Stori ya kusisimua - Taxi

Stori ya kusisimua - Taxi

Dah hicho kisauti ulichotumia kumuita bishop lazima aje tu yaani kimepenya mpaka moyoni
🤦‍♀️🤦‍♀️🤦‍♀️🤦‍♀️ngoja tuone kama atakuja kweli
 
Taxi - (87)

Akaanza kulisogelea lile kabati huku akielekeza bastola yake, kiza kilichokuwepo mle ndani hakikumzuia kuona kila kitu, alikuwa makini kusikiliza kila sauti aliyoitilia shaka, alizidi kulisogelea lile kabati kwa tahadhari, alipolifikia akafungua milango huku bastola ikiwa imeshikwa vyema mkononi ikiwa tayari kwa lolote. Hakuona mtu. Akachakura chakura nguo kuhakikisha lakini hakukuwa na mtu. Akatweta.

* * * * *

“Hivi, uliwezaje kunifanyia hivi? Labda sikuwa muhimu kwako…” Sammy alisema huku akimwangalia Tunu kwa utulivu.

Shhhhh! I’m so sorry…” Tunu alisema kwa sauti ya chini.

Sorry for what?” Sammmy aliuliza kwa sauti tulivu.

For everything…”

“Hata siamini, hata baada ya miaka kumi na moja kupita bado unaonekana mrembo kwelikweli…” Sammy alichombeza baada ya kitambo kifupi cha ukimya. Tunu hakujibu, alibaki kimya huku tabasamu likiwa limeupamba uso ake.

Sammy alishusha pumzi, akajaribu kuvuta picha kukumbuka alivyokutana na Tunu miaka kumi na moja iliyokuwa imepita kwenye mahafali ya wanafunzi waliomaliza kidato cha sita ya Shule ya Wasichana ya Jangwani jijini Dar es Salaam, siku hiyo Tunu alikuwa mmoja wa wanafunzi wahitimu wa kidato cha sita.

Wakati huo Sammy alikuwa na umri wa miaka ishirini na nne tu na hakuwa na muda mrefu tangu ahitimu Shahada ya Kwanza ya Utalii na Biashara (Tourism With Business BA Honours) katika Chuo Kikuu cha Westminster nchini Uingereza.

Ilibakia kidogo tu angekufa kwa mshtuko wa moyo siku alipomwona Tunu kwa mara ya kwanza. Siku hiyo Sammy alikuwa ameambatana na Elli wakiwa wamepewa mwaliko wa Grace, dada wa Elli ambaye pia alikuwa mmoja wa wahitimu wa kidato cha sita. Wakiwa pale macho ya Sammy yalikuwa yakiangaza huku na huko. Wasichana walikuwa wamependeza kwelikweli, walikuwa wakicheza, wakicheka na kufurahi.

Mara Sammy akamwona msichana mmoja aliyekuwa ameketi kwa utulivu mno kuliko wasichana wengine. Alikuwa amemwona kabla lakini hakuwa amemtilia maanani, safari hii alimtulizia macho. Macho yao yakagongana. Sammy akashtuka sana. Huyu hakuwa msichana wa kawaida, alikuwa jamali aliyeumbika.

Sammy aliweza kuuona waziwazi urembo wa binti huyo japo alikuwa amevaa joho refu na pana lililokuwa limefunika maungo yake. Kwa nukta kadhaa alijikuta akiduwaa na kumkodolea macho. Pumzi zikampaa.

Akabaki kumtazama kuanzia miguuni hadi kichwani huku akijiambia kimoyomoyo, katika maisha yake hakupata kuhisi hali kama ile aliyoihisi muda ule kwa sababu ya msichana, tena kiumbe cha shani kama hicho! Amewahi kukutana na wasichana wengi warembo lakini alikiri kuwa hakuwahi kupatwa na hali kama ile iliyomtokea kwa mrembo huyo.

Muda wa kucheza muziki ulipowadia Sammy hakutaka kujivunga, alikwenda moja kwa moja hadi pale alipokuwa ameketi Tunu na kuinama kidogo kwa heshima huku akiweka mkono wake kifuani, “Naomba tucheze tafadhali. Kama utaniruhusu, wimbo mmoja tu.”

Tunu alimtazama kwa kitambo kama aliyekuwa akijishauri kisha bila kuongea neno wakaingia uwanjani na kuanza kulisakata. Kwanza kwa haya kidogo maana walikuwa hawafahamiani. Walicheza kimyakimya. Taratibu muziki ukaanza kuifukuza haya hiyo na miondoko yao ikaanza kurandana kiasi cha kuwavutia watu ambao hawakuwa wakicheza.

Watu wengi walijikuta wakiwaangalia wao tu, wengine kwa kuvutiwa na uchezaji wao, na wengine kwa husuda. Walipendeza mno wakawa kama pacha. Wimbo ule ukaisha na wimbo wa pili wa taratibu ukaanza, hawakuondoka. Walianza kuucheza huku wamekumbatiana. Kila mmoja alisahau kama kulikuwa na watu wengine wakiwaangalia. Hisia zao zilikuwa huru, wakiburudika mwili na roho, akili zao zikijiona kama waliofika safari yao baada ya kuvuka milima na mabonde.

“Unaitwa nani mrembo wangu?” Sammy alimuuliza Tunu huku mikono yake ikipapasa nyama za mgongo na kiuno chake.

“Naitwa Tunu,” Tunu alisema kwa sauti ya chini huku akiipitisha mikono yake nyuma ya shingo ya Sammy na kufanya chuchu za matiti yake kukitekenya kifua cha Sammy. Alisahau kabisa kama macho ya watu yaliyokuwa yakiwatazama. Sammy akajikuta akiwa na wakati mgumu wa kupambana na joto kali la mwili wa Tunu lililomfanya ajisikie faraja ya aina yake.

“Tunu nani?”

“Tunu Robin,” alinong’ona, “Na wewe?”

“Samuel Kambona, ila wewe niite Sammy…” Sammy alisita kidogo, kisha akaongeza, “Kwa kweli leo nimefurahi sana kukutana na wewe.”

“Kweli?” Tunu aliuliza kama mtoto mdogo.

“We unadhani nani asingefurahia kukutana na mrembo kama wewe? Au nani asingetamani kutaka kumkumbatia mrembo kama wewe? Hakika siku ya leo nitaikumbuka katika maisha yangu,” Sammy alisema huku akiupapasa mgongo wa Tunu. Tunu alifumba macho yake huku akiusikilizia mpapaso ule wa mikono ya Sammy.

“Najua kukutana kwetu hakukuwa kwa bahati mbaya, kila jambo huja kwa kusudi lake, na hii kwetu ndiyo nafasi nzuri. Unaonaje tukaifanya siku ya leo kuwa ya kukumbukwa zaidi kwenye maisha yetu,” Sammy alimwambia Tunu huku akimwangalia usoni.

“Ki vipi?” Tunu aliuliza huku akionesha mshangao kwa mbali, hakuonekana kuelewa maneno ya Sammy yalikuwa na maana gani.

“Sidhani kama nitaweza kuendelea kuishi kama sitapata penzi lako…” Sammy alisema kwa sauti ya kunong’ona.

“Ningetamani sana iwe hivyo lakini miye sijawahi kufanya mapenzi na mwanamume yeyote,” Tunu alisema huku akimtazama Sammy kwa aibu.

“Kweli!” Sammy aling’aka kwa mshangao uliochanganyika na shauku, shauku hiyo ikaipalilia hamu ya kutaka kumpata Tunu.

Mara wakashtuka baada ya kuhisi eneo lote lilikuwa limetawaliwa na ukimya. Kumbe muziki ulikuwa umekwisha kitambo! Ni wao wawili tu ndio waliokuwa wamebaki wima kwenye eneo la kuchezea muziki. Kwa aibu wakaondoka na kuongozana kwenda kukaa. Lakini huo haukuwa mwisho, walipanga na kukutana siku iliyofuata.

Sammy alimchukua Tunu hadi kwenye nyumba aliyokuwa amepanga eneo la Makumbusho, Kijitonyama. Siku hiyo Tunu alikuwa amevaa blauzi na kaptula ya kitenge. Kaptula ile iliishia juu ya magoti yake na kuifichua minofu ya miguu na mapaja yake yaliyonona.

“Nimekuja mara moja tu kukusalimia, sitakaa muda mrefu,” Tunu alisema huku akiitazama saa yake ya mkononi mara tu walipoingia ndani. Hata hivyo, Tunu alikuwa akimtazama Sammy kwa macho ya wizi, macho yake yalikuwa yamelegea kama aliyekuwa amekula kungu, sura yake ilionekana wazi kumsubiri Sammy afanye kitu.

Sammy aligundua kuwa Tunu alikuwa amekolea ingawa haikuwa rahisi kwake kukubali moja kwa moja, akamshika mkono. Hakuleta pingamizi lolote, kwani alionekana kutojiweza na uso wake aliuinamisha chini kwa aibu. Alimvutia kifuani kwake akamkumbatia. Tunu alijigandamiza kwenye mwili wa Sammy na kutulia huku akihema kwa nguvu.

Sammy hakuendelea kusubiri, alimbeba hadi kitandani, akamwangusha kama mzigo. Tunu pumzi zilimpaa! Kilichofuata baada ya hapo kilimfanya ahisi kuchanganyikiwa. Alijikuta akiwa taabani huku akiyashuhudia maumivu ya kupendeza yaliyokuwa yakimuua taratibu kama mgonjwa taabani. Yote yaliyotendeka kwenye mwili wake hakuwahi kuyaona ndotoni au hata kuyafikiria.

Mambo yanazidi kunoga, teksi inazidi kuzua mambo na sasa imewaunganisha tena Sammy na Tunu. Je, nini kitafuata baada ya hapo? Sammy atamsaliti Joyce? Je, Tunu hana mume? Na vpi kuhusu uvamizi nyumbani kwa Sammy, Winifrida yupo wapi? Usikose kufuatilia stori hii ya kusisimua...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom