Stand ya Loliondo Kibaha aibu kwa Serikali ya Mkoa wa Pwani

Songambele

JF-Expert Member
Nov 20, 2007
4,697
2,559
Bado changamoto nyingi tulizonazo zinasababishwa na watawala na serikali zetu za kiafrika. Kwa Akili ya kawaida na viongozi wenye Akili timamu hawawezi kulazimisha kila Bus dogo linaloenda kwa Mattias, kongowe au mlandizi kupitia Loliondo.

Miundombinu ya kuingia njia hiyo ndio shida ilipo, kwanza Kona Kali ya kuchepukia katika high way ya morogoro hili tumemwachia mwenyezi ila siku yeyote pale wanapasuka watu ila hatuombei itokee.

Kikitokea chochote asitafutwe mchawi. pili barabara yenyewe ni mbovu na inaharibu magari na kupoteza muda kwa watu wanaokwenda mbali. Tatu stand yenyewe ni aibu kwa serikali ya Jamhuri ya muungano na mkoa wa pwani.

Ni kweli Pwani wanakaa waswahili lakini waswahili wapenda vitu vizuri sio huu ujinga wa Loliondo. Nne mie kwa hesabu yangu ya ngumbalu ni Zaidi ya Bus 100 ziko katika njia hii na stand haifai hata kwa gari 10 kuitumia kwa wakati na kubwa kuliko ni Geshi la Polisi ndio wamegeuza dambwe la kuchukulia rushwa, njia mbaya na lazima kupita madereva wakichepuka wanakutana na wala rushwa.

Kunaulazima gani wanaokwenda Mlandizi kupitia Loliondo, kwanini tusichague wenyewe tokea mbezi tupunguze jam na usumbufu kama hakuna anayeshuka tuokoe muda. Kwanini iwe lazima wakati miundombinu haiko tayari kuhudumia watu wengi.
 
Stendi ya liliondo ndo wapi mkuu,, iko wapi hiyo,, mana nina miaka takribani miaka kumi na kadhaa sijapita hiyo njia ijapokuwa mie mwenyeji sana wa hayo maeneo uliyoyataja
 
Nikiwa ninaenda Vigwaza inakera sana gari kupitia kule Loliondo. Ni mbali, muda unaenda.

Ila kuna baadhi ya gari hupitia Tumbi na kutokezea Picha ya Ndege. Hizi angalau kidogo!
 
Bado changamoto nyingi tulizonazo zinasababishwa na watawala na serikali zetu za kiafrika. Kwa Akili ya kawaida na viongozi wenye Akili timamu hawawezi kulazimisha kila Bus dogo linaloenda kwa Mattias, kongowe au mlandizi kupitia Loliondo.

Miundombinu ya kaingia njia hiyo ndio shida ilipo, kwanza Kona Kali ya kuchepukia katika high way ya morogoro hili tumemwachia mwenyezi ila siku yeyote pale wanapasuka watu ila hatuombei itokee.

Kikitokea chochote asitafutwe mchawi. pili barabara yenyewe ni mbovu na inaharibu magari na kupoteza muda kwa watu wanaokwenda mbali. Tatu stand yenyewe ni aibu kwa serikali ya Jamhuri ya muungano na mkoa wa pwani.

Ni kweli Pwani wanataka waswahili lakini waswahili wapenda vitu vizuri sio huu ujinga wa Loliondo. Nne mie kwa hesabu yangu ya ngumbalu ni Zaidi ya Bus 100 ziko katika njia hii na stand haifai hata kwa gari 10 kuitumia kwa wakati na kubwa kuliko ni Geshi la Polisi ndio wamegeuza dambwe la kuchukulia rushwa, njia mbaya na lazima kupita madereva wakichepuka wanakutana na wala rushwa.

Kunaulazima gani wanaokwenda Mlandizi kupitia Loliondo, kwanini tusichague wenyewe tokea mbezi tupunguze jam na usumbufu kama hakuna anayeshuka tuokoe muda. Kwanini iwe lazima wakati miundombinu haiko tayari kuhudumia watu wengi.
Ile stand walidhani watu wataifata badala ya Stand Kufata watu.

Kihasibu pale ni hasara tupu na Stand naona inaota nyasi tu.
 
Sijui Kama Pwani Kuna uongozi unaojalimaslahi ya wanànchi. Ni kweli pale magari yanapochepukia sio rafiki kabisa.

RTO yupo, mkuu wa mkoa yupo, mkuu wa wilaya yupo, mkurugenzi yupo.
Wote kwa pamoja wanasubiri watu wamwage damu pale ndio waonekane kwenye tv.
Kuna umuhimu gani magari yapite Loliondo.
Kama wangekua na akili, angalau haya magari yangepita tumbi hospitali kuwapunguzia shida wagonjwa na wasaidiziwa wao.
Kila ukipanda hizi daladala utasikia watu wakisema Bora makonda angeletwa mkoa wa Pwani maana umedorora Sana.
 
Jamani mnanivunja moyo nilikuwa na hamu ya kununua kiwanja cha kujenga huko, kwani watu wanasifu Kibaha mjini mzuri, unakuwa kwa kasi, mipango miji iko vizuri.
 
Back
Top Bottom