Stori ya kusisimua - Taxi

Stori ya kusisimua - Taxi

Dah, nilichelewa kuiona nikalazimika kukimbia mbio, hatimaye nimewafikia. Asante sana Bishop Hiluka kwa stori hii, uko vizuri sana. Nakumbuka nilipokuja nyumbani Tz miaka mitatu iliyopita nilibahatika kuona tamthilia yenye jina hili la TAXI ambayo ilirushwa na Azam TV na wahusika walikuwa na majina ya Sam, Joy n.k., kama sikosei mwandishi ulikuwa wewe mwenyewe ila ilitengenezwa na Uhai Production. Mbona uliikatisha maana ilionekana kama episode nne hivi halafu haikuendelea?
 
Dah, nilichelewa kuiona nikalazimika kukimbia mbio, hatimaye nimewafikia. Asante sana Bishop Hiluka kwa stori hii, uko vizuri sana. Nakumbuka nilipokuja nyumbani Tz miaka mitatu iliyopita nilibahatika kuona tamthilia yenye jina hili la TAXI ambayo ilirushwa na Azam TV na wahusika walikuwa na majina ya Sam, Joy n.k., kama sikosei mwandishi ulikuwa wewe mwenyewe ila ilitengenezwa na Uhai Production. Mbona uliikatisha maana ilionekana kama episode nne hivi halafu haikuendelea?
Ni kweli, stori hii mwanzoni niliiandika kwa ajili ya tamthilia ili irushwe Azam TV, niliingia mkataba na Uhai Production, nafasi ya Sam alicheza Gabo; Madame alicheza Natasha na walipata gari moja la kizamani zuri sana likatumika kama teksi... lakini wale jamaa longolongo sana. Kulikuwa na Mnigeria mmoja ambaye ndiye alikuwa mkurugenzi na mdada mmoja wa Kiitaliano, walikuwa ni zaidi ya waswahili, stori waliipenda sana ila kwenye malipo sasa, mmh. Nikaachana nao na kuondoka na stori yangu,..
 
Ni kweli, stori hii mwanzoni niliiandika kwa ajili ya tamthilia ili irushwe Azam TV, niliingia mkataba na Uhai Production, nafasi ya Sam alicheza Gabo; Madame alicheza Natasha na walipata gari moja la kizamani zuri sana likatumika kama teksi... lakini wale jamaa longolongo sana. Kulikuwa na Mnigeria mmoja ambaye ndiye alikuwa mkurugenzi na mdada mmoja wa Kiitaliano, walikuwa ni zaidi ya waswahili, stori waliipenda sana ila kwenye malipo sasa, mmh. Nikaachana nao na kuondoka na stori yangu,..
Dah, pole mkuu. Lakini naamini walikulipa chako kabla hujaachana nao! Na vipi walikosa mtu wa kuiendeleza?
 
Dah, pole mkuu. Lakini naamini walikulipa chako kabla hujaachana nao! Na vipi walikosa mtu wa kuiendeleza?
Walinilipa ingawa walikuwa wanalalamika eti nalipwa pesa ndefu sana, nikawauliza kwani wakati tunaingia mkataba hamkujua kama ni ndefu. Wasingeweza kuiendeleza stori kwa kuwa ni mali yangu na mimi ndiye niliyetoa idea ya Taxi kuwa character, wao mwanzoni walitaka niandike stori kuhusu Taxi Driver, nikawaambia kuwa stori za Taxi Driver zimeshatoka nyingi sana, itakuwa kama marudio tu, ndipo nikaja na idea hii ambayo teksi yenyewe ni stori kwani ina siri kubwa sana kiasi cha makundi zaidi ya matatu kila moja likitaka liwe la kwanza kuipata kabla ya wengine. Anyway ngoja nisije nikafunguka na kumaliza utamu. Mkuu, naingia chimbo kwanza ili baadaye nirudi nitupie hata episode mbili...
 
Kaka hilo wazo kifanyie kazi.Maelezo yanamchosha msomaji inabidi upunguze.usikatae ushauri uko na mantiki.usifanye kwa mazoea fanya kwa ufanisi
Sasa mkuu what makes u think u are right?! Msomaji gani anakerwa mbona mie ndo napeeeenda napatamsisimko kama nipo eneoni kibaya kwako kwa mwingine dhahabu we chuja utakacho chukua ukifika kwa maelezo usopenda vunga
 
shikamoo shemeji,uko vizuri mwenyezi mungu akujalie mafanikio mengi zaidi
Ni kweli, stori hii mwanzoni niliiandika kwa ajili ya tamthilia ili irushwe Azam TV, niliingia mkataba na Uhai Production, nafasi ya Sam alicheza Gabo; Madame alicheza Natasha na walipata gari moja la kizamani zuri sana likatumika kama teksi... lakini wale jamaa longolongo sana. Kulikuwa na Mnigeria mmoja ambaye ndiye alikuwa mkurugenzi na mdada mmoja wa Kiitaliano, walikuwa ni zaidi ya waswahili, stori waliipenda sana ila kwenye malipo sasa, mmh. Nikaachana nao na kuondoka na stori yangu,..
 
Nimekakumbuka kale ka nyimbo kanakoimba alosto alosto

Taxi - (84)

ILIPOISHIA

“Hivi, yule bwana anayeendesha lile gari la kizamani aina ya Cadillac DeVille atarudi kweli, maana nilikuwa nahitaji huduma yake lakini nashangaa hadi sasa sijamwona!” Tunu alimuuliza yule mhudumu huku akipitisha ulimi wake kulamba midomo yake.

“Sina uhakika, kwani huna namba yake ya simu umpigie?” yule mhudumu aliuliza huku akiyatupa macho yake kutazama kwenye meza aliyoketi mzungu na wanawake wawili wa kibantu waliokuwa wakimwita.

“Ningekuwa nayo wala nisingehangaika kukuuliza,” Tunu aliuliza ma kuminya midomo yake.

“Basi endelea kusubiri, maana subira yavuta heri,” yule mhudumu alisema na kuanza kupiga hatua kwenda kwenye ile meza alikoitwa. Tunu alishusha pumzi na kujiegemeza kwenye kiti chake na kuyatupa tena macho yake kwa yule mwanadada aliyeketi peke yake ambaye hakulijua jina lake.

Alimwona akiinamisha kichwa chake kama aliyeona kitu katika bilauri yake ya bia, alitazama ndani ya ile bilauri kwa kitambo kisha aliinua uso wake taratibu kwa madaha kana kwamba alikuwa anaigiza filamu, mara macho yao yakakutana. Kwa dakika nzima macho yao yalitulia yakitizamana kama ambao walikuwa wakisomana fikra zao, kisha yule mwanadada aliyahamisha macho yake na kutazama kando.

SASA ENDELEA...

Muda huo huo simu yake ya mkononi ikaanza kuita, ilikuwa ni simu ghali ya kisasa aina ya Samsung Galaxy Fold. Yule msichana aliitazama kwa kitambo akionekana kama aliyekuwa akijishauri iwapo aipokee au aipotezee, akabana taya zake na kuipokea kisha akaipeleka moja kwa moja sikioni.

Alionekana kuwa mtulivu sana alipokuwa akiongea na simu, muda wote alipokuwa akiongea alikuwa akimtupia Tunu jicho la wizi na baada ya mazungumzo ya takriban dakika mbili alikata simu na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

Sasa alionekana kuanza kukosa uvumilivu, aliitazama tena saa yake na kukunja sura yake kisha akachukua chupa ya bia iliyokuwa juu ya meza na kumimina bia katika bilauri, bilauri ilijaa na bia kuanza kumwagika juu ya meza hali akiwa hana habari, alikuwa amezama kwenye lindo la mawazo.

Aliposhtuka bia ile ilikuwa imemlowesha kwenye sketi yake, akashtuka na kuruka huku akijaribu kuyaepuka macho ya watu yaliyokuwa yakimtazama kwa mshangao, alichukua tishu na kujifuta huku akisonya. Muda huo huo mhudumu alifika kwenye meza yake na kufuta meza huku akimpa pole.

Baada ya mhudumu kuondoka yule msichana alinyanyua bilauri yake na kuigida bia yote iliyokuwemo katika bilauri hiyo kisha akaikita ile bilauri juu ya meza na kunyanyuka, huku akimtazama Tunu kwa jicho la wizi akachukua simu yake na kuelekea maliwato.

