Stone Town, Zanzibar alasiri hii...

Stone Town, Zanzibar alasiri hii...

Kalipia kodi huyo mwache ajitawale.na ukizingatia karibia 70% kama sikosei ya budget ya smz yategemea kutoka kwenye tourism....wacha ale raha kila siku analipia 9 usd ya hotel levy kwa ZRB huyo
 
44029743_1866643770038373_1892101246152605696_n.jpg
Nailaumu mamlaka inayoshughulikia utalii Zanzibar hasa kisiwa cha Unguja. Ni ukweli usiopingika kuwa Zanzibar ni nchi ya kiislam na sidhani kama huyo dada angeelekezwa vizuri na madereva wa Taxi au wananchi wenye busara na lugha ya staha ambao wamejaaliwa kwa kufunzwa au kubarikiwa kuwa na uwezo wa kuhodhi hasira zao, wangemueleza huyo dada kuwa tunajitolea hata dera la bure ili ujisitiri.
Huyo mzungu hana nia mbaya kabisa na pengine ni mtu mstaarabu, ila inabidi aambiwe. Rome kwa mfano, kuna strict dress code hasa ukitembelea Basillica, hata gardens za Vatican dress code ni mabega na magoti yasionekane. Hii wazungu wanajua, na kuna walinzi watakutoa kwenye foleni usipofuata.
Mwisho, huyo mwanamke angekua mweusi (Naenda kuvinjari unguja karibu kila mwaka) hasa wakenya, wasouth na watanzania bara huwa wanatukanwa na vijana wadogo wa unguja ingawa wengi siku hizi huwa wanajisitiri Stonetown na kujiachia beach kama Nungwi etc... Kwa hiyo wazanzibari wana uwezo wa kubadilisha hili kwa staha kabisa na kila mtu akafaidika.
 
Joto kali, hata mie kesho ntavaa hivohivo kuelekea Mtwara.
 
Write your reply...Kila Jambo linalohusu Zanzibar lazima lilete sintofahamu humu ....lazima muelewe tunazungumzia Zanzibar sio Dar au Rukwa!!!
 
Lakini wanaponunua ticket wanaelezwa kuwa kujiachia ni kwenye mazingira ya hoteli uliyofikia nje jizibe maungo.
 
Back
Top Bottom