Blaki Womani
JF-Expert Member
- Feb 28, 2011
- 11,228
- 13,448
Tunataka liwe kama bunge la Kenya
Na walimteua wamevunjwa miguu juziInaonekana Spika wa Bunge hana nguvu za kuongoza vikao hivyo vya bunge; Tatizo ni kuwa hakugombea aliteuliwa
mama makinda wabunge hawakuheshimu wewe au hawamheshimu spika wa bunge?
Tafakari, chukua hatua.
Tunataka liwe kama bunge la Kenya
Hii ndio aina ya wabunge tulionao kwenye Bunge letu wanaowakilisha wananchi kazi kweli kweliImeandikwa na Basil Msongo, Dodoma; Tarehe: 13th April 2011
SPIKA wa Bunge, Anne Makinda, leo amepata wakati mgumu kuongoza kikao cha uchaguzi wa wajumbe kwenye taasisi mbalimbali za kibunge kwa kuwa wabunge walikuwa wanajibishana na kusababisha vurugu bungeni.
"Msitumie wingi wenu kutuburuza, mmezoea kutuburuza, tufunge mlango tupigane" walisema wabunge na kusababisha vurugu bungeni kwa takribani dakika kumi.
Mabishano hayo yalisababisha Spika akasirike na kuwaeleza wabunge kuwa walikuwa wanafanya mambo ya kijinga.
Vurugu hizo zilianza baada ya Mbunge wa Nyamagana, Ezekia Wenje (Chadema), kusema bungeni kuwa, mchakato wa kuwapata wagombea wa nafasi hizo ulifanywa kwenye dark market.
Wabunge wanaoaminika kuwa ni wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), walishinikiza Mbunge huyo afute kauli yake, Makinda akamtaka Wenje afute kauli yake.
Wenje alisimama lakini hakufuta kauli yake, baadhi ya wabunge wakawa wanapiga kelele kushinikiza afukuzwe wakitumia maneno ‘out out out, atoke nje .
Wabunge hao walimtaka Mbunge huyo atoke, akanywe kikombe cha Babu, Loliondo.
Mara kwa mara Spika alilazimika kuwatuliza wabunge kwa kuwataka wamsikilize Mbunge aliyekuwa anazungumza.
Makinda aliwaeleza wabunge kuwa wanapaswa kutambua kuwa wananchi wamewachagua, na walikuwa wanawaangalia.
"Kwa nini mnafanya fujo isiyokuwa na akili… waheshimiwa wabunge tunafanya mambo ya kijinga" alisema Makinda lakini wabunge waliendelea kurushiana maneno.
Kwa mara nyingine Spika alimtaka Wenje afute kauli yake kwa kumweleza kuwa alikuwa amemtukana yeye Makinda na wajumbe wote wa Kamati ya Uongozi ya Bunge.
Alimweleza Wenje kuwa wao wote ni watu wazima na ni jambo la kawaida kwa Mbunge kufuta kauli bungeni.
Alimuuliza Wenje kwamba ingemgharimu shilingi ngapi kufuta kauli yake, na akamuuliza Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe kama Mbunge huyo angefanya hivyo, ingemgharimu kiasi gani.
Baadhi ya wabunge waliendelea kushinikiza Wenje afukuzwe, na kelele hizo zilizidi baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Frederick Werema, kumweleza Spika kuwa ulikuwa wakati mwafaka kwake kumuamuru Wenje atoke nje ya Bunge.
Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto, alisema ni kweli Kamati ya Uongozi ya Bunge ilikutana kuzungumzia suala hilo, lakini hazikutolewa fomu ili wagombea wajaze.
Zitto alisema, kamati hiyo si dark market lakini haikuwa sahihi kuitafsiri visivyo kauli ya Wenje, wao (wabunge) wote ni wanasiasa, wawe na ngozi ngumu.
Baadhi ya wabunge waliendelea kusisitiza kuwa Wenje atoke, Zitto akawajibu kuwa hatoki, na wabunge wengine wakasema "hatoki mtu, tutatoka wote"
Makinda alimpa Wenje fursa nyingine ya kufuta kauli yake, Mbunge huyo akasema, hakusema Kamati ya Uongozi ni dark market, ila alimaanisha mchakato uliotumika, ma mwishoni akasema, anafuta maneno dark market, anaweka white market.
Iko siku tu.wangechapana makonde kabisa lol
Naam waache wachapane tu, na kama CDM wanataka msaada basi kuchapana huko kutaendelea mpaka uraiani. Watanzania tumechoshwa na Bunge la usanii linalotetea upuuzi miaka nenda miaka rudi.
hivi wakianza kutwangana mama makinda atabaki na meno mangapi?mama makinda wabunge hawakuheshimu wewe au hawamheshimu spika wa bunge?
Tafakari, chukua hatua.
tena hii fujo ingeletwa huku uraiani ccm wanajifanya kuwa na wanachama 5.34 million tungejionea wako wapi???wangechapana makonde kabisa lol
Makinda ana gamba gumu lisilovulika? Tutaona deadline ya siku 90 walotoa waoem
kheeeee heeee heeee....eeeh!Huyo Masauni anakakamaa kweli kuongea kiingereza inaonekana hajawahi kukiongea tangu alipomaliza mitihani ya chuo kikuu
natamani sana Zitto awe mbunge wangu,mimi mbunge wangu sijui hata kama anaijua internet hajui kitu kinachoendelea duniani anajua kusoma tu magazeti nina huo uhakika. Na zitto kuwa hapa online inawezekana aliacha computer yake au simu yake ikiwa online, so sio shida kabisa na wala hakuna tatizo lolote , nyie watu wa ccm mnataka muerevuke nyie tu ili meundelee kutuibia sioThere are currently 190 users browsing this thread. (71 members and 119 guests)
Yaan huku bunge linaendelea Zitto yuko JF, Je kweli tuna wabunge?
- Zitto (10.22.10)