Tunu alikuwa ametulia tuli akinywa mvinyo wake taratibu huku akijifanya kutoona kilichokuwa kikiendelea kwa yule msichana, alihisi kuwepo kwa jambo lisilo la kawaida na kujikuta akitamani kufuatilia ili ajue lakini hakufanya hivyo kwa kuhofia kuchanganya mambo, kwani hakuwepo pale kwa jambo jingine lolote isipokuwa lile lililompeleka hapo.

* * * * *

Saa tatu na ushee usiku, Joyce alikuwa kasimama barazani akionekana kutokuwa katika hali nzuri japo alijitahidi kuwa mtulivu sana. Alikuwa amevaa vazi la kulalia, kiunoni kajifunga khanga na kiganja cha mkono wake wa kushoto kakitumbukiza ndani ya khanga kwa mbele. Mkono wa kulia ulikuwa ameshika simu yake akiigongagonga kwenye shavu lake la kulia. Alionekana yuko mbali sana kimawazo.

Mtoto wake Pendo hakuwa amelala hadi muda huo, alikuwa amesimama kando yake akiwa ameng'ang'ania khanga ya mama yake. Joyce hakuonekana kumjali bali akili yake ilikuwa mbali, nje kabisa ya mahala pale aliposimama.

Joyce aliitazama ile simu aliyoishika, akashusha pumzi na kutafuta namba ya Sammy, akabofya ili kupiga lakini ghafla akaonekana kughairi na kuikata. Muda huo huo akasikia mvumo wa gari lililokuwa likisogea eneo lile. Joyce akatega vyema sikio lake kwa makini akijaribu kubaini sauti ya mvumo ule.

Gari lilipofika usawa wa nyumba yao likaongeza mwendo na kupitiliza na kumfanya Joyce aume meno yake kisha akayaachia, aliganda pale pale asijue la kufanya. Mara mvumo mwingine wa gari ukasikika tena ukisogea eneo lile na kupita. Joyce aliuma tena meno yake huku machozi yakimlengalenga.

Alishusha pumzi na kumtupia jicho Pendo aliyekuwa bado kamng’ang’ania khanga yake huku akimwangalia usoni kwa udadisi bila kusema jambo. Joyce alimtazama Pendo na kushtuka, akaufunika uso wake kwa khanga kujifuta machozi. Kisha aligeuka na kuingia sebuleni.

Hapo sebuleni alisimama karibu na kabati la vyombo. Pendo naye alimfuata kila aendako, pia alisimama huku akiendelea kumwangalia mama yake usoni kwa udadisi. Alikwisha hisi kuwepo kwa jambo lisilo la kawaida lakini hakuthubutu kuuliza.

Joyce alionekana kuzidiwa na mawazo, bila kufikiri akipiga ngumi ukutani kwa nguvu na kumshtua sana Pendo aliyemtazama mama yake kwa hofu. Joyce alishindwa kuvumilia, alichuchumaa pale alipokuwa amesimama, akajiegemeza na ukuta na kuanza kulia kimya kimya kwa uchungu huku uso akiwa kaufutika kwenye khanga aliyojifunga. Pendo alisogea pambeni kwa hofu.

Muda huo huo Winifrida alitokea sebuleni akiwa na uso wa mshangao, hofu na udadisi. Aliangaza macho yake na kumwona Joyce akiwa kajikunyata ukutani huku akilia kilo cha kwikwi. Winifrida alimtazama kwa wasiwasi na macho yake yakahamia kumtazama Pendo ambaye alikuwa amesimama kando akiwa ameduwaa, alikuwa anamshangaa mama yake huku machozi yakimlengalenga machoni.

Winifrida alifyatuka haraka toka pale alipokuwa amesimama na kumfuata Pendo, alimshika na kumnyanyua kisha akaelekea naye chumbani huku akimtuliza na kumwacha Joyce bado kajikunyata akilia kwa uchungu.

* * * * *

Tunu aliitazama saa yake kwa mara ya mia moja, dakika nyingine therathini na tano zilikuwa zimepita, zaidi ya muda aliokuwa ameukadiria. Alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kunyanyua bilauri iliyokuwa na mvinyo, akapiga funda kubwa na kuunywa mvinyo wote uliokuwemo.

Uso wake ulionesha wasiwasi, alishusha pumzi na kumtupia jicho yule mwanadada aliyekuwa ameketi peke yake akinywa bia taratibu, akamwona sasa akiwa ameketi na mtu mwingine, mwanamume ambaye kwa mtazamo tu alionekana kunuka fedha. Uso wake ulikuwa umetulia akionekana hana wasiwasi na anacho kila kitu ambacho angeweza kukihitaji duniani.

Tunu hakutaka kuendelea kukaa hapo huku akiwa hajui mtu aliyekuwa akimsubiri angefika saa ngapi, alitaka kunyanyuka lakini akasita baada ya kumwona mwanamume mmoja mrefu na mweupe mithili ya chotara wa kizungu akiingia ndani ya ukumbi. Mwanamume huyo mwenye sura ya tabasamu muda wote alikuwa anatembea kwa madaha huku akizungusha macho yake kutazama watu walioketi mle ukumbini. Mkononi alikuwa ameshika funguo za gari lake akizungusha kwenye kidole chake cha shahada.

Inaendelea...

CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater Bigjahman moneytalk marybaby nipo2 ram kisukari Smart911 Madame S carbamazepine Astelia culture gal Prisoner of hope Mine eyes kuku mweus Thad hearly Shunie moneytalk Tumosa Mine eyes Kudo swahiba92 ludist Toyota escudo Clkey macson3 boga la kiangazi LEGE Smart911 Richard irakunda skfull popie Krizy Beat hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Mlenge Kacheda mjasiliamali Laki Si Pesa cocochanel kinusikwetu big jambo mludego Shupavu Kacheda mjasiliamali Mweweso Songa Heri esiankiki mnadhimu mkuu wa jf red apple
 
Taxi - (85)

Mwanamume yule alikuwa amevaa suti ghali ya kijivu ya single button, brandi ya Piacenza kutoka nchini Italia, shati jeusi la mikono mirefu lenye kola ndogo, brandi ya Maria Santangelo kutoka Italia na viatu vyeusi vya ngozi halisi ya mamba.

Baadhi ya watu waliokuwa wameketi ndani ya ukumbi ule na wahudumu wa ule mgahawa walionekana kumchangamkia sana wakati akiwapita kiasi cha kumfanya Tunu ahisi labda alikuwa mtu mkubwa au mmiliki wa ule mgahawa. Alimtazama kwa makini huku akijaribu kuwaza, alihisi kumwona sehemu, si tu kwamba alimwona sehemu bali walionana.

Mwanamume yule ni Sammy na wakati akipiga hatua zake alionekana kusita kidogo baada ya kumwona Tunu, aliyatuliza macho yake kwenye uso wa Tunu huku akijaribu kuvuta kumbukumbu. Wakaangaliana kama waliokuwa wanasomana mawazo yao. Tunu akamkubuka na kuachia tabasamu. Alikumbuka kuwa alimwona kule Mzizima TV, walipishana mlangoni wakati akitoka na yeye Tunu akiingia. Bila shaka ndiye mmiliki wa lile gari la kizamani aina ya Cadillac DeVille.

Kwa upande wake, Sammy alijikuta akikihisi msisimko wa ajabu ambao hajawahi kuuhisi kwa mwanamke mwingine zaidi ya mkewe tangu alipofunga ndoa, msisimko ulikuwa ukimtambaa mwilini mwake na kuzifanya nywele zake kumsimama. Alishusha pumzi ndefu kama bata dume huku akiwa ameduwaa asipate cha kusema. Alianza kujishangaa, kwani alijikuta akibabaika kidogo kwa uzuri wa mwanadada yule kiasi kwamba moyo wake uliraruka kwa shauku ya kutaka kuongea naye.

Bila kujua alijikuta akipiga hatua kuelekea kwenye meza ya Tunu, akaketi huku akiendelea kuyatuliza macho yake kwenye uso wa Tunu, aliweka funguo za gari lake juu ya meza huku jicho lake likiwa halitoki kwenye uso wa Tunu. Alijikuta akimkodolea macho huku akiyasanifu mengi ya huba mbele ya hua aliyejitanashati kikweli kweli mbele ya macho yake!

Akiwa mbele yake alianza kujiuliza, mwanadada huyo ni nani na amewahi kumwona wapi! Kwenye televisheni? Kama ndiyo, je, ni mwigizaji? Mwanamuziki? Mwanamitindo? Hakupata jibu ingawa jambo moja ni kwamba alijua kuwa angeweza kuwa yeyote katika sanaa zote za maonesho, filamu ikitangulia.

Tunu aliuona mduwao katika uso wa Sammy. Yeye pia alikuwa na mshangao wake, hakutegemea kama mtu aliyemfanya kufunga safari kutoka mbali, kilometa zaidi ya elfu moja, kumfuata kisha akapata kibarua cha kusubiri kwa zaidi ya saa nne pasipo kuwa na uhakika wa kuongea naye, eti angeweza kujileta mwenyewe kwenye meza yake! Lakini, mbona kama wamewahi kukutana sehemu nyingine kabla ya siku hiyo? Walikutana wapi na lini? Walikuwa wanafanya nini?

“Gift!” Sammy aliita kwa sauti iliyoonesha wazi kuwa hakuwa na uhakika huku akiendelea kumkazia macho Tunu kwa makini, “Your name is Gift, right?” Sammy aliuliza kwa sauti iliyoonesha mshangao mkubwa.

Kwa sekunde chache Tunu alibaki amemkodolea macho Sammy akiwa hajui aseme nini, hakuweza kabisa kumjibu bali alimtazama kwa makini. Hakujua alilipata wapi jina hilo. Ni jina hilo ndilo lililomfanya aduwae kwani japo halikuwa jina lake halisi lakini kuna mtu mmoja tu alipenda kumwita hivyo. Alikuwa mwanamume wake wa kwanza ‘aliyemwondolea utoto’ wake na kumwingiza katika dunia ya wakubwa. Mwanamume yule alikuwa amelitafsiri jina la Tunu kwa Kiingereza akimwita ‘Gift’ kumaanisha tunu au zawadi.

Tunu akajiuliza, mwanamume huyu aliyeketi mbele yake alikuwa amelijuaje jina hilo? Alijaribu kuvuta kumbukumbu…

“Siwezi kuwa nimekufananisha! Pengine sikuwahi kuwa mtu muhimu kwako! Sikuwa kitu kwako, ndiyo maana ukaamua kutupa jongoo na mti wake!” Sammy alisema baada ya kuona Tunu akiwa bado anamtazama bila kusema neno lolote.

Oh my God, Sammy!” Tunu alimaka kwa mshangao mkubwa baada ya kumkumbuka, alimtumbulia Sammy macho kwa mshangao na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

* * * * *

Takriban mita hamsini toka nyumba aliyokuwa akiishi Sammy, pikipiki lililowachukua Spoiler na Dulla Mcomoro lilisimama, hawakuwa na haraka, walibaki juu ya pikipiki na kusoma kwanza mazingira. Spoiler alizima taa za pikipiki na hata pikipiki yenyewe kisha wakaendelea kukaa hapo kwa takriban dakika tano hivi.

Kisha Spoiler akaiwasha tena pikipiki na kuiondoa taratibu akiivuka ile nyumba ya Sammy huku wakiichunguza kwa makini, wakazunguka na kutokea mtaa wa nyuma na kuiegesha pikipiki kwenye kichochoro kimoja cha nyumba jirani, si mbali sana kutoka nyumba ile ya Sammy.

Kwa tahadhari kuwa Spoiler na Dulla wakajongea hadi kwenye nyumba ya Sammy, Spoiler akadanda juu ya ukuta uliozungushwa katika ile nyumba na kuchungulia ndani, hakuona mtu. Kwa haraka akarukia ndani ya fensi ya ile nyumba na kutua bila kishindo kama paka.Alisimama pale kwa muda akihakikisha usalama, kisha akampa ishara Dulla aingie na kumwelekeza aelekee upande mwingine wa nyumba kulikokuwa na karo la kuhifadhi maji taka.

Spoiler akaelekea kwenye mlango wa jikoni uliounganishwa na dirisha la kioo na kukomea hapo, kisha akachungulia ndani, kulikuwa na mwanga hafifu uliokuwa unatokea kwenye korido na sebuleni, dirisha lilikuwa limefunikwa na pazia jepesi kwa ndani lakini kupitia uwazi mdogo pembeni ya dirisha lile Spoiler aliweza kuona ndani. Alitazama kwa makini, hakuona dalili ya kuwepo mtu eneo lile.

Alijaribu kukisukuma kile kioo cha dirisha upande mmoja lakini hakufanikiwa kwani kilikuwa kimefungwa kwa ndani na komeo. Akalivua begi lake na kutoa pini ndogo yenye kung’aa kama dhahabu, akaikunja kwa mikono yake iliyofunikwa na glavu halafu akaizamisha kwenye kitasa na kukorokochoa, mlango ukafunguka!

Inaendelea...
 
Taxi - (86)

Akajitoma ndani kwa tahadhari huku akimpa ishara Dulla Mcomoro amlinde. Dula aliishika vyema bastola yake huku akiwa makini kumlinda Spoiler. Spoiler alitokea jikoni, akasimama kwa sekunde kadhaa akijaribu kuyatega masikio yake kusikiliza kama kungekuwa na sauti yoyote ambayo angeitilia shaka, hakusikia. Akaanza kutembea kwa tahadhari kuelekea kwenye korido pana ya kuelekea vyumbani.

Muda huo Dulla alikuwa ameingia jikoni na kubana kwenye ukuta akijaribu kuchunguza eneo lile kwa makini, akahisi kusikia sauti ya mtu upande wa sebuleni akishusha pumzi. Akachungulia na kumwona mwanamke mmoja akiwa amejiegemeza na ukuta sebuleni, amevaa vazi la kulalia na kiunoni alikuwa amejifunga khanga akiwa anatazama nje kupitia dirisha la sebuleni.

Dulla akainua kidole kimoja juu kumwashiria Spoiler aliyekuwa anataka kuelekea vyumbani kwamba kulikuwa na mtu mmoja.sebuleni.

Joyce alionekana kuwa na huzuni na machozi yalimlengalenga machoni. Alijaribu kuyazuia kwa kupepesa macho lakini yakadondoka. Akajifuta kwa viganja. Akiwa bado amesimama hapo mara akasikia sauti ya chombo kuanguka sakafuni, alisikiliza kwa makini na kugundua kuwa sauti ile ilitokea jikoni.

“Winnie! We Winnie kuna nini?” Joyce aliita kwa wasiwasi akidhani ni Winifrida alikuwa jikoni lakini kulikuwa kimya. Joyce akaamua kwenda jioni kuona kulikuwa na nini, alipokuwa hatua moja tu kutoka pale alipokuwa amebana Dulla akasita baada ya kuhisi kulikuwa na mtu kajificha. Moyo ulipiga kite baada ya kuona kivuli cha mtu aliyekuwa ameshika bastola mkononi akimwelekezea.

Joyce alitaka kupiga kelele lakini Spoiler aliyerudi haraka na kujificha nyuma yake akamuwahi na kumbana kisha akamvutia jikoni na kumbananisha na ukuta huku akimwekea kisu shingoni.

“Shhhhhh! Usijaribu kupiga kelele la sivyo tutakuua wewe na familia yako yote,” Spoiler alisema kwa sauti ya kunong’ona kwenye sikio la Joyce, Joyce aliogopa sana na kubaki akitetemeka.

“Sammy yupo wapi?” Spoiler alimuuliza Joyce kwa sauti ya chini huku akimkazia macho yaliyowaka kwa ghadhabu.

“Hajarudi bado,” Joyce alijibu huku jasho la woga likimtoka.

“Usinidanganye, naweza kukufanya kitu kibaya sana kama nitagundua kuwa umenidanganya,” Spoiler alimuuliza Joyce huku akizidi kumbana kwenye ukuta.

“Kweli hajarudi, siwezi kukudanganya,” Joyce alijitetea huku akikitazama kwa hofu kisu alichoshika Spoiler.

“Humu ndani mnaishi watu wangapi?” Spoiler alimuuliza Joyce huku akikipisha kisu chake kwenye shavu la Joyce katika namna ya kumwogofya.

“Wanne. Mimi, mume wangu na watoto wawili,” Joyce alisema kwa woga. Spoiler alimtazama machoni akayaamini maneno yake na kumtaka waelekee sebuleni, walipofika sebuleni wakamwamuru akae sakafuni huku Spoiler akimwekea kisu shingoni. Dulla alisimama kando, karibu na kabati la vyombo huku bastola yake ikimwelekea Joyce.

“Tafadhali naomba msiniue,” Joyce alisema kwa sauti ya kitetemeshi huku akiwa ameyatoa macho kwa woga.

Sauti yake ikapenya hadi kwenye chumba walichokuwa wamelala Winifrida na Pendo. Winifrida alifumbua macho yake na kusikiliza kwa makini huku akiyatupa macho yake dirishani. Hakuona kitu chochote cha kukitilia shaka. Akajiuliza ina maana alikuwa anaota? Hapana. Ile haikuwa ndoto kwani hakuwa amepitiwa usingizi japo alikuwa amelala kitandani.

Mara akakumbuka, kuna muda aliruhusu usingizi kumpitia na aliota ndoto ya kutatanisha iliyomfanya asipate tena usingizi. Katika ndoto hiyo aliota kwamba alikuwa analia, kilikuwa kilio cha msiba! Lakini hii haikuwa ndoto, alikuwa amemsikia wifi yake Joyce kwa masikio yake mawili. Je, ni nani alitaka kumuua Joyce? Sammy? Kwa nini amuue? Winifrida alijiuliza lakini akakosa jibu.

Alijiinua taratibu kutoka pale kitandani na kusimama huku akiwa na hofu, moyo wake ulikuwa unakwenda mbio isivyo kawaida. Akaanza kupiga hatua taratibu akisogea mlangoni kwa tahadhari kubwa huku akijaribu kuyatega masikio yake kama angeweza kusikia chochote. Mara akasikia sauti nzito ambayo hakuitambua, haikuwa sauti ya Sammy, ilikuwa sauti ngeni kabisa masikioni mwake, “Sema ukweli, Sammy kaenda wapi?”

“Mimi sijui, tangu alipoondoka hapa mchana sijui kaenda na wala hatujawasiliana,” Joyce alijibu kwa hofu.

Winifrida akashtuka sana na kujikunyata pale mlangoni kwa hofu, mara akaisikia tena ile sauti nzito ikisema, “Dee, cheki chumba kimoja kimoja na yeyote utakayemkuta huko mlete hapa.” Winifrida alihisi haja ndogo ikimtoka.

Dulla aliondoka haraka eneo lile na kuifuata korido pana iliyoelekea vyumbani, aliiona milango mitano, milango miwili ikiwa upande wa kulia na milango mingine mitatu upande wa kushoto. Dulla akaufuata mlango wa kwanza upande wa kulia na kugundua ulikuwa wa kuingia jikoni. Akauacha na kuufuata mlango wa pili.

Aliufikia na kukiminya kitasa cha mlango kisha akausukuma, mlango ukafunguka, chumba hakikuwa na mtu yeyote kwa kuwa kilikuwa chumba cha Sammy na mkewe Joyce. Akatoka na kuufuata mlango wa kwanza kushoto, kilikuwa chumba cha maliwato ya wote, mlango uliofuata pia hakukuwa na mtu yeyote, kilikuwa chumba cha wageni.

Sasa kilibaki chumba kimoja tu kilichokuwa mwisho upande ule wa kushoto ambacho aliamini kwamba kilikuwa chumba cha watoto. Dulla akafika na kushika kitasa cha mlango, akakiminya na kuusukuma lakini mlango ulikuwa umefungwa kwa funguo. Akakiminya kitasa kile mara tatu mfululizo na kukiachia, mlango ukafunguka.

Akaingia chumbani kwa tahadhari na kumkuta mtoto Pendo amelala. Dulla alisimama pale kwa kitambo akijaribu kujiuliza, mtoto mmoja, je, mwingine yuko wapi? Akahisi kuna jambo halikuwa sawa. Akaanza kupiga hatua taratibu huku akielekeza bastola yake pale kitandani, kisha akainama kuangalia uvunguni mwa kitanda, hakuona mtu. Akaguna na kugeuka kutazama kila sehemu, akaliona kabati la nguo la ukutani na kuachia tabasamu.

Akaanza kulisogelea lile kabati huku akielekeza bastola yake, kiza kilichokuwepo mle ndani hakikumzuia kuona kila kitu, alikuwa makini kusikiliza kila sauti aliyoitilia shaka, alizidi kulisogelea lile kabati kwa tahadhari, alipolifikia akafungua milango huku bastola ikiwa imeshikwa vyema mkononi ikiwa tayari kwa lolote. Hakuona mtu. Akachakura chakura nguo kuhakikisha lakini hakukuwa na mtu. Akatweta.

Endelea kufuatilia...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom