Spika akalia kuti kavu

Amesahau kuwa aliahirisha siku ya msiba wa KANUMBA??????????????????? WACHAWI HAWA CCM

Wewe ndo umesahau,wabunge wenu tena kutoka pande zote ndo walioahirisha kuhudhuria kikao cha Bunge kwasababu ya Kanumba,nakumbuka vizuri kumuona kupitia luninga Mh Sugu,Idd Azzan na wengineo wengi tu wakipita karibu na jeneza la Marehemu Kanumba RIP
 
Namtetea mama Makinda kwa nguvu zote; jana wakati Hamadi Rashid anatoa hoja huyu Mama wa watu alikua anasinzia na aliposhtuka akajua wameomba kuahirisha kwa sababu ya CDM au CUF na kwa akili yake yote alipomuona Mbunge wa Wawi akajua ni wale wale tu ndio maana alikataa hadi Nchimbi alipoingilia kati.
 
Kwani hawa wabunge wa Zanzibar ni wazamiaji ili wawahi kwenda kupiga mbizi na kuokoa watu au wanataka kwenda kuuza sura kwa wapiga kura wao?


Nadhani angekufa mama yako ndio ungeona ni sawa kuomba kuahirisha shughuli za bunge.
 
Cjaona kukalia kwake kuti kavu! Kauli hiyo ya mbunge wa unguja siwezi ichukulia kwa userious,,normally watu/wawakilishi wa visiwani hawamaanishi wanacholilia.
 
Bajeti ya wizara ya mambo ya ndani na wizara ya Ulinzi zisipite mpaka mawaziri wao waeleze ni kwanini walishindwa kuizuia hiyo boat isizame.
wasingeweza ingewazidi nguvu mawiziri wenyewe wawili tu boti ina watu mamia afu walikuwa mbali na eneo la tukio.ebo
 
Spika kung’olewa?

Baadhi ya wabunge wameanza kuwahamasisha wenzao kupiga kura ya kutokuwa na imani na Spika wa Bunge.
Wabunge hao walifikia hatua hiyo kwenye kikao cha dharura walichokifanya jana katika Ukumbi wa Pius Msekwa kwa lengo la kufanya maandalizi ya kwenda Zanzibar kuhudhuria msiba wa wenzao waliozama katika ajali meli ya Skagit.

Mbunge wa Mji Mkongwe, Muhammad Ibrahimu Sanya (CUF), alisema Spika Makinda hana utu ndiyo maana aligoma kuahirisha shughuli za Bunge ili kutoa nafasi ya watu kushiriki kwenye jambo hilo.

“Huyu Spika hatufai, yaani vifo vikitokea kwa watu wa Bara yeye ndiyo ataona kuna uzito…hapa alikufa Amina Chifupa tukaahirisha Bunge, sasa iweje wenzetu wamekufa kule Zanzibar yeye akatae kuahirisha shughuli za Bunge? Jamani tujipange kupiga kura za kutokuwa na imani naye, ameonyesha kushindwa kulihimili Bunge,” alisema.

Mbunge mwingine kutoka Zanzibar alisema hawaoni sababu ya kuendelea na mjadala wa bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa sababu wapiga kura wao ndio waliofariki dunia.

“Tuna raha gani ya kuendelea kujadili hotuba ya bajeti, huyu Spika tumedhihirisha hana uwezo wa kutuongoza, hatufai, waliokufa kule ni binadamu si paka wala wanyama,” alisema.

Chanzo:Tanzania daima

ni ngumu ndani ya bunge lililojaa wabunge wa CCM Ambao kiuhalisia wanapoingia bungeni akili zao huziacha nje ya Bunge.
 
Mmmh sidhani kama huyo mbunge alikosea sana...maana Spika alidai kwamba kama ajali ingekuwa imetokea karibu na Bunge(which justifies kuwa alikua anaongelea Bara) ndio kungekuwa na mantiki ya kuhairisha kikao cha bunge.
Lakini hebu tuwe practical wapendwa, Kikao kimeahirishwa kwa sababu tu ya hiyo ajali (kwamba upo uwezekano ya kuwa baadhi ya wabunge wa zenj na bara wanaweza kuwa na ndugu zao ndani ya hiyo meli) au kwa sababu kuna kitu wabunge wanaweza kufanya kusaidia katika uokozi au shuguli yoyote inayohusina na ajali hiyo. Kwa maoni yangu, huyo mbunge hakukosea na Spika pia hakukosea sana ila anaweza kuwa ameeleweka ndivyo sivyo. Tuwe wavumilivu sana wakati huu tunapoombleza!
 
... Wabunge wa Zanzibar hawana haki ya kulalamika kuhusiana na maamuzi ya Makinda maana kwa mara ya kwanza walipewa nafasi ya kuchagua kati ya Makinda na Mabere Marando, wao kwa ujumla wao (bila kujali ni CUF au CCM) walimchagua Makinda ili kuwakomoa chadema. Kwa kufanya hivyo, walichuma janga, sasa ni wakati wa kula na wa kwao! Nani hakujua kwamba Makinda ni "mweupe"?
 
Lakini hebu tuwe practical wapendwa, Kikao kimeahirishwa kwa sababu tu ya hiyo ajali (kwamba upo uwezekano ya kuwa baadhi ya wabunge wa zenj na bara wanaweza kuwa na ndugu zao ndani ya hiyo meli) au kwa sababu kuna kitu wabunge wanaweza kufanya kusaidia katika uokozi au shuguli yoyote inayohusina na ajali hiyo. Kwa maoni yangu, huyo mbunge hakukosea na Spika pia hakukosea sana ila anaweza kuwa ameeleweka ndivyo sivyo. Tuwe wavumilivu sana wakati huu tunapoombleza!

Ukweli ni kwamba alikosea, na isingekuwa busara za Nchimbi kikao cha bunge kingeendelea mpaka lihamba.
Bunge linaendeshwa kwa sheria na wala sio hisia mkuu, tukio lolote la huzuni linalogusa Taifa moja kwa moja huwa kunakuwa na utaratibu wa kuhairisha kikao cha bunge ili kujumuika na wahanga. Hii haijalishi kuwa wabunge wana uhusiano wa moja kwa moja na wahanga au lah! Kilichotokea ni janga la kitaifa.

Unajua Mama Makinda inabidi abadilike, siku zote anaendesha Bunge katika itikadi zile zile za Mwalimu na mwanafunzi.
Inabidi asanuke na kugundua kuwa pale sio shuleni ni bungeni...na sasa hivi yeye ni Spika na sio mwalimu.
 
Kwa hiyo nyie mnataka spika airishe bunge wakati hakua na taarifa sahihi? Spika alikua anasubiri taarifa ya serikali ndio atoe uamuzi.
 
Ukweli ni kwamba alikosea, na isingekuwa busara za Nchimbi kikao cha bunge kingeendelea mpaka lihamba.
Bunge linaendeshwa kwa sheria na wala sio hisia mkuu, tukio lolote la huzuni linalogusa Taifa moja kwa moja huwa kunakuwa na utaratibu wa kuhairisha kikao cha bunge ili kujumuika na wahanga. Hii haijalishi kuwa wabunge wana uhusiano wa moja kwa moja na wahanga au lah! Kilichotokea ni janga la kitaifa.

Unajua Mama Makinda inabidi abadilike, siku zote anaendesha Bunge katika itikadi zile zile za Mwalimu na mwanafunzi.
Inabidi asanuke na kugundua kuwa pale sio shuleni ni bungeni...na sasa hivi yeye ni Spika na sio mwalimu.
Taarifa rasmi ilikua haijatolewa bungeni we ulitaka aairishe bila kua na uhakika na kile kinachozungumzwa?
 
Jamani msimlaumu huyu Gaucho, yeye ni sawa na msukule, hana maamuzi yoyote mpaka aulize kwa waliomuweka hapo kwenye hicho kiti, bila ya shaka mawasiliano yalikuwa magumu alikuwa anasubiri maelekezo toka kwa Rostam Aziz.
 
mama ni janga la mjengo,hajui nini anachotakiwa kufanya,anatoa maamuzi ya jikoni infront of mass,na hiyo ya kutokuwa na imani hata mtoto wa primary anafahamu,ukiona mtu ameshindwa kusolve ya familia yake ya jiran ni kimeo
 
Hao CUF walikuwa hawajui hilo? wenzao CDM wanalalama kila siku wanawaona wajinga, sasa leo yamewakuta wamejua! tembea uyaone na wameyona sasa
 
Taarifa rasmi ilikua haijatolewa bungeni we ulitaka aairishe bila kua na uhakika na kile kinachozungumzwa?
Kama hakuwa na taarifa hakutakiwa kupinga hoja kwa utashi bali kwa vifungu vya sheria.
Halafu hivi taarifa za msiba ni mpaka upigiwe simu ndio uamini?
 
Back
Top Bottom