Stori ya kusisimua - Taxi

Stori ya kusisimua - Taxi

Taxi - (106)

ILIPOISHIA

“Kwani ni nani aliyewajulisha polisi kuhusu uwepo wa watu hao nyumbani kwako?” Tunu alizidi kumsaili Sammy akionesha shauku ya kutaka kujua.

“Hapo ndipo penye kizungumkuti, hajulikani nani aliwapigia simu, tumemuuliza Winifrida lakini amekana kupiga simu, ingawa polisi wanadai kuwa mpigaji alikuwa mwanamke na aliwaambia kuwa alikuwa amejificha ndani ya nyumba hiyo iliyovamiwa!”
“Kwani Winifrida ana simu?”

“Hana,” Sammy alijibu pasipo kufikiri.

“Una uhakika?” Tunu aliuliza kwa sauti iliyoonesha shaka fulani, bado alikuwa ameyatuliza macho yake usoni kwa Sammy katika namna ya kuyasoma mawazo yake.

Sammy alifikiria kidogo na kushusha pumzi, akatingisha kichwa chake taratibu kushoto na kulia kukataa. “Hata sijui!”

“Kwa hiyo polisi wanasemaje, wamekwisha wabaini waliofanya tukio hilo?” Tunu aliuliza baada ya kufikiria kwa kitambo kidogo.

“Bado wanaendelea na upelelezi, ila nilipozungumza nao leo asubuhi walisema kuwa wamebaini vitu vichache, hususani alama za viatu walivyokuwa wamevaa watu hao na maganda ya risasi.”

ENDELEA...

“Nadhani huo ni mwanzo mzuri...” Tunu alisema na kushusha pumzi za ndani kwa ndani. “Hata hivyo, itakuwa vizuri ukifahamu kuwa mlengwa wa tukio hilo ulikuwa ni wewe na wala siyo mkeo.”

Sammy alionesha kushtuka kidogo, alimtazama Tunu kwa kitambo kirefu bila kusema neno na kushusha pumzi. Kisha alimudu kuuliza, “Kwa nini unasema hivyo?”

“Fikiria mwenyewe, umepigiwa simu kuwa mwanao amezidiwa jambo ambalo ni uongo, ukiwa njiani unatekwa na watu wanaotafuta memory card ambayo kwa vyovyote itakuwa na siri fulani, unapofika nyumbani unakuta mkeo kapigwa risasi na mambo mengine mengi yanayokifanya kisa hiki kuwa katika mlolongo mrefu! Hudhani pengine simu uliyopigiwa ilikuwa ndiyo simu ya kifo chako mwenyewe?” Tunu aliuliza na kushusha pumzi. “Kuwa makini Sammy, usimwamini mtu yeyote kirahisirahisi, hata kama ni mimi!”

Sammy alimtazama Tunu kwa mshangao kama aliyeona kiumbe cha kushangaza toka sayari za mbali, akajikuta akifikiria kidogo na kushusha pumzi. Alihisi kuwepo kwa ukweli kwenye maneno ya Tunu, maana alivyokuja kuambiwa bi kwamba hata simu aliyokuwa amepigiwa na Joyce usiku kuhusu ugonjwa wa Pendo ilikuwa ni maelekezo toka kwa watu waliovamia nyumbani kwake.

“Kwa mlolongo huo naweza kukubaliana na wewe, hata hivyo, sioni kama nina maadui kiasi cha kutaka kuniua, kwani nimewakosea nini!” Sammy alisema baada ya kitambo kifupi cha ukimya.

“Huwezi kujua, unaweza kudhani huna adui kumbe wapo, tena maadui wenye nguvu kubwa kiuchumi na hata kisiasa! Na huenda katika shughuli zako ukawa umeingilia maslahi ya watu fulani wakubwa...” Tunu alisema huku akimkazia macho Sammy kuona kama maneno yale yalikuwa yanamwingia. “Na inaonekana kabisa watu hao wanahisi kuwa una kitu au taarifa fulani nyeti zinazowahusu.”

Sammy alihisi jasho jepesi likimtoka mwilini na ubaridi wa woga ukimwingia na kupenya hadi kwenye mifupa yake. Maneno ya Tunu yalimpeleka mbali, yalimrudisha kwenye mzozo wake na Spoiler baada ya kugunduliwa kuwa alikuwa amesikia siri za Mr. Oduya.

“Ni Mr. Oduya!” Sammy aliwaza. “Huyu mzee si wa kumfanyia mchezo hata kidogo. Mambo machache niliyoyasikia kutoka kwake yananipa picha tosha kuwa huyu mzee ni mafia na ndiye amehusika kwenye tukio hili. Hata hivyo, kupambana naye inataka ujasiri mkubwa.”

Alipowaza mara picha ya Spoiler akimfuata pale nje ya ukuta wa Udzungwa Beach Resort siku ile alipopewa barua ya kusimamishwa kazi ikamjia Sammy kichwani. Akakumbuka kila neno la kitisho aliloambiwa na Spoiler, hasa kuhusu familia yake: “very soon nitapafahamu nyumbani kwako, nitamfahamu mkeo na hata shule wanayosoma watoto wako, kama unao… hivyo usinilazimishe kufanya kitu utakachokuja kukijutia baadaye...

Sammy akajikuta akisisimkwa mwili wake huku damu ikianza kumchemka na kukimbia kwenye mishipa yake ya damu, aliikumbuka vyema kauli hiyo na roho ilimuuma sana kwa kutochukua tahadhari, aliuma meno yake kwa hasira. Alikuwa anahofia. Moyo wake ulikuwa unakita kwa nguvu na kwa kasi. Haya mambo hayakuwa katika nyanja yake kabisa!

“Kwa kitendo hiki walichomfanyia mke wangu ni lazima walipe na ikibidi wafikishwe katika vyombo vya sheria kujibu mashtaka dhidi yao,” Sammy aliapa kimoyomoyo. Ni wazi ujio wa Tunu ulikuwa umemfumbua macho.

“Jaribio lao la kwanza lilikuwa kuniteka mimi ili wapate memory card ambayo hata sijui inahusu nini, limegonga mwamba. Jaribio la pili la kumtumia mke wangu anipigie simu pia limegonga mwamba, lakini wamefanikiwa kumpiga risasi na sasa anapumulia mashine... nina hakika hawataishia hapo, lazima watatafuta namna nyingine ya...” Sammy aliyekuwa ametopea kwenye lindi la mawazo alikatishwa na sauti ya Tunu.

“Sammy!” Tunu aliita. “Najua una maswali mengi unayotaka kuyafahamu kuhusu hao waliompiga risasi mkeo. Nitakusaidia kupata majibu yote lakini nakuomba usiniulize chochote kuhusu namna nitakavyofanya. Kitu cha msingi ni kufahamu tu kwamba nipo hapa kukusaidia,” Tunu alisema na kushusha pumzi.

“Gift, ni kweli nina mengi sana ninataka kuyafahamu. Mengi sana yanayohusu huu mlolongo wa visa na mikasa hadi mke wangu kupigwa risasi. Lakini pia ninataka kufahamu mengi yanayokuhusu wewe, kuanzia usiku wa siku ile tuliokuwa pamoja kisha ukatoweka kama moshi na kuniachia maumivu yaliyochukua miaka mingi kupoa, hadi jana ulipotokea tena.”

“Usijali, Sammy, tuna mengi ya kuzungumza ila kwa sasa tuangalie kwanza afya ya mkeo, pia mazingira haya si rafiki sana kuzungumza mambo hayo,” Tunu alisema na kulamba midomo yake na ukimya mfupi ukapita.

“Kikubwa kwa sasa ni kumwombea mgonjwa apone, mambo mengine ya nani walimpiga risasi yatajulikana. Ni yeye ndiye mwenye majibu ya waliompiga risasi walikuwaje na yawezekana labda alizifahamu sura zao ndiyo maana wakafanya hivyo ili kupoteza ushahidi,” Tunu alisema baada ya kitambo kile cha ukimya.

“Halafu ninahitaji kuzungumza na Winifrida, sijui nitampataje?” Tunu aliuliza na kumfanya Sammy amwangalie kwa udadisi zaidi.

“Gift, naomba uniambie ukweli wewe ni nani hasa! Are you a cop?” Sammy aliuliza huku akimkazia macho Tunu.

“Kwa nini umeuliza hivyo?”

“Nataka tu kufahamu, maana hata maswali yako yote uliyoniuliza ni ya kipolisi. Ni ya mtu mwenye taaluma ya intelijensia anayetafuta taarifa za kiuchunguzi ili azifanyie kazi.”

Tunu aliachia tabasamu lililozaa kicheko hafifu huku akiyaondosha macho yake toka usoni kwa Sammy, akakaa kimya kwanza kwa sekunde kadhaa kisha akamtazama tena Sammy huku akishusha pumzi. Alionesha kuwa na jambo zito sana ndani yake ambalo asingependa kuliweka wazi.

“Hamna shida kama haujisikii kuniambia,” Sammy alisema huku akitabasamu. “I can understand. Ila siku utakayojisikia kuniambia ukweli you know how to get me.”

Inaendelea...

CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater Bigjahman moneytalk marybaby nipo2 ram kisukari Smart911 Madame S carbamazepine Astelia culture gal Prisoner of hope Mine eyes kuku mweus Thad hearly Shunie Tumosa Mine eyes Kudo swahiba92 ludist Toyota escudo Clkey macson3 boga la kiangazi LEGE Smart911 Richard irakunda skfull popie Krizy Beat hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Mlenge Kacheda mjasiliamali Laki Si Pesa cocochanel kinusikwetu big jambo mludego Shupavu Kacheda mjasiliamali Mweweso Songa Heri esiankiki mnadhimu mkuu wa jf red apple the-sniper MR KUO dan oseko
 
Taxi - (107)

“Wala siyo hivyo, ukweli ni kwamba mimi siyo polisi. I'm just concerned as a close friend... Nataka nionane na mdogo wako kwa kuamini kama kweli ana jambo analijua basi ataniambia, I know how to deal with...” Tunu alisema na kuachia tabasamu pana.

“Sina sababu ya kutokukuamini, hata hivyo, nimefurahi sana kukuona tena after so many years. Nimefurahi japo imekuwa ni kipindi kigumu na cha mshtuko mkubwa. Sikutegemea kabisa kama...” Sammy alisema kwa huzuni lakini akasita baada ya watu watatu kufika.

Walikuwa wanawake wawili na mwanamume mmoja, jirani zao kule Tabata Chang’ombe, waliopita kumjulia hali Joyce.

* * * * *

Saa nne kamili asubuhi, katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, magurudumu ya ndege aina ya Bombardier DASH8 Q400 ya shirika la ndege la Tanzania yaligusa ardhi kwenye kiwanja hicho huku tayari abiria wakiwa wamejiandaa kwa tukio lile la kutua kwa ndege. Ndege hiyo ilikuwa inatokea jijini Tanga.

Muda mfupi baada ya ndege ile kusimama, milango ya ndege ilifunguliwa na hapo abiria wakaanza kushuka. Kati ya abiria hao walikuwepo abiria wawili mume na mke waliokuwa na sura zilizosawajika zikiwa na huzuni isiyoelezeka. Hawa walikuwa ni Rafael Jengo na Bi. Pamela Jengo, wazazi wa Joyce.

Rafael Jengo alikuwa mrefu mwenye sura ya ucheshi na umbo kubwa lililopendeza. Alikuwa amevaa suti nadhifu ya rangi ya kijivu na shati jeusi lililomkaa vyema na kumpendeza. Miguuni alikuwa amevaa viatu vyeusi vya ngozi na mkono wake wa kushoto alivaa saa nzuri ya mkononi. Umri wa Rafael Jengo wa miaka hamsini na nne bado ulikuwa haujatosha kabisa kuzipokonya nguvu zake mwilini.

Bi. Pamela alikuwa mnene wa wastani, hakuwa mfupi wala mrefu bali alikuwa na kimo cha wastani na alikuwa mweupe. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na nane. Wakati wanashuka toka kwenye ndege Rafael Jengo alikuwa akimtazama mkewe Bi. Pamela akiwa na uso uliosawajika kidogo pasipo kusema neno lolote huku akionekana kuipa utulivu akili yake.

Mara waliposhuka kwenye ile ndege wakaingia kwenye jengo namba mbili la kiwanja kile cha ndege cha kimataifa lenye migahawa ya kisasa na ofisi mbalimbali za utawala. Kwa kuwa hawakuwa na mizigo yoyote mikubwa waliwatangulia abiria wengine wenye mizigo wakapenya haraka na kutoka nje ya jengo la kiwanja kile cha ndege cha kimataifa.

Dereva mmoja wa teksi mjanja akawawahi haraka kabla ya wenzake baada ya kuhisi hitaji lao. Dereva yule alikuwa mzee wa makamo, mrefu na mwembamba mwenye sura ya ucheshi akiwa amevaa kofia nyeusi ya kapelo, shati jeupe, suruali ya nyeusi na makubasi ya ngozi miguuni, aliwahi kuwapokea mizigo waliyokuja nayo na kuwafungulia mlango wa taxi yake hata kabla hawajaafikiana naye au kumweleza hitaji lao. Kwa ushawishi ule hawakuwa na pingamizi, hivyo wakaingia ndani ya gari.

Mara tu walipoingia ndani ya ile taxi yule dereva akawatazama kwa makini huku akiachia tabasamu la kirafiki. “Sijui niwapeleke wapi, ndugu zangu?” yule dereva taxi aliwauliza huku tabasamu la kindugu likiendelea kutawala usoni kwake.

“Tupeleke Amana,” Rafael Jengo alisema, na muda huo huo ile taxi ikaondoka na kuanza kuyaacha maegesho ya magari ya kile kiwanja cha ndege, kisha ikaingia katika barabara ya Nyerere na safari ya kuelekea Amana ikaanza.

* * * * *

Kwenye viunga vya maegesho vya hospitali ya Amana, Tunu alikuwa ameketi kwa utulivu ndani ya gari dogo la kifahari aina ya BMW X6 xDrive 50i jeusi alilokuja nalo. Gari lile lilikuwa haliungurumi. Alikuwa nyuma ya usukani wake akionekana kutafakari sana juu ya kazi iliyokuwa mbele yake. Alikuwa analitazama kwa makini gari la Sammy aina ya Cadillac DeVille.

Alikuwa na mambo kadhaa ya kuyashughulikia na hakujua angeanza na lipi, hata hivyo alikuwa amepata mahali pazuri pa kuanzia baada ya mazungumzo yake na Sammy, mwanamume aliyemwondolea utoto wake na kumwingiza katika dunia ya watu wazima.

Hakutegemea kabisa kukutana na Sammy katika mazingira yale ya utata. Alijihisi alikuwa na jukumu la kumsaidia Sammy kama njia ya kudumisha uhusiano wao uliopotea kwa takriban miaka kumi na moja. Siyo Sammy aliyekuwa ameathirika na kupotezana kwao, hata yeye pia alikuwa katika wakati mgumu, alishindwa kabisa kumtoa Sammy moyoni mwake.

Aliikumbuka vyema siku aliyokwenda nyumbani kwa Sammy, yale waliyoyafanya na ahadi walizopeana baada ya hapo, na wakati akiondoka hakujua kama wasingeonana tena kwani aliporudi nyumbani kwa shangazi yake huko Sinza alikuta taarifa za kifo cha baba yake aliyekuwa mwanasiasa maarufu mjini Tabora. Alitakiwa kusafiri kwenda Tabora asubuhi ya siku iliyofuata na hakuweza tena kuwasiliana na Sammy kwani hakuwa amechukua namba yake ya simu.

Tunu alikuwa amezaliwa mkoani Tabora akiwa mtoto wa mwisho katika familia ya watoto wanne, yeye akiwa mtoto pekee wa kike. Baada ya mazishi hakurudi jijini Dar es Salaam, alibaki Tabora kumsaidia mama yake hadi matokeo ya mtihani wake wa kidato cha sita yalipotoka ambapo Tunu alikuwa miongoni mwa wanafunzi waliofanya vizuri zaidi kitaifa, na hivyo kupata udhamini wa kusomeshwa bure chuo kikuu.

Siku alipofika jijini Dar es Salaam alimtafuta Sammy bila mafanikio, nyumba aliyokuwa akiishi alikuwa amehama na hakuna aliyejua alihamia wapi. Baada ya kuhangaika kumtafuta kila alikodhani angemwona hatimaye Tunu alikata tamaa ya kumpata, kwani pia alikuwa na muda mfupi sana wa kujiandaa kabla ya safari.

Muda ulipofika aliondoka kwenda masomoni nchini Marekani katika Taasisi ya Teknolojia ya Georgia (Georgia Tech). Huko Marekani Tunu alisoma kwa miaka minne akibobea na kuhitimu Shahada ya Kwanza katika Computer System Analysis.

Aliporudi nchini alichaguliwa kujiunga na programu maalumu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania kwa ajili ya vijana wasomi walioandaliwa kwenda kuchukua mafunzo ya awali ya ujasusi. Baada ya kumaliza mafunzo ya kijeshi Tunu alilitumikia jeshi kwa muda mfupi na kituo chake kilikuwa Lugalo jijini Dar es Salaam.

Inaendelea...
 
Poti 2po 2gether 2pia maana leo hapa msalato mnadani hapaelewekieleweki
 
Taxi - (107)

“Wala siyo hivyo, ukweli ni kwamba mimi siyo polisi. I'm just concerned as a close friend... Nataka nionane na mdogo wako kwa kuamini kama kweli ana jambo analijua basi ataniambia, I know how to deal with...” Tunu alisema na kuachia tabasamu pana.

“Sina sababu ya kutokukuamini, hata hivyo, nimefurahi sana kukuona tena after so many years. Nimefurahi japo imekuwa ni kipindi kigumu na cha mshtuko mkubwa. Sikutegemea kabisa kama...” Sammy alisema kwa huzuni lakini akasita baada ya watu watatu kufika.

Walikuwa wanawake wawili na mwanamume mmoja, jirani zao kule Tabata Chang’ombe, waliopita kumjulia hali Joyce.

* * * * *

Saa nne kamili asubuhi, katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, magurudumu ya ndege aina ya Bombardier DASH8 Q400 ya shirika la ndege la Tanzania yaligusa ardhi kwenye kiwanja hicho huku tayari abiria wakiwa wamejiandaa kwa tukio lile la kutua kwa ndege. Ndege hiyo ilikuwa inatokea jijini Tanga.

Muda mfupi baada ya ndege ile kusimama, milango ya ndege ilifunguliwa na hapo abiria wakaanza kushuka. Kati ya abiria hao walikuwepo abiria wawili mume na mke waliokuwa na sura zilizosawajika zikiwa na huzuni isiyoelezeka. Hawa walikuwa ni Rafael Jengo na Bi. Pamela Jengo, wazazi wa Joyce.

Rafael Jengo alikuwa mrefu mwenye sura ya ucheshi na umbo kubwa lililopendeza. Alikuwa amevaa suti nadhifu ya rangi ya kijivu na shati jeusi lililomkaa vyema na kumpendeza. Miguuni alikuwa amevaa viatu vyeusi vya ngozi na mkono wake wa kushoto alivaa saa nzuri ya mkononi. Umri wa Rafael Jengo wa miaka hamsini na nne bado ulikuwa haujatosha kabisa kuzipokonya nguvu zake mwilini.

Bi. Pamela alikuwa mnene wa wastani, hakuwa mfupi wala mrefu bali alikuwa na kimo cha wastani na alikuwa mweupe. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na nane. Wakati wanashuka toka kwenye ndege Rafael Jengo alikuwa akimtazama mkewe Bi. Pamela akiwa na uso uliosawajika kidogo pasipo kusema neno lolote huku akionekana kuipa utulivu akili yake.
Mara waliposhuka kwenye ile ndege wakaingia kwenye jengo namba mbili la kiwanja kile cha ndege cha kimataifa lenye migahawa ya kisasa na ofisi mbalimbali za utawala. Kwa kuwa hawakuwa na mizigo yoyote mikubwa waliwatangulia abiria wengine wenye mizigo wakapenya haraka na kutoka nje ya jengo la kiwanja kile cha ndege cha kimataifa.

Dereva mmoja wa teksi mjanja akawawahi haraka kabla ya wenzake baada ya kuhisi hitaji lao. Dereva yule alikuwa mzee wa makamo, mrefu na mwembamba mwenye sura ya ucheshi akiwa amevaa kofia nyeusi ya kapelo, shati jeupe, suruali ya nyeusi na makubasi ya ngozi miguuni, aliwahi kuwapokea mizigo waliyokuja nayo na kuwafungulia mlango wa taxi yake hata kabla hawajaafikiana naye au kumweleza hitaji lao. Kwa ushawishi ule hawakuwa na pingamizi, hivyo wakaingia ndani ya gari.

Mara tu walipoingia ndani ya ile taxi yule dereva akawatazama kwa makini huku akiachia tabasamu la kirafiki. “Sijui niwapeleke wapi, ndugu zangu?” yule dereva taxi aliwauliza huku tabasamu la kindugu likiendelea kutawala usoni kwake.

“Tupeleke Amana,” Rafael Jengo alisema, na muda huo huo ile taxi ikaondoka na kuanza kuyaacha maegesho ya magari ya kile kiwanja cha ndege, kisha ikaingia katika barabara ya Nyerere na safari ya kuelekea Amana ikaanza.

* * * * *

Kwenye viunga vya maegesho vya hospitali ya Amana, Tunu alikuwa ameketi kwa utulivu ndani ya gari dogo la kifahari aina ya BMW X6 xDrive 50i jeusi alilokuja nalo. Gari lile lilikuwa haliungurumi. Alikuwa nyuma ya usukani wake akionekana kutafakari sana juu ya kazi iliyokuwa mbele yake. Alikuwa analitazama kwa makini gari la Sammy aina ya Cadillac DeVille.
Alikuwa na mambo kadhaa ya kuyashughulikia na hakujua angeanza na lipi, hata hivyo alikuwa amepata mahali pazuri pa kuanzia baada ya mazungumzo yake na Sammy, mwanamume aliyemwondolea utoto wake na kumwingiza katika dunia ya watu wazima.

Hakutegemea kabisa kukutana na Sammy katika mazingira yale ya utata. Alijihisi alikuwa na jukumu la kumsaidia Sammy kama njia ya kudumisha uhusiano wao uliopotea kwa takriban miaka kumi na moja. Siyo Sammy aliyekuwa ameathirika na kupotezana kwao, hata yeye pia alikuwa katika wakati mgumu, alishindwa kabisa kumtoa Sammy moyoni mwake.

Aliikumbuka vyema siku aliyokwenda nyumbani kwa Sammy, yale waliyoyafanya na ahadi walizopeana baada ya hapo, na wakati akiondoka hakujua kama wasingeonana tena kwani aliporudi nyumbani kwa shangazi yake huko Sinza alikuta taarifa za kifo cha baba yake aliyekuwa mwanasiasa maarufu mjini Tabora. Alitakiwa kusafiri kwenda Tabora asubuhi ya siku iliyofuata na hakuweza tena kuwasiliana na Sammy kwani hakuwa amechukua namba yake ya simu.

