Kijana mwauame hanyoi nywele za nyuma kwa wembe utahanithika

Anonymous77

JF-Expert Member
May 29, 2022
299
845
Wanaume wenzangu karibu hapa tujadili ya yakale ya wazee wetu vijana wengi siku hizi hawana adabu wala hawataki kushika maneno ya wazee wao vijana wanyoa "QADHA" vijana wasiosikia la mzazi, vijana wabishi hakuna wasolijua, vijana waso na aibu wafiraji.

Vijana waso na ubunifu wacheza kamari, vijana waso na nguvu za kiume, vijana waso na heshima kwa wazee, vijana wavaao nguo za kubana zinazochora mwili mpaka makalio, vijana wavivu wanopenda kushinda vijiweni asubuhi mpaka jioni angali wazee wetu kijiwe lilikuwa ni jioni baada ya kutoka shamba, vijana wanaopanda panda juu ya meza kucheza miso misondo, vijana wavaa heleni waso sikia la muidhini.

Haya ndio matokeo ya kutokuheshimu wazee vijana wanageuka kuwa mashoga vijana wa kupiga kimoja chali vijana wanakufa na stress za maisha wakiwa na miaka 20 tu wakati wazee wetu walikuwa wanapeleka moto unaambiwa kwa fundi selemara kila siku kulikuwa hakuishi kuletwa kwa Chaga mbovu kila kukicha, wazee wetu walimiliki Wanawake 4 na watoto 38 pamoja na yote hawakufa na stress za maisha mpaka miaka 98 wanadunda na Bado wakiitwa kwenye 6x6 wanasukuma moto wanarudisha heshima ya neno mwanaume.

Kijana wewe una miaka 20 unapeleka demu kimoja unakata pumzi kijana ambae leo ukipata mtoto moja tu unamkimbia mke wako kisa kushinda kutoa huduma Kwa mtoto, wakati Mzee wako alikuwa anahudumia watoto 38 katika hao 38. Mmoja wapo ni wewe ambao leo mitaa imekubariki jina la "kijana wa hovyo" ewe kijana ni nani alikwambia uyakimbie ya wazee wako ona sasa yanayokufika leo ni huzuni.

KIJANA MWANAUME HANYOI NYWELE ZA NYUMA KWA WEMBE UTAHANITHIKA.
Hii ni kauli ya wazee wako wa kale kijana vuzi la nyuma halinyolewi na wembe utahanithika. Wazee ambao leo hutaki kusikia kuhusu wao ndio maana unateseka kama kenge alovamia kazi ya mamba.
 
Back
Top Bottom