Soma kisa hiki cha utapeli, ujifunze kitu

Mr mutuu

JF-Expert Member
Jan 27, 2023
2,027
10,035
Aisee Kuna kisa kimoja Cha utapeli nikikumbuka huwa nacheka sana, japo sio changu kilimtokea mshkaji wangu mmoja.

Jamaa anadai walikuwa na kijiwe Chao wanakutana washkaji wengi tu, kulikuwa na pool table na vile vimashine vya kubet, anadai kijiwe kilikuwa na vijana wengi matozi tu na smart phone zilizoshiba.

Kuna siku walikuja wazee wawili wamevaa mashati ya tigo... Wakamvuta jamaa mmoja pembeni wakamuambia kuna mchongo wa pesa wanahitaji kama vijana 14 wanatakiwa kuchimba mashimo kwa ajili ya minara mipya. Jamaa kusikia vile akachomoa akamwambia kwa kijiwe hiki sidhani kama Kuna mtu atakubali kazi za kuchimba mashimo

Wale wazee wakamwambia kijana tunakupa fursa ujue, hizi ni kazi za kampuni... Wanalipa 100,000 per day ila tunatafuta watu tuwalipe 60 per day sisi Tule 40 Cha juu, baada ya kusikia vile jamaa kama kashawishika akaenda kwa wenzake akawapa mchongo. Wakashauriana weee baadae wakawarudia wale wazee kwa sharti la kulipwa 80k kwa siku na chakula mchana wapewe.

Jamaa akawa ananiambia kijiweni kwao sio kwamba watu Wana njaa sana ila waliona ni uzembe kukataa kazi jioni unarudi na 80k yako safi kabisa... Basi wale wazee wakawakubalia ila kwa sharti kuwa vifaa vya kufanyia kazi watatafuta vijana wenyewe.

Watu wakatafuta vifaa wakakutana meeting point asubuhi, wazee wakaja wakawa wanalalamika kuwa gari ya ofisi imepata shida kidogo ila mpaka jioni Itakua sawa, hivyo wakakodi virikuu viwili vijana wakapanda wakawapeleka maporini huko

Sasa sijui wale wazee walifanya scout ya eneo maana anakuambia hakuna watu Kule yaani ni pori kweli... Basi Kila mtu akapewa eneo lake la kuchimba shimo, halafu wakatenganishwa yaani huwezi kumuona mwenzako... Kazi ikaanza bana, jamaa anakuambia wamekomaa kuchimba mashimo kuanzia saa 4 mpaka saa 8 yaani ni kazi kazi, saa 8 Kuna Mzee mmoja akapita kuanzia kwa mtu wa kwanza anachukua order ya chakula kuulizia wanakula nini. Sasa Mzee ukishampa order yako anakuomba umuazime simu apige yake imeisha chaji.. sasa kumbe huu mtindo alikuwa anafanya kuanzia kijana wa kwanza mpaka wa mwisho..na kumbuka hapo mpo mbalimbali hamuonani

Jamaa wamepiga kazi mpaka kufika saa 10 Wanaona mbona msosi haufiki, ikabidi mmoja atoke kumuuliza mwenzake, sasa katika kuambiana wakaja kugundua kuwa wote simu zao wamempa Mzee, ndo kuanza kuwazungukia wenzao kuwauliza... Aisee Mzee alipita na simu zote 14...

Ndiyo kugundua kuwa washapigwa, angalia huku na Kule wazee hawapo...jamaa ikabidi wachukue vifaa vya watu waanze kurudi kwa mguu, yaani jamaa anasema hapo wamechafuka vibaya sana na bado umebeba vifaa vyako barabarani mpaka kuja kupata usafiri ni kama kilomita 7....

Jamaa njiani wakawa wanatukana ila anasema inafika mahali wanakaa chini wanaanza kuchekana.... Jamaa alinihakikishia waliapa wakikutana na wale wazee watawaua, sio kwa kuwaibia simu.... Bali kwa mashimo Yale waliowachimbisha
 
Aisee Kuna kisa kimoja Cha utapeli nikikumbuka hua nacheka sana, japo sio changu kilimtokea mshkaji wangu mmoja

Jamaa anadai walikua na kijiwe Chao wanakutana washkaji wengi tu, kulikua na pool table na vile vimashine vya kubet, anadai kijiwe kilikua na vijana wengi matozi tu na smart phone zilizoshiba....
Huu utapeli uko siku nyingi na una versions nyingi. Kuna mwingine kama huu huu lakini watu walichuliwa kuchimba kaburi.

Matapeli walivyokuwa washenzi, wakachukuwa na mama Ntilie na chakula chake kwenda kuwalisha, wakakodi na gari yaani walipoondoka waliacha kundi lwa watu limetapeliwa kila mmoja na bidhaa yake.

Nikipata muda nitaelezea ilivyokuwa japo sikumbuki vizuri sehemu nyingine.
 
Back
Top Bottom