Tunu alikuwa amezaliwa mkoani Tabora akiwa mtoto wa mwisho katika familia ya watoto wanne, yeye akiwa mtoto pekee wa kike. Baada ya mazishi hakurudi jijini Dar es Salaam, alibaki Tabora kumsaidia mama yake hadi matokeo ya mtihani wake wa kidato cha sita yalipotoka ambapo Tunu alikuwa miongoni mwa wanafunzi waliofanya vizuri zaidi kitaifa, na hivyo kupata udhamini wa kusomeshwa bure chuo kikuu.

Siku alipofika jijini Dar es Salaam alimtafuta Sammy bila mafanikio, nyumba aliyokuwa akiishi alikuwa amehama na hakuna aliyejua alihamia wapi. Baada ya kuhangaika kumtafuta kila alikodhani angemwona hatimaye Tunu alikata tamaa ya kumpata, kwani pia alikuwa na muda mfupi sana wa kujiandaa kabla ya safari.

Muda ulipofika aliondoka kwenda masomoni nchini Marekani katika Taasisi ya Teknolojia ya Georgia (Georgia Tech). Huko Marekani Tunu alisoma kwa miaka minne akibobea na kuhitimu Shahada ya Kwanza katika Computer System Analysis.
Aliporudi nchini alichaguliwa kujiunga na programu maalumu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania kwa ajili ya vijana wasomi walioandaliwa kwenda kuchukua mafunzo ya awali ya ujasusi. Baada ya kumaliza mafunzo ya kijeshi Tunu alilitumikia jeshi kwa muda mfupi na kituo chake kilikuwa Lugalo jijini Dar es Salaam.

Inaendelea...
Nice story............
 
Taxi - (107)

“Wala siyo hivyo, ukweli ni kwamba mimi siyo polisi. I'm just concerned as a close friend... Nataka nionane na mdogo wako kwa kuamini kama kweli ana jambo analijua basi ataniambia, I know how to deal with...” Tunu alisema na kuachia tabasamu pana.

“Sina sababu ya kutokukuamini, hata hivyo, nimefurahi sana kukuona tena after so many years. Nimefurahi japo imekuwa ni kipindi kigumu na cha mshtuko mkubwa. Sikutegemea kabisa kama...” Sammy alisema kwa huzuni lakini akasita baada ya watu watatu kufika.

Walikuwa wanawake wawili na mwanamume mmoja, jirani zao kule Tabata Chang’ombe, waliopita kumjulia hali Joyce.

* * * * *

Saa nne kamili asubuhi, katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, magurudumu ya ndege aina ya Bombardier DASH8 Q400 ya shirika la ndege la Tanzania yaligusa ardhi kwenye kiwanja hicho huku tayari abiria wakiwa wamejiandaa kwa tukio lile la kutua kwa ndege. Ndege hiyo ilikuwa inatokea jijini Tanga.

Muda mfupi baada ya ndege ile kusimama, milango ya ndege ilifunguliwa na hapo abiria wakaanza kushuka. Kati ya abiria hao walikuwepo abiria wawili mume na mke waliokuwa na sura zilizosawajika zikiwa na huzuni isiyoelezeka. Hawa walikuwa ni Rafael Jengo na Bi. Pamela Jengo, wazazi wa Joyce.

Rafael Jengo alikuwa mrefu mwenye sura ya ucheshi na umbo kubwa lililopendeza. Alikuwa amevaa suti nadhifu ya rangi ya kijivu na shati jeusi lililomkaa vyema na kumpendeza. Miguuni alikuwa amevaa viatu vyeusi vya ngozi na mkono wake wa kushoto alivaa saa nzuri ya mkononi. Umri wa Rafael Jengo wa miaka hamsini na nne bado ulikuwa haujatosha kabisa kuzipokonya nguvu zake mwilini.

Bi. Pamela alikuwa mnene wa wastani, hakuwa mfupi wala mrefu bali alikuwa na kimo cha wastani na alikuwa mweupe. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na nane. Wakati wanashuka toka kwenye ndege Rafael Jengo alikuwa akimtazama mkewe Bi. Pamela akiwa na uso uliosawajika kidogo pasipo kusema neno lolote huku akionekana kuipa utulivu akili yake.
Mara waliposhuka kwenye ile ndege wakaingia kwenye jengo namba mbili la kiwanja kile cha ndege cha kimataifa lenye migahawa ya kisasa na ofisi mbalimbali za utawala. Kwa kuwa hawakuwa na mizigo yoyote mikubwa waliwatangulia abiria wengine wenye mizigo wakapenya haraka na kutoka nje ya jengo la kiwanja kile cha ndege cha kimataifa.

Dereva mmoja wa teksi mjanja akawawahi haraka kabla ya wenzake baada ya kuhisi hitaji lao. Dereva yule alikuwa mzee wa makamo, mrefu na mwembamba mwenye sura ya ucheshi akiwa amevaa kofia nyeusi ya kapelo, shati jeupe, suruali ya nyeusi na makubasi ya ngozi miguuni, aliwahi kuwapokea mizigo waliyokuja nayo na kuwafungulia mlango wa taxi yake hata kabla hawajaafikiana naye au kumweleza hitaji lao. Kwa ushawishi ule hawakuwa na pingamizi, hivyo wakaingia ndani ya gari.

Mara tu walipoingia ndani ya ile taxi yule dereva akawatazama kwa makini huku akiachia tabasamu la kirafiki. “Sijui niwapeleke wapi, ndugu zangu?” yule dereva taxi aliwauliza huku tabasamu la kindugu likiendelea kutawala usoni kwake.

“Tupeleke Amana,” Rafael Jengo alisema, na muda huo huo ile taxi ikaondoka na kuanza kuyaacha maegesho ya magari ya kile kiwanja cha ndege, kisha ikaingia katika barabara ya Nyerere na safari ya kuelekea Amana ikaanza.

* * * * *

Kwenye viunga vya maegesho vya hospitali ya Amana, Tunu alikuwa ameketi kwa utulivu ndani ya gari dogo la kifahari aina ya BMW X6 xDrive 50i jeusi alilokuja nalo. Gari lile lilikuwa haliungurumi. Alikuwa nyuma ya usukani wake akionekana kutafakari sana juu ya kazi iliyokuwa mbele yake. Alikuwa analitazama kwa makini gari la Sammy aina ya Cadillac DeVille.
Alikuwa na mambo kadhaa ya kuyashughulikia na hakujua angeanza na lipi, hata hivyo alikuwa amepata mahali pazuri pa kuanzia baada ya mazungumzo yake na Sammy, mwanamume aliyemwondolea utoto wake na kumwingiza katika dunia ya watu wazima.

Hakutegemea kabisa kukutana na Sammy katika mazingira yale ya utata. Alijihisi alikuwa na jukumu la kumsaidia Sammy kama njia ya kudumisha uhusiano wao uliopotea kwa takriban miaka kumi na moja. Siyo Sammy aliyekuwa ameathirika na kupotezana kwao, hata yeye pia alikuwa katika wakati mgumu, alishindwa kabisa kumtoa Sammy moyoni mwake.

Aliikumbuka vyema siku aliyokwenda nyumbani kwa Sammy, yale waliyoyafanya na ahadi walizopeana baada ya hapo, na wakati akiondoka hakujua kama wasingeonana tena kwani aliporudi nyumbani kwa shangazi yake huko Sinza alikuta taarifa za kifo cha baba yake aliyekuwa mwanasiasa maarufu mjini Tabora. Alitakiwa kusafiri kwenda Tabora asubuhi ya siku iliyofuata na hakuweza tena kuwasiliana na Sammy kwani hakuwa amechukua namba yake ya simu.

Tunu alikuwa amezaliwa mkoani Tabora akiwa mtoto wa mwisho katika familia ya watoto wanne, yeye akiwa mtoto pekee wa kike. Baada ya mazishi hakurudi jijini Dar es Salaam, alibaki Tabora kumsaidia mama yake hadi matokeo ya mtihani wake wa kidato cha sita yalipotoka ambapo Tunu alikuwa miongoni mwa wanafunzi waliofanya vizuri zaidi kitaifa, na hivyo kupata udhamini wa kusomeshwa bure chuo kikuu.

Siku alipofika jijini Dar es Salaam alimtafuta Sammy bila mafanikio, nyumba aliyokuwa akiishi alikuwa amehama na hakuna aliyejua alihamia wapi. Baada ya kuhangaika kumtafuta kila alikodhani angemwona hatimaye Tunu alikata tamaa ya kumpata, kwani pia alikuwa na muda mfupi sana wa kujiandaa kabla ya safari.

Muda ulipofika aliondoka kwenda masomoni nchini Marekani katika Taasisi ya Teknolojia ya Georgia (Georgia Tech). Huko Marekani Tunu alisoma kwa miaka minne akibobea na kuhitimu Shahada ya Kwanza katika Computer System Analysis.
Aliporudi nchini alichaguliwa kujiunga na programu maalumu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania kwa ajili ya vijana wasomi walioandaliwa kwenda kuchukua mafunzo ya awali ya ujasusi. Baada ya kumaliza mafunzo ya kijeshi Tunu alilitumikia jeshi kwa muda mfupi na kituo chake kilikuwa Lugalo jijini Dar es Salaam.

Inaendelea...
 
Taxi - (107)

“Wala siyo hivyo, ukweli ni kwamba mimi siyo polisi. I'm just concerned as a close friend... Nataka nionane na mdogo wako kwa kuamini kama kweli ana jambo analijua basi ataniambia, I know how to deal with...” Tunu alisema na kuachia tabasamu pana.

“Sina sababu ya kutokukuamini, hata hivyo, nimefurahi sana kukuona tena after so many years. Nimefurahi japo imekuwa ni kipindi kigumu na cha mshtuko mkubwa. Sikutegemea kabisa kama...” Sammy alisema kwa huzuni lakini akasita baada ya watu watatu kufika.

Walikuwa wanawake wawili na mwanamume mmoja, jirani zao kule Tabata Chang’ombe, waliopita kumjulia hali Joyce.

* * * * *

Saa nne kamili asubuhi, katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, magurudumu ya ndege aina ya Bombardier DASH8 Q400 ya shirika la ndege la Tanzania yaligusa ardhi kwenye kiwanja hicho huku tayari abiria wakiwa wamejiandaa kwa tukio lile la kutua kwa ndege. Ndege hiyo ilikuwa inatokea jijini Tanga.

Muda mfupi baada ya ndege ile kusimama, milango ya ndege ilifunguliwa na hapo abiria wakaanza kushuka. Kati ya abiria hao walikuwepo abiria wawili mume na mke waliokuwa na sura zilizosawajika zikiwa na huzuni isiyoelezeka. Hawa walikuwa ni Rafael Jengo na Bi. Pamela Jengo, wazazi wa Joyce.

Rafael Jengo alikuwa mrefu mwenye sura ya ucheshi na umbo kubwa lililopendeza. Alikuwa amevaa suti nadhifu ya rangi ya kijivu na shati jeusi lililomkaa vyema na kumpendeza. Miguuni alikuwa amevaa viatu vyeusi vya ngozi na mkono wake wa kushoto alivaa saa nzuri ya mkononi. Umri wa Rafael Jengo wa miaka hamsini na nne bado ulikuwa haujatosha kabisa kuzipokonya nguvu zake mwilini.

Bi. Pamela alikuwa mnene wa wastani, hakuwa mfupi wala mrefu bali alikuwa na kimo cha wastani na alikuwa mweupe. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na nane. Wakati wanashuka toka kwenye ndege Rafael Jengo alikuwa akimtazama mkewe Bi. Pamela akiwa na uso uliosawajika kidogo pasipo kusema neno lolote huku akionekana kuipa utulivu akili yake.
Mara waliposhuka kwenye ile ndege wakaingia kwenye jengo namba mbili la kiwanja kile cha ndege cha kimataifa lenye migahawa ya kisasa na ofisi mbalimbali za utawala. Kwa kuwa hawakuwa na mizigo yoyote mikubwa waliwatangulia abiria wengine wenye mizigo wakapenya haraka na kutoka nje ya jengo la kiwanja kile cha ndege cha kimataifa.

Dereva mmoja wa teksi mjanja akawawahi haraka kabla ya wenzake baada ya kuhisi hitaji lao. Dereva yule alikuwa mzee wa makamo, mrefu na mwembamba mwenye sura ya ucheshi akiwa amevaa kofia nyeusi ya kapelo, shati jeupe, suruali ya nyeusi na makubasi ya ngozi miguuni, aliwahi kuwapokea mizigo waliyokuja nayo na kuwafungulia mlango wa taxi yake hata kabla hawajaafikiana naye au kumweleza hitaji lao. Kwa ushawishi ule hawakuwa na pingamizi, hivyo wakaingia ndani ya gari.

Mara tu walipoingia ndani ya ile taxi yule dereva akawatazama kwa makini huku akiachia tabasamu la kirafiki. “Sijui niwapeleke wapi, ndugu zangu?” yule dereva taxi aliwauliza huku tabasamu la kindugu likiendelea kutawala usoni kwake.

“Tupeleke Amana,” Rafael Jengo alisema, na muda huo huo ile taxi ikaondoka na kuanza kuyaacha maegesho ya magari ya kile kiwanja cha ndege, kisha ikaingia katika barabara ya Nyerere na safari ya kuelekea Amana ikaanza.

* * * * *

Kwenye viunga vya maegesho vya hospitali ya Amana, Tunu alikuwa ameketi kwa utulivu ndani ya gari dogo la kifahari aina ya BMW X6 xDrive 50i jeusi alilokuja nalo. Gari lile lilikuwa haliungurumi. Alikuwa nyuma ya usukani wake akionekana kutafakari sana juu ya kazi iliyokuwa mbele yake. Alikuwa analitazama kwa makini gari la Sammy aina ya Cadillac DeVille.
Alikuwa na mambo kadhaa ya kuyashughulikia na hakujua angeanza na lipi, hata hivyo alikuwa amepata mahali pazuri pa kuanzia baada ya mazungumzo yake na Sammy, mwanamume aliyemwondolea utoto wake na kumwingiza katika dunia ya watu wazima.

Hakutegemea kabisa kukutana na Sammy katika mazingira yale ya utata. Alijihisi alikuwa na jukumu la kumsaidia Sammy kama njia ya kudumisha uhusiano wao uliopotea kwa takriban miaka kumi na moja. Siyo Sammy aliyekuwa ameathirika na kupotezana kwao, hata yeye pia alikuwa katika wakati mgumu, alishindwa kabisa kumtoa Sammy moyoni mwake.

Aliikumbuka vyema siku aliyokwenda nyumbani kwa Sammy, yale waliyoyafanya na ahadi walizopeana baada ya hapo, na wakati akiondoka hakujua kama wasingeonana tena kwani aliporudi nyumbani kwa shangazi yake huko Sinza alikuta taarifa za kifo cha baba yake aliyekuwa mwanasiasa maarufu mjini Tabora. Alitakiwa kusafiri kwenda Tabora asubuhi ya siku iliyofuata na hakuweza tena kuwasiliana na Sammy kwani hakuwa amechukua namba yake ya simu.

Tunu alikuwa amezaliwa mkoani Tabora akiwa mtoto wa mwisho katika familia ya watoto wanne, yeye akiwa mtoto pekee wa kike. Baada ya mazishi hakurudi jijini Dar es Salaam, alibaki Tabora kumsaidia mama yake hadi matokeo ya mtihani wake wa kidato cha sita yalipotoka ambapo Tunu alikuwa miongoni mwa wanafunzi waliofanya vizuri zaidi kitaifa, na hivyo kupata udhamini wa kusomeshwa bure chuo kikuu.

Siku alipofika jijini Dar es Salaam alimtafuta Sammy bila mafanikio, nyumba aliyokuwa akiishi alikuwa amehama na hakuna aliyejua alihamia wapi. Baada ya kuhangaika kumtafuta kila alikodhani angemwona hatimaye Tunu alikata tamaa ya kumpata, kwani pia alikuwa na muda mfupi sana wa kujiandaa kabla ya safari.

Muda ulipofika aliondoka kwenda masomoni nchini Marekani katika Taasisi ya Teknolojia ya Georgia (Georgia Tech). Huko Marekani Tunu alisoma kwa miaka minne akibobea na kuhitimu Shahada ya Kwanza katika Computer System Analysis.
Aliporudi nchini alichaguliwa kujiunga na programu maalumu ya Jeshi la Wananchi wae Tanzania kwa ajili ya vijana wasomi walioandaliwa kwenda kuchukua mafunzo ya awali ya ujasusi. Baada ya kumaliza mafunzo ya kijeshi Tunu alilitumikia jeshi kwa muda mfupi na kituo chake kilikuwa Lugalo jijini Dar es Salaam.

Inaendelea...

💃💃💃aseh!! hii story n balaa yaan inapunguza muwaho upele na kuondoa halala na stress 😀😃shukran mkubwa bishop kwa uzi mtamu
 
Taxi - (108)

Akiwa Lugalo alipata pia mafunzo maalumu ya kijeshi (Special Forces and Tactical Weapons Training) na baadaye kupelekwa nchini Israel katika taasisi ya IDC Herzliya (ICT International Institute for Counter-Terrorism) ambako alihitimu shahada ya umahiri ya ujasusi ikihusisha pia masuala ya usalama wa ndani na mapambano dhidi ya ugaidi na teknonojia ya habari na mawasiliano.

Akiwa huko huko Israel alipata pia mafunzo ya kujihami katika michezo ya karate and judo na kufanikiwa kupata mkanda mweusi. Aliporejea nchini alianza kazi katika Idara ya Usalama wa Taifa na muda mfupi tu tangu alipojiunga idarani hapo alionesha uwezo mkubwa sana kiasi cha kuaminiwa na kupewa nafasi mbalimbali za kufanya kazi ndani na nje ya nchi.

Pamoja na kusafiri sehemu mbalimbali duniani, akikutana na watu mbalimbali na wakati fulani aliangukia kwenye uhusiano na mmoja wa mabosi wa mamlaka ya mawasiliano nchini, Nelson Mtokambali, bado hakuweza kumtoa Sammy moyoni mwake. Na sasa alikuwa amekutana naye katika mazingira yale, ingawa hakujua kama bado alimhitaji, lakini aliapa kumsaidia ili wote waliofanya kitendo kile walipe gharama za uhalifu wao.

Alizinduka toka katika mawazo yale, akatazama kushoto kwake kulikokuwa na gari la Sammy aina ya Cadillac DeVille. Akashusha pumzi na kuwasha injini ya gari lake kisha akaliondoa taratibu na kutoka kwenye geti la kuingilia na kutokea la hospitali ya Amana, halafu akakata kushoto akiifuata barabara ya lami iliyokwenda kuungana na barabara ya Uhuru.

Tunu alilipita gari moja jeusi aina ya Toyota Alphard jeusi lililokuwa na vioo vyenye tinted nyeusi iliyomzuia mtu kuona waliokuwemo ndani, likiwa limeegeshwa kando ya barabara ile ya lami, jirani na mgahawa mmoja uliopakana na ukuta wa hospitali ile ya Amana. Gari lile lilikuwa linanguruma taratibu. Ndani ya gari hilo kulikuwa na watu wawili, wanaume wa kazi. Spoiler na Job.

Spoiler na Job walikuwa makini wakifuatilia kila kilichokuwa kikiendelea eneo lile, ni kama vile walikuwa wanangoja kitu. Masikioni mwao walikuwa wamevaa vifaa maalumu vya usikivu na mawasiliano. Waliliona lile gari BMW X6 xDrive 50i jeusi wakati liliwapita, wakamtambua Tunu aliyekuwa akiendesha lile gari. Walimwona akikunja kuingia upande wa kushoto na kuifuata barabara ya Uhuru.

“Leo ndiyo leo,” Spoiler alisema akiwa anatafuna Big G. “Endapo tukimpata Tunu, kazi yetu itakuwa imekwisha...” Spoiler alisema na kumpa ishara Job ambaye aliliondoa gari kuelekea kule lilikoelekea gari la Tunu.

Tunu alikuwa ameshazipita kona kadhaa za mitaa ya Ilala ili kukwepa foleni katika barabara ya Uhuru wakati alipoukumbuka wajibu wake. Alikizungusha kichwa chake taratibu kutazama nyuma na hapo mwili wake ukajikuta ukiingiwa na ubaridi wa ghafla.

Moyo wake ukaanza kupiga kite kwa nguvu huku mwenendo wa mapigo yake ukianza kwenda katika utaratibu usiozoeleka, koo lake nalo likakaukiwa na mate. Gari aina ya Toyota Alphard jeusi lililokuwa na vioo vyenye tinted nyeusi iliyomzuia kuona waliokuwemo ndani lilikuwa limemfungia mkia kwa nyuma.

Tunu alikuwa na uhakika kuwa wale watu walikuwa wakimfuata yeye, kwani alikuwa ameliona lile gari nje ya hospitali ya Amana likiwa limeegeshwa kando ya barabara ya kutokea hospitali.

Lile gari Toyota Alphard jeusi lilikuwa nyuma yake kiasi cha umbali wa mita hamsini hivi likiwa limeacha gari moja katikati yao, na alihisi kuwa namba zake zilikuwa za bandia. Hata hivyo, kwa uzoefu wake aliweza kugundua kuwa dereva wa gari hilo hakuwa mzoefu mzuri katika kufuatilia windo.

Tunu alilitazama lile gari kwa makini huku akijiuliza kuwa watu wale ni akina nani na kwa nini wamfuatilie. Je, ni watu wa Mr. Oduya? Akaanza kushikwa na wasiwasi, hata hivyo aliamua kuachana nao na kuyakaza macho yake kutazama mbele huku akijitahidi kulisahau gari lile kwa muda, aliipa utulivu akili yake ianze kufanya kazi.

Tayari muda wa dakika takribani kumi na tano ulikwisha yeyuka tangu Tunu alipotoka pale hospitali ya Amana, aligundua hivyo baada ya kuitazama saa yake ya mkononi iliyoonesha vizuri kupitia mishale yake ya dhahabu ilivyokuwa ikimetameta.

Baada ya sekunde chache alifikia uamuzi wa kuwapoteza kwa kuwa hakutaka watu wale wafahamu ni wapi alipokuwa akielekea. Akapanga kubadilisha mwelekeo. Aliutazama mshale wa mafuta ukamwonesha kuwa alikuwa na mafuta ya kutosha kuweza kuzunguka jiji la Dar es Salaam mpaka jioni bila kusimama. Akatabasamu na kuongeza mwendo.

* * * * *

Katika hospitali ya Amana, Sammy alikuwa ametulia nje ya chumba alimolazwa Joyce, alikuwa akitafakari kuhusu mazungumzo yake na Tunu huku akijaribu kujiuliza maswali yaliyokosa majibu. Alitamani sana kufahamu kilichotokea kwa Tunu, alikuwa wapi siku zote? Anafanya kazi gani?

Alikuwa na hamu kubwa ya kutaka kufahamu mengi kuhusu Tunu, ni wapi alikuwa katika kipindi hiki chote cha miaka kumi na moja tangu walipoachana! Pamoja na kupotezana miaka yote hiyo lakini bado Tunu aliendelea kuonekana mrembo sana. Alikuwa bado ni Gift yule yule mwenye mvuto wa ajabu.

Wakati akizidi kuwaza mara akawaona watu wawili wakija na walipofika karibu akawatambua mara moja, walikuwa wazazi wake Joyce, Bwana na Bibi Jengo. Akasimama na kuwalaki.

Mambo yanazidi kupamba usikose kufuatilia mkasa huu wa kusisimua hadi mwisho...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom