Spika akalia kuti kavu

Spika akalia kuti kavu

Kama hakuwa na taarifa hakutakiwa kupinga hoja kwa utashi bali kwa vifungu vya sheria.
Halafu hivi taarifa za msiba ni mpaka upigiwe simu ndio uamini?
kwa hiyo angetumia vifungu kupinga ungekua mpole sasa? au shida yako hapa ni nini? Yeye alisema hana taarifa rasmi kwa hiyo hawezi kuahirisha bunge kienyeji! angefanya hivyo kwa bahati mbaya ingekua taarifa sio ya kweli mngekuja hapa mkamlaumu anatoa maamuzi bila ya kua nataarifa sahihi. Wabongo bwana
 
Wabunge wa CUF na viongozi wao ni wanafiki kwelikweli...hivi leo ndio wanatambua kuwa huyu mama hafai kuwa spika? Mbona CHADEMA tulisema tangu siku ile anachaguliwa na tumeendelea kupigana nae ili kuleta usawa pale bungeni? Nadhani imefika wakati tupiganie haki nyakati zote, sio wakati ambapo maslahi yako yameguswa ndio usema spika hafai. Na sina uhakika kama hawa wabunge wa CUF wakirudi baada ya msiba huu wataonyesha wanachokitamka kwa sasa kama sio wataanza kupambana na CHADEMA ili kuwasiadia wanandoa wenzao CCM.
 
Nia ya Spika haikuwa kukataa ile hoja ya Mh. Hamad Rashid bali alikuwa hajapata taarifa za kutosha kuhusiana na ajali hiyo
 
kwa hiyo angetumia vifungu kupinga ungekua mpole sasa? au shida yako hapa ni nini? Yeye alisema hana taarifa rasmi kwa hiyo hawezi kuahirisha bunge kienyeji! angefanya hivyo kwa bahati mbaya ingekua taarifa sio ya kweli mngekuja hapa mkamlaumu anatoa maamuzi bila ya kua nataarifa sahihi. Wabongo bwana

Uliangalia bunge?
Ninahisi uelewa wangu na wako ni tofauti...am calling this off bro
 
Acheni hizo kwani ajali ingetokea ziwa Tanganyika au Victoria wao wangeahirisha Baraza lao la Wakakilishi? Hii ni Tanganyika ni nchi nyingine mama spika bravo. Muungano hamuutaki mnatung'ang'a nini jamani, Uamusho hoyee.

Tanganyika ipo wapi wewe ? Unatafutwa kufungwa ? Lile ni bunge lilitokana na nchi mbili na baraza la Wawakilishi ni la nchi ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ,wakati mwengine jaribu kuandika kama mtu mwenye akili.
 
Uliangalia bunge?
Ninahisi uelewa wangu na wako ni tofauti...am calling this off bro
Shida ya wabongo ndio hii kukumbia hoja haya baba safari njema endelea kulalamika
 
kwani hawa wabunge wa zanzibar ni wazamiaji ili wawahi kwenda kupiga mbizi na kuokoa watu au wanataka kwenda kuuza sura kwa wapiga kura wao?

unajua maana ya uongozi au hadhi ya bunge kwa watanzania? Ulishawahi kufiwa na ndugu wa karibu, mfano baba, mama, mjomba, shangazi, mpwa, au mwanao? Usamehewe bure ila si lazima udhihirishe uvundo ulokuwa nao kwa wengine hasa ktk matukio ya kuhuzunisha kama haya!
 
Shida ya wabongo ndio hii kukumbia hoja haya baba safari njema endelea kulalamika

Hakuna anayelalamika, hapa tunajadili na ndio maudhui ya jukwa hili..
Ningekua nakimbilia hoja nisingechangia hii mada..
Nina shughuli nyngi za kufanya na sina muda wa kuendeleza mabishano hapa
 
unajua maana ya uongozi au hadhi ya bunge kwa watanzania? Ulishawahi kufiwa na ndugu wa karibu, mfano baba, mama, mjomba, shangazi, mpwa, au mwanao? Usamehewe bure ila si lazima udhihirishe uvundo ulokuwa nao kwa wengine hasa ktk matukio ya kuhuzunisha kama haya!
Spika hakua na taarifa sahihi juu ya tukio, huwezi kuairisha bunge kama unahairisha safai ya kariakoo. Lazima mambo haya yafuate kanuni bana sio kukurupuka tu
 
Hakuna anayelalamika, hapa tunajadili na ndio maudhui ya jukwa hili..
Ningekua nakimbilia hoja nisingechangia hii mada..
Nina shughuli nyngi za kufanya na sina muda wa kuendeleza mabishano hapa
mara useme unachangia mara useme unabishana mbona sikuelewi?
 
Wabunge wa CUF na viongozi wao ni wanafiki kwelikweli...hivi leo ndio wanatambua kuwa huyu mama hafai kuwa spika? Mbona CHADEMA tulisema tangu siku ile anachaguliwa na tumeendelea kupigana nae ili kuleta usawa pale bungeni? Nadhani imefika wakati tupiganie haki nyakati zote, sio wakati ambapo maslahi yako yameguswa ndio usema spika hafai. Na sina uhakika kama hawa wabunge wa CUF wakirudi baada ya msiba huu wataonyesha wanachokitamka kwa sasa kama sio wataanza kupambana na CHADEMA ili kuwasiadia wanandoa wenzao CCM.

HAWA ccm-B hawakujua kuwa CCM ni bwana wao mpaka akubali, wako hatarini kupigwa ban kwenye serikali ya umoja wa wachawi.Waliingia kichwa kichwa hawakujua kuwa wenzao wanaendesha nchi kwa njia za giza.Ni kutoa kafara kwenda mbele na sasa CUF wavumilie watapoteza sana ndugu zao.CCM ndiyo zao hizo wamezoea
 
Stela Manyanya na Mwigullu wako wapi? Hii ajali haina mkono wa CHADEMA kweli!
 
Kwamba msiba wa Chifupa bunge liliahirishwa halina uzito kwa sababu bunge hilohilo liliahirishwa alipofariki mbunge wa Zanzibar(Uzini) wakati akienda msibani Zanzibar.

Suala hapa sio Zanzibar au Tanganyika,ni ukosefu wa busara ya kawaida ya spika Makinda.
Yupo rigid sana na kanuni kiasi kwamba hachanganyi na busara kidogo.Hakuna kifungu cha kulifanya bunge liahirishe shughuli zake kwaajili ya dharula iliyotokea anachoweza kukitumia mbunge zaidi ya alichokitumia Hamad jana.Nafikiri kwa hali yoyote mbunge yeyote angegonga mwamba kwani spika alihitaji kanuni "Kama kuna meli itazama bahari ya hindi na shughuli za bunge zikiendelea basi mbunge yeyote anaweza kusimama wakati hakuna mbunge mwingine anaongea kumuomba spika ahairishe bunge ili wabunge wakashiriki na wanaowawakilisha kwenye dharula".Kwakuwa hakuna kanuni kama hiyo kwa Spika wetu tusingetarajia kitu kama waziri asingeomba kuitoa hoja yake mezani,kanuni ambayo Makinda alikuwa labda akiisubiri!
Kitu kidogo tu cha kusoma alama za nyakati kinamfanya spika makinda aonekane ni mtu katili ambaye hawezi kutumia busara zaidi ya kanuni za bunge.


Simtofautishi na mzazi aliyewapa watoto wake kanuni ya kugonga mlango wa chumbani kwake kabla hawajaingia.Siku ikitokea dharula labda nyumba inaungua moto yeye akiwa ndani hajui na watoto wakakimbia hadi chumbani kwake bila kufuata kanuni ya kugonga mlango kwaajili ya kujiokoa haraka.Mzazi badala ya kuanza kushuhulika na dharula ya moto yeye anaanza kuwaadhibu watoto kwa kwa kutozingatia kanuni ya kugonga mlango!
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Binafsi, sioni sababu hata kidogo ya kutumia kodi ya watanzania kugharamia vikao vya bunge kwa sasa. Nitaeleza:

Wabunge ni wawakilishi wa wananchi, wanaongea yale waliyotumwa na wananchi, lakini chini ya Makinda wabunge wamezibwa midomo na hivyo hoja za wananchi hazijadili. Kwa kutoruhusu wawakilishi wa wananchi kuwasilisha yale waliyotumwa maana yake bunge sasa linageuzwa kuwa rubber- stamp.

Uhuru wa mhimili huu mkubwa, mhimili wenye mamlaka ya kuisamamia serikali sasa haupo tena. Makinda kwa sababu anazozijua yeye mwenyewe amegeuza huu mhimili kuwa idara ya serikali.

Serikali inaleta hoja mezani ili ijadiliwe, lakini Spika anaonekana kuruhusu mijadala ile inayompendeza yeye (spika) kwa kisingizio cha kanuni! Spika amesahau kabisa kwamba anapomziba mbunge mdomo maana yake amewaziba mdogo pia wananchi waliomtuma mbunge huyo. Kanuni sio msahafu, na haiwezekani tafrisi ya mtu mmoja - spika ndiyo iwe tu sahihi.

Tukumbuke huyu Spika hajasoma sheria, naibu wake hajasoma sheria, katibu wa bunge naye hajasoma sheria. Hivyo team yote ya juu ya bunge ni kama wapita njia in terms of sheria. Na matokeo yake ndiyo haya tunayoona sasa. Hata madai kwamba wabunge hawawezi kujadili hoja ambayo iko mahakami ni tafsiri pototu. Tanzania wanafuata British law, na chini ya sheria zetu unaweza kabisa kujadili hoja ambayo kesi iko mahakamani bila kuathiri mwenendo wa kesi.

Ukitizama mwenendo mzima wa bunge tangu mwezi June hadi sasa, hakuna jambo lolote la maana lililopitishwa zaidi ya ku-rubber stamp hoja za serikali.

Sasa kama Spika yuko pale kuimarisha huo mfumo wa rubber-stamp kwanini watumie kodi ya wananchi kulipa posho wabunge 300+ kwa kazi ambayo inaweza kufanyika kwa siku 3 au 4? Kwanini wasipitishe vifungu vyote kwa wizara zote kwa pamoja ili waokoe fedha za watanzania? Nasema tena, hakuna haja ya kuweza wabunge Dodoma kwa miezi kadhaa, wapitishe vifungu kwa pamoja bila ya mipasho na ngonjera na haraka warudi uraini.
 
Huyo bibi makinda amewekwa na ccm kulinda ccm, anatekeleza majukumu kama alivyotumwa na ccm, leo mnalalamika Hoja ngapi za Upinzani anazipinga na kuzuia mbona mlikua kimya? wabunge wametaka wajadili mgomo wa madocta amekataa, wajadili kipigo cha ulimboka amekataa, ccm inatekeleza sera zake za kinyama
 
Ndio waliompigia kura kwa kishondo hawa. Kweli mzee small ni mjukuu.
 
Back
Top Bottom