Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Asante sana bishop.hadithi nzuri mno.ila naona watuhumiwa wamekamatwa kizembe zembe. Halafu kama imeishia njiani maana jacky na yasmine wametoroka that's it
Yule bwana wa jacky sijui vipi nae? .ila asante sana
 
Nimefurahishwa na uadilifu wa ASP kombo wangekuwa waswahili wetu hawa wangejipongeza kwa robo ya mpunga ule ingefika B peke yake hizo M yule giriki angezisikia tu
 
Kizungumkuti! - 77

Na Bishop Hiluka

Ghafla Jacky akafanya jambo ambalo hakuna yeyote aliyekuwa amelitarajia, aliruka hewani kutoka pale alipokuwa amesimama na kutua nje ya kile chumba na kubonyeza namba fulani kwenye kile kisanduku kilichokuwa na namba kando ya ule mlango wa ofisi. ASP Komba alishtuka na kuruka juu kumfuata Jacky, bastola ikiwa mkononi, lakini alikuwa amechelewa! Mlango ukajifunga.

Kwa sekunde kadhaa ASP Komba na Sajenti Mapambano wakachanganyikiwa wasijue wafanye nini, fahamu zilipokuja kuwarudia, ASP Komba alishusha pumzi ndefu kana kwamba alikuwa ametoka kwenye mbio ndefu za marathoni.

Endelea...

What are we going to do?” (Tutafanyaje) Sajenti Mapambano aliuliza kwa wasiwasi.

The bastard has escaped. We must do something to get out of here,” (Mwanaharamu katoroka. Lazima tufanye kitu tutoke humu) ASP Komba alisema huku akijaribu kuufungua ule mlango uliokuwa umejifunga bila mafanikio.

“Inaonekana chumba hiki kina mambo makubwa tusiyoyafahamu. Tunachotakiwa ni kutafuta namna ya kujiokoa kutoka humu ndani haraka kabla hayajatukuta makubwa,” ASP Komba alimwambia Sajenti Mapambano huku akionesha kukata tamaa.

Kisha kama mtu aliyekumbuka jambo alichukua simu yake kisha akapiga simu ofisini kwake akiwafahamisha kilichotokea na kuwaomba waongeze nguvu na wamlete mtaalamu wa Tehama.

* * * * *

Saa kumi na mbili jioni, ndani ya ofisi za Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kanda Maalumu, kwenye jengo la kituo kikuu cha polisi jijini Dar es Salaam, ASP Komba alikuwa ameketi kwenye kiti chake cha kuzunguka.

Mkononi alikuwa ameshika faili kubwa ambalo alikuwa akilipitia na kuhakiki zile taarifa. Mara mlango wa ile ofisi ukagongwa mara moja na kufunguliwa, kisha Nassos Chatzopoulos, mkurugenzi mkuu wa The Jacarandah Group akaingia na kutembea taratibu huku akionekana mnyonge sana.

ASP Komba alimtazama Nassos Chatzopoulos na kuachia tabasamu huku akimuelekeza kiti. Nassos aliketi kwenye kile kiti huku akimtazama ASP Komba kwa umakini.

I’m sorry to bother you, Mr Nassos, but I’ve called you to give you a final report of our case on the part of the investigation,” (Samahani nimekusumbua, bwana Nassos, lakini nimekuita ili nikupe taarifa ya mwisho ya kesi yetu kwa upande wa upelelezi) ASP Komba alimweleza Nassos huku akiendelea kutabasamu.

Okay, officer, but I'm desperate to get back my money, however, I don't know where you've got?” (Sawa, afande, lakini mimi nimeshakata tamaa kabisa ya kuzipata fedha zangu, hata hivyo, sijui mmefikia wapi?) Nassos Chatzopoulos alisema na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

All your money was found…” (Fedha zako zote zimepatikana…)

Impossible, all!” (Haiwezekani, zo-te!) Nassos aliuliza huku akinyanyuka kutoka kwenye kile kiti kwa mshtuko mkubwa, alimkodolea macho ASP Komba kwa mshangao akiwa haamini kile alichokisikia.

All and have been stored within the central police cabinet of the stolen money. You’ll be given once the case has ended,” (Zote na zimehifadhiwa ndani ya kabati kuu la polisi la fedha zilizoibiwa. Utakabidhiwa mara tu kesi itakapomalizika) ASP Komba alisema huku akishusha pumzi.

When?” (Lini?) Nassos aliuliza kwa shauku kubwa.

It won't take long. The defendants will be brought to court tomorrow morning, and we’ll make sure the case goes quickly because all the evidences are there,” (Haitachukua muda. Washtakiwa watakafikishwa mahakamani kesho asubuhi, na sisi tutahakikisha kesi inakwenda haraka maana vielelezo vyote vipo) ASP Komba alimwambia Nassos huku akilifunga lile faili na kuliweka kwenye droo ndogo ya meza yake.

How many defendants are there?” (Kwani washtakiwa wenyewe ni wangapi?) Nassos alimuuliza ASP Komba kwa shauku huku sura yake ikianza kuonesha nuru.

They were three defendants but now they are only two. Yusuf Akida, the employee of the Commercial Bank and the notorious criminal called Liston George. The first defendant, a woman who was the key arranger of all strategies, called Jackline Mgaya has managed to escape,” (Walikuwa watatu lakini kwa sasa wapo wawili tu. Yusuf Akida, yule mfanyakazi wa Benki ya Biashara na mhuni maarufu anaitwa Liston George. Mshtakiwa wa kwanza mwanamke aliyekuwa mratibu mkuu wa mipango yote, anayeitwa Jackline Mgaya amefanikiwa kutoroka) ASP Komba alisema na kumfanya Nassos kushangaa kidogo.

I heard even my attendant, Jasmine Kombo is involved in theft! Will she not be brought to court?” (Si nilisikia hata yule mhudumu wangu, Jasmine Kombo kuwa amehusika kwenye wizi! Kwani yeye hatafikishwa mahakamani?) Nassos aliuliza kwa mshangao.

She’d have been brought if she were present,” (Kama angekuwepo angefikishwa) ASP Komba alisema huku akizilamba kingo za midomo yake kwa ulimi.

If she were present! What do you mean, officer, I’ve heard she’s admitted in hospital?” (Kama angekuwepo! Unamaanisha nini, afande, si nimesikia amelazwa hospitali?) Nassos aliuliza huku akizidi kushangaa. ASP Komba alivuta pumzi ndefu kisha akazishusha taratibu.

She has also escaped this midday after the interrogation,” (Pia katoroka leo mchana baada ya mimi kutoka kumhoji) ASP Komba alisema, Nassos akaguna. Wakatazamana kwa kitambo kifupi na kuangua kicheko.

Kicheko chao kilikatizwa na simu ya ASP Komba iliyoanza kuita, ASP Komba alitaka kuipuuza ile simu lakini alipoitazama kwa makini akashtuka sana baada ya kugundua kuwa ilikuwa inatoka kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Evance Hiza. Akaipokea haraka na kuiweka sikioni.
Hello!” ASP Komba alisema kwa unyenyekevu.

“Habari yako, ASP?” sauti nzito ya IGP Hiza ikasikika kutoka upande wa pili wa ile simu.

“Nzuri, afande!” ASP Komba alijibu kwa sauti ya ukakamavu.

“Umefikia wapi huko?” IGP Hiza aliuliza kwa shauku.

“Tumekamilisha kazi, afande,” ASP Komba alijibu kwa ukakamavu.

“Unasema…?”

“Nasema tumekamilisha ile kazi, afande.”

“Mmefanikiwa kuzipata fedha zote zilizoibwa?”

“Ndiyo, afande, fedha zote zipo salama na zimehifadhiwa ndani ya kabati kuu la polisi la fedha zilizoibiwa,” ASP Komba alisema huku akimtupia jicho Nassos.

“Vipi watu walioshiriki katika wizi wa mabilioni pale benki, mmefanikiwa kuwakamata?”

“Ndiyo, afande, tunao watuhumiwa wawili na mmoja ametoroka… wengine watatu wamekufa katika operesheni,” ASP Komba alisema huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.

IGP Hiza alinyamaza kwa sekunde kadhaa, kisha akaibuka, “Mbali na wewe, ni nani mwingine alikuwa mstari wa mbele katika kuongoza upelelezi huo?”

“Msaidizi wangu, Sajenti Mapambano.”

“Yupo ofisini sasa hivi?”

“Hapana, nimempa mapumziko ya siku mbili, ataingia kazini keshokutwa asubuhi. Vipi afande?” ASP Komba aliuliza huku akionekana kupata shaka kidogo.

“Wanasema mcheza kwao hutunzwa. Kuna nafasi zimetoka za askari kwenda masomoni Toronto, Canada mwezi ujao, nataka nimpe nafasi hiyo Sajenti Mapambano akaongeze ujuzi…” IGP Hiza alisema na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Na wewe jina lako tayari lipo mezani kwa Rais, utakuwa mmoja wa maofisa wa polisi watakaopewa kamisheni na Rais wa Tanzania kuwa Makamishna wasaidizi wa Polisi, kwa hiyo utapanda nafasi mbili zaidi kutoka Mrakibu Msaidizi wa Polisi hadi Kamishna Msaidizi wa Polisi. Na ukishapewa kamisheni tu nakuhamishia Arusha kuwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa,” IGP Hiza alisema na kumfanya ASP Komba akenue meno yake kwa furaha.

“Ninashukuru sana, afande, ninashukuru sana…” ASP Komba alisema kwa nyenyekevu. IGP Hiza akakata simu.

MWISHO.
0685 666964
Daah Carlos kafa kizembe sana...

Jacky nimependa kujiamini kwake na namna anvyojibu maswali...

Safi sana...

Chapter closed...


Cc: mahondaw
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom