Songwe: Wanawake watishia kufanya mgomo wa kubeba mimba hadi ujenzi wa Zahanati ukamilike Wilayani Mbozi

Songwe: Wanawake watishia kufanya mgomo wa kubeba mimba hadi ujenzi wa Zahanati ukamilike Wilayani Mbozi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
Wanawake katika Kijiji cha Kilimampimbi, Kata ya Kilimampimbi Wilayani Mbozi Mkoani Songwe wametishia kufanya mgomo wa kubeba mimba mpaka ujenzi wa Zahanati ya Kijiji ukamilike ili kuepuka changamoto wanazopitia wakati wa kujifungua.

Wakizungumza na EATV baadhi ya Wanawake kijijini hapa wamesema tayari wameshaanza kutumia njia za uzazi wa Mpango kwa lengo la kutopata ujauzito kutokana na changamoto wanazopata kwenye matibabu hasa huduma ya kujifungua pamoja na kwenda Kliniki za kila mwezi huduma ambayo wanaipata katika vijiji jirani ambavyo viko mbali na makazi yao hivyo huongeza gharama wawapo nje na makazi yao.

Licha kukamilika kwa ujenzi wa boma la Zahanati ya kijiji na Serikali kutoa fedha kiasi cha Shilingi Milioni 50 tangu Mwaka 2024 bado Zahanati hiyo haijakamilika.

Kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wanawake wakidai kunyanyaswa wanapofuata huduma katika vijiji vya jirani.
 
Miaka 60+ ya uhuru kuna maeneo bado hayana zahanati 😳
 
Kuzaa ama kutozaa ni hiari ya mtu, kama wazazi wetu hawakuwa na zahanati karibu 100km lakini walizaa why leo ukute hata 20km tayari unapata zahanati eti ugome kuzaa? Huo ni ujinga na haupaswi kuwa mfano wa kuigwa.
 
mgomo wa ajabu sana --- nchi ngumu sana hii
 
Wanawake katika Kijiji cha Kilimampimbi, Kata ya Kilimampimbi Wilayani Mbozi Mkoani Songwe wametishia kufanya mgomo wa kubeba mimba mpaka ujenzi wa Zahanati ya Kijiji ukamilike ili kuepuka changamoto wanazopitia wakati wa kujifungua.

Wakizungumza na EATV baadhi ya Wanawake kijijini hapa wamesema tayari wameshaanza kutumia njia za uzazi wa Mpango kwa lengo la kutopata ujauzito kutokana na changamoto wanazopata kwenye matibabu hasa huduma ya kujifungua pamoja na kwenda Kliniki za kila mwezi huduma ambayo wanaipata katika vijiji jirani ambavyo viko mbali na makazi yao hivyo huongeza gharama wawapo nje na makazi yao.

Licha kukamilika kwa ujenzi wa boma la Zahanati ya kijiji na Serikali kutoa fedha kiasi cha Shilingi Milioni 50 tangu Mwaka 2024 bado Zahanati hiyo haijakamilika.

Kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wanawake wakidai kunyanyaswa wanapofuata huduma katika vijiji vya jirani.
Sasa wasiposhika ujauzito wanamkomoa nani?
 
Back
Top Bottom