Soma kisa hiki cha utapeli, ujifunze kitu

Huu utapeli uko siku nyingi na una versions nyingi. Kuna mwingine kama huu huu lakini watu walichuliwa kuchimba kaburi.

Matapeli walivyokuwa washenzi, wakachukuwa na mama Ntilie na chakula chake kwenda kuwalisha, wakakodi na gari yaani walipoondoka waliacha kundi lwa watu limetapeliwa kila mmoja na bidhaa yake.

Nikipata muda nitaelezea ilivyokuwa japo sikumbuki vizuri sehemu nyingine.
Sisi kwetu walikusanywa wapishi (Kikundi cha Akinamama); nyama yote ya buchani; bidhaa mbalimbali za sokoni; canter mbili hadi wachinjaji wa mbuzi. Mwishoni, wote wakaachwa kwenye mataa zikiibwa simu tu za akinamama wote.
 
Aisee Kuna kisa kimoja Cha utapeli nikikumbuka huwa nacheka sana, japo sio changu kilimtokea mshkaji wangu mmoja.

Jamaa anadai walikuwa na kijiwe Chao wanakutana washkaji wengi tu, kulikuwa na pool table na vile vimashine vya kubet, anadai kijiwe kilikuwa na vijana wengi matozi tu na smart phone zilizoshiba.

Kuna siku walikuja wazee wawili wamevaa mashati ya tigo... Wakamvuta jamaa mmoja pembeni wakamuambia kuna mchongo wa pesa wanahitaji kama vijana 14 wanatakiwa kuchimba mashimo kwa ajili ya minara mipya. Jamaa kusikia vile akachomoa akamwambia kwa kijiwe hiki sidhani kama Kuna mtu atakubali kazi za kuchimba mashimo

Wale wazee wakamwambia kijana tunakupa fursa ujue, hizi ni kazi za kampuni... Wanalipa 100,000 per day ila tunatafuta watu tuwalipe 60 per day sisi Tule 40 Cha juu, baada ya kusikia vile jamaa kama kashawishika akaenda kwa wenzake akawapa mchongo. Wakashauriana weee baadae wakawarudia wale wazee kwa sharti la kulipwa 80k kwa siku na chakula mchana wapewe.

Jamaa akawa ananiambia kijiweni kwao sio kwamba watu Wana njaa sana ila waliona ni uzembe kukataa kazi jioni unarudi na 80k yako safi kabisa... Basi wale wazee wakawakubalia ila kwa sharti kuwa vifaa vya kufanyia kazi watatafuta vijana wenyewe.

Watu wakatafuta vifaa wakakutana meeting point asubuhi, wazee wakaja wakawa wanalalamika kuwa gari ya ofisi imepata shida kidogo ila mpaka jioni Itakua sawa, hivyo wakakodi virikuu viwili vijana wakapanda wakawapeleka maporini huko

Sasa sijui wale wazee walifanya scout ya eneo maana anakuambia hakuna watu Kule yaani ni pori kweli... Basi Kila mtu akapewa eneo lake la kuchimba shimo, halafu wakatenganishwa yaani huwezi kumuona mwenzako... Kazi ikaanza bana, jamaa anakuambia wamekomaa kuchimba mashimo kuanzia saa 4 mpaka saa 8 yaani ni kazi kazi, saa 8 Kuna Mzee mmoja akapita kuanzia kwa mtu wa kwanza anachukua order ya chakula kuulizia wanakula nini. Sasa Mzee ukishampa order yako anakuomba umuazime simu apige yake imeisha chaji.. sasa kumbe huu mtindo alikuwa anafanya kuanzia kijana wa kwanza mpaka wa mwisho..na kumbuka hapo mpo mbalimbali hamuonani

Jamaa wamepiga kazi mpaka kufika saa 10 Wanaona mbona msosi haufiki, ikabidi mmoja atoke kumuuliza mwenzake, sasa katika kuambiana wakaja kugundua kuwa wote simu zao wamempa Mzee, ndo kuanza kuwazungukia wenzao kuwauliza... Aisee Mzee alipita na simu zote 14...

Ndiyo kugundua kuwa washapigwa, angalia huku na Kule wazee hawapo...jamaa ikabidi wachukue vifaa vya watu waanze kurudi kwa mguu, yaani jamaa anasema hapo wamechafuka vibaya sana na bado umebeba vifaa vyako barabarani mpaka kuja kupata usafiri ni kama kilomita 7....

Jamaa njiani wakawa wanatukana ila anasema inafika mahali wanakaa chini wanaanza kuchekana.... Jamaa alinihakikishia waliapa wakikutana na wale wazee watawaua, sio kwa kuwaibia simu.... Bali kwa mashimo Yale waliowachimbisha
Kila mtu hujaribiwa kwa tamaa yake mwenyewe :D
 
Mmh, yaani kila mmoja alipokuwa akimpa simu huyo mzee alikuwa akiendelea na shughuli ya kuchimba mashimo bila kuangalia mzee anaelekea wapi na simu yake? Kuna wingi wa chumvi kwenye mboga.
Mzee umewahi kumuamini mtu...Kwasababu kama yye ndo kasaleta kuchimba na yeye mwenyewe kawapa deal la 80k per day huwez kumtilia shaka hata kidgo
 
Jamani yaan mashimo ya minara yachimbwe umbali gani huo kwamba kila mtu anachimba mashimo ya mnara mmoja halafu mpo watu 14 ina maana hiyo minara ipo 14 imekuwa nguzo za umeme au.
Haya maswali unajiuliza sasa baada ya kujua ni matapeli. Lakini kwa mtu aliye kijiweni na ameambiwa kuna mshiko wa kufa mtu hakumbuki. BTW kwani waliambiwa kazi inaisha siku hiyo hiyo baada ya kuchimba mashimo 14? Si mnaambiwa hapa ndiyo pa kuanzia na mtaendelea hata mwezi mmoja kila siku. Kuhusu umbali, sidhani kama ukiwa mrefu kuna mtu atashtuka.
 
Mmh, yaani kila mmoja alipokuwa akimpa simu huyo mzee alikuwa akiendelea na shughuli ya kuchimba mashimo bila kuangalia mzee anaelekea wapi na simu yake? Kuna wingi wa chumvi kwenye mboga.
Ungesikia wahanga waliotapeliwa walivyokuwa wanaelezea kwenye radio siku moja usingesema kuna chumvi hapa. Hao matapeli ni wataalam kweli kweli na wanajua ku act. Wanaenda kuchukuwa mpaka mama ntilie (wanamtapeli) anakuja kuwapikia. Magari wanakodisha, yaani ukienda kwenye eneo la tukio unakuta watu wengi kila mmoja anashughulika. Unapoambiwa nipe simu huwezi kuwa na wasiwasi hata kidogo.
 
Ungesikia wahanga waliotapeliwa walivyokuwa wanaelezea kwenye radio siku moja usingesema kuna chumvi hapa. Hao matapeli ni wataalam kweli kweli na wanajua ku act. Wanaenda kuchukuwa mpaka mama ntilie (wanamtapeli) anakuja kuwapikia. Magari wanakodisha, yaani ukienda kwenye eneo la tukio unakuta watu wengi kila mmoja anashughulika. Unapoambiwa nipe simu huwezi kuwa na wasiwasi hata kidogo.
Watu bana wanapenda kubisha tu, hii ishu ukishapigwa ndo unaanza kuziona red flags
 
Aisee Kuna kisa kimoja Cha utapeli nikikumbuka huwa nacheka sana, japo sio changu kilimtokea mshkaji wangu mmoja.

Jamaa anadai walikuwa na kijiwe Chao wanakutana washkaji wengi tu, kulikuwa na pool table na vile vimashine vya kubet, anadai kijiwe kilikuwa na vijana wengi matozi tu na smart phone zilizoshiba.

Kuna siku walikuja wazee wawili wamevaa mashati ya tigo... Wakamvuta jamaa mmoja pembeni wakamuambia kuna mchongo wa pesa wanahitaji kama vijana 14 wanatakiwa kuchimba mashimo kwa ajili ya minara mipya. Jamaa kusikia vile akachomoa akamwambia kwa kijiwe hiki sidhani kama Kuna mtu atakubali kazi za kuchimba mashimo

Wale wazee wakamwambia kijana tunakupa fursa ujue, hizi ni kazi za kampuni... Wanalipa 100,000 per day ila tunatafuta watu tuwalipe 60 per day sisi Tule 40 Cha juu, baada ya kusikia vile jamaa kama kashawishika akaenda kwa wenzake akawapa mchongo. Wakashauriana weee baadae wakawarudia wale wazee kwa sharti la kulipwa 80k kwa siku na chakula mchana wapewe.

Jamaa akawa ananiambia kijiweni kwao sio kwamba watu Wana njaa sana ila waliona ni uzembe kukataa kazi jioni unarudi na 80k yako safi kabisa... Basi wale wazee wakawakubalia ila kwa sharti kuwa vifaa vya kufanyia kazi watatafuta vijana wenyewe.

Watu wakatafuta vifaa wakakutana meeting point asubuhi, wazee wakaja wakawa wanalalamika kuwa gari ya ofisi imepata shida kidogo ila mpaka jioni Itakua sawa, hivyo wakakodi virikuu viwili vijana wakapanda wakawapeleka maporini huko

Sasa sijui wale wazee walifanya scout ya eneo maana anakuambia hakuna watu Kule yaani ni pori kweli... Basi Kila mtu akapewa eneo lake la kuchimba shimo, halafu wakatenganishwa yaani huwezi kumuona mwenzako... Kazi ikaanza bana, jamaa anakuambia wamekomaa kuchimba mashimo kuanzia saa 4 mpaka saa 8 yaani ni kazi kazi, saa 8 Kuna Mzee mmoja akapita kuanzia kwa mtu wa kwanza anachukua order ya chakula kuulizia wanakula nini. Sasa Mzee ukishampa order yako anakuomba umuazime simu apige yake imeisha chaji.. sasa kumbe huu mtindo alikuwa anafanya kuanzia kijana wa kwanza mpaka wa mwisho..na kumbuka hapo mpo mbalimbali hamuonani

Jamaa wamepiga kazi mpaka kufika saa 10 Wanaona mbona msosi haufiki, ikabidi mmoja atoke kumuuliza mwenzake, sasa katika kuambiana wakaja kugundua kuwa wote simu zao wamempa Mzee, ndo kuanza kuwazungukia wenzao kuwauliza... Aisee Mzee alipita na simu zote 14...

Ndiyo kugundua kuwa washapigwa, angalia huku na Kule wazee hawapo...jamaa ikabidi wachukue vifaa vya watu waanze kurudi kwa mguu, yaani jamaa anasema hapo wamechafuka vibaya sana na bado umebeba vifaa vyako barabarani mpaka kuja kupata usafiri ni kama kilomita 7....

Jamaa njiani wakawa wanatukana ila anasema inafika mahali wanakaa chini wanaanza kuchekana.... Jamaa alinihakikishia waliapa wakikutana na wale wazee watawaua, sio kwa kuwaibia simu.... Bali kwa mashimo Yale waliowachimbisha
hiii dunia hiii hapana

Sent from my Infinix X606D using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom