Special thread: Vikaragosi vya Masoud Kipanya

Special thread: Vikaragosi vya Masoud Kipanya

Tusaidiane kuelewA wengine hatujaelewa anamaanisha mini?View attachment 829459

tyre dogo linawakilisha CHAMA kimoja... sikitaji

tyre kubwa linawakilisha CHAMA kimoja pia.. sikitaji

hilo gari lina plate number ya TZ.. means ni NCHI YA TZ.

tyre za nyuma zipo sawa kabisa.. means Watanzania.. tunaburuzwa na hizo Tyre za mbele mbili

sas TAFSIRI ya moja kwa moja.. ipo siku hicho ki tyre kidogo kitaishiwa nguvu na kuvunjika... jambo ambalo litapelekea SAFARI ya Hilo gari kufikia TAMATI.
 
nimeelewa yafuatayo:

Gari maana yake ni serikali ya TZ.

Gari ina usukani lakini haina dereva maana yake Tanzania haina raisi mathubuti kwa sasa.

neo TANZANIA limeandikwa mbele ya gari maana yake maslahi ya taifa ndilo neno linalonadiwa sana na wanasiasa wa sasa lakini kiuhalisia hakuna anayejeli maslahi ya Tz, wanajali matumbo yao.

Tairi la kushoto ni kubwa kuliko matairi yote maana yake nguvu za utawala wa nchi zimeelemea upande mmoja pasipo kujali mambo mengine, kwa mfano; kuhangaisha wapinzani na wanaoikosoa serikali kwa kuwakamata kamata na kuwafungulia kesi za ajabu ajabu.

Tairi kubwa kuwa mbele upande wa kushoto maana yake jambo inalolishikilia sana serikali la kutesa wanaoikosoa lipo upande usio na nguvu yaani upande wa kushoto, yaani wananchi wengi hawalikubali.

mkao wa picha unaonyesha wananchi wamesimama upande wa huku ilipo tayiri kubwa na ndipo mchukua picha alisimama pia.

tayiri kubwa kuwa mbele maana yake nyingine ni kuwa gari inaenda kwa kasi maana tayiri hiyo inasapoti hivyo ila huenda ikaenda kasi kwa jambo fulani halafu ikapeleka gari shimoni au huenda ikapelekea gari kurudi nyuma ghafla na kuanguka maana uzito emeelemea nyuma hasa upande wa kuume.

setimila ya kushoto inaangalia chini maana yake dereva hataweza kuona kinachokuja nyuma yake badala yake ataendesha gari bila kujali wa nyuma yake, kwa mfano, wastaafu mnawashwa washwa.

tairi la kulia ni la piki piki maana yake upande wa dereva hauko salama kabisa gari yaweza pinduka wakati wowote maana uzito umeelemea huko.

rangi ya njano kwenye plate maana yake utajiri wa tanzania ndo kitu kinachopewa kipaumbele kuliko hata wananchi wenyewe, utasikia wakisema faru john lazima apelekwe hospitalini ulaya kutibiwa, utasikia mbwa atafutwe haraka sana, utasikia .. .................................

barabara ina udongo mwekundu maana yake gari inakanyaga hatari ktk safari yake, kwa mfano kunyima haki za msingi kama za kujieleza ambapo watu wengi wanaanza kuwa na kinyongo na vyombo vya dola ambavyo ni sehemu ya serikali tena vinawazuia kusema ya moyoni.

gari ipo kwenye mteremko maana yake inaseleleka kwa kasi huku haina dereva na lazima tu itapinduka huko mbeleni,

barabara ni fupi maana yake mda si mrefu gari hiyo haitafika mbali lazima itavurugikiwa tu.
 
Tanzania inaendeshwa na Viongozi wenye mawazo tofauti, huyu anakurupuka na hili, yule anaenda na style hii,yaani ni mambo changanyikeni tu
 
Kipanya bwaaana.Kuna tairi tatu hapo,ya Trekta,Boda boda na lile la mwisho.Mpaka hapo inatosha.Nikuulize nani ameelewa hii nchi toka miaka flani hivi nyuma.Mara mbwa...mara nitapiga shangazi zako....diriiimu liner ....bomba.....Sgr......Hatukopi mara tukopeshwe tumalizie Sgr.....pesa zetu wenyewe..deni linakua uchumi unakua ..tunatumia hela zetu wenyewe kujenga miradi yoote.Rambi rambi Kagera...Mara mtu kavaa suti na raba..ajali hakuna tena Waziri ndani ya Serikali yetu ajali paaa...Jamaa kala shaba yupo ubelgji mpaka leo.Fatma kule anatafutwa..Serikali ya CCm na sera na taratibu zote na si ya wananchi.
Hilo gari likitembea .....................😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀
 
hahaaa hadi Tyre la baiskeli sijui boda+ ...duuhh
 
Mimi nimeielewa hivi..hizo tairi hazifanani ,hii ni hali ya sasa ya hamahama ya wanasiasa kuelekea upande mwingine na hii inaudhohofisha upinzani..upinzani ukidhohofika nchi haiwezi kuendelea kwani kunakuwa hakuna wakosoaji wazuri wa serikali..so nchi haiwezi kwenda mbele,,na ni kama unavyoona hapo kwenye picha ya gari,,gari hilo haliwezi kuenda mbele zaidi ya kudondoka bondeni,sababu tairi hazijabalance au kukaribiana size
 
Akili ndogo kuongoza akili kubwaa
Kipanya mwenyewe yupo doomed,halafu ndio tumsikilize maoni yake,jiulize aliondoka Clouds kwa makeke akarudi ameufyata,mwenyewe tuanashindwa kuhangaika na yake
 
Hizo gurudumu ambazo ndio zinaiwezesha gari kutembea hazipo sawa au haziendani

Hvyo ni vigumu kwa gari kwenda mbele na hata likifanikiwa mwendo wake si salama kabsa huenda baadhi ya gurudumu zikaharibika ikawa ndo mwisho wa safari
Kweli hiyo gari haiwezi kwenda popote, alaf unaambiwa we are on the right truck!!!!
 
Mmiliki wa gari ni mbovu kichwani kuliko gari lenyewe linavyoonekana.
 
Tanzania tunasonga mbele ingawa kuna watu wanatukwaza!
 
Inabidi Bw Masoud arahisishe mchoro wake, akipitia mawazo ya kila mtu, atagundua ni jinsi gani alivyotuchanganya.
 
Mi napata shida,mbona pamoja na tairi moja kuwa kuuuuubwa lkn gar mbona halijaegemea upande mmoja?
 
Dreamliner wakati hata usafiri wa mabasi ni gharama kwa raia.

Flyover mjini huku serikali inahamia Dom badala ya kujenga mji mpya ambako hakujajengeka.

Kila leo Dar inabomolewa, msishangae miaka 10 ijayo makao makuu ya serikali yakarudi Dar.
 
Back
Top Bottom