Nimebaini kuwa adui mkubwa wa Taifa la Tanzania kwa sasa ni Dk.Tulia Ackson ambaye mambo yote machafu yamefia mikononi mwake na taifa likiwa halijua linatokaje kwenye mkwamo huu. Mfano wa mambo yaliyofia mikononi mwa Tulia na Bunge lake.
1. Mkataba wa Bandari Serikali iliupeleka Bungeni tangu mwezi wa Februari 2023 Spika amekaa nao kwa miezi mitano hadi Juni 2023 ndiyo anauleta Bungeni tena kwa dharura na kujadiliwa siku moja na kupitishwa na kusababisha balaa linaloendelea sasa.
2. Ripoti ya CAG amepelekewa tangu mwezi Machi huku ikionyesha ufisadi mkubwa wa matrilioni ya fedha yeye ameikalia anasema hadi Novemba ndiyo itajadiliwa wakati mwenzake Spika Makinda alipopelekewa ripoti ya CAG na kuonyesha ufisadi wa Escrow aliitisha bunge la dharura kujadili hoja ya Escrow hakusubiri bunge la Novemba.
3. Kuna Mbunge aliomba indwe tume kuchunguza suala la bei ya Mafuta tangu Mwaka jana Juni 2022 ili ukweli ufahamike kuhusu biashara nzima ya mafuta, Spika akakataa ushauri huo wa kuunda tume kwa kuwalinda hao wahusika leo nchi inalia kila kona tatizo la mafuta
Ni dhahiri anayeshabikia na kusababisha Serikali kuchafuliwa na kutukanwa kwa kiwango hiki na wananchi wengi kupoteza imani na Serikali yao ni huyu Spika wa Bunge ambaye mambo yote yanayohitaji uamuzi ameyakalia ofisini kwake kwa manufaa binafsi.
Kila jambo Rais analiwahisha Bungeni kwa ajili ya hatua lakini Spika akifika yeye anazunguka na mambo hayo kwa faida anazojua yeye.
1. Mkataba wa Bandari Serikali iliupeleka Bungeni tangu mwezi wa Februari 2023 Spika amekaa nao kwa miezi mitano hadi Juni 2023 ndiyo anauleta Bungeni tena kwa dharura na kujadiliwa siku moja na kupitishwa na kusababisha balaa linaloendelea sasa.
2. Ripoti ya CAG amepelekewa tangu mwezi Machi huku ikionyesha ufisadi mkubwa wa matrilioni ya fedha yeye ameikalia anasema hadi Novemba ndiyo itajadiliwa wakati mwenzake Spika Makinda alipopelekewa ripoti ya CAG na kuonyesha ufisadi wa Escrow aliitisha bunge la dharura kujadili hoja ya Escrow hakusubiri bunge la Novemba.
3. Kuna Mbunge aliomba indwe tume kuchunguza suala la bei ya Mafuta tangu Mwaka jana Juni 2022 ili ukweli ufahamike kuhusu biashara nzima ya mafuta, Spika akakataa ushauri huo wa kuunda tume kwa kuwalinda hao wahusika leo nchi inalia kila kona tatizo la mafuta
Ni dhahiri anayeshabikia na kusababisha Serikali kuchafuliwa na kutukanwa kwa kiwango hiki na wananchi wengi kupoteza imani na Serikali yao ni huyu Spika wa Bunge ambaye mambo yote yanayohitaji uamuzi ameyakalia ofisini kwake kwa manufaa binafsi.
Kila jambo Rais analiwahisha Bungeni kwa ajili ya hatua lakini Spika akifika yeye anazunguka na mambo hayo kwa faida anazojua yeye.