South Africa nitafikaje?

South Africa nitafikaje?

shibekijijini

JF-Expert Member
Joined
May 26, 2015
Posts
358
Reaction score
478
Ndugu zanguni,

Kwanza kabisa nawasalimieni wote.

Naomba mnisaidie mimi nina kiasi cha Shilingi Lack 5 cash, nahitaji msaada wa kufika tu South Africa. Swali langu kubwa linalonitesa ni kwamba, nikitoka Dar kwa njia ya Bus nikifika South Africa mwisho wa Bus huo mji unaitwaje? Na je nitapata Guest ya kulala ya bei ndogo? Na ni sh ngapi? Na ili nipate hiyo Guest itabidi niusafiri au nielekee wapi?

Nb; Nikifika huko sitegemei kurudi Tz, ujuzi nilionao ni IT lakini pia nilishawahi kuwa fundi viatu. Je huko naweza kupata ajira? Lakini pia niko vizuri kwa kulima hasa kwa kutumia jembe la mkono.

Asante.
 
Kwanini usianzishe kiwanda cha viatu hapahapa kusaidia "Tanzania ya viwanda"?
Asante kwa ushauri mzuri sana, Lakini kumbuka kwa mtaji huo ni ngum sana, Hasa ukizingatia mazingira ninayo ishi. Nadhani ingekuwa vzr km ungenishauri kulingana na Topic. Kuninyima kote na kukusanya hicho kiasi lengo kuu ni kwenda S. A.
 
Fastjet laki 3 tu, hiyo lakimbili iliyobaki unaanzia maisha, naskia south Wanaruhusu raia kutoka TZ akae miezi mitatu bila visa.. So hapo ukishaingia kule utajua ufanye nini ili uwakwepe polisi au upate work permit ya professional yako..
 
Je unajua unataka kwenda mji gani? Kama utapanda basi, ama ndege, kituo chako cha mwisho ni Johannesburg. Kutoka hapo ndio uamue kama unaenda cape town, Pretoria au Durban etcetera.
 
Fastjet laki 3 tu, hiyo lakimbili iliyobaki unaanzia maisha, naskia south Wanaruhusu raia kutoka TZ akae miezi mitatu bila visa.. So hapo ukishaingia kule utajua ufanye nini ili uwakwepe polisi au upate work permit ya professional yako..
Kwa njia ya Bus haifai?
 
Je unajua unataka kwenda mji gani? Kama utapanda basi, ama ndege, kituo chako cha mwisho ni Johannesburg. Kutoka hapo ndio uamue kama unaenda cape town, Pretoria au Durban etcetera.
Asante ndugu. Sasa Jo, Begi. Kuna guest house za bei ya chini? Maana siunajua sehem mpya.
 
Wewe unahangaika ili upate shibe, mbona shibe ipo kijijini?.

Alafuunasema wewe ni mzuri kwenye jembe la mkono kwani kijijini kwenu hakuna mashamba???
Tuanzie kwanza hapo kabla sija Kukaribisha RUN BAG. SA.
 
Kwa njia ya Bus haifai?
Kwanjia ya Bus inafaa, sema utasumbuana na askari wa mipakani, utazunguka sana, utatoa rushwa sana, ila kama una makaratasi, haina shida... Na kama una pasport bora utumie ndege tu.. Kuna watu wanakufa sana kwa njia ya bus
 
Wewe unahangaika ili upate shibe, mbona shibe ipo kijijini?.

Alafuunasema wewe ni mzuri kwenye jembe la mkono kwani kijijini kwenu hakuna mashamba???
Tuanzie kwanza hapo kabla sija Kukaribisha RUN BAG. SA.
Kiongozi mashamba yapo, Lakini tatizo ni nyezo, Lakini pia wakati mwingine kutembea ni sehem ya kuongeza maarifa, sio lazima kubaki mahari /sehem moja. Asante
 
Kwanjia ya Bus inafaa, sema utasumbuana na askari wa mipakani, utazunguka sana, utatoa rushwa sana, ila kama una makaratasi, haina shida... Na kama una pasport bora utumie ndege tu.. Kuna watu wanakufa sana kwa njia ya bus
Ktk hatua za awali Nimejaribu kufatilia passport nimeambiwa ni elfu 500 kwani unapo zungumzia karatasi unamanisha zile ambazo niza muda mfupi km miezi 3? Kuna miaka ya nyuma nilikwenda Uganda nilicho pewa Kwenye ofisi za migration nilipewa karatasi moja tu ambayo ukifika mpakani unagongewa mhuri, bila Shaka umemanisha hyo. Mi ntajitahidi niwe na karatasi au pass ili mradi wakose visingizio vya rushwa, sitaki njia za panya
 
Kwanjia ya Bus inafaa, sema utasumbuana na askari wa mipakani, utazunguka sana, utatoa rushwa sana, ila kama una makaratasi, haina shida... Na kama una pasport bora utumie ndege tu.. Kuna watu wanakufa sana kwa njia ya bus
Umesema kuna watu wanakufa, wanakufa kwa sababu zipi? Safari ndefu au?
 
mkuu usije uku sauzi baki home afadhali uje mwezi wa 6
 
Back
Top Bottom