii siyo ile ya Rais Sakaya Mkiete, hii ni ya Dk. Funguo, na mfumo wote ndani ya CCU umebadilika, sidhani kama hao mabilionea wana ushawishi mkubwa ndani ya chama, labda nje ya chama. Hata hivyo, bado sina wasiwasi na nguvu yako ingawa hupaswi kujipa uhakika sana,” Balozi Mageuzi alisema huku akimwangalia Mr. Oduya kwa makini.

“Kwa nini unasema hivyo, Balozi?” Mr. Oduya aliuliza huku akimkazia macho Balozi Mageuzi.

“Kwa hali ilivyo, hamasa ya kuwania uteuzi imeongezeka sana ndani ya chama. Ila bado imeendelea kuwa siri ni nani na nani watajitosa kuwania uteuzi. Lakini najua mheshimiwa Tumbo na Dk. Hussein Abbas watawania…” Balozi Mageuzi alisema na kuongeza.

Usikose kufuatilia mkasa huu wa kusisimua ili kujua kitakachoendelea...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom